Sura ya 21
Uamuzi Wako Kumtumikia Mungu
1. Tuna sababu gani kwa kutoa shukrani na sifa kwa Yehova Mungu?
KUNA mengi sana ya kumshukuru na kumsifu Yehova Mungu. Kwa rehema yeye amefanya mpango kwetu kwa kujifurahisha uzima wa milele. Amekwisha kufanya mpango wa kufuta matokeo ya dhambi ambayo huleta mauti kwa kumtoa Mwanawe mwenyewe kama dhabihu ya ukombozi. Kusudi la Mungu kufurahisha milele watoto wake wa kidunia maskani ya paradiso karibu litatimizwa! Je! mpango huu wa upendo wa Mungu haufanyi moyo wako kufurika na shukrani kwake Yeye?—Yohana 3:16; 1 Yohana 4:9-11.
2. (a) Juu ya msingi wa mambo ambayo umejifunza sasa, nia yako ni nini kuelekea Yehova? (b) Ikiwa twampenda Yehova kweli kweli, tutaongozwa kufanya nini
2 Kweli, hakuna mmoja wetu ajuaye kila kitu juu ya Yehova na njia zake. Yeye ni mkubwa sana hata wanadamu watakuwa wakijifunza sikuzote mambo mapya kuhusu yeye. (Warumi 11:33) Lakini juu ya msingi wa yale ambayo umekwisba kujua, je! wewe huthamini kwamba kila kitu akifanyacho ni haki na kwamba kuna kila sababu kwa kumtumaini yeye kabisa? Je! wewe husadikishwi kwamba kweli yeye avipenda viumbe vyake, kwamba yeye ni mwenye rehema na huruma, lakini, wakati uo huo, ni mkamilifu katika haki na hekima? (Zaburi 86:5, 10, 15) Ikiwa hivi ndivyo uonavyo juu ya Yehova Mungu, utaongozwa kumtumikia Yeye, na hapana kitu kitakachokuzuia.
3. (a) Ni njia gani mbili zilizo wazi kwa watu wote? (b) Ni uchaguzi gani utakaoongoza kwenye furaha iliyo kubwa zaidi?
3 Njia mbili zi wazi kwa wanadamu wote. Moja inaongoza kwenye mauti na nyingine inaongoza kwenye uzima wa milele. (Kumbukumbu la Torati 30:19, 20) Wewe utachukua ipi? Kufanya uamuzi wa kumtumikia Yehova kutakuongoza wewe kwenye furaha iliyo kubwa zaidi iwezekanayo, sasa na hata milele. Kama mtunga zaburi alivyosema: “Heri mtu yule amchaye [Yehova], apendezwaye sana na maagizo yake.”—Zaburi 112:1.
WAKF NA UBATIZO
4. Wakati mtu anapoamua kwamba kweli anataka kufanya mapenzi ya Mungu, ni jambo gani linalofaa kwake kulifanya?
4 Wakati upendo kwa Mungu unapokuongoza hata unataka kufanya mapenzi yake, basi inafaa kwamba umwendee yeye katika sala kupitia kwa Yesu Kristo na kusema tamaa yako ya kuwa mmoja wa watumishi wake, ukitembea katika nyayo za Mwanawe. Inafaa kwamba umwambie Yehova kwamba unataka kuwa wake na kwamba unataka kufanya mapenzi yake sasa na kwa wakati wote ujao. (Zaburi 104:33) Katika njia hii unajiweka mwenyewe wakf kwa Mungu. Hili ni jambo la mtu peke yake, tena la faraghani. Hakuna mtu mwingineo awezaye kukufanyia jambo hili.
5. (a) Ukiisha kufanya wakf wake kwa Mungu, ni nini ambacho yeye anakutazamia kufanya? (b) Ni msaada gani unaopatikana kwako katika kuishi kupatana na wakf wako?
5 Ukiisha kufanya wakf wako kwa Yehova kufanya mapenzi yake, yeye atakutazamia kuutimiza. Siyo jambo jepesi. Jithibitishe mwenyewe kuwa mtu mwenye kutumainiwa kwa kushikamana kwa uaminifu na uamuzi huu au wakf kwa muda ambao utaishi. (Zaburi 50:14) Ibilisi atatumia kila njia iwezekanayo kukufanya uvunje imani na Yehova. Lakini Yehova mwenyewe atakuwa pamoja nawe. Sikuzote unaweza kugeukia kwake katika sala, naye atakutegemeza. Pia, kama vile ulivyokwisha kujifunza, Mungu analo tengenezo apa hapa duniani, na humo ndimo utakamowapata Wakristo waliokomaa watakaofurahi kukutia moyo na tegemezo kwa njia ya upendo.—1 Petro 5:8, 9; 3:12; 1 Wathesalonike 5:11.
6. Kwa nini Yesu alimwendea Yohana Mbatizaji kwenye Mto wa Yordani, na tunajifunza nini kutokana na jambo hili?
6 Kuamua wewe mwenyewe kumtumikia Yehova na kuonyesha azimio hill katika sala ni jambo la muhimu. Lakini kuna jambo fulani zaidi. Hili lilionyeshwa na Yesu Kristo, aliyetutolea sisi kiolezo cha kufuata. Kumbuka, Yesu alifanya zaidi kuliko kumwambia Baba yake kwamba yeye alikuwa amekuja kufanya mapenzi Yake. (Waebrania 10:7) Wakati alipoanza utumishi wake kama mhubiri wa ufalme wa Mungu Yesu alimwendea Yohana Mbatizaji, kwenye Mto wa Yordani, na akabatizwa majini.—Mathayo 3:13-15.
7. (a) Biblia inaonyeshaje kwamba Mungu alikubali ubatizo wa Yesu? (b) Kwa nini ubatizo ulioamriwa na Yesu si wa watoto wachanga?
7 Biblia inafunua kwamba Yehova Mungu alikubali ubatizo wa Yesu. Inasema kwamba, katika pindi hiyo ya muhimu, “mbingu ilifunuka na roho takatifu katika umbo la kimwili mfano wa njiwa ikashuka juu yake, na sauti ikatoka mbinguni: ‘wewe u Mwanangu, mpendwa; mimi nimekukubali wewe.’” (Luka 3:21, 22, NW) Kwa kuwa Yesu aliweka kiolezo, imewapasa Wakristo waliojiweka wakf siku hizi wabatizwe pia. Hasa, Yesu aliwaamuru wafuasi wake kufanya watu wa mataifa yote kuwa wanafunzi ndipo kuwabatiza wanafunzi hawa wapya. Huu sio ubatizo wa watoto wachanga. Ni ubatizo wa watu ambao wamegeuka kuwa waamini, baada ya kuamua kumtumikia Yehova. —Mathayo 28:19; Matendo 8:12.
8.Eleza maana ya ubatizo wa Kikristo.
8 Basi, ubatizo wa Kikristo unaonyesha nini? Siyo kuoshwa kwa dhambi za mtu, kwa sababu kusafishwa kwa dhambi huja kupitia kwa imani katika Yesu Kristo tu. (Waefeso 1:7) Badala yake, ni onyesho la hadhara, likishuhudia kwamba mmoja amefanya wakf mzito kwa Yehova Mungu na anajitoa mwenyewe kwake ili kufanya mapenzi Yake. Hivyo, ubatizo usionwe kama kitu kisicho na maana sana. Ni takwa kwa wote ambao kwa utii hutembea katika nyayo za Yesu Kristo.
9. (a) Kwa sababu ya njia ambayo Yesu alibatizwa, jinsi gani ubatizo wa Kikristo hutimizwa? (b) Ikiwa wewe unataka kubatizwa ni nani katika kundi imekupasa umjulishe jambo hill?
9 Biblia inasema kwamba, baada ya ubatizo wake, Yesu “akapanda kutoka majini.” Kweli alikuwa ametelemka majini hata Yohana angeweza kumzamisha kabisa. (Mathayo 3:16; Yohana 3:23) Hivyo, haikuwa ni kunyunyiziwa tu na maji. Ubatizo wa Kikristo unaofaa hutimizwa kwa kumwagiza mtumishi wa Mungu aliyejitoa—mwanamume, kama vile Yohana Mbatizaji alivyokuwa mwanamume—amzamishe kabisa mtu katika maji kisha kumwinua tena. Ikiwa wewe umeamua kumtumikia Yehova na unataka kubatizwa, basi julisha jambo hili kwa mwangalizi wa kundi la mashahidi wa Yehova unaloshirikiana nalo. Yeye atafurahi kukusaidia wewe, bila malipo yo yote kwa ubatizo.
HUDUMA YA KIKRISTO
10. (a) Ni nia gani ya Yesu ambayo imempasa Mkristo awe nayo? (b) Wakati Yesu alipokuwa hapa duniani, ni nini kilichokuwa ndiyo mapenzi ya Mungu kwake?
10 Bila shaka, wakf na ubatizo sio mwisho kwa mtu kwa kufanya mapenzi ya Mungu. Hivi ni mwanzo tu. Vinaonyesha mwanzo wa maisha ya furaha ya kumtumikia Yehova, na tumaini la kuendelea kuishi milele, kufanya mapenzi yake. Imempasa sikuzote Mkristo aliye wakf awe na nia ya Yesu Kristo, aliyesema: “Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka, nikaimalize kazi yake.” (Yo-liana 4:34) Sehemu kubwa ya kazi ya Mungu kwa Yesu duniani ilikuwa kuhubiri ufalme wa Mungu, na kuweka msingi kwa tengenezo lenye kuhubiri kuendeleza utendaji huu baada ya kufa kwake. Hayo yalikuwa ndiyo mapenzi ya Mungu kwake, na kwa uaminifu Yesu aliyafanya.—Luka 4:43; Yohana 17:4.
11. (a) Kupatana na maneno ya Yesu katika Mathayo 24:14, ni nini yaliyo mapenzi ya Mungu kwa Wakristo leo? (b) Kwa nini kazi hii ni ya haraka?
11 Ni nini yaliyo mapenzi ya Mungu kwa Wakristo leo? Kwao ni kufanya kazi ile ile ya kuhubiri, yenye haraka kubwa. Unabii wa Biblia hufunua pasipo shaka kwamba sisi tunaishi sasa wakati wa “mwisho wa taratibu ya mambo.” Na Yesu alihubiri juu ya wakati huu: “Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa yote; na hapo ndipo ule mwisho utakapokuja.” (Mathayo 24:3, 14, NW) Ni mapenzi ya Mungu kwamba kazi hii ya kuhubiri ifanywe sasa. Onyo kuhusu mwisho wa taratibu hii mbovu lazima litolewe. Watu wapole lazima waonyeshwe mahali pa salama. Je! wewe utashiriki katika kazi hii?—Sefania 2:2, 3; Mithali 24:11, 12.
12. (a) Kazi ya kuhubiri inafanywaje? (b) Je! amri ya Yesu ‘kufanya wanafunzi’ inahusu Wakristo wote?
12 Yesu Kristo aliweka mfano katika kufanya huduma. Yeye alihubiri kila mahali, katika miji na vijiji, katika nyumba na katika mahali pa hadhara—hata kwa mwanamke kando ya kisima cha maji. (Yohana 4:7, 21-24) Mkristo wa kweli leo ataufuata mfano wa Yesu. Yeye atahubiri kwa kila nafasi. Yeye hatangojea watu waje kwake, bali atajitahidi kuwatafuta watu wenye kusikiliza. “Enendeni,” Yesu akaamuru, “mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi.” (Mathayo 28:19; tazama pia 10:11-13.) Amri hii inahusu Wakristo wote—vibarua na wake wa nyumbani, watu wazee na vijana—hata kama ilivyowahusu katika karne ya kwanza.—Matendo 4:13; Warumi 16:1.
13. Ni wapi ambapo kazi nyingi ya kuhubiri inapofanywa?
13 Wakristo wa kwanza walifuata agizo na mfano wa Yesu, wakifanya jitihada ya pekee ya kuzuru watu katika nyumba zao. (Luka 8:1; 10:1-6; Matendo 5:42) Mtume Paulo alisema: “Sikujiepusha katika kuwatangazia neno lo lote liwezalo kuwafaa, bali naliwafundisha waziwazi, na nyumba kwa nyumba.” (Matendo 20:20) Hii ingali ndiyo njia kubwa ambayo Wakristo wa kweli huendesha huduma yao katika wakati wetu.
14. Mungu hutusaidlaje sisi katika huduma?
14 Wale washirikio katika kazi hii ya maana hawafanyi hivyo kwa nguvu zao wenyewe. Yehova Mungu ndiye awasaidiaye. Kwa njia ya roho yake yeye huwastahilisha na kuwatia nguvu kwa huduma. (2 Wakorintho 3:5, 6; 2 Timotheo 4:17) Kupitia kwa tengenezo lake lionekanalo yeye hutayarisha mazoezi na msaada, pasipo gharama yo yote ya fedha, kwa mashahidi wake wote. Wewe, pia, waweza kujifurahisha faida za mpango huu, penye Jumba la Ufalme la mahali penu.
15. Wakati mtu aamuapo kumtumikia Mungu, ni baraka gani tele ambazo amewekewa akiba?
15 Wakati unapofanya uamuzi wa moyo wote kumtumikia Yehova Mungu, utapata baraka nyingi. Furaha ambayo umekuwa nayo katika kujifunza kweli juu ya Yehova na kusudi lake itakuzwa sana kadiri utakavyoishiriki na wengine na kuona mabadiliko mazuri ambayo inaleta katika maisha zao. (Matendo 20:35; Yohana 13:7) Kadiri utakavyolitumia zaidi sana Neno la Mungu katika maisha yako mwenyewe utavutwa karibu zaidi na Muumba wako. Utajifurahisha ulinzi wake wa upendo katika njia ambazo hujazipata kamwe kabla yake. (Ufunuo 7:9-17) Kweli, mwendo wako utaufurahisha moyo wa Mungu mwenyewe. (Mithali 27:11) Tena zitakuwa furaha zako namna gani wakati utakapoona utimizo wa maneno ya mtunga zaburi: “Wenye furaha ni watu ambao Mungu wao ni Yehova!”—Zaburi 144:15, NW,