Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • tr sura 19 kur. 163-169
  • Heshima ya Kimungu kwa Uhai na Damu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Heshima ya Kimungu kwa Uhai na Damu
  • Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ‘KUMWAGA DAMU YA MWANADAMU’
  • ‘JIEPUSHENI WENYEWE NA DAMU’
  • Maoni ya Mungu Kuhusu Uhai
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Kuokoa Uhai kwa Damu—Jinsi Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Heshimu Zawadi ya Uhai
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Azimio Letu Imara Juu ya Uhai na Damu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
Pata Habari Zaidi
Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
tr sura 19 kur. 163-169

Sura ya 19

Heshima ya Kimungu kwa Uhai na Damu

1. Ijapokuwa ulimwengu u mzoevu wa jeuri, Biblia hutufundishaje sisi kuona uhai?

JINSI tungekuwa salama zaidi ikiwa kila mtu alikuwa na heshima ya kimungu kwa uhai na damu! Lakini watu wengi hawana heshima ya namna hiyo. Jeuri na umwagaji wa damu vinaongezeka kila mahali. Katika mahali pengi uhai wa mtu umo hatarini ikiwa anatembea tu katika barabara akiwa peke yake usiku. Hivyo ulimwengu umekuwa mzoevu wa jeuri kwamba, hata kwa tafrija, watu huketi kwa saa nyingi na kuutazama katika televisheni au katika sinema. Walakini, Biblia inatufundisha sisi kwamba uhai ni kitu fulani ambacho ni kitakatifu. Je! wewe unauona kwa njia hiyo?

2. Kwa nini huenda mafundisho ya Biblia juu ya uhai na damu yakawashangaza watu wengine?

2 Nia zisizopatana na maandiko zimeenea sana leo kwamba mafundisho ya Biblia juu ya shauri hili huenda yakawashangaza watu wengine kwanza. Walakini, Mtungaji wa Biblia, ambaye pia ni Mpaji wa uhai na Muumba wa damu, ndiye Mamlaka Kuu kupita yote juu ya jambo hili. Sheria zake lazima ziheshimiwe.—Zaburi 36:5-9; Isaya 55:8, 9.

‘KUMWAGA DAMU YA MWANADAMU’

3. (a) Ni kwa nani Mungu alisema kwanza juu ya uzito wa kutwaa uhai wa kibinadamu? Kwa nini? (b) Baada ya Gharika, jinsi gani Mungu alitia mkazo wa thamani ya uhai? (c) Je sheria hiyo imechakaa?

3 Kwanza ilikuwa kwa Kaini, mwana wa Adamu, kwamba Yehova akasema juu ya uzito wa kuharibu uhai wa kibinadamu. Mungu alikuwa amekwisha kumwonya Kaini kwamba hasira yake ingeweza kumwongoza katika dhambi, lakini Kaini alidharau onyo hili na akamshambulia nduguye Habili, akimnua. Kisha Mungu akasema: “Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi.” Kwa umwagaji wake wa damu kwa uasi wa sheria Kaini alipaswa awe na madaraka kwa Mungu. (Mwanzo 4:6-11) Baada ya gharika ya siku za Nuhu, Mungu alitia tena mkazo kwamba uhai wa kibinadamu ni wenye thamani machoni pake. “Damu yenu ya uhai wenu nitaitaka,” ndivyo Mungu alivyosema. “Atakayemwaga damu ya mwanadamu, damu yake huyo itamwagwa na mwanadamu; maana kwa mfano wake Mungu alimfanya mwanadamu.” (Mwanzo 9:5, 6) Amri hiyo haikuchakaa kamwe. Inahusu wanadamu wote leo kama wazao wa Nuhu. Kwamba serikali za kibinadamu hushughulika na wavunja sheria kupatana na sheria hiyo ya kimungu au sivyo, Yehova atataka hesabu kwa wale ambao kwa kuasi sheria huharibu uhai.

4. Ikiwa tunataka uzima wa milele, ni lazima tuondoe nini kabisa katika maisha zetu ili tusihatirishe maisha za wengine?

4 Walakini, ili kudumu bila hatia mbele za Mpaji wa uhai, kunatakiwa zaidi. Katika 1 Yohana 3:15 imeandikwa: “Kila amehukiaye ndugu yake ni mwuaji: nanyi mnajua ya kuwa kila mwuaji hana uzima wa milele ukikaa ndani yake.” Ikiwa tunataka uzima wa milele, lazima tuondoe kabisa katika maisha zetu chuki yote kwa wanadamu wenzetu. Mungu hatawahifadhi hata kuingia katika taratibu yake mpya watu ambao, kama Kaini, hudharau onyo la kimungu na kuhatirisha maisha za wengine kwa hasira zao za hamaki. Maoni ya kimungu ya uzima yanataka kwamba tujifunze kuwapenda wanadamu wenzetu.-1 Yohana 3:11, 12; Mathayo 5:21, 22.

5. Ni moni gani ya Maandiko kuelekea kuharibu kwa mimba?

5 Ikiwa tunafuata kufikiri kwa Mungu juu ya shauri hili, tutathamini pia kwamba uhai ni mtakatifu sana haidhuru labda mtu ni mzee sana au ni mchanga sana. Neno la Mungu linaonyesha kwamba hata uhai wa kitoto ambacho bado kuzaliwa katika tumbo la uzazi la mamaye ni wenye thamani sana kwa Yehova. (Kutoka 21:22, 23; Zaburi 127:3) Lakini mamilioni ya mimba huharibiwa kila mwaka katika dunia yote. Huku kuharibu kwa mimba ni uvunjaji wa sheria ya Mungu, kwa maana mimba ya kibinadamu ndicho kiumbe chenye uhai na hakipaswi kiharibiwe. Ikiwa mume na mke waliooana wanataka wasiwe na watoto zaidi kwa sababu ya wekevu, afya au sababu nyingine, hilo ni shauri lao wenyewe, na njia ambayo katika hiyo wanafanya jambo hili zaidi ni shauri lao kutengeneza wenyewe. Lakini lazima tuka.bili jambo la kwamba mazoea ya kuharibu mimba hayaonyeshi heshima ya kimungu kwa uhai.

‘JIEPUSHENI WENYEWE NA DAMU’

6. (a) Ni nani aliye na haki kamili ya kusema ni jambo gani laweza, kufanywa na damu? (b) Wakati Mungu alipotoa ruhusa ya kula nyama ya wanyama, ni sheria gani ambayo alitoa juu ya damu?

6 Mara nyingi Biblia takatifu hutumia neno “damu” kusimama badala ya “uhai.” Hii ni kwa sababu uhai au nafsi imo katika damu. (Mambo ya Walawi 17:11) Kwa kuwa Mungu ndiye Muumba wa damu, yeye ajua zaidi juu yake kuliko ye yote wa sisi, naye ana haki kamili kusema ni jambo gani laweza kufanywa nayo. Ilikuwa kwanza baada ya Gharika ya dunia yote kwamba Mungu akawapa wanadamu ruhusa ya kula nyama ya wanyama. Hivyo wakati huo aliwapa pia sheria yake juu ya damu, akisema: “Kila kiendacho kilicho hai kitakuwa chakula chenu, kama nilivyowapa mboga za majani, kadhalika nawapeni hivi vyote. Bali nyama pamoja na uhai, yaani, damu yake, msile.” (Mwanzo 9:3, 4) Nyama ya wanyama yaweza kuliwa, lakini si damu.

7. (a) Baraza yenye kuongoza ya Wakristo wa kwanza iliandika nini juu ya damu? (b) Jinsi gani uamuzi huo huonyesha uzito wa ‘kujiepusha na damu’?

7 Baadaye, sheria hiyo ilitiwa katika amri zilizopewa kwa taifa la Israeli, na Neno la Mungu huifanya kuwa ya lazima kwa Wakristo pia. Baada ya ku-zungumza kwa ukamili matakwa ya Mungu kwa Wakristo, baraza yenye kuongoza ya kundi la kwanza la Kikristo ikawaandikia waamini wasio Wayahudi: “Roho takatifu na sisi wenyewe tumependelea tusiongeze mzigo zaidi kwenu, isipokuwa mambo haya ya lazima, mjiepushe wenyewe na vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu na kujiepusha na damu na kujiepusha na vitu vilivyonyongwa na kujiepusha na uasherati. Ikiwa mnajiepusha wenyewe kwa uangalifu na mambo haya, mtafanikiwa. Afya njema kwenu!” (Matendo 15:28, 29, NW) Hivyo, nasi, pia, lazima ‘tujiepushe na damu.’ Na kufanya kwetu hivyo ni jambo zito, likiwa limewekwa kwa usawa pamoja na kuepuka uasherati na ibada ya sanamu.

8. (a) Ikiwa mnyama hakuondolewa damu, je! ingefaa nyama yake iliwe? (b) Je! damu ichanganywe katika aina yo yote ya chakula? (c) Kwa nini damu ya kibinadamu si takatifu kidogo?

8 Ni wazi kutokana na jambo ambalo Mungu husema juu ya damu kwamba tusile nyama ya mnyama ambaye hakuondolewa damu. (Kumbukumbu la Torati 12:15, 16) Wala haitupasi kula damu yenyewe ya mnyama au kwa kuichanganya na vyakula vingine. Lakini je! ni damu ya wanyama tu ndiyo inayohusika? Bila shaka Mungu hakuwakataza wanadamu wasile damu ya wanyama huku akiwaruhusu kula damu ya kibinadamu, kana kwamba ilikuwa takatifu kidogo! Alieleza jambo hili waziwazi baadaye wakati aliposema kwa Waisraeli: “Mtu awaye yote . . . atakayekula damu, ya aina yo yote, nitakunja uso wangu juu ya mtu huyo alaye damu.”—Mambo ya Walawi 17:10.

9. Mwandikaji wa kwanza wa Kikristo alisema nini juu ya (a) sababu kwa nini wengine walikunywa damu wakati huo? (b) maoni ya Wakristo wa kwanza juu ya damu?

9 Jambo hili lilieleweka sana na Wakristo wa kwanza. Hata ijapokuwa ilisadikiwa na watu wengi kwamba kunywa damu ya binadamu mwingine kungefaidi afya ya mtu, Wakristo walijua kwamba afya njema idumuyo, ya kimwili na ya kiroho pia, ilitegemea juu ya utii kwa Mungu. Hivyo, Tertullian, mwandikaji wa Kikristo wa karne za pili na za tatu C.E., ali-sema: “Hao, pia, ambao penye maonyesho ya michezo ya kushindana, kwa sababu ya kuponya kwa kifafa, hunywa kwa kiu cha pupa damu ya wavunja sheria waliouawa kiwanjani, wakati inapotiririka moja kwa moja kutoka kwa kidonda, halafu huondoka kwa haraka—wao ni watu wa nani? . . . Mtahayarike kwa sababu ya njia zenu mbaya mbele ya Wakristo, ambao hawana hata damu ya wanyama penye mlo wa vyakula vilivyo rahisi na vya asili; wajiepushao na vitu vilivyonyongwa na vinavyojifia vyenyewe. . . . Ili kuthibitisha jambo kwa mfano mmoja, washawishi Wakristo kwa damu, kwa sababu mnajua sana kwamba jambo ambalo kwa hilo mnajaribu hivyo kuwakosesha wao huliona kuwa haramu.” Wao walielewa sheria ya Mungu kutia damu ya kila aina, damu ya wanyama na ya kibinadamu.

10. (a) Eleza kwa nini kupokea kutiwa damu katika mishipa kweli si tofauti na ‘kula.’ (b) Onyesha mfano kwamba ‘kujinyima damu’ humaanisha kutokuitia katika miili yetu hata kidogo.

10 Namna gani njia ambayo kwa hiyo damu ya kibinadamu hutumiwa leo? Madaktari wa dawa, wakijua nguvu yenye kudumisha uhai ya damu, hutumia damu bila kuzuiwa kwa kuitia katika mishipa kwa kutibu wagonjwa wao. Je! jambo hili lapatana na mapenzi ya Mungu? Labda watu wengine watafikiri kwamba kutiwa damu katika mishipa siyo ‘kula’ halisi. Lakini je! si kweli kwamba wakati mgonjwa anapokuwa hawezi kula kupitia kwa kinywa chake, madaktari mara nyingi humlisha kwa njia ile ile inayotumiwa kwa kutia damu katika mishipa? Ebu yachunguze maandiko kwa uangalifu na utaona kwamba yanatuambia ‘kujiepusha na damu’ na ‘kujinyima damu.’ (Matendo 15:20, 29, NW) Maana yake ni nini? Ikiwa daktari alikuambia ujiepushe na kileo, je! jambo hilo lingemaanisha kwamba haikupasi kukitwaa kitia kwa kinywa chako bali kwamba ungeweza kukipitisha moja kwa moja katika mishipa yako? La hasha! Hivyo, pia, ‘kujinyima damu’ kunamaanisha kutokuitia katika miili yetu hata kidogo.

11. (a) Je! ‘kujinyima damu’ huleta shida yo yote halisi juu ya watumishi wa Mungu? (b) Jambo gani hutokea kwa wagonjwa wengi ambao hupokea kutiwa damu katika mishipa? (c) Je! madaktari wanaweza kuwa hakika kwamba mtu atakufa asipopewa damu?

11 Je! jambo hili huwaweka watumishi wa Mungu katika shida kwa kulinganisha na watu ambao hudharau Biblia na hukubali kutiwa damu katika mishipa? La, haliwaletei shida halisi yo yote. Usisahau kwamba, mara baada ya kuwaambia Wakristo ‘kujiepusha wenyewe na damu,’ Andiko husema: “Ikiwa mnajiepusha wenyewe kwa uangalifu na mambo haya, mtafanikiwa. Afya njema kwenu!” (Matendo 15:29, NW) Mungu aliandikisha jambo hilo katika Biblia kwa kusudi. Yeye ajua anachosema! Yeye ajua zaidi juu ya damu kuliko wajuavyo madaktari ambao ijapokuwa huenda wawe na makusudi mazuri, jitihada zao hazifanyizi sikuzote matokeo yanayotamaniwa. (Marko 5:25-29) Jambo la hakika ni kwamba, ijapokuwa wingi wa wagonjwa huendelea kuishi baada ya kutiwa damu katika mishipa, wengi huwa wenye maradhi kama matokeo ya kutiwa damu katika mishipa na maelfu hufa kila mwaka kama matokeo ya moja kwa moja ya kutiwa damu katika mishipa. Ziko namna nyingine za utabibu usioleta madhara ya namna hiyo. Huenda daktari akamwambia mtu kwamba atakufa sasa hivi asipokubali kutiwa damu katika mishipa, lakini huenda mgonjwa afe hata ijapokuwa akubali kutiwa damu katika mishipa. Kwa upande mwingine, kama ujuavyo, wako wagonjwa wengi ambao hupona ijapokuwa mabashiri ya daktari kwa kinyume.

12. (a) Kwa nini si jambo la hekima kwa mtu kujaribu kuokoa uhai wake kwa kuvunja sheria ya Mungu? (b) Je! uhai wetu wa sasa ni wenye thamani zaidi kuliko uaminifu kwa Mungu?

12 Kwa bahati yenye shaka ya kwamba labda mtu anaweza kudumishwa hai kwa miaka michache zaidi katika taratibu hii ya mambo, je! ingekuwa akili nzuri kwa mtu kumpa Mungu kisogo kwa kuvunja sheria yake? Ikiwa tunajaribu kuokoa uhai wetu, au nafsi, kwa kuvunja sheria ya Mungu, tutaupoteza hata milele. Ndiyo sababu kwa nini Yesu alisema: “Mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona.” (Mathayo 16:25) Hivyo mwendo wa hekima sikuzote ni kuwa na tumaini katika haki ya sheria ya Mungu na imani kamili kwamba, ikiwa ni lazima Mungu aweza kutupa sisi uzima tena kwa njia ya ufufuo katika taratibu yake mpya ya mambo. (1 Wathesalonike 4:13, 14) Kwa njia hiyo tutaonyesha heshima ya kimungu kwa uhai. Hatutaona uhai wetu wa sasa kama wenye thamani zaidi kuliko uaminifu kwa Mungu. Badala yake, tutakaza macho yetu penye mpango wa Mungu wa uzima wa milele kwa wale watembeao katika njia ya kweli.

13. (a) Kuliko kwa njia ya kutia damu katika mishipa, jinsi gani peke yake wokovu unaweza kupatikana? (b) Ni jambo gani ambalo ni lazima kwetu kufanya ili kuwa bila “hatia kwa damu ya mtu awaye yote” kama mtume Paulo alivyokuwa?

13 Kama isivyokuwa kamwe kabla yake, kuna haja ya haraka kwa watu kila mahali kupata maoni ya Mungu ya uzima. Lazima wajifunze juu ya mpango ambao Yehova Mungu mwenyewe amefanya kwa kuokoa uhai. Yeye alimtuma Mwanawe Yesu Kristo kumwaga damu yake mwenyewe ya uhai kwa ajili ya wale watumiao imani, na akamfufua kutoka kwa wafu. (Waebrania 13:20, 21) Si kwa njia ya kutia damu katika mishipa bali ni kwa njia tu ya kutumia imani katika damu ya Yesu iliyomwagwa kwamba wokovu unaweza kupatikana. Tena ni jambo la haraka kupata na kutumia imani hiyo sasa kabla taratibu hii ya zamani ya mambo haijaufikia mwisho wake. Ikiwa tumejifunza juu ya mpango huu wa upendo, basi imetupasa kujiona lazima kuwaambia wengine juu yake. Huruma ya kimungu kwa ajili ya maisha za watu wengine itatuongoza kufanya kwa bidii na kwa ujasiri. (Ezekieli 3:17-21) Tukitimiza daraka hili na kuendelea nalo mpaka wote watakapopata nafasi ya kusikia, tutaweza kusema, kama vile mtume Paulo alivyosema: “Mimi sins hatia kwa damu ya mtu awaye yote. Kwa maana sikujiepusha na kuwahubiria habari ya kusudi lote la Mungu.”—Matendo 20:26, 27.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki