Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g21 Na. 1 kur. 8-9
  • Jinsi ya Kuwa Wenye Furaha na Kuridhika

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kuwa Wenye Furaha na Kuridhika
  • Amkeni!—2021
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Fanya Kazi kwa Bidii
  • Uwe Mnyoofu
  • Uwe na Maoni Yanayofaa Kuhusu Pesa
  • Chagua Kupata Elimu Bora Zaidi
  • Maoni Yenye Usawaziko Kuhusu Pesa
    Amkeni!—2015
  • Je, Pesa Ndio Chanzo cha Uovu Wote?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Pesa
    Amkeni!—2014
  • Tunapaswa Kuwa na Maoni Gani Kuhusu Pesa?
    Amkeni!—2007
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2021
g21 Na. 1 kur. 8-9
Mama na kijana wake wakitembea wakiwa wameridhika kwenye eneo la biashara nchini India ambapo watu wengi wanatamani kununua vitu vya gharama ya juu.

Jinsi ya Kuwa Wenye Furaha na Kuridhika

Sisi sote​—iwe ni waseja au tumefunga ndoa, vijana au wazee—tunataka kuwa na furaha na kuridhika. Muumba wetu anataka tuhisi hivyo pia, hivyo, ametupatia ushauri bora sana.

Fanya Kazi kwa Bidii

“Afanye kazi kwa bidii, akifanya kazi njema kwa mikono yake, ili awe na kitu cha kumgawia mtu mwenye uhitaji.”​​—WAEFESO 4:28.

Muumba wetu anatutia moyo tuwe na maoni yanayofaa kuhusu kazi. Kwa nini? Mtu anayefanya kazi kwa bidii ana furaha kwa sababu anaweza kujiandalia mahitaji yake na yale ya familia yake. Hata anaweza kumsaidia mtu mwingine mwenye uhitaji. Mwajiri wake atamthamini sana. Kwa hiyo, mfanyakazi mzuri anaweza kudumisha kazi yake. Maandiko yanaonyesha kwamba matokeo ya kufanya kazi kwa bidii ni “zawadi kutoka kwa Mungu.”​—Mhubiri 3:13.

Uwe Mnyoofu

“Tuna hakika kwamba tuna dhamiri nyoofu, kwa kuwa tunataka kujiendesha kwa unyoofu katika mambo yote.”​​—WAEBRANIA 13:18.

Ikiwa sisi ni wanyoofu, tutajiheshimu, tutakuwa na amani ya akili, na tutalala usingizi mnono. Zaidi ya hilo, wengine watatuamini na kutuheshimu. Watu wasio wanyoofu wanajinyima wenyewe vitu hivyo vizuri. Pia, dhamiri zao zinaweza kuwasumbua, nao wanaishi kwa wasiwasi wakihofu kwamba siku moja watakamatwa kwa sababu ya kutokuwa wanyoofu.

Uwe na Maoni Yanayofaa Kuhusu Pesa

“Njia yenu ya maisha iwe bila upendo wa pesa, huku mkiridhika na vitu mlivyo navyo.”​​—WAEBRANIA 13:5.

Tunahitaji pesa ili tununue chakula na mahitaji mengine ya msingi. Hata hivyo, kupenda pesa ni hatari sana. Kunaweza kumfanya mtu atumie wakati wake na nguvu zake zote kujitahidi kupata pesa nyingi zaidi. Kwa sababu anajitahidi sana kupata pesa zaidi, uhusiano wake na mwenzi wake wa ndoa unaweza kuharibika, anaweza kukosa muda wa kuwa pamoja na watoto wake, na hata kudhuru afya yake. (1 Timotheo 6:9, 10) Isitoshe, mtu anayependa pesa anaweza kushawishika kwa urahisi kutokuwa mnyoofu. Mwanamume mmoja mwenye hekima alisema hivi: “Mtu mwaminifu atapata baraka nyingi, lakini anayeharakisha kupata utajiri hatabaki bila hatia.”​—Methali 28:20.

Chagua Kupata Elimu Bora Zaidi

“Ilinde hekima inayotumika na uwezo wa kufikiri.”​​—METHALI 3:21.

Elimu bora inatusaidia tuwe watu wazima wenye kutegemeka na pia wazazi bora. Lakini elimu ya shuleni pekee haitoshi kutupatia kila kitu tunachohitaji na kuwa na furaha. Ili tufanikiwe kikweli katika nyanja zote za maisha, tunahitaji elimu ambayo Mungu anatupatia. Maandiko yanasema hivi kuhusu mtu anayemsikiliza Mungu: “Kila jambo analofanya litafanikiwa.”​—Zaburi 1:1-3.

Nina Furaha na Nimeridhika

“Katika eneo ninaloishi, watu wengi hujitahidi sana kupata elimu ya juu zaidi, utajiri, na umaarufu. Lakini, hata baada ya kutimiza malengo yao, bado wanahangaika kupata furaha ya kweli. Biblia ilinisaidia kutambua jambo la muhimu zaidi maishani. Nilijifunza kwamba pesa zinaweza kuwa ulinzi kwa kiasi fulani, lakini haziwezi kununua furaha au upendo wa kweli. Nina furaha na nimeridhika kwa sababu Biblia inanisaidia kufanya maamuzi yenye hekima kuhusu pesa na kazi.”​​—Kishore.

Kishore.

Jifunze zaidi:

Ili kupata ushauri mwingine kutoka kwa Muumba wetu kuhusu ajira, pesa, na elimu, tembelea tovuti ya jw.org/sw na utazame chini ya kichwa MAFUNDISHO YA BIBLIA > AMANI NA FURAHA.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki