Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 1/15 uku. 6
  • Jibu Linaloridhisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jibu Linaloridhisha
  • Amkeni!—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Uhai Ulianzaje?
    Habari Zaidi
  • “Kutano Lenye Kutajirisha Kweli Kweli”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Unaweza Kupata Wapi Majibu?
    Amkeni!—2004
  • Je, Mashahidi wa Yehova Wanaamini Kwamba Dunia Iliumbwa kwa Siku Sita Zenye Urefu wa Saa 24?
    Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi Kuhusu Mashahidi wa Yehova
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2015
g 1/15 uku. 6
Biblia iliyofunguliwa

HABARI KUU | UHAI ULIANZAJE?

Jibu Linaloridhisha

BAADA ya kuchunguza uthibitisho watu wengi wamekubali kwamba viumbe hai viliumbwa. Fikiria mfano wa Antony Flew, profesa wa falsafa ambaye pindi moja alikuwa mtetezi wa fundisho la kwamba hakuna Mungu. Alipojifunza kuhusu sheria za asili za ulimwengu na viumbe mbalimbali, Flew alibadili maoni yake. Akinukuu msemo wa wanafalsafa wa kale aliandika: “Tunapaswa kukubali jibu sahihi hata ikiwa si jibu tulilotarajia.” Profesa Flew alikubali uthibitisho unaoonyesha kwamba kuna Muumba.

Gerard, aliyetajwa katika makala iliyotangulia anaamini kwamba kuna Muumba. Ingawa amesoma sana na ni mwanasayansi, alisema hivi: “Sikupata uthibitisho wowote kwamba uhai ulitokana na vitu visivyo hai. Kwa kuwa kuna mpangilio mzuri ulimwenguni na viumbe wengi wa pekee, basi lazima kuwe na Aliyebuni na Kupanga mambo yote.”

Kama vile mtu anavyoweza kumjua mchoraji kwa kuchunguza michoro yake, Gerard alijua sifa za Muumba kwa kuchunguza uumbaji. Pia alijifunza Biblia, kitabu cha Mungu. (2 Timotheo 3:16) Katika Biblia alipata majibu ya maswali kuhusu chanzo cha uhai na suluhisho la matatizo ya wanadamu. Basi akaamini kwamba Biblia pia ilitungwa na Mungu.

Kama Gerard alivyosema, Biblia ina majibu mazuri yanayoridhisha. Tunakuhimiza uyachunguze.

Je, Wajua?

BIBLIA HAIPINGANI NA SAYANSI. Badala ya hivyo, inawatia moyo watu wachunguze uumbaji. (Isaya 40:26) Ingawa Biblia si kitabu cha sayansi, inakubaliana na mambo hakika ya kisayansi. Kwa mfano, Biblia haiungi mkono mafundisho ya uwongo kuhusu uumbaji. Haisemi kwamba dunia iliumbwa kwa siku sita halisi zenye urefu wa saa 24 kila moja. Katika kitabu cha Mwanzo neno “siku” limetumiwa kumaanisha kipindi kirefu cha wakati.a

a Kwa habari zaidi, soma broshua Uhai—Ulitokana na Muumba? iliyochapishwa na Mashahidi wa Yehova pia inapatikana kwenye www.jw.org/sw.

Biblia Inafundisha Kwamba . . .

UHAI UNATOKANA NA UHAI MWINGINE. “Kwa maana kwako wewe [Mungu] iko chemchemi ya uzima.”—Zaburi 36:9.

MUNGU ALIUMBA WANYAMA NA MIMEA “KULINGANA NA AINA ZAKE.” (Mwanzo 1:11, 12, 21, 24, 25) Biblia haielezi mipaka ya aina hizi za viumbe na mimea. Hivyo inawezekana kuwe na tofauti hata katika aina moja ya viumbe au mimea.

MUNGU ALIWAUMBA WANADAMU WAKIWA NA UWEZO WA KUONYESHA SIFA KAMA ZAKE. Sifa hizo zinatia ndani upendo, wema, na haki. “Mungu akaendelea kusema: ‘Na tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu.’”—Mwanzo 1:26.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki