Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g21 Na. 3 kur. 14-15
  • Kwa Nini Ni Jambo Muhimu Kujua Ikiwa Kuna Muumba?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Ni Jambo Muhimu Kujua Ikiwa Kuna Muumba?
  • Amkeni!—2021
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Maisha yako yatakuwa na kusudi
  • Utapata mwongozo unaotegemeka wa kukusaidia kwenye maisha ya kila siku
  • Utapata majibu ya maswali yako
  • Utakuwa na tumaini la wakati ujao
  • Je, Kuna Mungu? Hilo Linakuhusuje?
    Amkeni!—2015
  • Ukweli Kumhusu Mungu
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Biblia Inatupatia Tumaini
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Biblia Inatupatia Tumaini
    Furahia Maisha Milele—Masomo ya Kwanza ya Biblia
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2021
g21 Na. 3 kur. 14-15
Marafiki wakifurahia kuangalia wanyama walio juu ya mti.

Kwa Nini Ni Jambo Muhimu Kujua Ikiwa Kuna Muumba?

Je, kuna umuhimu wowote wa kujua ikiwa kuna Muumba au la? Ikiwa mambo tuliyozungumzia yanakuthibitishia kwamba Mungu mweza-yote yupo, basi huenda ukahitaji kuchunguza uthibitisho kwamba Biblia iliongozwa na roho yake. Na ikiwa utatumaini yale ambayo Biblia inasema, utanufaika kwa njia zifuatazo.

Maisha yako yatakuwa na kusudi

BIBLIA INASEMA: “[Mungu] alitenda mema, akiwapa ninyi mvua kutoka mbinguni na majira ya mavuno, akiwashibisha kwa chakula na kuijaza mioyo yenu furaha.”​—Matendo 14:17.

INAMAANISHA NINI? Kila kitu unachofurahia duniani ni zawadi kutoka kwa Muumba. Utazithamini zaidi zawadi hizo ukitambua kwamba Mtoaji wa zawadi hizo anakujali wewe kibinafsi.

Utapata mwongozo unaotegemeka wa kukusaidia kwenye maisha ya kila siku

BIBLIA INASEMA: “[Utaelewa] lililo la uadilifu na la haki na lililo sawa, njia yote ya lililo jema.”​—Methali 2:9.

INAMAANISHA NINI? Akiwa Muumba wako, Mungu anajua mambo unayohitaji ili uwe na furaha. Kwa kuchunguza Biblia, unaweza kupata masomo yatakayokunufaisha sasa.

Utapata majibu ya maswali yako

BIBLIA INASEMA: “Nawe utapata ujuzi kumhusu Mungu.”​—Methali 2:5.

INAMAANISHA NINI? Kutambua kwamba Muumba yupo kutakusaidia kupata majibu ya maswali muhimu, kama vile: Maisha yana kusudi gani? Kwa nini watu wanateseka sana? Ni nini kinachotupata tunapokufa? Unaweza kupata majibu yenye kuridhisha kwenye Biblia.

Utakuwa na tumaini la wakati ujao

BIBLIA INASEMA: “‘Ninajua vizuri mawazo ninayofikiria kuwaelekea ninyi,’ asema Yehova, ‘mawazo ya amani, wala si ya msiba, ili niwape ninyi wakati ujao na tumaini.’”​—Yeremia 29:11.

Tazama video yenye kichwa Tunawezaje Kuwa na Hakika Kwamba Yale Yaliyoandikwa Katika Biblia Ni ya Kweli? na Ni Nani Aliyeitunga Biblia? kwenye jw.org/sw. Unaweza kutafuta video hizi kwa kuandika maneno “Biblia ni ya kweli” au “aliyeitunga Biblia” kwenye sehemu ya kutafuta.

INAMAANISHA NINI? Mungu anaahidi kwamba wakati ujao ataondoa uovu, mateso, na hata kifo. Ukitumaini ahadi za Mungu za wakati ujao, tumaini hilo litakusaidia kukabiliana na matatizo ya kila siku kwa ujasiri.

Jinsi baadhi ya watu walivyonufaika kwa kuamini kwamba kuna Muumba

Cyndi.

“Sikuzote ninashangazwa na jinsi ambavyo Mungu anatusaidia katika nyanja mbalimbali maishani. Anatusaidia kujua mambo ya kutanguliza maishani, kudumisha uhusiano mzuri na wengine, na jinsi ya kuwa rafiki yake.”​—Cyndi, Marekani.

Elise.

“Maisha yangu yamekuwa yenye kuridhisha na kufurahisha kwa sababu ya kuamini kuna Muumba. Hilo linanifurahisha kwa sababu kuna mambo mengi ya kujifunza kumhusu, kuhusu uumbaji wake, na kuhusu Neno lake.”​—Elise, Ufaransa.

Peter.

“Kutumia mambo ambayo Muumba wetu anatufundisha kwenye Biblia hunifanya niwe na furaha zaidi. Hunisaidia nisiwachambue-chambue wengine, nijali mahitaji yao, na niridhike. Pia, kumenisaidia kuwa baba bora.”​—Peter, Uholanzi.

Liz.

“Kabla ya kujifunza kumhusu Mungu, maisha yangu yalikuwa kula, kulala, na kujitahidi kuwahi kazini. Sikuwa na furaha. Sasa ninaona maisha kuwa zawadi bora zaidi —zawadi tunayopaswa kuifurahia na kuitunza.”​—Liz, Estonia.

Adrien.

“Mimi ni mtu mwenye mahangaiko sana. Lakini kujua kwamba uovu, ukosefu wa haki, na mateso yatakwisha kumenisaidia kukabiliana na hali hiyo.”​—Adrien, Ufaransa.

Ona majibu ya Biblia ya maswali muhimu maishani. Tazama video Kwa Nini Ujifunze Biblia?​—Video Nzima.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki