Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 11/15 kur. 12-13
  • Jinsi ya Kuwapongeza Watoto

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kuwapongeza Watoto
  • Amkeni!—2015
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • CHANGAMOTO
  • Kumfundisha Mtoto Wako Kuwa Mstahimilivu
    Msaada kwa Ajili ya Familia
  • Msifuni Yehova Mungu Wetu
    Mwimbieni Yehova
  • Msifuni Yehova Mungu Wetu!
    ‘Mwimbieni Yehova kwa Shangwe’
  • Kupitia Macho ya Mtoto
    Amkeni!—1990
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2015
g 11/15 kur. 12-13
Mtoto anachora picha huku baba yake akimshika begani

MSAADA KWA AJILI YA FAMILIA | KULEA WATOTO

Jinsi ya Kuwapongeza Watoto

CHANGAMOTO

Watu fulani huamini kwamba hakuna ubaya kumpongeza mtoto kupita kiasi. Wengine huamini kwamba mtoto anapopongezwa sana ataharibika na kuhisi ana haki ya kupewa chochote au kufanya jambo lolote.

Mbali tu na kufikiria unampongeza mtoto kiasi gani, unapaswa pia kufikiria unampongeza kwa njia gani. Ni pongezi ya aina gani itakayomtia moyo mtoto wako? Ni ya aina gani itakayomzuia asifanye maendeleo? Unawezaje kutoa pongezi yenye matokeo mazuri zaidi?

MAMBO UNAYOPASWA KUJUA

Pongezi hazilingani. Fikiria yafuatayo.

Kupongeza kupita kiasi kunaweza kuwa na madhara. Wazazi fulani huwapongeza watoto hata wakati hawastahili wakidhani itawasaidia wajiamini zaidi. Lakini Dakt. David Walsh anaonya kwamba watoto “wanaweza kutambua unapowapongeza lakini humaanishi unayosema. Wanaweza pia kutambua ikiwa hawastahili [pongezi hizo] na huenda wakaamua kuwa wewe si mtu mwenye kuaminika.”a

Kupongeza uwezo wa asili. Huenda binti yako ana kipaji cha kuchora. Ungependa kumpongeza kwa uwezo huo, jambo ambalo litamsaidia kuboresha uchoraji wake. Lakini huenda hilo likawa na madhara. Pongezi zinazokazia tu kipaji fulani zinaweza kumfanya mtoto wako afikiri ustadi anaopaswa kufuatilia ni ule ambao hauhitaji jitihada zozote. Huenda hata akaogopa kujifunza mambo mapya, akihofu kwamba atashindwa. Anaweza kujiambia hivi: ‘Ikiwa jambo linahitaji jitihada nyingi, huenda sina uwezo wa kulifahamu, basi kwa nini nilijaribu?’

Ni vizuri zaidi kupongeza jitihada. Watoto wanaopongezwa kwa ajili ya bidii na uvumilivu na si tu kwa vipaji vyao wanajifunza jambo muhimu—kwamba ili mtu awe na ustadi katika jambo fulani anahitaji subira na jitihada. Kitabu Letting Go With Love and Confidence kinasema kwamba wakijua jambo hilo, “watatia bidii ili kufikia malengo yao . . . na ikiwa hawatafaulu, hawatajiona kuwa wameshindwa, bali wanajifunza.”

MAMBO UNAYOWEZA KUFANYA

Mpongeze kwa jitihada zake, si uwezo wa asili tu. Huenda ukamsaidia zaidi mtoto wako unapomwambia, “Ninaona umejitahidi sana kuchora picha hii,” badala ya kusema, “Una kipaji cha uchoraji.” Zote mbili ni pongezi, lakini bila kukusudia njia ya pili inaweza kumfanya mtoto afikiri kwamba hawezi kukuza ustadi wa kufanya jambo lingine lolote isipokuwa vipaji alivyozaliwa navyo.

Unapompongeza mtoto wako kwa jitihada yake, unamfundisha kwamba mazoezi yataboresha uwezo wake wa kufanya mambo. Hivyo mtoto wako atajifunza mambo mapya akiwa na uhakika zaidi.—Kanuni ya Biblia: Methali 14:23.

Msaidie asikate tamaa anaposhindwa. Watu wema hukosea, labda hata mara kadhaa. (Methali 24:16) Lakini wakikosea hawakati tamaa, wanajifunza kutokana na makosa yao na kusonga mbele. Unaweza kumsaidiaje mtoto wako asitawishe mtazamo huo mzuri?

Kazia jitihada alizotia kufanya jambo fulani. Fikiria mfano huu: Labda mara nyingi unamwambia binti yako, “Una kipaji cha hesabu,” lakini pindi fulani anaanguka mtihani wa hesabu. Huenda akaamini kwamba amepoteza kipaji chake kwa hiyo hana haja ya kuongeza bidii.

Hata hivyo, unapokazia jitihada yake, unamsaidia kuwa mvumilivu. Kwa hiyo, badala ya kuona jambo hilo kuwa kizuizi ataliona kuwa la kawaida tu. Badala ya kukata tamaa, atajaribu njia nyingine au ataongeza bidii.—Kanuni ya Biblia: Yakobo 3:2.

Mweleze makosa yake kwa njia inayojenga. Unapomweleza mtoto wako makosa yake kwa njia inayofaa, hatavunjika moyo. Pia, ikiwa kwa kawaida unampongeza mtoto wako kwa njia inayofaa, huenda akawa tayari kusikiliza unapomweleza jinsi anavyoweza kufanya maendeleo. Kisha wewe na yeye mtafurahia mafanikio yake.—Kanuni ya Biblia: Methali 13:4.

a Kutoka katika kitabu No: Why Kids—of All Ages—Need to Hear It and Ways Parents Can Say It.

MAANDIKO MUHIMU

  • “Kwa kila kazi ngumu hutokea faida.”—Methali 14:23.

  • “Sisi sote hujikwaa mara nyingi.”—Yakobo 3:2.

  • “Nafsi ya wenye bidii itanoneshwa.”—Methali 13:4.

KUKABILIANA NA CHANGAMOTO MPYA

Biblia inatueleza kuhusu watu waliotimiza mambo fulani yaliyozidi uwezo wao. Kwa mfano, Musa alisita alipoagizwa aende kwa mfalme mwenye nguvu na mkaidi wa Misri. Alisema hivi: “Mimi si msemaji mzuri.” (Kutoka 4:10) Yeremia pia alihisi hivyo alipoagizwa kuwa nabii. Alisema hivi: “Mimi hakika sijui jinsi ya kusema, kwa sababu mimi ni mvulana tu.” (Yeremia 1:6) Hata hivyo, Musa na Yeremia walitimiza migawo yao vizuri sana.

Tunajifunza nini? Uwezo wa mtoto wako hautegemei tu vipaji vyake. Mpongeze kwa jitihada zake, na huenda akakushangaza kwa kutimiza mengi kuliko alivyofikiri kuwa anaweza.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki