Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp16 Na. 1 uku. 15
  • Usihangaike

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Usihangaike
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
  • Habari Zinazolingana
  • Mathayo 6:34—“Msihangaike Kamwe Kuhusu Kesho”
    Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
  • Ishi Ukifikiria ya Kesho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Ninaweza Kukabilianaje na Mahangaiko?
    Vijana Huuliza
  • Mtupie Yehova Mahangaiko Yako Yote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
wp16 Na. 1 uku. 15

HEKIMA YA KALE INAYOFAA LEO

Usihangaike

KANUNI YA BIBLIA: “Acheni kuhangaika juu ya nafsi zenu.”—Mathayo 6:25.

Mwanamke anaangalia risiti akiwa na wasiwasi

Inamaanisha nini? Yesu alisema hayo katika Mahubiri yake ya Mlimani. Kulingana na kamusi moja ya Biblia, kitenzi cha Kigiriki kinachotafsiriwa “kuhangaika” kinaweza kumaanisha “jinsi mtu anavyotenda kukabiliana na umaskini, njaa, na matatizo ya kila siku maishani mwake.” Mara nyingi mahangaiko hutokana na kuwa na wasiwasi kuhusu mambo yatakayotukia wakati ujao. Ni jambo la kawaida na linalofaa kuhangaikia mahitaji yetu ya kimwili na hali za wapendwa wetu. (Wafilipi 2:20) Hata hivyo, Yesu aliposema, “acheni kuhangaika,” alikuwa akiwashauri wafuasi wake kutokuwa na wasiwasi bila sababu yoyote, yaani, kuogopa kupita kiasi kitakachotokea kesho kwa kuwa kufanya hivyo kutafanya mtu akose shangwe leo.—Mathayo 6:31, 34.

Je, hekima hiyo inafaa leo? Ni jambo la hekima kufuata ushauri wa Yesu. Kwa nini? Baadhi ya vitabu vinasema kwamba watu wanapokuwa na wasiwasi sana, mfumo wa fahamu hufanya kazi saa zote, na hali hiyo inatajwa kuwa “chanzo cha magonjwa kama vile vidonda vya tumbo, shinikizo la damu, na pumu.”

Yesu alitaja sababu ya msingi kwa nini tunapaswa kuepuka kuhangaika. Alisema kwamba kuhangaika hakuna faida. Yesu aliuliza hivi: “Ni nani kati yenu kwa kuhangaika anaweza kuongeza kipimo cha mkono mmoja kwenye uhai wake?” (Mathayo 6:27) Kuwa na wasiwasi au kuhangaika kupita kiasi hakutaboresha au kuongeza muda tutakaoishi. Mara nyingi mambo huwa tofauti sana na matarajio yetu. Msomi mmoja anasema hivi: “Kuhangaikia wakati ujao ni kupoteza wakati na wakati ujao hauwi mbaya sana kama tunavyoutarajia.”

Mwanamke akifanya kazi bustanini

Tunawezaje kuepuka kuhangaika? Kwanza, mtegemee Mungu. Ikiwa Mungu anawapa chakula ndege na kuyavisha maua hivi kwamba yanavutia, je, hatawapa mahitaji ya msingi wanadamu wanaomwabudu? (Mathayo 6:25, 26, 28-30) Pili, kazia fikira mambo ya leo. Yesu alisema, “Msihangaike kamwe juu ya kesho, kwa maana kesho itakuwa na mahangaiko yake yenyewe.” Je, hukubali kwamba “unatosha kila siku ubaya wake”?—Mathayo 6:34.

Kwa kufuata ushauri wenye hekima aliotoa Yesu, tunaweza kuepuka matatizo mengi. Zaidi ya hayo, tutapata amani ya akili, ambayo Biblia inaiita “amani ya Mungu.”—Wafilipi 4:6, 7.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki