Sura ya 12
Utawala wa Haki Wafanya Dunia kuwa Paradiso
1. (a) Ni hali gani zinazoonyesha haja kwa utawala wa haki juu ya dunia yote? (b) Je! bado Mungu ataifanya dunia kuwa
JINSI wanadamu huhitaji sana utawala wa haki juu ya dunia yote! Kila mtu lazima akubali kwamba sayari hii leo siyo paradiso. Ufukara na njaa ndiyo mambo yanayoyapata mamilioni za watu kila siku. Miji yenye sura isiyopendeza huiondolea dunia wingi wa uzuri wake wa asili na kuitia hewa na maji yanayoizunguka sumu. Zaidi na zaidi miji inajaa uvunjaji wa sheria, ambapo watu huogopa kutoka katika nyumba zao usiku. Jinsi hii ni tofauti na kusudi la awali la Mungu kwa wanadamu! Lakini jinsi ni vyema kujua kwamba Mungu hakuliacha kusudi lake! Kwa maana yeye hutuhakikishia sisi: “Neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure.” (Isaya 55:11; tazama pia Mwanzo 2:8, 15; 1:28.) Bado yeye ataifanya dunia hii kuwa paradiso yenye fahari.
2. Jinsi gani twaweza kuokoka na kuingia katika taratibu mpya
2 Karibuni Yehova ataikomesha taratibu mbovu iliyopo. Ikiwa wewe unapata kibali cha Yehova sasa, huenda utapendelewa kuokoka na kuingia katika taratibu mpya ya Mungu. Hili litamaanisha nini kwako?
USIMAMIZI WA HAKI
3. Ni njia gani ya Mungu kwa kurudisha haki?
3 Kwa karibu miaka elfu sita, haja kubwa zaidi kupita zote za wanadamu imekuwa ni kurudishwa katika upatano kamili na Yehova Mungu, Muumba wao. (2 Wakorintho 5:20) Ili kurudisha haki kwenye sayari hii Yehova mwenyewe amefanya mpango kwa “usimamizi katika kiasi kikamilifu cha nyakati zilizowekwa.” Usimamizi huu au utawala ni kupitia kwa ufalme wa Kristo. Kama tulivyokwisha kuona, Ufalme umekwisha kuanza kutawala katika mbingu na karibuni utachukua madaraka kamili ya mambo ya dunia. Ni nini kusudi lake kubwa katika kufanya hivi? “Kukusanya vitu vyote pamoja tena katika Kristo, vitu vilivyomo katika mbingu na vitu vilivyomo katika dunia.” (Waefeso 1:9, 10, NW) Usimamizi huu ndiyo njia ya Mungu kwa kuwaleta wale wote wanaoishi duniani katika upatano kamili na utawala wake wa kimbinguni. Hiki ndicho kitu tuombeacho wakati tunaposema: “Ufalme wako uje, mapenzi yako yatimizwe, papa duniani kama huko mbinguni.” —Mathayo 6:9, 10.
4. (a) Ni mabadiIiko gani ambayo Ufalme utaleta kwa uhusiano wa wanadamu? (b) Kwa nini hapatakuwapo tena vita, na hii itakuwa na maana gani kwa wanadamu?
4 Hii itakuwa na maana gani kuhusu uhusiano wa kibinadamu? Kuungana katika ibada safi ya Baba yao wa kimbinguni, watu wa makabila yote na mataifa ya watu wataishi pamoja kama jamaa moja ya ndugu na dada! (Matendo 10:34, 35; 17:26) Kuwa na ufalme wa Mungu kupitia kwa “Mfalme wa Amani” ukitawala juu ya dunia nzima, dunia haitagawanywa tena kwa jinsi ya siasa. Hapatakuwapo utukuzo wenye kiburi wa mataifa kuchochea chuki, mapigano na umwagaji wa damu. (Isaya 9:6, 7) Silaha za vita zo zote zenye hatari ya kifo zitakazosalia baada ya Har-Magedoni zitaharibiwa upesi milele. (Ezekieli 39:9, 10; Zaburi 46:8, 9) Kwa hiyo hapatakuwapo tena magazeti yenye orodha ya watu waliokufa katika vita, hapana tena wafanywao na vita kuwa wajane wala mayatima, hapana tena nyumba na miji iliyobomolewa kwa makombora. Lo! hii itakuwa baraka namna gani kwa wanadamu!
5. Kwa nini hapatakuwapo udhalimu chini ya utawala wa Kristo?
5 Kutoka katika kiti chake cha enzi cha mbinguni Yesu Kristo atasimamia mambo ya kidunia katika njia ambayo italeta faida zenye kudumu. Lo! jinsi kwa ajabu yeye amekwisha kuonyesha sifa zake, hata kuutoa uhai wake mwenyewe kwa ajili ya wale ambao watakuwa raia zake! Tena, maandishi ya Biblia huonyesha kwamba hapana kitu—vishawishi, mikazo, kushutumiwa, hata mauti yenyewe—kingeweza kumzuia Yesu asifanye kilicho chema. Basi, tunaweza kuwa hakika kwamba chini ya utawala wake hapatakuwapo udhalimu wala rushwa.—Isaya 11:2-5.
6. Yesu ni mtu wa aina gani, hata imetupasa kuwa wenye shukrani kuwa naye kama Mtawala?
6 Je! wewe usingemthamini, pia, mtawala ambaye sikuzote husema kweli? Yesu ndiye mtu wa aina hiyo. (Yohana 1:14; 18:37) Tena ni nani ambaye asingejiona kuvutwa kwa mtu ambaye huonyesha fadhili za kweli na kupendezwa kwa unyofu wa moyo katika wengine? Wakati Yesu aliposafiri huku na huku akitangaza habari njema, Biblia hutuambia sisi kwamba yeye alitumia kwa wingi uwezo ambao Mungu alikuwa amempa yeye kuponya wagonjwa, wote wagonjwa kwa kimwili na wagonjwa katika njia ya kiroho. (Mathayo 9:35, 36) Ijapokuwa ingalikuwa jambo la maana sana kuishi katika wakati wa huduma ya kidunia ya Yesu, itakuwa jambo la maana zaidi kuishi duniani wakati yeye atakapoutumia uwezo huu kwa ajili ya wanadamu wote.
7. Ni watu wa aina gani hao watakaotawala pamoja na Yesu katika ufalme wake wa kimbinguni?
7 Watakaoshirikiana na Yesu katika ufalme wake wa kimbinguni watakuwa ni 144,000 wafalme na makuhani waliochukuliwa kutoka miongoni mwa wanadamu na kukamilishwa na Mungu. (Ufunuo 5:10) Hawa, pia, ni watu ambao huthibitisha upendo wao wa haki mpaka kufa.—Ufunuo 14:1, 4, 5; 2:10.
8. (a) Je! watakuwapo wajumbe waonekanao wa ufalme wa Kristo wa kimbinguni? (b) Ni nani atakayewachagua?
8 Lakini je! serikali hii ya kimbinguni itakuwa na wajumbe wo wote waonekanao? Ndiyo, bila shaka! Kwani, hata sasa usimamizi wa kimbinguni huwaweka wanaume waaminifu kama wajumbe wake katika kundi la Kikristo, wakifanya hivyo kwa njia ya roho takatifu ya Mungu. (Isaya 32:1, 2; Matendo 20:28) Hivyo tunaweza kuwa hakika kwamba Kristo ataona kwamba wanaume wa kweli duniani wamepewa mgawo kuwakilisha serikali ya Ufalme, kwa maana ndipo atakapokuwa akiongoza mambo ya kidunia. Kwa sababu wanaume hawa humwakilisha Mfalme katika njia ya pekee, Biblia huwait.a “wakuu.” Hawa wote watakuwa wamethibitisha uaminifu wao kwa Mungu na upendo wao kwa wanadamu wenzio. Roho ile ile ya Mungu imwongozayo Mfalme wao wa kimbinguni itawaongoza na wao pia.—Zaburi 45:16.
9. Je! rangi ya ngozi ya mtu au mahali pake pa uzaliwa pataongoza jinsi atakavyotendewa wakati huo?
9 Wala taifa, wala rangi, wala mahali pa uzaliwa hapatahusiana na njia ambayo wajumbe hawa wakuu watatumia sheria za haki za Mungu. (Kumbukumbu la Torati 10:17; Warumi 2:11) Wakifuata mfano wa Mfalme wao, “wakuu” watatumikia kwa unyenyekevu na kwa kusaidia, wakileta burudisho kwa wanadamu wenzao. Lakini watakuwa imara katika kutegemeza haki ya Mungu.—Mathayo 11:29; 20:25-28.
10. Kwa kutofautisha na kutokuwa na usalama na hofu inayoenea sana leo, zitakuwapo hali gani chini ya utawala wa haki wa Kristo?
10 Dunia ikiisha kuondolewa watenda mabaya wote, uvunjaji wa sheria hautaruhusiwa kamwe kusitawi tena. (Zaburi 37:9-11) Hapatakuwapo tena kamwe haja ya mapolisi, magereza, pingu za mikono, kamsa za kuonya wevi, kasha za chuma za kuwekea vitu vyenye thamani, kufuli na funguo. Chini ya utawala wa haki wa Ufalme, utajua kwamba ye yote apigaye hodi mlangoni pako ni rafiki. Kutakuwapo uhuru kamili wa hofu ya dhara lo lote. Hapatakuwapo tena kabisa ye yote wa kuogopa kutembea polepole nje usiku kutazama nyota, kazi ya mikono ya Muumba. Hata kama vile ni kweli kwa habari ya kundi la Mungu leo katika njia ya kiroho, ndivyo ilivyo wakati huo katika njia halisi, “watakaa salama salimini, wala hapana mtu atakayewatia hofu.”—Ezekieli 34:28.
UHURU WA DHAMBI WALETA AFYA NA UZIMA
11. Zaidi ya kutumikia kama wafalme, ni katika nafasi gani nyingine washiriki wa serikali ya kimbinguni ya Kristo watatumikia? Kwa nini?
11 Programu ya kwanza ya Ufalme itachukua muda wa miaka elfu moja. Katika wakati huo Yesu Kristo na washiriki wa serikali yake ya mbinguni watatumikia si kama wafalme tu bali pia kama makuhani wa Mungu kwa ajili ya raia zao wote za kibinadamu. (Ufunuo 20:6) Kwa nini? Kwa sababu itakuwa lazima kwa watu wote duniani kuwekwa “huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu” ili wawe na “uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu.” (Warumi 8:21) Hata baada ya waovu kuharibiwa, waokokaji wa kidunia bado watakuwa wasiokamilika kwa sababu ya dhambi waliyorithi kutoka kwa Adamu. Tamaa mbaya za mwili wao usiokamilika zitakuwa bado zikipiga vita juu ya tamaa njema za akili na moyo. (Warumi 7:21-23) Hivyo, kukubaliwa kabisa katika jamaa ya Mungu ya wana, wao wanahitaji kwanza utumishi wa makuhani wa mbinguni wa Mungu. Ni jambo gani ambalo hawa watafanya?
12. (a) Ni uwezo gani wa aina yake washiriki wa ufalme wa kimbinguni wa Kristo watakuwa nao? (b) Watu watafika kwenye hali gani yenye furaha?
12 Wao watakuwa na uwezo ambao umekuwa ukikosekana katika serikali zote za kibinadamu mpaka sasa: uwezo wa kusafisha watu dhambi na kutokukamilika. Uwezo huu umo katika ukuhani wa mbinguni wa Mungu kwa njia ya dhabihu ya ukombozi wa Yesu. Wakati huo Mwana wa Mungu na makuhani washiriki wake watatumia faida za dhabihu ya Yesu moja kwa moja kwa watiifu wote. (Yohana 1:29; 1 Yohana 2:2) Mpango huu unafananishwa katika Biblia kwa “mto wa maji ya uzima” wa mfano kutoka katika “kiti eha enzi cha Mungu, na cha MwanaKondoo” na “majani ya mti huo ni ya kuwaponya mataifa.” (Ufunuo 22:1, 2) Kwa kufanya maendeleo yenye kuendelea katika haki na kwa kuwa na msaada wa ukuhani wa mbinguni, wao watakuwa vijana na wenye nguvu polepole, mpaka watakapoufikia ukamilifu wa afya katika akili na mwili. Watawekwa huru kwa ukamili na utumwa kwa dhambi na mauti iliyorithiwa kutoka kwa Adamu.—Yohana 11:26.
13. (a) Jinsi gani Ufunuo 21:4 husimulia baraka ambazo Ufalme utaleta? (b) Ni jambo gani ambalo Yesu alifanya wakati alipokuwa duniani linaloonyesha kwamba anaweza kutokeza baraka hizi?
13 Naam, katika njia hii, Mungu “atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.” (Ufunuo 21:4) Jinsi itakavyokuwa ajabu kujifurahisha afya kamili! Hata kama vile Mwana wa Mungu alivyowaponya wenye ukoma na akawaponya vilema na vipofu wakati alipokuwa duniani, vivyo utawala wake wa haki utakomesha maradhi yote na maumivu. (Marko 1:40-42; Yohana 5:5-9; Mathayo 9:35) Haja kwa mahospitali na bima za afya itatoweka wakati huo! Kwa kuondolewa kwa magonjwa na mauti, chanzo cha machozi cha ulimwenguni pote kitatoweka. (1 Wakorintho 15:25, 26) Jinsi itakavyokuwa ajabu kujifurahisha uhuru kamili wa dhambi, na kuweza kufikia kwa ukamilifu kanuni za haki za Mungu katika msemo, wazo na mwenendo!
KUWAKARIBISHA WATU WANAORUDI KUTOKA KWA WAFU
14. Ni tumaini gani kwa wafu ambalo Yesu alifunua katika Yohana 5:28, 29?
14 Liko pia taraja la furaha la kwamba wapenzi wako ambao wamekufa wataweza kujifurahisha baraka za utawala wa haki wa Mwana wa Mungu juu ya dunia. Yesu alifunua tumaini kwa mamilioni yasiyohesabika ya watu ambao wamekufa, akisema: “Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. Nao watatoka.” (Yohana 5:28, 29) Lo! utakuwa wakati wenye furaha yenye kusisimua namna gani wakati kwanza habari inapelekwa kama umeme kuzunguka dunia ikisema: “Wafu wanafufuka!”
15. Kwa nini twaweza kuwa na uhakika kwamba Yesu atawafufua wafu?
15 Twaweza kuwa na uhakika kamili kwamba jambo hili litatimizwa. Ukumbuke kwamba, alipokuwa duniani, Yesu hakuponya wagonjwa na viwete peke yao; aliwafufua na watu waliokufa pia. (Mathayo 11:2-6) Jambo hili lilionyesha uwezo wa ajabu wa Mungu wa kufufua wafu, uwezo ambao amempa Yesu Kristo. Labda unakumbuka pindi moja wakati Yesu alipokuja nyumbani pa mtu aliyekuwa amefiwa na bintiye mwenye umri wa miaka kumi na miwili. Akisema kwa msichana mfu, Yesu akasema: “Msichana, nakuambia, Inuka.” Matokeo yalikuwa nini? Biblia inatuambia hivi: “Mara akasimama yule kijana, akaenda.” Wazazi wake na watazamaji wengine walitendaje kama matokeo ya mwujiza huu? “Mara wakashangaa mshangao mkuu.” Walikuwa na furaha nyingi hata wasijiweze.—Marko 5:35, 38-42; tazama pia Yohana 11:38-44; Luka 7:11-16.
16. Ni nani watakaofufuliwa kutoka kwa wafu, na jinsi gani jambo hili litawahusu walio hai?
16 Wakati paradiso itakaporudishwa duniani, Yesu atautumia tena uwezo wake kuwafufua wafu. Kwa maana Biblia inatuhakikishia kwamba “kutakuwa na ufufuo wa wafu, wenye haki na wasio haki pia.” (Matendo 24:15) Lo! itakuwako furaha namna gani duniani pote wakati kikundi baada ya kikundi cha watu waliokufa wanarudi kwenye uhai! Ebu wazia kutakuwa kukutana tena kwa furaha na jamaa wapenzi namna gani! Badala ya orodha ya majina ya watu waliofariki, yamkini kutakuwako matangazo ya watu ambao wamefufuka sasa hivi kuleta furaha kwa wapenzi wao.
17. Kwa nini si tatizo kwa Mungu kuwakumbuka wote wale watakaofufuliwa?
17 Mamilioni nyingi za watu wamekufa, lakini jambo hilo halileti tatizo kwa Mungu. Yeye aweza kuwakumbuka wote. Kwani, Biblia inatuambia kwamba Mungu “huihesabu idadi ya nyota, huzipa zote majina.” (Zaburi 147:4) Ebu fikiri jambo hilo lina maana gani. Inasemekana kwamba yako mamia ya mamilioni ya makundi ya nyota, na ndani ya kila kundi mkiwa mamia ya mamilioni ya nyota, na hata hivyo Mungu aijua kila nyota kwa jina. Kwa kulinganisha nazo hesabu ya wanadamu wote ambao wamewahi kuishi ni ndogo sana. Hivyo haitakuwa vigumu kwa Mungu kuwakumbuka wote ambao wamekufa na ambao huja chini ya mpango wa ukombozi wa Kristo. (Mathayo 19:26) Watarudishwa kwenye uhai apa hapa duniani. Ni pendeleo lenye kusisimua namna gani kuwapo kuwakaribisha wanaporudi kutoka kwa wafu!
18. Katika ufufuo, je utaweza kuwatambua wale ambao uliwajua kabla hawajafa? Kwa nini?
18 Wakati watakaporudi je! watakuwa ni watu wale wale? Je! sisi tutawajua? Ndiyo! Hata wanadamu wanaweza kuhifadhi kwa muda mrefu picha na sauti penye utepe kwa matumizi ya baadaye kwa televisheni. Mungu aweza kufanya hata zaidi kuliko na hilo. Wakati wa kufufuka yeye aweza kumpa kila mtu mwili unaofaa, kama vile alivyofanya wakati wa kumwumba mtu wa kwanza, kisha atie tena katika ubongo kumbukumbu zile zile za mambo yote ambayo mtu huyo alijifunza na mambo yaliyompata wakati wa maisha yake ya zamani. Hivyo katika ufufuo mtu huyo atatoka na utu ule ule aliokuwa nao wakati wa kufa, kama vile Yesu aliyefufuka alivyotunza utu wake mwenyewe. (Ebr. 13:8) Wewe utawatambua wale uliowajua kabla hawajafa. Ni tumaini la ajabu namna gani!—Ayubu 14:13-15.
19. Kitabu cha Ufunuo huonyesha nini kwa habari ya wafu? Basi ni nini itatoweka?
19 Mtume Yohana alipewa njozi ya matukio haya yenye kusisimua yatakayotukia wakati wa utawala wa Kristo, na inapatikana katika kitabu cha Ufunuo. Njozi yake huonyesha kwamba mauti na Hades (kaburi la kawaida la wanadamu) ‘zitawatoa hao wafu waliokuwamo ndani yake.’ Hapana mtu atakayeachwa ndani yake. Ndipo mauti iliyokuja kwa sababu ya dhambi iliyorithiwa itatoweka milele. (Ufunuo 20: 13, 14; Isaya 25:8) Nyumba za vilio na mawe ya makaburi vitatoweka! Makaburi hayatabaki kuharibu uzuri wa dunia ya paradiso.
20. (a) Ni nafasi gani itakayofunguliwa kwa watakaofufuliwa, na itakuwa lazima wafanye nini? (b) Ni juu ya msingi gani watakaohukumiwa? (c) Jinsi gani mabadiliko yatakavyotukia katika njia za watu ambao zamani wamekuwa wenye hatari sana?
20 Wale watakaofufuliwa kwenye uhai duniani watatoka waje kwenye nafasi ya kupata uzima wa mile-le katika paradiso. Utakuwa kwao wakati wa elimu. “Vitabu” vilivyo na maagizo ya Mungu ndani yake vitafunguliwa, na ili wageuze akili zao kupatana na mapenzi ya Mungu, itakuwa lazima wafuate yaliyomo katika vitabu hivi. Watahukumiwa “kila mtu kwa kadiri ya matendo yake”; yaani, matendo watakayotenda baada ya kufufuliwa na baada ya kujifunza yaliyomo katika “vitabu.” (Ufunuo 20:11-13) Kwa kuitikia elimu itakayotolewa, hata wale ambao hapo kwanza walikuwa wa hatari sana kama wanyama wa mwitu watabadili njia zao, kama vile wengi wa-mekwisha kufanya wakati wa kuja katika ushirika wa kundi la Kikristo.—Isaya 11:9; 26:9; 35:8, 9.
DUNIA YARUDIA KWENYE HALI ZA PARADISO
21. Ni baraka gani ya utawala wa Ufalme inatajwa katika Isaya 25:6?
21 Maendeleo katika haki yataleta baraka za kimwili pia. Kutakuwako utimizo halisi wa maneno ya unabii ya Isaya 25:6: “Na katika mlima huu [Yehova] wa majeshi atawafanyia mataifa yote karamu ya vitu vinono.” Hapana mtu kamwe atakayejua tena maumivu makali na udhaifu wa njaa kali. Lakini Mungu ataitayarishaje karamu hii?
22. (a) Kama ionyeshwavyo katika Biblia, jinsi gani shibe hii ya kimwili itakavyotolewa? (b) Dunia nzima itageuzwa kwenye hali gani?
22 Wakati Waisraeli walipokuwa watu wateule wa Mungu, baraka yake iliwaletea fanaka kubwa. Mashamba yao yalizaa mazao bora ya nafaka. Bustani zao za matunda zilizaa matunda bora. Yehova aliwafungulia “hazina yake nzuri, nayo ni mbingu, kwa kutoa mvua ya nchi [yao] kwa wakati wake.” (Kumbukumbu la Torati 28:12; tazama pia mstari wa 8.) Baraka za namna iyo hiyo zitakuwa nyingi kwa kiasi kilicho kamili sana chini ya utawala wa ufalme wa Kristo. (Zaburi 67:6, 7) Raia za kidunia za Ufalme watatimiza amri ambayo Adamu na Hawa hawakuitimiza kamwe. ‘Wataitiisha’ dunia, kuifanya dunia nzima kuwa paradiso. Ilikuwa kuhusu taraja la namna hiyo, na akiwa na tumaini la ufufuo akilini, kwamba Yesu akamwambia mtenda mabaya mwenye kuhurumia aliyefishwa pamoja na yeye: “Kweli nakuambia leo hivi, Utakuwa pamoja nami katika Paradiso.”—Luka 23:39-43, NW.
23. Jinsi gani Zaburi zisimuitavyo hali yenye furaha itakayokuwamo duniani?
23 Ndipo dunia nzima itakapoonyesha furaha. Itakuwa kana kwamba mashamba yake ya majani na milima, miti yake na maua, mito yake na bahari, vyote vinafurahia utawala wa haki wa Yehova. (Zaburi 96: 11-13; 98:7-9) Hewa safi hataichafuliwa tena. Kila mto na kijito vitametameta na maji ya baridi na yaliyo safi. Hakutakuwako tena kuharibu kwa nchi.
24. Utawala wa Kristo utawafanyia wanadamu nini kwa habari ya kuumba kwa wanyama?
24 Dunia yote—misitu yake, makonde yake, milima yake—itakuwa shamba moja zuri, lenye aina nyingi za wanyama na ndege wenye rangi nyingi. Hivi, pia, vitatiishwa chini ya utawala wa hekima wa Mwana wa Yehova. Na katika “dunia ijayo inayokaliwa na watu” yeye atavileta vyote katika utiisho usio na madhara wa wanadamu.—Waebrania 2:5-8, NW; Zaburi 8:4-8.
JARIBU LA MWISHO LAAMUA USTAHILI WA UZIMA WA MILELE
25. (a) Mwishoni mwa miaka ya kwanza elfu moja, Ufalme utakuwa umetimiza nini? (b) Ndipo jaribu gani litatukia, na kwa nini?
25 Ufalme wa Mungu kupitia kwa Kristo utatawala kwa umilele wote. Walakini, mwishoni mwa miaka ya kwanza elfu moja utakuwa umetimiza kusudi la pekee kuelekea dunia. Utakuwa umeondoa kila alama ya udhalimu. Wanadamu wote duniani watasimama kama viumbe vikamilifu mbele ya kiti cha enzi cha Hakimu Mkuu kupita wote, Yehova Mungu. Wao watakuwa sawa na wanadamu wakamilifu wa kwanza katika Edeni katika kila jambo. (1 Wakorintho 15: 24) Je! watastahili kupewa na Mungu haki kwenye uzima wa milele? Itafaa kwamba raia za Ufalme wajaribiwe juu ya upendo wao kwa utawala wa haki wa Mungu. Yehova atawapa nafasi kuonyesha uaminifu wao. Jinsi gani? Kwa kumfungua Shetani na malaika zake wabaya kutoka katika hali yao ya kizuizi katika “shimo refu lisilopimika.” (NW) (Ufunuo 20:7) Kwa jaribu hili kila mtu peke yake katika jamaa ya Mungu ya kidunia atakuwa na pendeleo la kutoa jibu la peke yake kwa mwito wa kuthibitisha uaminifu uliotokezwa na Shetani kwa Baba yao wa mbinguni.
26. Matokeo yatakuwa nini kwa (a) wale wadumuo kuwa waaminifu kwa Mungu? (b) wale wampindukiao Mungu? (c) Shetani na malaika zake wabaya?
26 Wale wadumuo kuwa waaminifu kwa Mungu wa-tahukumiwa kustahili uzima wa milele. Yehova atawapa haki hii, akiandika majina yao katika ‘kitabu chake cha uzima.’ Ye yote ambaye kwa kuasi atampindukia Mungu ataangamizwa katika “mauti ya pili.” Ndipo, Shetani Ibilisi, pamoja na malaika zake wabaya, watakapoangamizwa milele. (Ufunuo 20:710, 15) Dunia, wala sehemu nyingine yo yote ya ulimwengu wote mkubwa mno, haitasumbuliwa tena kamwe na dhambi na uasi, la, hasha. Ikifanywa kuwa paradiso ambamo haki itakuwamo, dunia itatumikia kwa wakati wote utakaofuata baada ya hapo kama kito cha sifa kwa jina la Yehova.
27. Ikiwa kweli tunataka uzima katika dunia ya paradiso, imetupasa tufanye nini sasa?
27 Je! kusudi la Mungu kwa utawala wa haki juu ya dunia ya paradiso hukuza heshima yako kwa haki yake? Je! linaongeza thamani yako ya hekima yake? Je! linakuongoza kuonyesha upendo wako kwake? Ikiwa ndivyo, basi imekupasa ufanye kadiri uwezavyo sasa kumtumikia yeye kwa moyo wote. Shiriki katika kuwaambia wengine habari za jina la Yehova na kusudi lake. (Zaburi 89:14-16; 1 Yohana 4:19) Ishi sasa kupatana na kanuni za haki za Mungu, na hivyo kujitayarisha kwa uzima wa milele katika dunia ya paradiso chini ya utawala wa haki wa Ufalme.
paradiso?
ya Mungu?
[Picha katika ukurasa wa 108]
Hata wafu walifufuliwa na Yesu