Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • tr sura 14 kur. 122-130
  • Jinsi ya Kutambua Dini ya Kweli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kutambua Dini ya Kweli
  • Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUTUMIA KANUNI
  • Kuitambua Dini ya Kweli
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Ibada Ambayo Mungu Anakubali
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Je! Umeipata Dini ya Kweli?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Kwa nini ni Hekima Kuichungaza Dini Yako
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
Pata Habari Zaidi
Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
tr sura 14 kur. 122-130

Sura ya 14

Jinsi ya Kutambua Dini ya Kweli

1. Kwa nini inapatana na kufikiri kwa akili na Maandiko kusema kwamba kuna dini ya kweli moja tu?

KUPATANA na kufikiri kwa akili hapana budi pawepo dini ya kweli moja tu. Hii inapatana na jambo la kwamba Mungu wa kweli “si Mungu wa machafuko, bali wa amani.” (1 Wakorintho 14: 33) Tena, Yesu Kristo aliwasema wale ambao hufuata dini ya namna hiyo kama wakimwabudu Mungu “katika roho na kweli,” na kweli haikosi upatano kamwe katika yenyewe. (Yohana 4:23, 24) Lakini waabudu hawa wa kweli leo ni akina nani? Jinsi gani wewe waweza kuwatambua na kujua kwamba ibada yao kweli ndiyo inayokubaliwa na Mungu?

2. (a) Je! wote wajidaio kuwa Wakristo wanafuata dini ya kweli? (b) Ni kanuni gani ambayo Yesu alitoa ambayo kwa hiyo tunaweza kupambanua baina ya watumishi wa kweli wa Mungu na watumishi wa uongo?

2 Jambo hili haliwezi kuamuliwa tu juu ya msingi wa ambacho watu na matengenezo hujidai kuwa. Katika Mahubiri yake juu ya Mlima, Yesu alionyesha kwamba wengi wangemwita “Bwana, Bwana,” wakijidai kuwa wamefanya mambo ya ajabu katika jina lake. Lakini yeye angesema kwao hivi: “Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.” Si maneno tu bali pia sura zaweza kuwa zenye kudanganya. Yesu alisema kwamba manabii wa uongo wangekuja katika mavazi ya kondoo, hali ndani wangefanana na mbwa mwitu wenye kunyafua. Walakini, alitupa sisi kanuni ambayo kwa hiyo tunaweza kupambanua baina ya watumishi wa kweli wa Mungu na watumishi wa uongo, akisema: “Kwa matunda yao mtawatambua.” Yeye alionyesha kwamba jambo ambalo kweli huamua kama sisi tu waabudu wa kweli wa Mungu si madai yetu matupu au hata kazi zetu zinazoonekana kuwa zenye kusifiwa, bali ni kufanya kwetu hasa mapenzi ya Baba wa kimbinguni. —Mathayo 7:15-23.

3. Ni onyo gani lililopewa na mtume Paulo huonyesha haja kwa kujihadhari?

3 Mfuasi mwaminifu wa Yesu, mtume Paulo, pia, alionyesha haja kwa kujihadhari. Yeye alionya kwamba wanadamu wengine wangejisingizia kuwa wahudumu wa haki lakini wangekuwa ni Wakristo wa uongo. Kwa nje huenda wasionekane wabaya. Lakini wakati wanapopimwa kwa msaada wa Neno la Mungu, Biblia, wanaonyeshwa kuwa wahudumu wa adui wa Mungu, Shetani, kwa maana kazi zao kweli zinapingana na mapenzi ya Mungu. (2 Wakorintho 11:13-15) Kufuata kwetu uongozi wa Wakristo wa uongo wa namna hiyo kungeweza kutokea tu katika kupoteza kwetu kwa uzima wa milele.

KUTUMIA KANUNI

4. Ni alama gani yenye kutokeza zaidi ya waabudu wa kweli wa Mungu?

4 Basi, ni zipi baadhi ya alama zenye kutambulisha za waabudu wa kweli wa Mungu? Ni matunda gani bora ambayo wao wangezaa? Biblia hutuambia sisi kwamba “Mungu ni upendo.” Kupatana na hili, Yesu alionyesha kwamba alama yenye kutokeza zaidi ya wale ambao hufuata mfano wake katika kumwabudu Mungu ni ya kwamba wao wangekuwa na upendo wao kwa wao. Yeye alisema: “Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.” (1 Yohana 4: 8; Yohana 13:35) Kwa upendo wa namna hiyo kuwa kweli alama yenye kutambulisha, usingeweza kuwa jambo tu la kusingizia kuwa mwema kwa mmoja na mwenzake, sivyo? Lazima uwe upendo ambao huongoza sana kila sehemu ya maisha ya kila siku ya mtu. Lazima uongoze jinsi mmoja awatendeavyo washiriki wengine wa nyumbani mwa mtu. Wapasa uongoze nia ya mtu kuelekea watu wa makabila na mataifa mengine. Waabudu wa kweli wa Mungu huonyesha upendo, si katika neno tu, bali pia katika tendo. Wao hutafuta kitu ambacho kweli kinafaa kwa faida ya wengine.—1 Yohana 3:18.

5. Jinsi gani matengenezo ya kidini na washiriki wao leo hupatana kwa habari ya alama hii kubwa ya dini ya kweli?

5 Je! matengenezo ya kidini ambayo umezoelea nayo yana alama hii ya utambulisho? Je! yanatia katika washiriki wake upendo ambao ni wenye nguvu ya kutosha ambao hudumu kuwa kweli hata katika nyakati za shida? Kwa mfano, wanafanya nini wakati mkazo baina ya mataifa ya kilimwengu unapoongoza kwenye vita? Mambo ya hakika huonyesha kwamba wingi wao wamekuwa na nia kwa washiriki wao kwenda katika uwanja wa mapigano na kuua waamini wenzao wa taifa lingine kwa amri ya wanadamu wa kilimwengu. Je! wewe unaona mwendo kama huo unapatana na Neno la Mungu na kweli unaonyesha roho ya Mungu?—1 Yohana 3:10-12; Mathayo 5:44.

6. (a) Je! wako watu ambao wameonyesha upendo wa kweli wa Kikristo hata katika nyakati za mapigano ya kilimwengu? (b) Jinsi gani upendo wao ni zaidi kuliko kujiepusha tu kufanya madhara kwa wengine?

6 Lakini, kama ujuavyo, si kila mtu amefuata mwendo huu. Wengine wameweza kusema kama mtume Paulo: “Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili; maana silaha za vita vyetu si za mwili.” (2 Wakorintho 10:3, 4) Wao hawakuwa na hatia ya kuishi kwa uongo kwa kusema, “Nampenda Mungu,” huku wakiwachukia ndugu zao wa taifa lingine. (1 Yohana 4:20, 21) Wale ambao kweli humwiga Yesu, hawajiepushi kufanya madhara kwa wengine tu, bali pia hudhihirisha upendo katika njia nyingine. Jinsi gani? Kwa umoja wao na Wakristo wenzao katika nchi zote, kwa njia ambayo wao hushughulika na majirani zao na kwa jitihada zao za upendo kuwasaidia wengine kujifunza juu ya Mungu. —Wagalatia 6:10.

7. Ni maoni gani kuelekea Biblia dini ya kweli hutia moyo, na jinsi gani Mwana wa Mungu aliweka kiolezo katika hili?

7 Alama nyingine ya dini ya kweli na ya wale ambao huifuata ni heshima kwa Neno la Mungu. Wakati Mwana wa Mungu alipokuwa duniani aliweka kiolezo katika hili kwa kuonyesha heshima ya juu sana kwa Maandiko yaliyoongozwa na roho ya Mungu. Yeye alitumia maneno yake kama mamlaka ya mwisho juu ya mambo. Sikuzote yeye aliwaelekeza wasikilizaji wake kwa Neno la Mungu, akiwatia moyo kulisoma na kulitumia. (Mathayo 19:4-6; Luka 24:44, 45) Yeye alionyesha heshima yake kuu kwa Biblia kwa kuishi kupatana na mafundisho yake kila siku. Utimizo wa Neno la Mungu ulimaanisha zaidi kwake kuliko hata maisha yake mwenyewe. (Mathayo 26:53-56) Yeye hakupunguza kamwe thamani ya Biblia; bali, aliwalaumu wale walioshindwa kufundisha kupatana nayo na waliojaribu kupunguza nguvu zake kwa mafundisho yao wenyewe.—Marko 7:9-13.

8. Ni aina gani ya usemi wa mapadre wa Kristendomu huonyesha kwamba wao hawafuati mfano wa Mwana wa Mungu na mitume wake katika jambo hili?

8 Twaweza kusema nini katika neno hili juu ya matengenezo mengi ya kanisa ya Kristendomu leo? Wakati usikiapo au kusoma maneno yanayosemwa na mapadre ambao hutaja sehemu za Biblia kama “hadithi za uongo,” au ambao hupendelea kisio la mageuzi badala ya mafundisho ya Biblia ya kuumba, je! wewe ungesema kwamba wanatia moyo heshima kwa Neno la Mungu? Au wakati usomapo maneno ambayo katika hayo viongozi wa kanisa wa namna hiyo hukanusha kwamba ngono baina ya watu wasiooana si mbaya kwa lazima, au kwamba tendo la kulalana wanaume kwa wanaume na wanawake kwa wanawake laweza kufaa sana, je! wewe ungesema kwamba wao wanatia moyo watu kuitumia Biblia kama uongozi wao? Bila shaka wao hawafuati mfano wa Mwana wa Mungu na mitume wake.—Mathayo 15:18, 19; Wagalatia 5:19-21; Warumi 1:24-27.

9. Kwa nini ibada hata ya wengi walio na Biblia haipendezi kwa Mungu?

9 Je! matunda yanayodhihirika katika maisha za washiriki wa makanisa haya yanaonyesha kwamba kweli wao huliheshimu Neno la Mungu? Kutokana na mambo ambayo wewe mwenyewe umeyaona, je! ungesema kwamba watu zaidi ambao huenda kwenye jengo la kanisa siku ya Jumapili wanatumia kanuni za Biblia katika maisha yao ya nyumbani na katika kushughulika kwao na watu wengine siku ya Jumatatu na wakati wa siku zinazobaki za juma? Neno la Mungu linaonyesha kwamba wako watu ambao huenda wanayo Biblia na hata huisoma lakini matendo yao huthibitisha kwamba wanamkana Mungu ambao wao hujidai kumjua. (Tito 1:16; Yohana 5:39, 40) Aina ya ibada ambayo wao huzoea haipendezi kwa Mungu, kwa sababu wao hawaliachi Neno lake litumie nguvu za kweli katika maisha zao.—2 Timotheo 3:5.

10. (a) Tunaweza kujuaje ikiwa matunda mabaya hayathibitishi mtu mmoja mmoja tu, bali tengenezo la kidini lenyewe kuwa baya? (b) Ni uamuzi gani mzito ambao ni lazima mtu aufanye ikiwa ameona kwamba si mafundisho yote ya kanisa lake hupatana na Biblia?

10 Kwanza labda mtu atasema kwamba ni padre mmoja tu ndiye mwenye makosa au washiriki fulani tu wa kanisa wasiotenda mema. Lakini ikoje ikiwa padre anayepunguza thamani ya Biblia anaendelea kushika cheo chake? Na ikoje ikiwa washiriki wa kanisa ambao hutenda mabaya wanaendelea kuwa wenye kukubaliwa na kanisa? Basi ndio wakati wa kukabili jambo la hakika la kwamba matunda mabaya huthibitisha tengenezo la kidini lenyewe kuwa baya. Ikiwa jambo hilo ni kweli, utaona kwamba miongoni mwa dini zote za aina hii si mafundisho yote hupatana na Biblia. Ikiwa umesoma sura zilizotangulia za kitabu hiki na kuangalia maandiko ya Biblia yanayopatikana mle, labda unaona kwamba jambo hili ni kweli kwa habari ya dini ambayo umekuwa ukishirikiana nayo. Ikiwa ndivyo, basi unalo tatizo zito. Ni tatizo la kufanya uamuzi ama kukubali ukweli wa Biblia ama kuukataa kwa kupendelea mafundisho ambayo Biblia haiungi mkono. (Matendo 17:11) Bila shaka, jambo ambalo unafanya lazima liwe uamuzi wako mwenyewe. Walakini, imekupasa kufikiria mambo kwa uangalifu, kwa kuwa uamuzi ambao unafanya utahusu hali yako na Mungu na matumaini yako ya uzima wa milele katika taratibu yake mpya.

11. (a) Dini ya kweli hulionaje jina la Mungu, kama ilivyoonyeshwa na Yesu Kristo? (b) Basi lazima tufanye nini ikiwa tutapata wokovu?

11 Takwa lingine la dini ya kweli ni kwamba lazima itakase jina la Mungu. Kwa nini hivyo? Kwa sababu wakati Yesu Kristo alipowafundisha wafuasi wake jinsi ya kusali, aliwaonyesha kwamba hili lingepaswa kuwa ndilo jambo la kwanza kufikiriwa. “Basi, lazima msali kwa njia hii,” alisema: “Baba yetu uliyemo katika mbingu, acha jina lako litakaswe.” (Mathayo 6:9, NW) Hii inamaanisha kuliweka jina wakf, kuliona kama jambo fulani takatifu. Bila shaka Yesu mwenyewe alifanya jambo hili. Yeye hakushindwa kutumia jina la Baba yake, wala yeye hakuliona kama lisilo la maana. Bali, katika sala kwa Baba yake, Yesu alisema: “Naliwajulisha jina lako, tena nitawajulisha hilo.” (Yohana 17:26) Yeye alijua kwamba ni kusudi la Mungu kwa jina lake kutukuzwa duniani mwote, naye aliweka mfano katika kulitangaza na kuliheshimu jina hilo. (Yohana 12:28; Isaya 12:4, 5) Pia, Maandiko yanaonyesha kwamba kusudi kubwa kwa kuwako kwa kundi ambalo Mungu ameliita kutoka katika ulimwengu ni kuwa “watu katika hao kwa ajili ya jina lake.” (Matendo 15:14) Ikiwa wewe utapata wokovu, wewe, pia, lazima ulijue na kuliheshimu jina la Mungu.—Warumi 10:13, 14.

12. (a) Je! makanisa yote kwa jumla yanapatana na takwa hili la ibada ya kweli? (b) Je! wako wo wote wanaoshuhudia jina la Mungu?

12 Sasa, tua na kujiuliza mwenyewe: Ni kikundi gani cha kidini ambacho kwa kutokeza zaidi kinajulikana kwa kulitangaza jina la Mungu, kama Yesu alivyofanya? Makanisa kwa jumla yanaepuka kutumia jina la Yehova; na ijapokuwa wengine kati yao husema kwamba wanapendelea aina ya “Yahweh,” hata aina hiyo hawaitumii mara nyingi. Wengine wamefika hata kwenye kiasi cha kuliondoa jina la Mungu katika tafsiri zao za Biblia. Kwa mfano, tafsiri ya Biblia ya Revised Standard Version, ambayo sasa inaenezwa kwa kuungwa mkono na wote Waprotestanti na Wakatoliki, huacha jina la Yehova kabisa, ijapokuwa linaonekana katika maandishi ya awali ya Kiebrania karibu mara elfu saba. Je! matengenezo haya yanapatana na takwa hili la dini ya kweli? Kweli, ni kikundi kipi kinachoshuhudia jina la Mungu, kama vile Yesu alivyofanya? (Ufunuo 1:5; Isaya 43:10-12) Ikiwa ilikubidi kusema kwa majirani zako na kutaja mara kwa mara Yehova, ukitumia jina lake takatifu, unadhani wao wangekushirikisha na tengenezo gani? Hilo si swali gumu kujibu. Kuna kikundi cha watu kimoja peke yake ambacho kwa kujulikana sana hufuata mfano wa Yesu katika habari hii.

13. (a) Ni jambo gani ambalo imewapasa waabudu wa kweli watangaze waziwazi kama tumaini la pekee la wanadamu? (b) Wanafanyaje hili?

13 Waabudu wa kweli pia hutangaza ufalme wa Mungu kama tumaini la wanadamu. Wasingeweza kufanya vingine na kuwa wenye kupendeza kwa Yehova Mungu, kwa sababu yeye amesema waziwazi kwamba Ufalme ndio mpango wake kwa kutawala dunia. (Danieli 2:44; 7:13, 14) Yesu aliweka mfano kwa kwenda kutoka mwisho mmoja wa nchi mpaka kwa mwisho mwingine “akihubiri na kuitangaza habari njema ya ufalme wa Mungu.” (Luka 8:1) Yeye na mitume wake walifanya jambo hili kwa kwenda kutoka kijiji kwa kijiji na “nyumba kwa nyumba.” (Matendo 20:20) Yesu alitabiri pia kwamba katika hizi “siku za mwisho” “habari njema ya ufalme” ingehubiriwa katika dunia yote kwa ushuhuda.—Mathayo 24:14.

14. (a) Badala ya ufalme wa Mungu, ni katika kupendelea nini mara nyingi tunawasikia viongozi wa dini wakisema na kuomba? (b) Ni watu gani ambao huja mlangoni pako wakihubiri Ufalme kama tumaini la kweli la wanadamu?

14 Mara nyingi leo tunawasikia viongozi wa dini wakisema kwa ajili ya matengenezo ya siasa kama vile Umoja wa Mataifa na kuyaombea. Lakini ni akina nani wanaofanya kazi ya kuhubiri habari njema juu ya ufalme wa Mungu kama Yesu alivyotabiri? Ikiwa mtu fulani anakuja mlangoni pako au mlangoni pa jirani yako na unamsikia akisema juu ya ufalme wa Mungu kama ndilo tumaini la kweli la wanadamu, unamshirikisha mtu huo na tengenezo gani? Huu ndio utendaji mkubwa wa wale ambao kwa kweli hufanya mapenzi ya Baba wa mbinguni kwa kumwiga Mwanawe Yesu.—1 Petro 2:21.

15. Litaje takwa lingine la maana la dini ya kweli, kama inavyoelezwa katika Yakobo 1:27.

15 Lakini takwa lingine la dini ya kweli ni la kwamba inajitenga na ulimwengu na mambo yake. Biblia, katika Yakobo 1:27, NW huonyesha kwamba, ikiwa ibada yetu itakuwa safi na isiyonajisiwa kutokana na maoni ya Mungu, lazima tujitenge sisi wenyewe “na ulimwengu pasipo mawaa.” Jambo hili ni la muhimu, kwa maana, “mtu awaye yote . . . anayetaka kuwa rafiki wa ulimwengu anajifanya mwenyewe kuwa adui wa Mungu.” (Yakobo 4:4, NW) Wewe unaweza kuthamini kwa nini jambo hili ni zito sana wakati ukumbukapo kwamba Biblia huonyesha kwamba mtawala wa ulimwengu ni adui mkuu wa Mungu, Shetani Ibilisi.—Yohana 12:31.

16. Kutokana na mambo ambayo umeyaona, je! makanisa yaliyomo katika jamii yako, na washiriki wao, kweli “si sehemu

16 Je! mambo ya hakika huonyesha kwamba makanisa yaliyomo katika jamii yako huthamini sana jambo hili? Je! mapadre, na pia washiriki wa makundi, kweli “si sehemu ya ulimwengu,” kama vile Yesu alivyosema kwamba wafuasi wake wa kweli wangekuwa? (Yohana 15:19, NW) Au je! wao wanajiingiza sana katika mambo ya kilimwengu, katika utukuzo wake wa mataifa, siasa zake na mashindano baina ya watu wa vyeo mbalimbali? Wewe huna haja ya mtu fulani mwingine kukujibia maswali haya. Matendo ya makanisa hutangazwa wazi po pote, nawe unajua ni jambo gani linalotukia ndani yao. Ikiwa wamo watu katika jamii yako ambao, kwa sababu ya dini yao, hujiepusha na matendo ya namna hiyo, bila shaka wewe unawajua pia ni akina nani.

17. (a) Ili kuwa dini ya kweli, lazima dini ya kweli ipatane na matakwa mangapi kati ya haya? (b) Kama inavyoonyeshwa na Biblia, kuna dini ngapi za kweli?

17 Sasa, baada ya kuchunguza alama hizi za kutambulisha za dini ya kweli ambayo Mungu ametupatia sisi katika Neno lake, neno letu la mwisho nini? Jambo la maana la kuamua si kwamba kikundi Fulani cha kidini kinaonekana kutimiza moja au mawili ya matakwa haya, wala kwamba baadhi ya mafundisho yake ya dini hupatana na Biblia au sivyo. Zaidi sana kuliko hivyo, dini ya kweli lazima ipatane katika mambo yote haya na mafundisho yake lazima yote yapatane kabisa na Neno la Mungu. Katika njia hii peke yake dini ya namna hiyo yaweza kweli kupendeza kwa Yehova Mungu. Hakuna dini nyingi zinazotimiza matakwa haya. Biblia huonyesha kwamba kuna “imani moja” tu.—Waefeso 4:5.

18. (a)  Kwa msaada wa ushuhuda, kitabu hiki kinaelekeza kwa akina, nani kama ndio waabudu wa kweli leo? Je! hivyo ndivyo uaminivyo? (b) Ni njia gani bora ya kufahamiana vizuri na mashahidi wa Yehova?

18 Basi, ni akina nani, ambao wamo katika kundi la waabudu wa kweli leo? Juu ya msingi wa ushuhuda unaojulikana au unaopatikana kwa watu katika sehemu zote za dunia, hatuna haja ya kusita kusema kwamba wao ni mashahidi wa Kikristo wa Yehova. Kwako kushiriki katika kusadikishwa huko lazima ufahamiane vizuri nao. Njia bora ni kuhudhuria mikutano yao penye Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova. Katika njia hii unaweza kutazama mwenyewe jinsi tengenezo lifanyavyo kazi na njia ambayo katika hiyo wale wanaoshirikiana nalo hulitumia Neno la Mungu katika maisha zao wenyewe. Kwa kuwa Mungu hutuhakikishia kwamba kuzoea dini ya kweli huleta uradhi mkubwa sasa na hufungua njia kwa uzima wa milele katika taratibu yake mpya ya mambo, bila shaka itakufaidi kufanya upelelezi wa namna hiyo. (Kumbukumbu la Torati 30:19, 20) Tunakukaribisha kwa furaha ufanye hivyo. Mbona usipeleleze sasa?

ya ulimwengu”?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki