Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • tr sura 9 kur. 75-81
  • Sababu Kwanini “Kundi Dogo” Huenda Mbinguni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sababu Kwanini “Kundi Dogo” Huenda Mbinguni
  • Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • WANGAPI WATAKWENDA MBINGUNI
  • JINSI MTU HUJUA KAMA YEYE YU MMOJA WA “KUNDI DOGO”
  • KURUDI KWA KRISTO
  • Ni Nani Wanaoenda Mbinguni, na kwa Sababu Gani?
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • “Msiogope, Enyi Kundi Dogo”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Ni Nani Ambao Kwa Kweli Wana Mwito wa Mbinguni?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Mbingu
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
Pata Habari Zaidi
Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
tr sura 9 kur. 75-81

Sura ya 9

Sababu Kwanini “Kundi Dogo” Huenda Mbinguni

1. (a) Wakati Yesu alipokuwa duniani, aliwaambia nini wafuasi wake juu ya uzima wa mbinguni? (b) Kwanini watu wengi hutaka kwenda mbinguni?

WAKATI Yesu Kristo alipokuwa angali yuko pamoja na wafuasi wake hapa duniani, alisema kwao juu ya uzima mbinguni. Aliwaambia kwamba alikuwa akienda kuwatayarishia mahali na ya kwamba wakati fulani, wao wangekuwa kule pamoja naye. (Yohana 14:1-3) Mamilioni ya watu wameweka mioyo yao juu ya uzima wa namna hiyo wa mbinguni. Kwao imemaanisha tumaini la ondoleo la taabu za maisha haya. Lakini je! wewe wajua kwa nini Mungu amefanya mpango kwa watu wengine kwenda mbinguni? Je! unajua jambo ambalo watafanya huko?

2. (a) Ufalme wa Mungu ni nini, na uko mahali gani? (b) Basi, wakati Yesu aliposema kwamba ”kundi dogo” lingeurithi ”ule ufalme,” hiyo ilimaanisha nini?

2 Wakati wa huduma yake ya kidunia Yesu alisema mengi juu ya “ufalme wa Mungu.” Aliwafundisha wafuasi wake kuomba kwamba, kwa njia ya ufalme, mapenzi ya Mungu yangefanyika hapa duniani. Hivyo, dunia ingekuwa maskani yenye kupendeza kwa wanadamu. Lakini ufalme, au serikali yenyewe, ingekuwa ile ya Mungu mbinguni, na kwa sababu hii matanyingi Yesu aliutaja kama “ufalme wa mbinguni.” (Mathayo 5:20; 6:9, 10) Jambo hili linatusaidia sisi kuelewa jambo alilomaanisha wakati aliposema: “Msiogope, enyi kundi dogo; kwa kuwa baba yenu ameona vema kuwapa ule ufalme.” (Luka 12:32) Naam, Mungu angelipa “kundi dogo” hili sehemu katika serikali ya mbinguni juu ya wanadamu wote.

3. Ufunuo 20:6 husema kwamba wale watakaofufuliwa kwenye uzima wa mbinguni watafanya nini kule?

3 Katika Ufunuo 20:6, NW tunasoma kuhusu wale ambao wangefufuliwa kwenye uzima wa mbinguni: “Watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo na watatawala kama wafalme pamoja naye kwa miaka elfu.” Yesu Kristo ndiye mfalme mkuu na kuhani mkuu, na waaminifu hawa ambao huchukuliwa kutoka katika dunia hutumikia pamoja naye.—Ufunuo 5:9, 10.

4. Kwa nini inafaa kwamba wale ambao Mungu hufanyia mpango kuwa katika ufalme wa mbinguni wanachukuliwa

4 Kwa nini wao huchaguliwa kutoka katika dunia kwa kazi ya namna hiyo? Kwa sababu ilikuwa ni hapa penye dunia hii ndipo mwito wa kuthibitisha haki ya utawala wa Yehova ulipotokezwa. Ilikuwa ni hapa ndipo uaminifu wa wanadamu kwa Mungu ungeweza kuwekwa katika jaribu chini ya upinzani kutoka kwa Ibilisi. Ilikuwa ni hapa ndipo Yesu alipothibitisha uaminifu wake kamili kwa Mungu chini ya jaribu na akautoa uhai wake kama ukombozi kwa wanadamu. Kwa hiyo ilikuwa ni kutoka katika dunia hii ndipo Yehova alipofanyia mpango wa kuchukua “kundi do-go” la watu kushirikiana na Mwanawe katika ufalme wa mbinguni. Wao ni watu ambao huonyesha imani kamili katika mpango wa Mungu kwa wokovu kupitia kwa Kristo. Wao ndio maisha zao humthibitisha Ibilisi kuwa mwongo wakati aliposhtaki kwamba wanadamu humtumikia Mungu kwa faida ya uchoyo tu. Yehova amekusudia kwa ajabu kuwatumia wao kwa utukufu wake.—Waefeso 1:9-12.

