Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • pe sura 30 kur. 250-255
  • Mambo Ambayo Lazima Ufanye Ili Uishi Milele

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mambo Ambayo Lazima Ufanye Ili Uishi Milele
  • Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • WAKF NA UBATIZO
  • MAPENZI ANAYOKUTAKA MUNGU UFANYE LEO
  • CHAGUA UZIMA WA MILELE KATIKA PARADISO DUNIANI
  • Uamuzi Wako Kumtumikia Mungu
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Kufanye Kumtumikia Mungu Milele Kuwe Lengo Lako
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • Je, Ninapaswa Kujiweka Wakfu kwa Mungu na Kubatizwa?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Ubatizo na Uhusiano Wako Pamoja na Mungu
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
Pata Habari Zaidi
Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
pe sura 30 kur. 250-255

Sura 30

Mambo Ambayo Lazima Ufanye Ili Uishi Milele

1. (a) Ni miendo gani miwili iliyo wazi kwako? (b) Unawezaje kuuchagua mwendo unaofaa?

YEHOVA MUNGU anakutolea wewe jambo zuri ajabu—uzima wa milele katika mfumo (taratibu) wake mpya wa mambo yenye uadilifu. (2 Petro 3:13) Lakini kuishi wakati huo kunategemea kufanya kwako mapenzi ya Mungu sasa. Ulimwengu mwovu wa sasa, pamoja na wote wanaoendelea kuwa sehemu yake, u karibu kutoweka, “lakini yeye anayefanya mapenzi ya Mungu anadumu milele.” (1 Yohana 2:17, NW) Hivyo ni lazima uchague ka-ti ya miendo miwili. Mmoja unaongoza kwenye kifo na mwingine kwenye uzima wa milele. (Kumbukumbu la Torati 30:19, 20) Ni mwendo upi ambao utachukua?

2. (a) Ukiwa na imani ya kweli, utasadikishwa juu ya nini? (b) Kumtumaini Mungu kama mtoto anavyomtumaini baba mwenye upendo kutakusaidiaje umtumikie yeye?

2 Unaonyeshaje kwamba unachagua uzima? Kwanza, lazima uamini Yehova na ahadi zake. Je! unasadikishwa kabisa kwamba Mungu yuko “na ya kwamba yeye anakuwa mthawabishaji wa wale wanaomtafuta kwa bidii”? (Waebrania 11:6, NW) Unahitaji kumtumaini Mungu kama vile mwana au binti anavyomtumaini baba mwenye upendo na mwenye rehema. (Zaburi 103:13, 14; Mithali 3:11, 12) Ukiwa na imani hiyo, hutakuwa na shaka kwamba shauri lake ni lenye hekima au kwamba njia zake zinafaa, hata iwapo nyakati nyingine hufahamu sana mambo yalivyo.

3. (a) Zaidi ya imani, ni jambo gani jingine linalohitajiwa? (b) Ni kazi gani zinazohitajiwa ili kuonyesha kwamba unachagua uzima?

3 Walakini, kuna mengi yanayohitajiwa kuliko imani tu. Vilevile ni lazima kuweko kazi za kuonyesha maoni yako ya kweli yalivyo juu ya Yehova. (Yakobo 2:20, 26) Je! wewe umefanya mambo yanayoonyesha kwamba unasikitika kwa kushindwa kufanya yaliyo mema hapo zamani? Je! moyo wako umekuongoza utubu au ufanye mabadiliko ili upatanishe mwendo wako wa maisha na mapenzi ya Yehova? Je! umegeuka, yaani, umekataa mwendo wo wote mbaya ambao huenda umekuwa ukiufuata, na je! umeanza kufanya mambo yale ambayo Mungu anataka? (Matendo 3:19; 17:30) Kazi za namna hiyo zitaonyesha kwamba weave unachagua uzima.

WAKF NA UBATIZO

4. (a) Ni jambo gani limepasa likuongoze ufanye mapenzi ya Mungu? (b) Unapoamua unataka kumtumikia Mungu, ni jambo gani linalofaa ulifanye?

4 Ni nini kinachopasa kikuongoze uchague uzima kwa kufanya mapenzi ya Mungu? Ni kuthamini. Ebu fikiri: Yehova amekupangia uweze kupata ondoleo la magonjwa yote, mateso yote, na hata kifo! Kwa zawadi yenye thamani sana ya kutoa Mwanaye amekufungulia njia inayoongoza kwenye uzima usio na mwisho katika dunia-paradiso. (1 Wakorintho 6:19, 20; 7:23; Yohana 3:16) Upendo wa Mungu unapokuongoza umpende yeye naye, imekupasa ufanye nini? (1 Yohana 4:9, 10; 5:2, 3) Imekupasa umfikie Mungu kwa jina la Yesu umwambie katika sala kwamba unataka uwe mtumishi wake, kwamba unataka uwe mali yake. Kwa njia hiyo unajiweka wakf kwa Mungu. Jambo hilo ni la kibinafsi, la faragha. Hakuna mwingine anayeweza kukufanyia hivyo.

5. (a) Ukiisha kujiweka wakf kwa Mungu, yeye anakutazamia ufanye nini? (b) Ni msaada gani unaoweza kujipatia ili utimize wakf wako?

5 Ukiisha kujiweka wakf kwa Mungu, yeye atakutazamia uutimize wakf huo. Hivyo jionyeshe kuwa mtu anayetimiza anayosema kwa kushikamana na uamuzi huo, au wakf huo, maadamu unaishi. (Zaburi 50:14) Ukiendelea kuwa karibu sana na tengenezo la Mungu linaloonekana, unaweza kusaidiwa na Wakristo wenzako watakaofurahia kukupa kipa-moyo na kukuunga mkono kwa upendo.—1 Wathesalonike 5:11.

6. (a) Unapoweka maisha yako wakf kwa Mungu, ndipo hatua gani inakuwa ya lazima? (b) Ubatizo una maana gani?

6 Walakini, ni lazima ufanye mengi zaidi ya kumwambia Yehova kwa faragha kwamba unataka uwe mali yake. Unahitaji uonyeshe mbele ya wengine kwamba umejiweka wakf umtumikie Mungu. Utafanyaje hivyo? Ni kwa kubatizwa katika maji. Ubatizo huo wa maji ni wonyesho wa waziwazi kwamba mtu ameweka maisha yake wakf kwa Yehova na anajitokeza ili afanye mapenzi Yake.

7. (a) Ni mfano gani ambao Yesu aliwekea Wakristo? (b) Kwa sababu gani ubatizo ambao Yesu aliamuru si wa vitoto vichanga?

7 Kwamba ubatizo wa maji ni takwa la maana inaonyeshwa na mfano wa Yesu Kristo. Yesu hakumwambia Baba yake kwamba alikuwa amekuja kufanya mapenzi Yake, na basi. (Waebrania 10:7) Alipokuwa akikaribia kuanza utumishi wake wa kuwa mhubiri wa ufalme wa Mungu, Yesu alijitokeza kwa Yehova akabatizwa katika maji. (Mathayo 3:13-17) Kwa kuwa Yesu aliweka kielelezo, wale leo wanaojiweka wakf kwa Yehova wafanye mapenzi yake imewapasa wabatizwe. (1 Petro 2:21; 3:21) Kwa kweli, Yesu aliamuru wafuasi wake wafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote kisha wawabatize wanafunzi hao wapya. Huo si ubatizo wa vitoto vichanga. Ni ubatizo wa watu ambao wamekuwa waamini, wamekwisha kuamua kumtumikia Yehova.—Mathayo 28:19; Matendo 8:12.

8. Ukitaka kubatizwa, ni nani katika kundi ambaye imekupasa ujulishe hilo, na kwa sababu gani?

8 Ikiwa umekwisha kuamua kumtumikia Yehova na unataka ubatizwe, imekupasa ufanye nini? Imekupasa ujulishe tamaa yako kwa mwangalizi-msimamizi wa kundi la Mashahidi wa Yehova unaloshirikiana nalo. Yeye, pamoja na wazee wengine katika kundi, watafurahia kurudia pamoja nawe taarifa unayohitaji kujua ili umtumikie Mungu kwa njia inayokubalika. Ndipo mpango unapoweza kufanywa ubatizwe.

MAPENZI ANAYOKUTAKA MUNGU UFANYE LEO

9. Noa alifanya jambo gani kabla ya gharika ambalo Mungu anakutaka ufanye sasa?

9 Kabla ya gharika, Yehova alimtumia Noa, “mhubiri wa uadilifu,” atoe onyo juu ya uharibifu uliokuwa ukija na kuelekeza watu kwenye mahali pa pekee pa usalama, kwenye safina. (Mathayo 24:37-39; 2 Petro 2:5, NW; Waebrania 11:7) Mapenzi ya Mungu ni kwamba sasa wewe ufanye kazi ya kuhubiri inayofanana na hiyo. Yesu alitabiri juu ya wakati wetu hivi: “Na habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.” (Mathayo 24:14, NW) Inawapasa wengine wajue mambo ambayo umejifunza juu ya makusudi ya Mungu ikiwa watauokoka mwisho wa mfumo (taratibu) huu na kuishi milele. (Yohana 17:3) Je! moyo wako hauongozwi ili ushiriki pamoja na wengine maarifa kayo yenye kutoa uzima?

10. (a) Ni mfano gani wa Yesu ambao kupenda watu kumepasa kutuongoze sisi tuufuate? (b) Sehemu kubwa ya kazi ya kuhubiri inafanywaje?

10 Fuata mfano wa Kristo. Yeye hakungoja watu waje kwake, bali yeye alikwenda kutafuta wale ambao wangesikiliza ujumbe wa Ufalme. Naye akawaagiza wafuasi wake—tena wote—wafanye ivyo hivyo. (Mathayo 28:19; Matendo 4:13; Warumi 10:10-15) Kwa kufuata agizo na mfano wa Kristo, Wakristo wa kwanza walifikia watu katika nyumba zao. Walikwenda “nyumba kwa nyumba” wakiwa na ujumbe wa Ufalme. (Luka 10:1-6; Matendo 20:20) Hiyo ingali ndiyo njia kuu ambayo Wakristo wa kweli wanatimiza huduma yao katika wakati wetu.

11. (a) Ni kwa sababu gani uhodari unatakwa ili kuweza kuhubiri juu ya ufalme wa Mungu, lakini kwa sababu gani si lazima tuogope? (b) Yehova anaionaje kazi tunayofanya?

11 Uhodari unatakwa ili kuweza kufanya kazi hiyo. Bila shaka Shetani na ulimwengu wake watajaribu kukuzuia, kama walivyojaribu kuzuia wafuasi wa kwanza wa Kristo wasihubiri. (Matendo 4:17-21; 5:27-29, 40-42) Lakini si lazima uogope. Kama vile Yehova alivyotegemeza na kutia nguvu Wakristo hao wa kwanza, atafanya vivyo hivyo kwako leo. (2 Timotheo 4:17) Basi uwe hodari! Onyesha kwamba kweli unampenda Yehova na unapenda wanadamu wenzako kwa kushiriki kikamili katika kazi ya kuokoa uhai ya kuhubiri na kufundisha. (1 Wakorintho 9:16; 1 Timotheo 4:16) Yehova hatasahau kazi yako, bali atakupa thawabu kwa wingi.—Waebrania 6:10-12; Tito 1:2.

12. Tunaweza kujifunza nini kwa mfano wa mke wa Loti?

12 Hakuna jambo bora sana ambalo mfumo (taratibu) huu wa kale unaweza kutoa, hivyo usifikiri hata kidogo kwamba unakosa jambo fulani kwa kuuacha. “Kumbukeni yaliyompata mke wa Loti,” Yesu alisema. (Luka 17:32, HNWW) Yeye pamoja na jamaa yake walipokwisha kukimbia kutoka Sodoma, alitazama kwa kuvitamani vitu walivyokuwa wameacha nyuma. Mungu alijua moyo wake ulikokuwa, naye akageuka kuwa nguzo ya chumvi. (Mwanzo 19:26) Usiwe kama mke wa Loti! Kaza macho yako juu ya mambo yaliyoko mbele, juu ya “uzima ulio kweli kweli” katika taratibu mpya ya Mungu yenye uadilifu.—1 Timotheo 6:19.

CHAGUA UZIMA WA MILELE KATIKA PARADISO DUNIANI

13. Yesu alionyeshaje lile chaguo ambalo ni lazima sote tulifanye?

13 Kweli kweli, kuna mambo mawili ya kuchagua. Kristo aliyalinganisha na uchaguzi wa mojayapo ya njia mbili. Njia moja, alisema, ni “pana.” Katika njia hiyo wasafiri wanaruhusiwa uhuru wa kujipendeza wenyewe. Walakini, ile njia nyingine “imesonga.” Ndiyo, wale walio katika njia hiyo wanatakwa watii maagizo na sheria za Mungu. Wale walio wengi, Yesu alisema, wanasafiri katika ile njia pana, na wachache tu katika njia iliyosonga. Ni njia gani ambayo wewe utachagua? Katika kufanya chaguo lako, kumbuka hili: Njia ile iliyo pana itafikia ghafula mwisho wake—uharibifu! Kwa upande mwingine, ile njia iliyosonga itakuongoza moja kwa moja kuingia katika mfumo (taratibu) mpya wa Mungu. Na humo utaweza kushiriki kuifanya dunia kuwa paradiso yenye utukufu, ambamo utaweza kuishi milele katika furaha.—Mathayo 7:13, 14.

14. Ni lazima uwe sehemu ya nini ili uokoke na kuingia katika mfumo (taratibu) mpya wa Mungu?

14 Usikate shauri kwamba kuna barabara au njia mbalimbali unazoweza kufuata ili upate uzima katika mfumo mpya wa Mungu. Kuna moja tu. Kulikuwako safina moja tu iliyookoka ile Gharika, si mashua nyingi. Na kutakuwako tengenezo moja tu—tengenezo la Mungu linaloonekana—litakalookoka ile “dhiki kubwa” inayokaribia haraka. Si kweli hata kidogo kwamba dini zote zinaongoza kwenye mradi mmoja. (Mathayo 7:21-23; 24:21) Ni lazima uwe sehemu ya tengenezo la Yehova, uwe ukifanya mapenzi ya Mungu, ili upokee baraka yake ya uzima wa milele.—Zaburi 133:1-3.

15. (a) Tunahitaji kufanya nini kila siku? (b) Ni tumaini gani ambalo si ndoto tu?

15 Kwa hiyo iweke waziwazi katika akili na moyo wako picha hiyo ya mfumo mpya wa mambo wa Mungu ulioahidiwa. Kila siku ifikirie ile zawadi ambayo Yehova Mungu anakutolea—kuishi milele katika Paradiso duniani. Hiyo si ndoto tu. Ni jambo halisi! Kwa maana ahadi hii ya Biblia itatimizwa hakika: “Waadilifu wenyewe wataimiliki dunia, nao watakaa milele juu yake. . . . Wale waovu watakapokatiliwa mbali, wewe utaona.”—Zaburi 37:29, 34, NW.

[Picha katika ukurasa wa 251]

Jiweke wakf kwa Yehova na kubatizwa

[Picha katika ukurasa wa 253]

“Kumbukeni yaliyompata mke wa Loti”

[Picha katika ukurasa wa 254]

Endelea kuiweka picha ya mfumo (taratibu) mpya wa Mungu iwe waziwazi katika akili na moyo wako

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki