Sura ya 2
Kwa nini ni Hekima Kuichungaza Dini Yako
1. (a) Kwa kuwa Mungu karibuni ataiharibu taratibu hii ya mambo, ni swali gani ambalo ni lazima kwetu kuuliza juu ya ibada yetu? (b) Ikiwa tunataka kufuata mwendo ambao Mungu huukubali, tutakiendea kitabu gani?
TUNAYO sababu nzuri kufikiri sana juu ya uhusiano wetu na Mungu. Kwa nini? Kwa sababu ushuhuda huonyesha kwamba karibuni Mungu atawaharibu waovu na kusimamisha taratibu yake mpya ya haki. Hivyo ni lazima kwetu kuuliza: “Je! ninamwabudu Mungu kwa njia ambayo yeye huikubali?” Si mwanadamu ye yote, bali Mungu, ambayo ni hakimu wa jambo linalompendeza yeye. Ili kupata maoni ya Mungu, lazima tuiendee Biblia. Mle ndimo yeye hutuambia waziwazi mwendo wa kufuata ikiwa tunataka kupata uzima wa milele. (Mithali 3:1, 2) Tukithamini anachosema na kukitumia katika maisha zetu, kitatokea katika baraka za ajabu kwetu, sasa na katika vizazi vitakavyokuja.
2. Ni maneno gani katika Biblia huonyesha kwamba dini zote hazipendezi kwa Mungu?
2 Tuchunguzapo ambayo Biblia husema juu ya shauri hili, tunapata nini? Je! inafundisha kwamba mamia ya mamilioni ya watu wafuatao dini katika njia nyingi sana mbalimbali wote humpendeza Mungu? Je! inaonyesha kwamba dini zote ni nzuri? Kutuwezesha kujua jinsi aonavyo shauri, Mungu aliandikisha usemi huu ulio waziwazi katika Neno lake: “Njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo. Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wacha che.” (Mathayo 7:13, 14) Jinsi maneno hayo hujibu maswali yetu waziwazi! Yaonyesha kwamba watu wengi hawamwabudu Mungu kwa njia impendezayo. Wachache tu ndio wako katika barabara iongozayo kwenye uzima.
3. Je! yako mambo yafanywayo katika jina la dini ambayo hayakubaliwi na, wewe?
3 Labda unajiona mwenyewe kukubali upesi jambo la kwamba dini nyingi hazikubaliwi na Mungu. Bila shaka yako mambo mengi yafanywayo katika jina la dini ambayo hayakubaliwi na wewe. Kwa mfano, ukitazama huku na huku katika makanisa na kuwaangalia watu wenye kuishi maisha za ufisadi lakini ambao husingizia kuwa wenye haki, unajua kwamba kuna kosa fulani. (2 Timotheo 3:4, 5) Na usomapo katika gazeti kwamba mapadre wengine hukubali waziwazi ngono baina ya watu wasiooa au wasioolewa na kwamba wanasema kwamba kulalana wanaume kwa wanaume na wanawake kwa wanawake kunaruhusika chini ya hali fulani, unajua sawasawa kwamba hivi si ndivyo Mungu asemavyo. Labda unakumbuka kwamba Mungu aliiharibu miji ya zamani ya Sodoma na Gomora. Na kwa nini? Kwa sababu walizoea mambo ya namna hiyo! Hivyo wajua kwamba Mungu hatakubali dini inayawaambia watu kwamba inaruhusika kutenda kama hivyo.—Yuda 7.
4. (a) Zaidi ya kuwa kwetu wenye adili na wenye fadhili, lazima tuangalie nini linginelo juu ya dint yetu, kwa sababu ya maneno ya Yesu katika Yohana 4:23? (b) Kwa nini ni lazima kwetu kuchunguza mafundisho ya dini ambayo tumerundishwa?
4 Walakini, bila shaka umewasikia watu wakisema hivi: “Haidhuru unaamini nini, mradi uishi maisha safi ya adili na kuwatendea majirani zako kwa fadhili.” Je! ndiyo hayo tu kwa kumwabudu Mungu katika njia yenye kukubalika? Mambo haya ni ya lazima, lakini Mungu hutaka zaidi. Mafundisho ya dini yanatiwa ndani pia. Biblia hutupasha habari kwamba “waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli.” (Yohana 4:23) Ikiwa ibada yetu itakubaliwa kwa Mungu, lazima ithibitishwe katika Neno la Mungu la kweli. Yesu aliwakaripia watu wale waliojidai kumtumikia Mungu lakini ambao walitegemea sana juu ya mapokeo ya wanadamu kuliko Neno la Mungu. Alitumia kwao maneno ya Mungu mwenyewe kutaka katika Isaya 29:13, akisema: “Nao waniabudu bure, wakifundisha mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu.” (Mathayo 15:9) Kwa kuwa hatutaki ibada yetu kuwa ya bure, ni muhimu kwa kila mmoja wetu kuichunguza dini yake.
5. Kwa nini ni lazima kwetu kuchunguza, si yale tu ambayo sisi peke yetu tunaamini, bali pia na mafundisho ya tengenezo lo lote la kidini ambalo labda tunashirikiana nalo?
5 Tunahitaji kuchunguza, si yale tu ambayo sisi peke yetu tunaamini, bali pia yanayofundishwa na tengenezo lo lote la kidini ambalo labda tunashirikiana nalo. Je! mafundisho yake yanapatana kabisa na Neno la Mungu, au msingi wake ni juu ya mapokeo ya wanadamu? Ikiwa sisi tu wapenda kweli, hakuna kitu cha kuogopa kwa uchunguzi wa namna hiyo. Lazima iwe tamaa ya kweli ya kila mmoja wetu kujifunza mapenzi ya Mungu ni nini kwetu sisi, kisha kuyafanya.—Yohana 8:32.
6. (a) Je! jambo la kwamba Biblia hutumiwa pindi kwa pindi kanisani huthibitisha kwamba mafundisho ya dini yote ya kanisa yanatoka katika Biblia? (b) Kwa nini ni lazima dini inayokubaliwa na Mungu ipatane na Biblia katika mambo yote madogo?
6 Jambo tu la kwamba labda washiriki wa kanisa wanayo Biblia au kwamba inasomwa kwao pindi kwa pindi kutoka jukwaani halithibitishi lenyewe kwamba mambo yote wanayofundishwa yamo katika Biblia. Ni vizuri kuwa na Biblia; yampasa kila mtu awe nayo. Lakini lazima tujue pia mambo ambayo inasema na kuyaamini. Ikiwa dini kweli huikubali Biblia kama Neno la Mungu, haitatumia sehemu fulani zake na kuzikataa sehemu nyingine. “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza.” (2 Timotheo 3:16) Kwa kuwa ni hivyo, dini inayokubaliwa na Mungu lazima ipatane katika mambo yake yote madogo na Biblia.
7. Kama inavyoonyeshwa na mtume Paulo, je! unyofu wa moyo peke yake wa waabudu unaonyesha kwamba dini yao inakubaliwa na Mungu?
7 Mtu anayetaka kumpendeza Mungu lazima awe na unyofu wa moyo. Lakini unyofu wa moyo peke yake haufanyi dini ya mtu kukubaliwa machoni pa Mungu. Mtume Paulo aliongozwa na roho ya Mungu kuandika kuhusu watu fulani katika, siku zake: “Nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa. Kwa maana, wakiwa hawaijui haki ya Mungu, na wakitaka kuithibitisha haki yao wenyewe, hawakujitia chili ya haki ya Mungu.” (Warumi 10:2, 3) Kama matokeo, unyofu wa moyo wao uliongozwa vibaya. Tatizo lao lilikuwa kwamba walikuwa wakitazama katika upande wenye makosa kwa maagizo. Walishikamana na taratibu ya kidini ya Kiyahudi, iliyokuwa imemkataa Mwana wa Mungu na hivyo yenyewe nayo ikakataliwa na Mungu.—Matendo 2:36, 40; Mithali 14:12.
8. Yesu Kristo alionyeshaje kwamba, si dini zote zinazojidai kuwa za Kikristo hukubaliwa na Mungu?
8 Namna gani, basi, dini zenye kuchukua jina la Kristo na kujidai kumkubali kama Bwana wao? Je! kuhubiri kwao katika jina lake huhakikisha kwamba wanakubaliwa na Mungu? Kwa sababu ya maandiko tuliyokwisha kuzungumza, labda umekata shauri kwamba sivyo. Ikiwa ni hivyo, basi kwa shauri hili unakubaliana na Yesu Kristo, yeye ambaye Mungu amemweka kama hakimu wa kimbinguni; kwa sababu yeye hutuonya sisi, akisema: “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako . . . ?Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.” —Mathayo 7:21-23.
9. Jambo gani zaidi ya maarifa ya Biblia ni la lazima kwa dini ya mtu ili impendeze Mungu?
9 Maarifa ya Biblia na ya mapenzi ya Mungu ni ya lazima kwa kibali cha Mungu. Lakini, kama vile Yesu alivyosema, ni kufanya kwa mapenzi hayo ndilo jambo la maana. Lazima mtu awe na kazi zinazopatana na mambo ambayo yeye amejifunza. (Yakobo 2:26) Basi, kumpendeza Mungu, lazima dini ya mtu ipatane kabisa na Biblia na itumiwe katika kila utendaji wa maisha.—Luka 6:46-49.
10. Ni matunda gani ambayo dini ya kweli itafanyiza katika maisha za kila mtu za wale waifuatao?
10 Yesu alisema kwamba ungeweza kutambua kama mtu hufuata dini ya kweli kwa “matunda” yake, yaani, mambo ayafanyayo. (Mathayo 7:20) Hali kadhalika, twaweza kuitambua dini kwa aina ya watu ambao inafanyiza. Dini ya kweli lazima ifanyize watu walio bora—wanaume na akina baba walio bora, wake na akina mama watoto walio bora. Lazima ifanyize watu walio wanyofu, ambao huwa tofauti na wengine kwa sababu wao hutenda yaliyo haki. Je! sivyo ungeitazamia dini ambayo kwa kweli humkaribisha mtu kwa Mungu? Mungu hutazamia mambo haya pia, nayo huamua kwamba dini inakubaliwa na Mungu ama sivyo.
11. Ni mwendo gani uliochukuliwa na watu katika Beroya ya zamani tutafanya vema kuufuata?
11 Bila shaka wewe hutaki kuwekwa katika jamii ya wale wanaokataliwa kuingia katika ufalme wa Mungu kwa sababu ya kushindwa kuyafanya mapenzi ya Mungu. Basi, itakuwa faida yako, kuzoelea Biblia sawasawa. Kitabu unachosoma sasa kimekusudiwa kukusaidia wewe ufanye hivyo. Ufuate mwendo wa hao Waberoya wa zamani ambao Neno la Mungu huwakubali kwa sababu “walilipokea lile neno kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo.”—Matendo 17: 11..
12. (a) Inawezekanaje upendo wetu kwa Mungu kujaribiwa, labda na rafiki na jamaa? (b) Lazima sikuzote tutafute kibali cha nani?
12 Kwa kadiri unavyolichunguza Neno la Mungu, utajifunza kwamba upendo wako kwa Mungu utajaribiwa. Huenda wawepo watu fulani, labda hata rafiki zako wa karibu au jamaa, ambao hawatakubali kuchunguza kwako kwa Maandiko. (1 Petro 4:4; Mathayo 10:36, 37) Labda watajaribu kukuvunja moyo. Labda watafanya hivi kwa unyofu wa moyo wote, kwa sababu wao hawazijui kweli za ajabu zipatikanazo katika Biblia. Labda unaweza kuwasaidia. Labda mara nyingine upingaji utatokea kwa watu wasiokuwa na upendo kwa Mungu. Iwapo jambo hili linatokea, kumbuka, kuwa na kibali cha Mungu ni kwa muhimu zaidi sana kuliko kuwa na kibali cha wanadamu. Ni Mungu, si mwanadamu, atakayekupa wewe uzima wa milele ikiwa wampenda yeye zaidi kuliko kila mtu na kila kitu kinginecho.—Mathayo 22:37-39.
13. Ikiwa tunatafuta kufanya mapenzi ya Mungu, imetupasa tuombee nini?
13 Sikuzote tazama kwa Mungu kwa msaada wake na uongozi. Endelea kuomba, kama alivyofanya mtunga zaburi: “Ee [Yehova], uisikie sala yangu . . . Unifundishe kuyatenda mapenzi yako, kwa maana ndiwe Mungu wangu.” (Zaburi 143:1, 10) Ikiwa kwa unyofu wa moyo wataka kujua na kuifuata dini ambayo yeye huikubali, yeye atajibu sala yako. Naye atakuleta katika shirika pamoja na wale ambao kwa hakika humwabudu “Baba katika roho na kweli.”—Yohana 4:23, tazama pia Mathayo 7:7, 8.