5. (a) Kwa nini ni mpango wa upendo wa Mungu kuweka

5 Kama wafalme na makuhani chini ya uongozi wa Yesu Kristo, watatumikia kutoka vyeo vyao vya kim-binguni katika kuyatimiza mapenzi ya Yehova kuelekea wanadamu. Jinsi itakuwa ajabu kuwa nao kama watawala wale ambao wamethibitishwa kuwa waaminifu kwa Mungu! (Ufunuo 20:4) Na jinsi kulivyo kupenda kwa Mungu kuweka katika cheo wale ambao wamepata ujuzi wa matatizo ambayo huwapata wanadamu wote! Bila shaka, wao, kama Kristo, watashughulika na raia zao katika njia ya kuelewa. (Waebrania 2:17, 18) Lo! itakuwa baraka namna gani kwa wakaaji wa dunia wakati makuhani hawa wa kimbinguni watakapotumia faida za dhabihu ya ukombozi ya Kristo kwao, wakiwaponya kwa kiroho, kwa moyoni na kwa kimwili mpaka watakapoufikia ukamilifu!—Ufunuo 21:2-4.

WANGAPI WATAKWENDA MBINGUNI

6. Ni wangapi watakuwamo katika “kundi dogo”?

6 Wale ambao wanaitwa na Mungu kushiriki katika utumishi wa mbinguni wa namna hiyo ni wachache katika hesabu. Kama Yesu alivyosema, wao ni “kundi dogo.” Miaka baada ya kurudi kwake mbinguni, Yesu alijulisha hesabu barabara katika njozi kwa mtume Yohana, ambaye akaandika: “Nikaona, na tazama, huyo Mwana-Kondoo amesimama juu ya mlima Sayuni, na watu mia na arobaini na nne elfu pamoja naye . . . walionunuliwa katika nchi.” (Ufunuo 14:1, 3) “Mwana-Kondoo” anayetajwa hapa, bila shaka, ni Yesu Kristo; na huu “mlima Sayuni” si duniani, bali mbinguni ambako Yesu aliko. (Yohana 1:29; Waebrania 12:22) Hivyo 144,000 ni watu ambao hufa duniani kama wanadamu na hufufuliwa kwenye uzima wa mbinguni kama viumbe vya kiroho, kama Yesu alivyokuwa. (Warumi 6:5) Ikilinganishwa na maelfu ya mamilioni ya watu ambao huishi duniani, wao, kweli, ni “kundi dogo.”

7. (a) Je! 144,000 ndio watakaopokea wokovu peke yao? (b) Ni kwa usemi gani Yesu aliwataja wale watakaoithi duniani?

7 Walakini, “kundi dogo” waendao mbinguni sio peke yao wapokeao wokovu. Kama tulivyokwisha kuona, wao watakuwa na raia za kidunia wenye furaha. Yesu aliwataja hawa kama “kondoo wengine” wake ambao “mkutano mkubwa” hata sasa wanamtumikia Mungu kwa uaminifu.—Yohana 10:16; Ufunuo 7:9, 15.

JINSI MTU HUJUA KAMA YEYE YU MMOJA WA “KUNDI DOGO”

8. Jinsi gani mtu ambaye ameitwa kwenda mbinguni hujua hilo?

8 Washiriki wa “kundi dogo” wanajua kwamba Mungu amewaita kwenye uzima wa mbinguni. Jinsi gani? Kwa njia ya utendaji wa roho ya Mungu, ambayo hutia na kukuza ndani yao tumaini la uzima wa mbinguni. Mtume Paulo, kama mmoja wa “kundi dogo,” aliandika: “Roho yenyewe hushuhudia pamoja na roho yetu kwamba sisi tu watoto wa Mungu. Basi, ikiwa sisi tu watoto, sisi tu warithi pia: warithi kweli wa Mungu, lakini warithi washirika pamoja na Kristo, tukiteswa pamoja ili tupate kutukuzwa pia pamoja.” (Warumi 8:16, 17, NW) Utendaji wa roho ya Mungu hubadili maoni yote ya mtu wa namna hiyo, hata kwamba mawazo yake na sala zake huwa juu ya kumtumikia Mungu na tumaini la kuufikia uzima mbinguni. Kuwa pamoja na Kristo mbinguni ni kwa muhimu zaidi kwake kuliko vifungo vyo vyote vya kidunia.

9. Kabla mtu hajaweza kuchanganua hali yake kuhusu uzima wa mbinguni, ni jambo gani ambalo ni la lazima?

9 Bila shaka wewe umefikiri juu ya jambo hili, na labda umekuwa ukitaka kujua kama wewe ndiwe utakayepokea uzima wa mbinguni. Kabla mtu hajaweza kuchanganua hali yake sawasawa, lazima aelewe mambo ambayo Biblia hufundisha juu ya jambo hili. Kwa nini? Kwa sababu roho takatifu ya Mungu inayoshuhudia kwamba mtu ameitwa kwenye utukufu wa kimbinguni ni roho ile ile iliyoongoza kuandikwa kwa Biblia. Tukiwa na hili akilini, na tuichunguze hali.

10. (a) Ni imani gani ambayo huenda imemfanya mtu kutumaini kwenda mbinguni? (b) Ni kweli gani za Biblia ambazo hazijulikani na wale ambao hufikiri kwamba watu wema wote huenda mbinguni?

10 Je! zamani wewe ulisadiki kwamba watu wote wema huenda mbinguni? Ikiwa ndivyo, na ikiwa kuishi maisha mema, bila shaka umekuwa ukitaraji kutiwa miongoni mwao. Labda pia umekuwa ukitumaini katika njia hii kuungana tena na wapenzi wako ambao ulikuwa umewapoteza katika mauti. Lakini wakati ulipokuwa una taraja hilo, je! ulijua kwamba Biblia husema kwamba watu waaminifu wa Mungu kama vile Mfalme Daudi na Yohana Mbatizaji hawakwenda mbinguni? (Matendo 2:29, 34; Mathayo 11:11) Je! ulijua wakati huo kwamba ni 144,000 waliochaguliwa kutoka katika miongoni mwa wanadamu wakati wa karne kumi na tisa zilizopita peke yao ndio wangepata uzima wa kimbinguni? Na ulijua wakati huo kwamba Biblia hutoa tumaini la uzima wa milele chini ya hali zenye haki apa hapa duniani kwa wote wengine ambao wangekuwa watumishi waaminifu wa Mungu?—Zaburi 37:10, 11, 29.

11. Kwa sababu ya mafundisho gani ya uongo kwa habari ya nafsi watu wengi hufikiri kwamba watakwenda mbinguni?

11 Ulipokuwa ukifikiri wakati huo juu ya uzima wa kimbinguni kwako mwenyewe, je! ulisadiki katika kutokufa kwa nafsi ya kibinadamu? Basi, kwa kueleweka, labda umekuwa ukitumaini kwamba nafsi yako ingekwenda mbinguni. Lakini ikiwa ulikuwa unalo tumaini la namna hiyo haikuwa kwa sababu roho ya Mungu ilikuwa ikikushuhudia? Kwa kinyume, kama unavyojua sasa, Neno la Mungu lililoongozwa na roho yake husema kwamba nafsi ya kibinadamu hufa na hutoweka. Basi wale wafao lazima wategemee juu ya Mungu kuwafufua kwenye mahali pawapo pote ambapo Mungu anawakusudia.—Ezekieli 18:4; 1 Wakorintho 15:35-38.

12. (a) Ni nani mwenye kuchagua watu watakaopokea uzima wa mbinguni? (b) Ni kwenye tumaini gani Mungu zaidi anawaelekeza watu leo?

12 Basi, katika jambo hili, lazima tutazame kwenye Maandiko kwa uongozi na tusiache maono ya moyoni, au imani za wakati uliopita zisizo za maandiko, zivuruge kufikiri kwetu. Wale ambao hupokea uzima wa kimbinguni sio watu ambao hujichagulia wenyewe; Mungu ndiye mwenye kufanya uchaguzi. (2 Wathesalonike 2:13, 14) Wao wameitwa kuacha nyuma washiriki wao wa karibu wa jamaa na rafiki na mam-bo yote ya kidunia kwa pendeleo la kushiriki kama wafalme wasaidizi na makuhani wadogo pamoja na Kristo na kama sehemu ya “bibi-arusi” wake. (Ufunuo 21:2) Ndilo jambo ambalo Mungu ameweka mbele yao, nao hulithamini sana. Lakini si lazima kuwa wa kikundi hicho cha kimbinguni kwa kupata ondoleo la taabu za maisha haya. Mungu awapenda “kondoo wengine” wake wa kidunia pia. Yeye huahidi kwamba ataifanya dunia hii kuwa paradiso, mahali ambapo maumivu na huzuni havitakuwapo tena. Mambo ya hakika huonyesha kwamba zaidi ni kwenye tumaini la uzima la namna hiyo la kidunia kwamba Mungu amekuwa akiwaelekeza watu katika miaka

ya karibuni.

13. (a) Ni nani ambao kwa kufaa hushiriki mkate na divai penye Ukumbusho wa kila mwaka wa mauti ya Kristo?

13 Walakini, kila mwaka, penye ukumbusho wa kila mwaka wa mauti ya Kristo, washiriki wachache wabakio wa “kundi dogo” ambao bado wapo duniani huadhimisha Ukumbusho wa mauti ya Kristo. Kama Yesu alivyoagiza, wao hushiriki mkate usiotiwa chachu na divai nyekundu, ambavyo ni mifano ikifananisha mwili na damu ambavyo Yesu alitoa kwa ajili ya wanadamu. Yesu alisema kwa wale ambao aliagiza kushiriki mifano hii kwamba alikuwa akifanya pamoja nao ‘agano kwa ufalme’; kwa hiyo wale ambao si warithi wa ufalme wa kimbinguni hawashiriki mifano. (Luka 22:19, 20, 29, NW) Walakini, wale ambao hutazamia kwenye uzima wa kidunia huwapo kila mwaka katika idadi kubwa kama watazamaji penye chakula cha Bwana cha jioni. Kama mtu anayependezwa sana katika maisha chini ya ufalme wa mbinguni, wewe pia imekupasa kuwa katika hudhurio.

KURUDI KWA KRISTO

14. Ni ahadi gani ambayo Yesu alifanya juu ya kuja tena?

14 Jioni kabla ya mauti yake Yesu Kristo aliwaahidi washiriki waaminifu wa “kundi dogo” kumi na mmoja kwamba yeye angekuja tena, akisema: “Naenda kuwaandalia mahali. . . . nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo.”—Yohana 14:2, 3.

15. (a) Ufunuo 1:7 husema nini juu ya kurudi kwa Kristo, na je! hili lieleweke kwa maana ya kuonekana? (b) Twajuaje kwamba wanadamu kwa jumla wasingemwona Kristo wakati wa kurudi kwake?

15 Je! huku kutakuwa kurudi kwa kuonekana, kwa jinsi ya kimwili? Labda wengine wataonyesha kwamba Ufunuo 1:7 husema: “Tazama, yuaja na mawingu; na kila jicho litamwona.” Je! hii inamaanisha kwamba watamwona kwa njia halisi kwa macho yao ya kimwili? Biblia haisemi kuona tu kwa macho yetu ya kimwili, bali kuona katika maana ya kwamba tunaelewa. Yesu alionyesha kwamba Mafarisayo wa kidini wa siku zake walikuwa vipofu ijapokuwa wao walisema, “Twaona.” Walikuwa vipofu kwa kiroho. (Yohana 9: 39-41; Isaya 43:8) Ni katika maana hiyo ya kuona kwa kiroho kwamba Ufunuo 1:7 wapaswa kueleweka. “Kila jicho” linafanywa ‘kumwona’ kwa sababu, hata ijapokuwa wakatae kuamini sasa, wakati Kristo atakapowafisha waovu, watajua ni nini linalotukia kwa sababu wameambiwa mbele. Walakini, kwamba Yesu asingerudi kwa kuonekana yeye alisema wazi: “Kitambo kidogo na ulimwengu hautaniona tena, bali ninyi mtaniona, kwa sababu mimi ni hai na ninyi mtakuwa hai.” (Yohana 14:19, NW) Wanadamu kwa jumla wasingemwona tena kwa sababu alijua angerudi mbinguni. Bali “kundi dogo” wangemwona kwa sababu alikuwa akitayarisha kuwachukua ili wawe pamoja naye kule.

16. Basi, kurudi kwa Kristo, humaanisha nini?

16 Kwa hiyo kurudi kwa Kristo hakumaanishi kwamba yeye hurudi kama mwanadamu kuishi duniani. Bali, humaanisha kwamba yeye hutwaa juu utawala wake wa kifalme kuelekea dunia na kwamba yeye hufufua “kundi dogo” lake kutoka kwa wafu kwenye thawabu yao katika mbingu. Kule ndiko wao hushiriki katika kutimiza kusudi la upendo la Mungu kwa ufalme wake. Wewe unaishi katika wakati ambapo wewe, pia, waweza kupata baraka kutoka kwa utawala huo wa Ufalme.—Ufunuo 11:15-18.

kutoka katika dunia hii?

katika cheo wale ambao wamepata ujuzi wa matatizo yanayowapata wanadamu wote? (b) Ni baraka gani ambazo wakaaji wa dunia watajifurahisha wakati makuhani hawa wa kimbinguni watakapozitumia faida za dhabihu ya ukombozi wa Kristo?

(b) Nani wengine huwapo?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki