Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • tr sura 20 kur. 170-180
  • Kujenga Maisha ya Furaha ya Jamaa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kujenga Maisha ya Furaha ya Jamaa
  • Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UHUSIANO WA MUME NA MKE
  • KULEA WATOTO KATIKA NJIA YA KIMUNGU
  • KUTATUA MATATIZO YA JAMAA
  • Kufanikisha Maisha ya Jamaa
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Jinsi ya Kufanya Maisha ya Familia Yako Yawe Yenye Furaha
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Faida Zenye Kudumu Kutokana na Kuifuata Biblia Kama Jamaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha
    Biblia Inatufundisha Nini?
Pata Habari Zaidi
Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
tr sura 20 kur. 170-180

Sura ya 20

Kujenga Maisha ya Furaha ya Jamaa

1. Kwa nini hakuna mahali pa bora zaidi kuliko Biblia pa kupata shauri juu ya maisha ya nyumbani?

KUONGEZA kwa kutoa kweli juu ya mambo

ya mafundisho ya dini, Biblia pia hutoa mashauri mengi mazuri kuhusu maisha ya nyumbani. Inatuonyesha jinsi ya kushindana kwa kufaulu na matatizo ya maisha ya kila siku. Hapana mahali ambapo tungeweza kupata shauri bora zaidi, kwa sababu Yehova, Mtungaji wa Biblia, pia ni Yeye aliyeanzisha ndoa na akapanga maisha ya jamaa.—Mwanzo 2:18, 22.

2. (a) Jinsi gani Yesu alielekeza kwenye umoja ambao umepaswa uwepo baina ya mume na mke? (b) Jambo hili huwataka wasitawishe nini?

2 Wakati Mungu alipomleta mwanamume na mwanamke wa kwanza pamoja kama mume na mke, alikazia umoja ambao lazima uwe baina yao. Yesu Kristo alielekeza kwenye jambo hili wakati aliposema: “Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke, akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja? Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja.” (Mathayo 19:4-6) Haikuwapasa wawe wenye kushindana. Wala haikuwapasa wawe kama watu wanaojuana tu walioishi katika nyumba moja. La, iliwapasa wawe “mwili mmoja.” Hivyo, imewapasa wenzi wa ndoa wasitawishe upendo mwingi kwa mmoja na mwenzake, na kutafuta kuvutwa pamoja katika umoja wa kusudi.

UHUSIANO WA MUME NA MKE

3. (a) Jinsi gani Waefeso 5:23 inasimulia cheo cha mume? (b) Hiki maana yake ni nini?

3 Ili maisha ya ndoa yawe yenye furaha kweli kweli, wote wawili mume na mke lazima wathamini vyeo walivyo navyo mmoja mmoja. Hivi havikuwekwa tu na desturi ya kienyeji. Vimeandikwa katika Neno la Mungu mwenyewe Biblia, na vinapatana na sifa ambazo Mungu alitia katika mwanamume na mwanamke wakati wa kuumba. Akijua jinsi alivyomwumba mwanamume, na kukumbuka kusudi ambalo alikuwa nalo, Yehova aliandika katika Neno lake kwamba “mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa.” (Waefeso 5:23) Hili inamaanisha kwamba mume ndiye atachukua uongozi nyumbani, akipanga kazi za jamaa na kuchukua madaraka kwa kufanya uamuzi wa mwisho. Lakini jambo hili halimpi mamlaka ya kuwa mkali au mtawala mkatili wa jamaa yake. —Wakolosai 3:19.

4. Ni mfano mzuri wa nani ambao imewapasa waume wa Kikristo wajifunze, na kuwa na faida gani?

4 Ijapokuwa wanaume wengi wametumia hali ya kuwa kichwa katika njia isiyo ya upendo, imewapasa waume wa Kikristo waepuke njia hii. Imewapasa wajifunze kwa uangalifu jinsi Yesu Kristo ametumia hali kuwa kichwa juu ya kundi la Kikristo, kisha wafuate mfano wake mzuri. Katika Waefeso 5:25 waume wanashauriwa hivi: “Wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake.” Kwa kufanya hivyo, hawatakuwa wanadai zaidi kutoka kwa wakeze, bali wataongoza mambo ya jamaa katika njia ambayo humburudisha kila mtu ahusuye.—Mathayo 11:28-30.

5. (a) Jinsi gani imempasa mke wa Kikristo amwone mume wake? (b) Ikiwa mke ni mwenye akili zaidi kuliko mume wake, anawezaje kutumia sifa hii katika njia yenye faida? (c) Ni madaraka gani ya wanawake walioolewa yameandikwa katika Tito 2:4, 5?

5 Mke, kwa upande wake, “asikose kumstahi mumewe.” (Waefeso 5:33) Kwa kuwa mume ndiye amepewa mamlaka na Mungu kuchukua uongozi, mke aweza kusaidia sana kuleta furaha ya jamaa kwa kunyenyekea kwa nia hali yake ya kuwa kichwa. (Wakolosai 3:18) Ikiwa yeye ni mwenye akili zaidi kuliko mumewe, kama ndivyo ilivyo mara nyingine, basi anaweza kutumia sifa hii kwa kusaidia mumewe katika daraka lake kama kichwa, badala ya kushindana naye au kudharau kile anachofanya. (Mithali 12:4) Kuna mengi kwake kufanya kuhusiana na maisha ya jamaa. Kwa kufaa Biblia huwatia moyo wanawake walioolewa “wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao; na kuwa wenye kiasi, kuwa safi, kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe.” (Tito 2:4, 5) Mke na mama watoto atimizaye kazi hizi atajipatia upendo wa kudumu na heshima ya jamaa yake. —Mithali 31:10, 11, 26-28.

6. (a) Ni jambo gani ambalo waume wengine hushindwa kufikiria kwa habari ya wake zao, hivyo kuacha nafasi kwa matatizo kuzuka? (b) Hivyo I Petro 3:7 huwashauri waume kufanya nini?

6 Matatizo huzuka katika nyumba nyingi wakati mu-me anaposhindwa kufikiria tabia za wanawake, maono ya moyoni, ya mkewe. Yampasa mume athamini jambo la kwamba mwanamke huona mambo kwa jinsi nyingine. Maono yake ya moyoni yanaitikia katika njia iliyo tofauti. Nguvu za mkewe si sawa kama zake. Hivyo shauri lililoongozwa na roho ya Mungu kwa waume ni hili: “Kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima.” (1 Petro 3:7) Wakati mume anapofanya hivi, anasaidia kuleta roho ya ufahamu na usalama nyumbani.

7. (a) Jinsi gani kutumia yaliyoandikwa katika Waebrania 13:4 husaidia kuleta hali ya usalama nyumbani? (b) Ni lazima kwamba Mkristo alale tu na nani, na kwa nini?

7 Ni jambo la kawaida miongoni mwa watu wa kilimwengu kwa usalama wa nyumbani kuharibiwa kidogo kidogo kwa sababu wanaume hulala na wanawake ambao si wake zao na wanawake hulala na wanaume ambao si waume zao. Lakini wale waishio kupatana na Neno la Mungu wanalindwa na huzuni na sikitiko ambavyo mwenendo wa namna hiyo huleta. Katika msemo ambao ni rahisi kuelewa Biblia huonya hivi: “Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.” (Waebrania 13:4) Hapana ruhusa kwa mwenendo wa ufisadi. Wale wanaotaka kuwa watumishi wa Mungu lazima waishi maisha safi. (1 Wathesalonike 4:3-8) Ni lazima kwamba walale tu na wenzi wao wenyewe wa ndoa wa halali, na wana madaraka mbele za Mungu kwa kufanya hivyo. (Mithali 5:15-21) Yapasa iwe tamaa ya moyo ya wote wawili mume na mke kusaidiana mmoja na mwenzake kuepuka kishawishi cho chote kuelekea kutenda mabaya. Wanaweza kufanya hivi kwa kufikiriana mmoja na mwenzake bila choyo.—1 Wakorintho 7:3-5.

8. (a) Ili ndoa ipate kuendelea vizuri, jambo gani lazima liwe ndilo la muhimu wa kwanza katika nyumba? (b) Basi ni nini imepaswa iwe sehemu ya njia ya maisha ya jamaa?

8 Walakini, ikiwa kifungo cha ndoa kitaendelea vizuri kupatana na kanuni za kimungu ambazo tumezungumza, lazima pia pawe mkazo wa kawaida juu ya mambo ya kiroho. Ibada ya Yehova Mungu imepasa iwe ya muhimu wa kwanza katika nyumba. Haipasi iachiliwe mbali kwa kupendelea jitihada za kupata mali zaidi za kimwili au kuwa na wakati zaidi kwa kufuatia anasa. (Luka 8:11, 14, 15) Sala ya jamaa na vipindi vya kawaida vya funzo la jamaa la Biblia lazima viwe sehemu ya njia ya maisha ya kila jamaa. Je! wewe unafanya mpango wa jambo hili katika nyumba yako?

KULEA WATOTO KATIKA NJIA YA KIMUNGU

9. Matatizo katika kuwalea watoto yanawezaje kushughulikwa kwa kufaulu?1

9 Wakati watoto wanapozaliwa, ni tamaa ya moyo ya wazazi wenye upendo kuona kwamba watoto wao wanakua kuwa wanaume na wanawake wazuri. Lakini si kazi rahisi. Yako matatizo mengi ambayo huzuka katika kulea watoto. Njia ya pekee ambayo haya yanaweza kushughulikwa kwa kufaulu ni kwa kutumia shauri katika Neno la Mungu.—Mithali 22:6; Kumbukumbu la Torati 11:18-21.

10. (a) Zaidi ya chakula, mavazi na nyumba ni jambo gani la muhimu ambalo watoto wanalihitaji sana? (b) Jambo hili limepaswa litayarishwe lini?

10 Kwa desturi wakati mwingi na jitihada hutakiwa kuona kwamba kuna chakula kinachofaa, mavazi safi na nyumba iliyo nadhifu kwa kuishi ndani yake. Lakini mara kwa mara Biblia huonyesha kwamba hayo siyo madaraka peke yake kamwe ya wazazi. Ni jambo la muhimu pia kuwatia watoto kwa kawaida katika programu ya jamaa ya mafundisho katika Neno la Mungu. (Zaburi 78:5-7) Si wakati wa vipindi vya kawaida vya funzo peke yake, bali katika nyakati nyingine pia imewapasa wazazi kuzungumza na watoto wao juu ya Yehova na njia zake. (Kumbukumbu la Torati 6:6, 7) Wakati jambo hili limekwisha kufanywa, watoto hujifunza kufikiri juu ya Mungu katika uhusiano na matendo vote ya maisha.

11. Ni nani aliye na daraka kuu kuona kwamba watoto wanapewa mafundisho katika Neno la Mungu, na jinsi gani Biblia huonyesha hili?

11 Zaidi, Maandiko huweka madaraka juu ya baba kama kichwa cha jamaa, kuona kwamba mafundisho haya yanapewa. Wakati anapofanya mpango kwa mafundisho haya na wakati yeye mwenyewe huchukua uongozi katika kuyatoa, jamaa nzima huvutwa karibu pamoja zaidi. Wakati uo huo, watoto hupewa aina ya malezi ambayo wanayahitaji sana. Hivyo ni jambo la muhimu kuweka moyoni maneno yaliyoandikwa katika Waefeso 6:4: “Akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya [Yehova].”—Tazama pia Mithali 4:1.

12. Kwa nini utii kwa wazazi haupaswi uonwe kama jambo la mchezo?

12 Sehemu ya “adabu . . . ya [Yehova]” ambayo ni lazima ifundishwe hutia wajibu wa mtoto kuwa mtii kwa wazazi wake. Hili si jambo la kuona kama mchezo, kwa sababu matumaini ya mtoto kwa uzima wa milele yanatiwa ndani. (Waefeso 6:1-3) Mungu ndiye ana-yetaka watoto wawatii wazazi wao. Jambo hili huonyesha hekima kwa upande wa wazazi ikiwa kwa uvumilivu na bila ugeugeu wanakazia somo hili katika akili na mioyo ya watoto wao.—Wakolosai 3:20, 23.

13. Jinsi gani kitabu cha Biblia cha Mithali hukazia haja ya kuwarudi watoto wakati wanapofanya kwa kukusudia jambo ambalo ni mbaya?

13 Vitakuwapo vipindi wakati jambo hili litakapotaka zaidi kuliko kumwambia tu mtoto jambo lililo jema. Wakati anapofanya kwa kukusudia jambo ambalo anajua kuwa ni mbaya, tendo lenye nguvu zaidi linatakiwa ili kutia mkazo uzito wa jambo ambalo amefanya. Kwa hekima Biblia husema hivi: “Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali.” (Mithali 22:15) Kwa sababu ya kutokukamilika kulikorithiwa watoto wanazaliwa na maelekeo ya kutenda mabaya, hivyo wanahitaji kurudiwa. Mzazi mwenye upendo hataachilia mbali jambo hili. Kama Mithali 13:24 isemavyo: “Ye-ye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe; bali yeye ampendaye humrudi mapema.”

14. Adabu yapaswa itoleweje katika nyumba ya Kikristo, na kuwa na matokeo gani mema?

14 Adabu inayotumiwa katika upendo ni kwa kusudi la kutoa faida idumuyo kwa mtoto. Haifanywi katika kufoka kwa hasira ya jeuri au matisho ya kupiga kelele sana. Hiyo siyo njia ya Kikristo. (Waefeso 4:31, 32) Lazima pawe uthabiti, lakini lazima pia hekima iwepo. Imewapasa wazazi wenyewe wawe wakiweka mfano mwema, si kwa kujisingizia haki—watoto huona upesi hilo—bali kwa unyofu, unyofu wa moyo. Na ikiwa wanafanya hivyo, watoto watasaidiwa kujua kwamba kanuni za haki za Mungu huongoza nyumba, na si mawazo yasiyo ya akili au hali ya moyo ya muda. Watoto hawataogopa kwamba watakuwa wenye kupatwa na adhabu isiyo ya haki. Badala yake, wao wataunganisha adhabu na uvunjaji wa kanuni zinazofaa za mwenendo mwema.

15. (a) Ni jambo gani ambalo imewapasa watoto wafundishwe juu ya: uongo? Wivi? Uasherati? (b) Jinsi gani wazazi wanaweza kuwalea watoto wao ili watatenda yaliyo mema hata wakati wako mbali na wazazi?

15 Miongoni mwa kanuni za haki kutoka katika Biblia zinazostahili mazungumzo mazito ya jamaa ni zile zinazoshughulika na kawaida za kimungu za maa-dili. Kwa mfano, watoto lazima wafundishwe kwamba, “kila mtu apendaye uongo na kuufanya” ni chukizo kwa Yehova. (Ufunuo 22:15; Mithali 6:16-19) Wivi, pia, katika aina yake yote mbalimbali, umepaswa uonwe kama uhalifu wa kawaida ya maadili ya Mu-ngu. (Waefeso 4:28; Warumi 13:9, 10) Watoto hawa lazima waonywe katika njia ambayo wataelewa, juu ya uasherati na jambo lo lote liwezalo kuongoza kwen- ye uasherati. (Waefeso 5:5; Mithali 5:3-14) Zungum-zeni pamoja kama jamaa matatizo ya aina mbalimbali yazukayo nyumbani, shuleni na katika michezo. Fi-kirieni pamoja juu ya maandiko yaonyeshayo aina ya mwenendo unaopendeza kwa Mungu. Katika njia hii watoto watajifunza jinsi ya kutumia Biblia katika maisha zao wenyewe. Itakuwa ulinzi, hata itakuwa kwamba wakati watoto wako mbali na wazazi wao shauri ambalo wamepokea litaendelea kuwaongoza.

—Mithali 6:20-23.

16. (a) Biblia inasema nini kwa habari ya matokeo ya rafiki wabaya? (b) Basi jinsi gani wazazi wanaweza kuonyesha hekima kwa habari ya aina ya rafiki ambao watoto wao huchagua?

16 Kufikiri kwa uangalifu pia lazima kutolewe kwa uchaguzi wa rafiki. Rafiki huvuta sana maisha ya mtu. Rafiki wazuri wana matokeo mema, lakini “mashirika mabaya huharibu mazoea mema.” (1 Wakorintho 15:33, NW) Mara kwa mara habari ya Biblia huonyesha jambo hili. (Mwanzo 34:1 2; Hesabu 25:1, 2) Huenda watoto wasithamini uzito wa jambo hili, lakini imewapasa wazazi wathamini. Hivyo ni ushuhuda wa hekima kwa upande wao kukazia jicho la upendo juu ya aina ya rafiki ambao watoto wao huchagua. Rafiki hawa hutia, si wale ambao watoto hucheza nao tu, bali pia na wale ambao juu yao wanasoma na wale ambao huwatazama katika sinema na katika televisheni.—Wafilipi 4:8.

17. Jambo gani linginelo litasaidia kufanya maisha ya jamaa kuwa yenye kutosheleza kweli kweli?

17 Walakini, ili maisha ya jamaa yawe yenye kutosheleza kweli kweli, kunahitajiwa zaidi kuliko kuepuka jambo lenye kudhuru. Imepasa pia pawe furaha ya kufanya mambo mazuri pamoja kama jamaa. Furaha halisi ya maisha ya jamaa inapotea wakati kila mmoja huenda njia yake mwenyewe bila kujali wengine. Lakini wakati kuna mazungumzo yenye kujenga ya jamaa, wakati mipango inapofanywa pamoja na kila mtu hufanya kazi pamoja kwa kuitimiza, jamaa huvutwa pamoja katika umoja. (Mithali 15:22) Jambo hili si gumu wakati upendo unapokuwa katika nyumba. Na upendo ni jambo la kawaida miongoni mwa wale ambao kweli wanamjua Mungu na wana roho yake.—1 Yohana 4:7, 8; Wagalatia 5:22, 23.

KUTATUA MATATIZO YA JAMAA

18. Jinsi gani shauri katika Wakolosai 3:12-14 hutusaidia sisi kutatua matatizo yo yote ya jamaa ambayo yamkini kuzuka?

18 Hata katika nyumba ambazo kwa kawaida ni zenye furaha, huenda matatizo yakazuka mara nyingine. Haya hutokea mara nyingi kwa sababu ya kuto-kukamilika kwa kibinadamu, au mikazo ya ulimwengu ambao katika huo tunaishi. Jambo gani limepaswa kufanywa wakati kunapozuka matatizo baina ya washiriki wa jamaa? Njia ya kutatua matatizo si yenye shida sana kuipata ikiwa tunakumbuka kwamba sisi sote sio wakamilifu. Si nje ya nyumba tu bali pia katika jamaa ndimo ni lazima tutumie shauri lililoongozwa na roho ya Mungu: “Jivikeni moyo wa rehema, utu wema, unyenyekevu, upole, uvumilivu, mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; kama [Yehova] alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi. Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu.”—Wakolosai 3:12-14; tazama pia Mithali 10:12; 19:11.

19. Wakati kunapozuka ugomvi baina ya watoto, ni jambo gani ambalo mmoja wa wazazi anaweza kufanya ambalo kweli lingekuwa lenye faida?

19 Wakati tatizo linaonekana kuwa nzito sana, ziko hatua ambazo zaweza kuchukuliwa kwa kutayarisha njia kwa msamaha wa upendo. Kwa mfano, wakati ugomvi unapozuka baina ya watoto, mmoja wa wazazi anaweza kukaa kitako pamoja nao, akisikiliza tatizo, halafu kutia moyo maneno yanayofaa ya kuomba radhi na msamaha unaohitajiwa. Katika vipindi hivi maandiko kama yale ambayo tumesoma sasa hivi yangeweza kusomwa tena kwa faida.

20 Wakati kunapozuka tatizo fulani baina ya mume na mke, jambo gani halitasaidia katika kutatua shauri hili, lakini ni jambo gani litakalosaidia?

20 Wakati tatizo linapokuwa baina ya mume na mke, bila shaka afadhali lisizungumzwe mbele ya watoto. Wala hali haitatengenezeka kwa kueneza manung’uniko kwa rafiki na majirani. Ijapokuwa labda mtu amechukizwa sana, kupaza sauti hakutafanya hali ziwe nzuri zaidi hata kidogo. (Mithali 29:22) Na pengo nalo litapanuka ikiwa wawili wanakaa siku nyingi bila kuzungumza kwa mmoja na mwenzake. Jambo la Kikristo kufanya ni kuzungumza tatizo pamoja, na azimio thabiti la kurejeza amani. Hata ikiwa mtu mwingine ni mkosaji, fanya upatanisho kuwa rahisi zaidi kwa fadhili zako mwenyewe. Ikiwa wewe ndiwe mwenye kosa, omba msamaha kwa unyenyekevu. Usiahirishe; shughulika na tatizo bila kukawia. “Jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka.” —Waefeso 4:26; tazama pia Mathayo 18:21-35.

21. (a) Je! talaka ndiyo njia ya kutatua matatizo ya ndoa? (b) Biblia husema ni nini ambayo ndiyo sababu ya pekee kwa talaka imwekayo mtu huru kuoa au kuolewa mara ya pili?

21 Ijapokuwa talaka ndilo jambo la kawaida katika ulimwengu, Biblia haishauri kutaliki kama ndiyo njia ya kutatua matatizo. Ndoa ni kifungo cha maisha, na isionwe kama jambo jepesi. (Warumi 7:2) Neno la Mungu linaruhusu sababu moja tu ambayo juu yake Mkristo anaweza kupata talaka ambayo humfanya yeye huru kuoa au kuolewa mara ya pili. Ni ipi hiyo? Ni uzinifu. Ikitukia, ni juu ya yule asiye na hatia kuamua kama anataka kuomba talaka au sivyo. (Mathayo 5:32) Walakini, tendo la talaka lisichukuliwe kamwe juu ya kudhania tu; lazima pawe ushuhuda wa waziwazi.

22. Ikiwa mtu alipata talaka kwa haraka kabla ya kujifunza sheria za Mungu na ameanza kuishi pamoja na mwenzi mwingine, imempasa afanye nini ikiwa anataka kumtumikia Yehova?

22 Zamani, kabla ya kujifunza matakwa ya haki ya Mungu, huenda watu wengine wamefanya haraka kuchukua talaka, na sasa wameanza kuishi na mwenzi mwingine. Ni jambo gani wawezalo kulifanya juu yake? Hawawezi kurudi nyuma na kuanza kuishi maisha zao kwa upya. Lakini, ikiwa wanataka kuwa na shirika katika utumishi wa Yehova Mungu, na wanaishi na mwenzi, imewapasa kuhakikisha kwamba ndoa yao ya sasa imeandikishwa kwa halali kwa serikali. Inawapasa wamwendee Mungu katika sala na kutafuta msamaha wake kwa mwendo wao wa zamani. Ndipo imewapasa kufanya bidii tangu wakati huu kuendelea kuishi kupatana na matakwa ya Mungu juu ya ndoa.

23. (a) Je! Biblia inatia moyo kutaka kutengana na mwenzi asiyeamini wakati matatizo yazukapo? (b) Jinsi gani anayeamini anaweza kusahihisha hali katika nyumba, pamoja na matokeo gani yawezekanayo?

23 Namna gani ikiwa mwenzi wako wa ndoa amekataa kujifunza Neno la Mungu pamoja nawe? Tena namna gani ikiwa wewe huwezi kuzungumza matatizo pamoja naye juu ya msingi wa kanuni za Biblia? Bado Biblia inakutia moyo wewe kukaa pamoja na usione kutengana kuwa ndiyo njia iliyo rahisi ya kutoka katika matatizo yako. Fanya kwa kadiri uwezavyo mwenyewe kusahihisha hali katika nyumba yako kwa kutumia jambo ambalo Biblia inasema juu ya mwenendo wako mwenyewe. Huenda wakati fulani, kwa sababu ya mwenendo wako wa Kikristo ukamvuta mwenzi wako. (1 Wakorintho 7:10-16; 1 Petro 3:1, 2) Tena lo! itakuwa baraka yako namna gani ikiwa uvumilivu wako wa upendo unathawabishwa katika njia hii!

24. Kwa muhtasari, jinsi gani wewe waweza kujenga maisha ya jamaa yenye furaha?

24 Kuna mengi yawezayo kufanywa katika kila nyumba katika kujenga kuelekea maisha ya jamaa yenye furaha zaidi. Tumia shauri la Biblia, na yatakuwapo matokeo mema! Acheni kila mtu katika jamaa kwa upendo atafute hali njema ya wengine, hivyo kuvitia nguvu vifungo vya jamaa. (Wakolosai 3:14) Zaidi ya yote, shiriki kwa umoja katika ibada ya kweli, ili ninyi nyote pamoja mtajifurahisha baraka tele za Yehova Mungu, Yeye awezaye kuitimiliza furaha yako kwa uzima wa milele.—Mithali 3:11-18.

[Picha katika ukurasa wa 176]

Vipindi vya kawaida vya funzo la Biblia lazima viwe sehemu ya njia ya maisha ya kila jamaa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki