Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 2/15 kur. 6-7
  • Viwango Vinavyomfaa Kila Mtu, Nyakati Zote—Upendo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Viwango Vinavyomfaa Kila Mtu, Nyakati Zote—Upendo
  • Amkeni!—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Kutegemezwa na Maadili Yanayodumu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Yaliyomo
    Amkeni!—2015
  • Jinsi Tunavyoweza Kukuza Upendo wa Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Chanzo cha Hali ya Juu Zaidi cha Hekima
    Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2015
g 2/15 kur. 6-7

HABARI KUU | JE, BIBLIA INA FAIDA LEO?

Viwango Vinavyomfaa Kila Mtu, Nyakati Zote—Upendo

KANUNI YA BIBLIA: “Jivikeni upendo, kwa maana huo ni kifungo kikamilifu cha muungano.”—Wakolosai 3:14.

FAIDA: Upendo unaotajwa mara nyingi katika Biblia si ule wa kimahaba au kimapenzi. Bali, Biblia huzungumzia zaidi kuhusu upendo unaoongozwa na kanuni, wenye sifa kama vile huruma, kusamehe, unyenyekevu, fadhili, upole, na subira. (Mika 6:8; Wakolosai 3:12, 13) Tofauti na hisia za kimahaba ambazo mara nyingi hufifia kadiri muda unavyopita, upendo huo huendelea kukua daima dawamu.

Brenda, mwanamke ambaye amekuwa katika ndoa kwa karibu miaka 30, anasema hivi: “Upendo kati ya watu waliofunga ndoa karibuni hauwezi kulinganishwa na kina cha upendo ambacho mume na mke huonyeshana kadiri muda unavyopita.”

Sam, mume ambaye amekuwa katika ndoa kwa zaidi ya miaka 12, anasema hivi: “Sikuzote mimi na mke wangu tumefurahia na hata kushangazwa na jinsi mashauri ya Biblia yalivyo rahisi kueleweka, na jinsi ambavyo kuyatumia huleta matokeo mazuri. Unapoyatumia, mambo yanakuwa shwari. Hata ingawa ningependa kusema kwamba nafuata mashauri ya Biblia nyakati zote, kuna wakati ambapo ninashindwa kufanya hivyo. Kwa mfano, ninapokuwa katika hali ya kuudhika upesi, kutaka kufanya nipendavyo, au ninapokuwa nimechoka. Nyakati kama hizo mimi humwomba Yehova anisaidie kushinda hisia zozote zisizofaa. Kisha ninamkumbatia mke wangu, na baada ya muda mfupi, hali inakuwa shwari kana kwamba hakuna jambo lolote baya lililotendeka!”

“Hekima huonyeshwa kwa matendo yake”

Yesu Kristo alisema “hekima huonyeshwa kwa matendo yake.” (Mathayo 11:19) Kwa msingi wa maneno hayo, ni Biblia pekee yenye hekima ya kweli. Imethibitika kwamba viwango na mafundisho yake huwanufaisha watu sikuzote. Viwango na mafundisho yake huwanufaisha watu wa nchi na tamaduni zote. Biblia inaelezea kwa kina kuhusu tabia za asili za wanadamu na hilo halishangazi kwa sababu Mtungaji wa Biblia ni Muumba wetu—Yehova Mungu. Hata hivyo, kufuata mafundisho ya Biblia kutatuthibitishia kwamba yeye ndiye chanzo cha viwango hivyo. Kwa hiyo, Biblia inatualika tufuate na kutumia viwango na mafundisho ya Yehova inaposema “onjeni mwone ya kuwa Yehova ni mwema.” (Zaburi 34:8) Je, utakubali mwaliko huo?

BIBLIA ILIBORESHA MAISHA YANGU

Linh, ni mwanamke anayeishi Kusini-Mashariki mwa Asia. Mwandishi wa Amkeni! alimhoji kuhusu jinsi ambavyo Biblia imeboresha maisha yake.

Ulilelewa katika dini gani?

Nililelewa katika familia ya Kibudha. Sikujua lolote kuhusu Mungu wa kweli.

Je, uliridhika na maisha yako?

La hasha! Nilikuwa na matatizo mengi sana. Sikujua jinsi ya kupanga matumizi ya pesa zangu, jinsi ya kupata marafiki wazuri, na nilishindwa kuwasaidia wazazi wangu walipopatwa na matatizo.

Maisha yako yamebadilika. Tueleze ilikuwaje?

Wasichana fulani Mashahidi wa Yehova walianza kunifundisha Biblia. Nilipokuwa na matatizo, niliwafikia na kuwaomba mwongozo. Hata ingawa walikuwa na umri mdogo kuliko mimi, walinipa mashauri mazuri sana—mashauri ambayo hayakutegemea maoni yao. Walinionyesha kile ambacho Biblia inasema.

Sasa kwa kuwa nimejionea manufaa ya kufuata mafundisho ya Biblia, ninasadiki kuwa Biblia ni kitabu kutoka kwa Mungu na kinaweza kumsaidia yeyote anayejitahidi kuishi kulingana na mambo anayojifunza. Ingawa elimu ya dunia ni muhimu, hekima ya Biblia ni bora zaidi.

Tafadhali fafanua jambo hilo.

Wazazi wangu walisoma hadi chuo kikuu na ni watu wanaoheshimiwa sana katika jamii. Licha ya hayo wameshindwa kupata suluhisho la matatizo yao. Isitoshe tayari wametalikiana na hawana furaha. Nilipokuwa chuo kikuu, tulifundishwa kwamba nyakati nyingine njia pekee ya kutatua matatizo katika jamii ni kutumia jeuri. Hata hivyo, Biblia inatuambia kwamba wanadamu hawawezi kuleta mafanikio ya kudumu kwa sababu Mungu hakuwaumba wakiwa na uwezo wala haki ya kujiongoza. Hiyo ndiyo sababu mifumo yote ya utawala wa mwanadamu imejaa ufisadi chungu nzima.a Hata hivyo tunapojinyenyekeza kwa Mungu, tunaweza kuboresha maisha yetu kwa kiwango kikubwa na kuwasaidia wengine.

Biblia imekusaidiaje?

Imenisaidia kwa njia nyingi. Sasa sihangaiki sana, na nina marafiki wazuri. Nimejifunza jinsi ya kupanga matumizi ya pesa zangu na angalau ninaweza kufunga safari kutembelea sehemu fulani. Zaidi ya yote, ninaweza kuwasaidia wengine wanapokuwa na uhitaji.

a Soma Mhubiri 8:9; Yeremia 10:23.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki