Sura ya 7
Je! Viko Viumbe Vibaya vya Kiroho?
1. (a) Je! Yesu alisadiki kwamba viko viumbe vibaya vya kiroho? (b) Yesu alimwita Ibilisi nini?
YESU KRISTO, aliyekuja duniani kutoka katika makao ya kiroho, alikubali kuwako kwa viumbe vibaya vya kiroho. Labda unakumbuka kwamba yeye alisema mara kwa mara juu ya Ibilisi, na ya kwamba alimwita “baba wa [uongo]” na “mwuaji.” (Yohana 8:44) Kwa ulinzi wetu wenyewe katika wakati huu wakati kusema uongo na uuaji vinaongezeka, tutafanya vema kuchunguza habari hii.
2. (a) Kinyume cha ambayo Yesu alifundisha, watu wengine husadiki Ibilisi ni nini? (b) Ni mambo gani yaliyompata Yesu akiwa na Ibilisi?
2 Kwa kweli, watu wengi hawasadiki kwamba viko viumbe vibaya vya kiroho. Hata wengine wanaojidai kutumia Biblia husema kwamba Shetani Ibilisi ni sifa ya uovu tu, si mtu wa kiroho asiyeonekana. Lakini je! mambo ya uhakika hukubaliana na imani yao? Namna gani juu ya mambo yaliyompata Yesu Kristo mwenyewe wakati Ibilisi alipomshawishi? Biblia hutuambia kwamba Ibilisi alimwonyesha Yesu falme zote za ulimwengu na akasema kwake: “Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia. Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie [Yehoval Mungu wako, umwabudu yeye peke yake.” Ndipo Ibilisi alipomwacha Yesu. —Mathayo 4:1-11.
3. (a) Jinsi gani mambo hayo yaliyompata Yesu huonyesha kwamba Ibilisi asingeweza kuwa sifa ya uovu tu? (b) Basi, Shetani Ibilisi, ni nini?
3 Wakati wa mambo hayo yaliyompata, Yesu ali-shawishiwa na nani? Na mtu halisi? au na sifa ya uovu tu? Ikiwa alishawishiwa na sifa ya uovu tu, ni katika nani sifa hii ilikaa? Je! uovu huu ulikuwa ndani ya Yesu Kristo? Ikiwa ndivyo, basi haingeweza kuwa kweli kwamba ndani yake mlikuwa hamna dhambi. Lakini Biblia, Neno la kweli la Mungu, hueleza waziwazi kwamba Yesu alikuwa “asiyekuwa na uovu, asiyekuwa na waa lo lote, aliyetengwa na wakosaji.” (Waebrania 7:26) Biblia pia husema: “Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake.” (1 Petro 2:22) Hivyo Yesu asingeweza kuwa akizungumza na “uovu” ndani yake mwenyewe. Yeye alikuwa akisema kwa kiumbe cha kiroho chenye uhai. Hivyo Maandiko na akili nzuri huonyesha wazi kwamba Shetani ni mtu halisi na aliye hai katika makao ya kiroho yasiyoonekana.—1 Petro 5:8.
IBILISI ALIYEJIFANYA MWENYEWE
4. Kutokana na ambayo tunajua juu ya Mungu, kwa nini twaweza kuwa hakika kwamba yeye asingemwumba mtu fulani mwovu?
4 Lakini ni katika njia gani Ibilisi alitokana? Kwa wazi, Mungu ‘ambaye kazi yake ni kamilifu’ asingemwumba mtu fulani mwovu. (Kumbukumbu la Torati 32:4) Yeye asingeumba viumbe vyenye akili ambavyo asingeweza kushirikiana navyo. Jambo la namna hiyo lingekuwa kinyume cha akili na upendo wa Mungu. —Zaburi 5:4-6.
5. (a) Jinsi gani kiumbe cha kiroho ambacho kikawa Ibilisi kilifuata mwendo mbaya? (b) Je! alikuwa nyoka wa vivi hivi aliyeweka wazo la uasi katika akili za Hawa?
5 Hivyo, kiumbe cha kiroho kisichoonekana ambacho baadaye kikawa Ibilisi hakina budi wakati mmoja kilikuwa kikamilifu, bila hitilafu kama kuumba kwa Mungu, kama vile mamilioni mengine yote ya ‘wana wa Mungu’ wa kimalaika. (Ayubu 38:7) Jinsi gani, basi, yeye akawa mbaya? Baada ya kuumbwa kwa mwanamume na mwanamke wa kwanza, kiumbe hiki cha kiroho kilifuata mwendo wa uasi juu ya Mungu. Yeye alisitawisha tamaa ya kuabudiwa na hivyo akawashawishi Adamu na Hawa kumwasi Mungu. Jinsi gani alifanya hivi? Biblia huonyesha kwamba nyoka alisema kwa Hawa, akimwambia uongo. Kama matokeo yeye akakosa kumtii Mungu. Ndipo alipomshirikisha mumewe katika kumpindukia Mungu. Lakini ni nani kwa kweli aliyetia wazo la uasi katika akili za Hawa? Je! alikuwa nyoka wa vivi hivi asiye na viungo vya usemi? La, alikuwako fulani aliyekuwa akisema akimfanya nyoka aonekane kana kwamba ndiye aliyekuwa akisema. Twajua kwamba mabingwa wengine wa kibinadamu wanaweza kusema maneno hali midomo karibu imefungwa, kufanya ionekane kana kwamba mnyama aliye karibu au sanamu ndiyo inayosema. Jinsi ilivyo rahisi zaidi kwa mtu asiyeonekana mwenye uwezo kupita wa kibinadamu kufanya hivi! Mungu alimfanya punda wa Balaamu kusema. (Hesabu 22: 28) Katika Edeni, Shetani alimtumia nyoka. Na hivyo Biblia hutambulisha Ibilisi, au Shetani, kama “nyoka wa zamani,” hivyo ndiye ambaye kwa kweli aliingiza uasi na uovu katika ulimwengu wote.—Ufunuo 12:9; 2 Wakorintho 11:3.
6. Jinsi gani kiumbe kikamilifu kingeweza kugeukia kwenye uovu?
6 Labda utataka kujua, ikiwa kiumbe hiki cha kiroho chenye akili sana kweli kilikuwa kikamilifu, jinsi gani kingeweza kugeukia kwenye uovu wakati kulipokuwa hakuna mtu wa kumshawishi? Biblia hujibu kwamba ilikuwa kwa njia ya kufikiri kwake juu ya wazo baya. (Yakobo 1:14, 15) Hakuna ubaya katika wenyewe kwa kuona uwezekano katika hali fulani. Kwa mfano, labda mtu akiwa katika nyumba ya mtu mwingine akaona fedha ipo mezani. Uwezekano wa kutwaa kwake ile fedha na kuitia mfukoni mwake upo pale. Lakini, kwa kuwa huo ungekuwa wivi, isingempasa hata kuifikiria. Au, wazo likimwingia katika akili zake, itampasa kuiacha. Lakini akiweka wazo katika akili zake na kulifanya kukua, ndipo tamaa mbaya inapotokea. Upesi huenda hii imwongoze kwenye kutenda tendo la uovu.
7. (a) Basi jinsi gani kiumbe hiki cha kiroho kikawa kiovu? (b) Ni nani, basi, aliyemfanya Shetani Ibilisi?
7 Vivyo, pia, na kiumbe kikamilifu cha kiroho. Uwezekano ulikuwako kule wa kutumia wanadamu wawili kwa kusudi lake mwenyewe kuliko kutimiza ambayo Mungu alitaka. Yeye akiwa kiumbe chenye uhuru wa hiari, yeye hakulifikiria tu bali alishindwa pia kuliondoa kutoka katika akili zake, na likamwongoza kwenye dhambi. Kama vile mtu ambaye zamani alikuwa mnyofu awezavyo kujifanya mwenyewe kuwa mwivi kwa kuiba, ndivyo na kiumbe hiki cha kiroho kilivyojifanya chenyewe kuwa Shetani kwa kutenda kama mpinzani wa Mungu; na akajifanya mwenyewe Ibilisi kwa kuwa mchongezi wa Mungu, kwa sababu ndiyo maana ya majina hayo.
8. Kwa nini haikuwa ni kukosea tu ambako Shetani alifanya?
8 Bila shaka, labda mmoja atasema, “Je! labda haikuwa ni kukosea tu alikofanya? Je! asingeweza kuomba radhi na hivyo akamaliza shauri pale pale?” Kwa kujibu, ni lazima tukumbuke kwamba mtu mkamilifu yu tofauti na sisi. Wakati atumiapo uhuru wa hiari yake, uchaguzi aufanyao si kwa sababu ya udhaifu au kutokukamilika. Watu wasiokamilika mara nyingi hukosea kwa sababu ya udhaifu uliorithiwa. Wanaweza kukiri makosa yao, kuomba radhi na kubadili mwendo wao. Lakini wakati kiumbe kikamilifu kinapochagua kufanya kosa, yeye hulifanya kwa makusudi naye hageuki baadaye kufanya mema. Hivi ndivyo ilivyokuwa habari ya yeye ambaye alijifanya mwenyewe kuwa Ibilisi.
VIUMBE VYA KIROHO VINGINE VYAJIFANYA VYENYEWE KUWA MASHETANI
9. Jinsi gani wengine wa malaika watakatifu wa Mungu walijifanya wenyewe kuwa mashetani?
9 Ibilisi hakuwa ndiye kiumbe cha kiroho peke yake kugeukia kwenye kutokutii na uovu. Mungu alikuwa ameumba idadi kubwa ya malaika watakatifu, mamilioni yao. Danieli 7:10 hufunua sehemu yao kama ikiwa 100,000,000. Habari ya Biblia katika Mwanzo 6:1-5 hueleza kwamba kabla ya gharika ya siku za Nuhu baadhi ya hawa ‘wana wa Mungu’ wa kiroho walichukua umbo la mwili kama wanadamu, yaani, walipaacha mahali pao mbinguni kama viumbe vya kiroho na wakajivika wenyewe miili yenye nyama. Na kwa nini? Ili kujifurahisha tamaa za kibinadamu kwa kuoa binti za wanadamu wenye sura nzuri. Hili lilikuwa tendo la kutokumtii Mungu, na Biblia hulishirikisha pamoja na matendo ya watu wa Sodoma na Gomora ambao ‘walifuata mambo ya mwili yasiyo ya asili.’ (Yuda 6, 7) Vivyo, pia, ilikuwa kinyume cha asili yao ya kimbinguni kwa malaika kushuka na kutafuta miili ya kibinadamu ya kufanya ngono nayo. Mwendo wao ulileta matokeo mabaya, kutia na watoto wasio wa kawaida, “watu hodari” walioitwa Wanefili. Kwa tendo lao la uasi, wana hao wa kiroho wa Mungu walijigeuza wenyewe kuwa mashetani na kujiweka wenyewe upande wa Ibilisi, ambaye ni “mtawala wa mashetani.”—Ma.thayo 9:34, NW.
10. (a) Wakati gharika, ya siku za Nuhu ilipokuja, jambo gani Iilitukia kwa malaika wasiotii waliokuwa wameoa binti za wanadamu? (b) Ni kwenye nini ongezeko katika kufanya makosa katika siku zetu latosha kutuamsha?
10 Wakati gharika ya siku za Nuhu ilipoharibu wanadamu wote waovu, malaika wasio waaminifu waliiondoa miili yao ya nyama na kurudia makao ya kiroho. Lakini hawakuruhusiwa kuwa sehemu ya tengenezo la Mungu la malaika watakatifu tena. Badala yake, walifungiwa katika hali iliyoshushwa ya giza la kiroho. (2 Petro 2:4) Tangu wakati wa Nuhu, Mungu hakuwaruhusu malaika hawa wa kishetani kuchukua umbo katika mwili kama walivyofanya wakati huo kabla yake. Lakini wanaweza bado kutumia uwezo wenye hatari juu ya wanaume na wanawake. Hasa, kwa msaada wa mashetani hawa Shetani anadanganya “ulimwengu wote.” (Ufunuo 12:9) Ongezeko kubwa katika kufanya makosa tulionalo duniani pote leo latosha kutuamsha kwa haja ya kujilinda juu ya kudanganywa nao.
IBILISI NDIYE “MTAWALA WA ULIMWENGU HUU”
11. Ni cheo gani alicho nacho Shetani kuhusu mataifa yote?
11 Mara tatu katika kitabu cha Biblia cha Yohana tunasoma kwamba Bwana Yesu Kristo alimwita Ibilisi “mtawala wa ulimwengu huu.” (Yohana 12:31; 14: 30; 16:11, NW) Katika 2 Wakorintho 4:4, NW yeye hutajwa kama “mungu wa taratibu hii ya mambo.” Basi, hii inamaanisha kwamba mataifa yote ya dunia wako chini ya utawala wa Shetani Ibilisi? Biblia hujibu: “Ulimwengu mzima uko katika uwezo wa yule mwovu.” (1 Yohana 5:19, NW) Hivyo Ibilisi, kama “mtawala wa ulimwengu,” hutumia nguvu kuu juu ya wanadamu, akiwadanganya na hata kutawala serikali za kisiasa.—Ufunuo 16:13, 14.
12. (a) Kupatana na Ufunuo 13:1, 2, ni kwa kitu gani Ibilisi hutoa nguvu na uwezo? (b) Jinsi gani toleo la Ibilisi kwa Yesu hutusaidia sisi kumtambua “mnyama” ni mfano wa nini? (c) Kwa kuwa masimulizi juu ya “mnyama” wa Ufunuo 13:1, 2 na yale juu ya wanyama wa njozi wa Danieli hutaja aina zile zile za wanyama, lazima “mnyama” afananishe nini?
12 Ukiifungua Biblia yako kwenye Ufunuo 12:9, utaona kwamba Ibilisi husimuliwa kama “joka” mkubwa. Katika sura ifuatayo, mistari ya 1 na 2, tunaambiwa kwamba joka huyu, Ibilisi, alitoa nguvu na kiti cha enzi na uwezo mwingi kwa kile kiitwacho kwa mfano “mnyama” kutoka katika bahari. Ni nini huyu “mnyama” wa mfano? Naam, Shetani ana mamlaka yake juu ya nini? Ni nini alitoa kwa Yesu Kristo? “Milki zote za ulimwengu.” (Luka 4:5-8) Upesi Yesu alilikataa toleo hilo, lakini yeye hakukana kwamba Ibilisi hakutawala juu ya milki za kisiasa za dunia. Kupatana na hili, Ufunuo 13:7 husema kuhusu “mnyama” wa mfano, kwamba “akapewa uwezo juu ya kila kabila na jamaa na taifa.” Tena, nabii Danieli alionyesha wanyama fulani walikuwa mifano ya nini? Ya “falme,” au serikali za kisiasa. (Danieli 7:2-7, 17, 23, NW) Kwamba wanyama wa mfano wa njozi ya Danieli na “mnyama” wa Ufunuo wana maana ile ile inaonekana kutokana na jambo la kwamba habari mbili aina ile ile ya viumbe: simba, dubu, chui na mnyama mwenye pembe kumi. (Ufunuo 13:1, 2) Hivyo “mnyama” hufananisha tengenezo zima la kisiasa la Ibilisi ambalo limetumia utawala ulio mfano wa mnyama juu ya dunia katika karne zote mpaka sasa. Si ajabu Yesu alisema: “Ufalme wangu sio wa ulimwengu huu.” Na si ajabu kwamba wafuasi wake wasingekuwa sehemu ya ulimwengu, yaani, wangeepuka kupitia katika shughuli zake.—Yohana 18:36; 17:14-16.
JITENGE NA KILA AINA YA UCHAWI
13. Uchawi ni nini, na kwa nini Biblia hutuonya sisi kujitenga nao?
13 Mojawapo za njia ambazo viumbe vibaya vya kiroho hupoteza wanaume na wanawake ni kupitia kwa uchawi. Uchawi ni nini? Ni kusema na viumbe vibaya vya kiroho, kupotezwa navyo moja kwa moja ama kupitia kwa binadamu au kwa chombo kingine. Biblia hutuonya sisi kujitenga na kila desturi inayohusiana na uchawi, kwa sababu uchawi humleta mtu chini ya uongozi wa mashetani.—Wagalatia 5: 19-21; Ufunuo 21:8.
14. Ni desturi gani fulani zinazohusiana na uchawi, na Mungu huwaonaje wale wageukiao kwenye desturi za namna hiyo?
14 Mungu hulaumu kila aina ya uchawi. Biblia hutuambia baadhi ya mambo haya yaliyokatazwa ni nini: uaguzi, uganga, kutazamia bao, ulozi, kuwaloga wengine (uwezo wa kumtia mtu hali kama ya usingizi na kumfanya atende mambo yanayoamriwa katika usingizi huo, uchawi, na kadhalika), kutafuta habari kutoka kwa mchawi au mpiga ramli na kuuliza habari za wafu. (Kumbukumbu la Torati 18:10-12; Isaya 8: 19) Yote haya ni imani katika uwezo wa mashetani, na wale wenye kugeukia kwenye desturi za namna hiyo hujifanya wenyewe adui za Mungu.—Mambo ya Walawi 19:31; 1 Mambo ya Nyakati 10:13, 14.
15. (a) Uaguzi ni nini, na ni nini baadhi ya njia ambazo watu hushiriki ndani yake leo? (b) Unajimu na uganga ulianzia wapi?
15 Uaguzi ndiyo mojawapo za aina za kawaida za uchawi. Ni jitihada ya kupata maarifa ya kisichojulikana au ya wakati ujao kwa njia ya kutazamia bao au kwa njia ya uwezo wa mashetani. (Matendo 16: 16) Ni nyingi njia ambazo kwa hizo uaguzi huzoewa leo, kama vile kwa njia ya fito za uaguzi, mizani, kukazia macho penye tufe ili kupata maarifa ya wakati ujao, mbao za kuagulia, ESP, yaani, uwezo wa kujifunza jambo fulani au kutokeza shani bila msaada wa milango ya akili, kuchunguza mistari ya mkono wa mtu, kujifunza mruko wa ndege fulani, kutazamia bao katika ndoto za mtu na katika matukio mengine katika maisha ya mtu na kisha kujaribu kuunganisha haya na wakati ujao. Kuna uaguzi pia kwa njia ya nyota, unaoitwa kwa kawaida unajimu. Huu ulianzia katika Babeli wa zamani, kama aina mbalimbali za mambo ya uganga zilivyoanza. Biblia huonyesha kwamba wote watumiao uaguzi hufanya dhambi kwa Mungu.—1 Samweli 15:22, 23.
16. Imetupasa tufanye nini ikiwa wakati wo wote tunasikia “sauti” kutoka katika makao yasiyoonekana ikisema kwetu?
16 Mojawapo za njia za kawaida ambayo katika hizo viumbe vibaya vya kiroho hupoteza watu ni kwa njia ya kusema nao, ama kupitia kwa mchawi ama kwa njia ya “sauti” kutoka katika makao yasiyoonekana. “Sauti” hujisingizia kuwa jamaa aliyekufa au kiumbe kizuri cha kiroho; lakini huu ni uongo! Kwa hakika sauti ni kiumbe kibaya cha kiroho ndicho kinachosema! Ni nini imekupasa kufanya ikiwa “sauti” ya namna hiyo inasema kwako? Naam, ni nini Yesu Kristo alifanya wakati mtawala wa viumbe vibaya vya kiroho aliposema kwake? Yesu alikataa mashauri ya Ibilisi, akisema: “Nenda zako, Shetani.” (Mathayo 4:10) Wewe pia unaweza kufanya hivyo. Pia, unaweza kuomba Yehova kwa msaada ukisali kwa sauti kuu na kutumia jina lake. Fuata mwendo huu wenye hekima, na usitege sikio kwa sauti za namna hiyo kutoka katika makao yasiyoonekana.—Mithali 18:10; Yako-bo 4:7.
17. Jinsi gani mtu aweza kuachana na uchawi leo kwa kufuata mfano wa Wakristo wa kwanza katika Efeso?
17 Lakini namna gani ikiwa mmoja amekuwa aki-shughulika katika baadhi ya dini za uchawi na sasa anataka kuachana na uchawi? Naam, wengi wa Wakristo wa kwanza katika Efeso walifanya nini wakati walipotaka kujitenga na mambo ya uganga? Biblia hutuambia sisi kwamba, baada ya kulikubali “neno la [Yehova]” lililohubiriwa na mtume Paulo, “wakakusanya vitabu vyao, wakavichoma moto mbele ya watu wote,” hata ijapokuwa vilikuwa vyenye thamani ya vipande vya fedha 50,000! (Matendo 19:19, 20) Mfano wao kuharibu vitu vilivyohusiana na desturi za uchawi ni wenye hekima kuufuata.
18. (a) Jambo gani litavipata viumbe vyote vibaya vya kiroho? (b) Kwa sababu ya hili, lazima tufanye nini ikiwa tunataka uzima wa milele?
18 Usidanganywe kwa sababu watu zaidi wanapendezwa na mambo ya siri. Viumbe vibaya vya kiroho vinaendeleza uchawi wa namna hiyo. Lakini majeshi haya ya viumbe vibaya vya kiroho, kutia na Ibilisi, hatimaye yataharibiwa. (Mathayo 25:41) Ikiwa wewe unataka uzima wa milele lazima uwe huru na uongozi wao kwa kuepuka kila aina ya uchawi.
IBILISI HUENDELEZA DINI YA UONGO
19. (a) Ni njia ipi iliyo kuu kupita zote ambayo kwa hiyo Ibilisi huwageuza wanadamu kutoka kwa Mungu? (b) Ni nini dini ya uongo? (c) Ikiwa mtu hujizoeza dini ya uongo, ni kwa nani kwa hakika mtu anatoa utumishi?
19 Isitushangaze kwamba Ibilisi na mashetani wake wanazo njia nyingi za kuwadanganya wanadamu, uchawi ni mojawapo za njia hizi. Basi, ni njia gani iliyo kubwa kupita yote ambayo kwa hiyo Ibilisi, “baba wa [uongo],” huwageuza wanadamu kutoka kwa, Mungu? (Yohana 8:44) Ni kwa njia ya dini ya uongo! Dini ya uongo ni ibada ambayo imejengwa juu ya mambo ya uongo na ambayo hupingana na Neno la kweli la Mungu, Biblia. Ndiyo sababu moja kwa nini Biblia husema wazi kwamba ikiwa mtu huabudu katika njia isiyopatana na Neno la Mungu, yeye kwa hakika huwatumikia mashetani, kwa sababu yeye anatenda kupatana na mambo ambayo wanataka na kwa kupingana na Mungu.—Kumbukumbu la Torati 32:16, 17; 1 Wakorintho 10:20.
20. Kama viongozi wa uvunjaji wa sheria, jinsi gani Ibilisi huwadanganya watu?
20 Ijapokuwa huenda dini za uongo zikaonekana kuwa nzuri, imetupasa kutambua kwamba Ibilisi anafanana na viongozi wengi wa kisasa wa kisirisiri wa uvunjaji wa sheria ambao hujisingizia kuwa watu wazuri. Kungeweza kuwa njia gani kwake ya werevu zaidi kudanganya watu na kuwatumikisha kwake kuliko kwa njia ya kutumia dini ambayo kwa nje huonekana ya haki? Kwamba Ibilisi angewapoteza watu kwa njia ya dini ambayo kwa nje hujidai kumtumikia Mungu inaonyeshwa katika Biblia. (Mathayo 7:22, 23) Hasa, mtume wa Kikristo Paulo alisema kwamba “Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru” na “watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki.”—2 Wakorintho 11:14, 15.
21. (a) Ni nini Biblia huonyesha kwa habari ya wakati ubakio kwa viumbe vibaya vya kiroho? (b) Kwa nini lazima mtu aachane na uchawi na dini zote nyingine za uongo?
21 Hivyo Yesu Kristo alikuwa hawazii tu jambo fulani wakati alipomwita Ibilisi “mtawala wa ulimwengu huu.” (Yohana 12:31, NW) Kweli kweli viko viumbe vibaya vya kiroho vikiudanganya “ulimwengu, wote.” Lakini ni “wakati mchache tu” ubakio kabla Ibilisi na malaika zake wabaya hawajazuiwa kufanya kazi. (Ufunuo 12:9, 12) Kwa sasa, jitenge na kila aina ya uchawi na kuachana na dini ambayo huenda inaonekana nzuri bali kwa hakika ina msingi juu ya uongo. Huwezi kushikamana na uchawi au uongo ingine wa kidini na kupata uzima wa milele katika taratibu mpya ya mambo ya Mungu, kwa sababu kweli peke yake ndiyo iongozayo kwenye uzima wa milele.—Waefeso 6:12, 16.