Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 3/15 kur. 3-6
  • Je, Kuna Mungu? Hilo Linakuhusuje?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Kuna Mungu? Hilo Linakuhusuje?
  • Amkeni!—2015
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • 1. KUSUDI LA MAISHA
  • 2. AMANI YA AKILI
  • 3. TUMAINI
  • 4. MSAADA WA KUKABILIANA NA MATATIZO NA KUFANYA MAAMUZI
  • JE, UTAFANYA UCHUNGUZI?
  • Ukweli Kumhusu Mungu
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Ni Nini Hufanya Maisha Yawe na Kusudi Halisi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Kwa Nini Ni Jambo Muhimu Kujua Ikiwa Kuna Muumba?
    Amkeni!—2021
  • Kusudi Lenyewe la Uhai
    Amkeni!—1992
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2015
g 3/15 kur. 3-6
Mtu ameketi huku akitazama safu za milima na anga lenye kupendeza

HABARI KUU

Je, Kuna Mungu? Hilo Linakuhusuje?

Watu wengi hawajui au hawajali ikiwa Mungu yuko. Hervé, aliyelelewa huko Ufaransa, anasema hivi: “Sishirikiani na dini yeyote ingawa naamini kwamba kuna Mungu. Jambo kuu kwangu ni kuishi kwa kutegemea akili. Na hilo halihitaji kutegemea mungu.”

Huenda wengine wakahisi kama John kutoka Marekani. Alisema hivi: “Nililelewa na wazazi wasiomwamini Mungu. Nilipokuwa kijana, sikuwa na hakika ikiwa Mungu yuko. Hata hivyo, wakati mwingine nilifikiria sana kuhusu jambo hilo.”

Je, umewahi kufikiria ikiwa Mungu yuko, na ikiwa yuko, je, maisha yana kusudi? Huenda umeona kwamba ni vigumu kuelezea mambo fulani maishani bila ya kukubali kwamba kuna Muumba, kama vile uhai haukujitokeza wenyewe au uchunguzi wa kisayansi unaoonyesha usawaziko unaofaa wa viumbe asili unaotegemeza uhai katika sayari yetu.—Tazama sanduku “Chunguza Uthibitisho.”

Fikiria umuhimu wa mambo yaliyotajwa hapo juu. Ni kama ishara zinazoongoza kwenye hazina. Utanufaika sana ukipata ukweli unaothibitisha kwamba Mungu yuko kupitia habari zenye kuaminika kumhusu. Chunguza mambo manne yafuatayo.

1. KUSUDI LA MAISHA

Mtu anasoma kitabu kikubwa akiwa na huzuni sana

Ikiwa kuna kusudi maishani, tungependa kujua kusudi hilo ni nini na ni kwa jinsi gani tunahusika. Kwa kweli, ikiwa hatujui kama Mungu yuko, basi tunaishi bila kujua ukweli muhimu zaidi katika ulimwengu.

Biblia inasema kwamba Mungu ndiye Chanzo cha uhai wote. (Ufunuo 4:11) Kujua hilo kutatusaidiaje kuwa na kusudi maishani? Ona kile ambacho Biblia inafundisha kuhusu hilo.

Wanadamu ni viumbe wa pekee sana ukilinganisha na viumbe wengine duniani. Kulingana na Biblia, tuliumbwa kwa mfano wa Mungu, yaani tuna uwezo wa kusitawisha sifa zake. (Mwanzo 1:27) Zaidi ya hilo, Biblia inafundisha kwamba wanadamu wanaweza kuwa rafiki wa Mungu. (Yakobo 2: 23) Tunaweza tu kuwa na maisha yenye kusudi tukiwa na uhusiano huo na Muumba wetu.

Inamaanisha nini kuwa rafiki ya Mungu? Marafiki wa Mungu wanaweza kuongea naye moja kwa moja. Naye anaahidi kwamba atawasikiliza na kuwasaidia. (Zaburi 91:15) Tukiwa rafiki wa Mungu tunaweza kujua maoni yake kuhusu mambo mengi. Hilo linaweza kutusaidia kujua majibu yenye kutegemeka ya maswali muhimu zaidi maishani mwetu.

Ikiwa hatujui kama Mungu yuko, basi tunaishi bila kujua ukweli muhimu zaidi katika ulimwengu

2. AMANI YA AKILI

Mtu akiwa na sura isiyo na mahangaiko

Kwa mfano, watu wengi wanaona ni vigumu kuamini kwamba kuna Mungu kwa sababu ulimwengu umejaa mateso. Wao huuliza, ‘Kwa nini Muumba mwenye nguvu zote anaruhusu uovu na kuteseka?’

Biblia inatoa jibu lenye kufariji linaloonyesha kwamba Mungu hakukusudia wanadamu wateseke. Hakukuwa na mateso wanadamu walipoumbwa. Pia, Mungu hakukusudia wanadamu wafe. (Mwanzo 2:7-9, 15-17) Je, ni vigumu kuamini hilo? Ni ndoto tu? Hapana. Kwa kweli ikiwa kuna Muumba mwenye nguvu zote ambaye sifa yake kuu ni upendo, basi tungetarajia awaandalie wanadamu aina hiyo ya uhai.

Wanadamu walijikuta namna gani katika hali hiyo mbaya? Biblia inaeleza kwamba Mungu aliwaumba wanadamu na kuwapa uhuru wa kuchagua. Sisi si mashine hivyo hatulazimishwi kumtii Mungu. Wazazi wetu wa kwanza walikataa mwongozo wa Mungu. Badala yake, walifuatia kwa ubinafsi mapendezi yao wenyewe. (Mwanzo 3:1-6, 22-24) Hiyo ndiyo sababu leo tunakabili hali ngumu.

Tunaweza kupata amani nyingi ya akili tunapojua kwamba Mungu hakukusudia wanadamu wateseke. Pamoja na hayo, tungependa kuona mwisho wa kuteseka. Tunahitaji kuwa na tumaini la wakati ujao.

3. TUMAINI

Sayari ya Dunia

Punde tu baada ya wanadamu kuasi, Mungu aliahidi kwamba angetimiza kusudi lake la mwanzoni kuhusu dunia. Hakuna lolote linaloweza kumzuia kutimiza kusudi lake kwa kuwa yeye ni mweza-yote. (Isaya 55:11) Hivi karibuni, Mungu ataondoa madhara yote yaliyosababishwa na uasi dhidi yake, kisha dunia na wanadamu wataishi kulingana na kusudi lake la mwanzoni.

Hilo linakuhusuje? Fikiria ahadi mbili kati ya nyingi zinazopatikana katika Biblia alizotoa Mungu kuhusu wakati wetu ujao.

  • UOVU UTAONDOLEWA NA KUTAKUWA NA AMANI DUNIANI KOTE. “Na bado muda kidogo tu, na mtu mwovu hatakuwako tena; nawe hakika utapaangalia mahali pake, naye hatakuwapo. Bali wapole wataimiliki dunia, nao watapata furaha yao tele katika wingi wa amani.” —Zaburi 37:10, 11.

  • HAKUTAKUWA NA MAGONJWA NA KIFO. “Na hakuna mkaaji atakayesema: ‘Mimi ni mgonjwa.’” (Isaya 33:24) “Yeye kwa kweli atameza kifo milele, na Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova hakika atafuta machozi katika nyuso zote.”—Isaya 25:8.

Kwa nini tunaweza kuamini ahadi za Mungu zinazopatikana katika Biblia? Kwa sababu unabii mwingi ulio katika Biblia tayari umetimizwa kikamili. Hata hivyo, tumaini la wakati ujao la kuondolewa kwa mateso haliondoi hali ngumu tunazokabili sasa. Mungu anatupa msaada gani zaidi?

4. MSAADA WA KUKABILIANA NA MATATIZO NA KUFANYA MAAMUZI

Mkono mmoja ukiufikia mkono wa mtu mwingine

Mungu anatupatia mwongozo unaotusaidia kukabiliana na matatizo na kufanya maamuzi vizuri. Maamuzi mengi ni madogo, lakini mengine yanaweza kuathiri maisha yetu kwa muda mrefu. Hekima tunayopata kutoka kwa Muumba wetu ni yenye kufaa sana kuliko hekima yoyote kutoka kwa wanadamu. Hekima yake ni bora kwa kuwa yeye ni Chanzo cha uhai wetu na anajua mambo yote ya wakati uliopita na ya wakati ujao. Kwa hiyo anajua tunahitaji nini ili tuwe na maisha bora.

Yehova Mungu aliwaongoza wanadamu kuandika mawazo yake katika Biblia. Tunasoma hivi katika Biblia: “Mimi, Yehova, ni Mungu wako, Yeye anayekufundisha ili ujifaidi mwenyewe, Yeye anayekufanya uende katika njia unayopaswa kutembea ndani yake.”—Isaya 48:17, 18.

Mungu ana nguvu zisizo na mipaka na yuko tayari kuzitumia ili kutusaidia. Biblia inamtaja Mungu kuwa baba mwenye upendo anayetaka kutusaidia. Inasema hivi: ‘Baba aliye mbinguni atawapa roho takatifu wale wanaomwomba!’ (Luka 11:13) Nguvu hiyo kutoka kwa Mungu inaweza kutuongoza na kutuimarisha.

Unawezaje kupata msaada huo kutoka kwa Mungu? Biblia inajibu hivi: “Yule anayemkaribia Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko na kwamba yeye huwa mthawabishaji wa wale wanaomtafuta kwa bidii.” (Waebrania 11:6) Ili usadiki kwamba Mungu yuko, unapaswa kuchunguza uthibitisho.

JE, UTAFANYA UCHUNGUZI?

Wakati unahitajiwa ili kutafuta ukweli kumhusu Mungu, lakini kwa hakika utafaidika ukifanya hivyo. Fikiria kisa cha Xiujin Xiao, aliyezaliwa China lakini sasa anaishi Marekani. Anasema hivi: “Ingawa niliamini fundisho la mageuzi, nilitamani kuijua Biblia. Kwa hiyo, nilianza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Katika mwaka wangu wa mwisho chuoni, nilikuwa na mambo mengi ya kufanya hivi kwamba nikakosa wakati wa kujifunza Biblia kwa ukawaida. Hivyo, nilikosa furaha. Nilipoanza tena kujifunza Biblia kwa bidii, nilipata shangwe moyoni.”

Je, ungependa kujifunza mengi zaidi kumhusu Muumba wetu, Yehova Mungu? Kwa nini usitumie wakati wako kufanya uchunguzi?

Biblia Inasema Nini Kuhusu Mungu?

Ujumbe wa Biblia kuhusu Mungu unaeleweka, unachochea fikira na kwa wengine ni wenye kushangaza.

  • Muumba wetu ni halisi, yeye ni Mungu mwenye utu na jina lake ni Yehova.a—Isaya 42:8.

  • Yehova Mungu hana mwanzo wala mwisho.—Zaburi 93:2; Isaya 40:28.

  • Mungu si hakimu mkali kama baadhi ya dini zinavyofundisha. Badala yake, sifa yake kuu ni upendo.—1 Yohana 4:8.

  • Mungu anapendezwa na wanadamu na ametuambia makusudi yake kuhusu maisha yetu.—Mhubiri 12:13; Mika 6:8.

Je, Biblia inafunua kila jambo kumhusu Mungu? Hapana. Biblia inasema kwamba tunajua tu “kingo za njia zake.”—Ayubu 26:14.

a Biblia nyingi zinatumia jina la cheo “BWANA” kuwakilisha herufi za Kiebrania YHWH, ambalo mara nyingi katika Kiswahili jina hilo hutafsiriwa “Yehova” au “Yahweh.”

Chunguza Uthibitisho

Machapisho yafuatayo yanaonyesha uthibitisho wa kuwapo kwa Muumba.

  • Jalada la broshua Maswali Matano Kuhusu Chanzo cha Uhai

    Maswali Matano Muhimu Kuhusu Chanzo cha Uhai

    Inapatikana katika lugha 47

    Kutoka katika ukurasa wa 12: “Watu wanaoamini nadharia ya mageuzi husema kwamba Mungu hakuhitaji kuingilia kati ili kutokeza uhai duniani. Hata hivyo, kadiri wanasayansi wanavyozidi kuelewa mambo fulani kuhusu uhai, ndivyo wanavyotambua kwamba haiwezekani kuwa ulijitokeza wenyewe.”

  • Jalada la broshua Uhai Ulitokana na Muumba?

    Uhai—Ulitokana na Muumba?

    Inapatikana katika lugha 80

    Kutoka katika ukurasa wa 24: “Watu wengi hudai kwamba sayansi huthibitisha kwamba masimulizi ya Biblia kuhusu uumbaji si ya kweli. Lakini, tofauti iliyopo, si kati ya sayansi na Biblia, bali ni kati ya sayansi na vikundi vya Wakristo Wahafidhina.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki