Sura ya 2
Barua Kutoka kwa Mungu
NIAMBIE, kitabu gani wakipenda zaidi kuliko vyote? Watoto wengine wangechagua kile kinachosimulia wanyama. Wengine wangechagua kitabu chenye picha nyingi. Inaweza kufurahisha kusoma vitabu hivyo.
Lakini vitabu bora katika ulimwengu wote ni vile vinavyotuambia kweli juu ya Mungu. Na kimoja cha vitabu hivyo kina faida zaidi kuliko vingine vyote. Unakijua ni kitabu gani?— Ni Biblia.
Kwa sababu gani Biblia ni ya maana sana?— Kwa sababu ilitoka kwa Mungu. Inatuambia juu yake na juu ya mambo mazuri ambayo atatufanyia sisi. Nayo inatuonyesha jambo la kufanya ili tumpendeze yeye. Ni kama barua kutoka kwa Mungu.
Sasa, Mungu angaliweza kuandika Biblia nzima mbinguni kisha ampe mwanadamu. Lakini hakufanya hivyo. Mawazo yalitoka kwa Mungu. Lakini aliwatumia watumishi wake duniani waandike karibu yote.
Alifanya hivyo namna gani?— Mfano waweza kutusaidia tufahamu. Watu wanaposikia sauti katika radio inatoka kwa mtu fulani mbali. Hawawezi kumwona, lakini wanaweza kusikia anayosema, sivyo?
Wanadamu wanaweza hata kufika kwenye mwezi katika roketi zao, nao wanaweza kupe-leka habari kutoka huko kuirudisha duniani. Ulijua hilo?— Ikiwa wanadamu wanaweza kufanya hivyo, je! Mungu anaweza kupeleka habari kutoka mbinguni?— Ndiyo anaweza! Naye alifanya zamani mbele ya wanadamu kuwa na radio na televisheni.
Musa ndiye mtu ambaye Mungu alisema naye. Musa hakuweza kumwona Mungu, bali aliweza kusikia sauti. Mamilioni ya watu walikuwako wakati hili lilipotukia. Waliona wakati Mungu alipotetemesha mlima wote, na kulikuwako ngurumo na umeme. Walisikia wakati sauti ilipotoka mbinguni. Walijua Mungu alikuwa amesema. Kisha Mungu akasema tena kwa Musa, naye Musa akaandika mambo ambayo Mungu alisema. Aliyoandika yamo katika Biblia.—Kutoka 19:3-20:21.
Hakuwa Musa peke yake aliyeandika. Mungu alitumia karibu watu 40 kuandika sehemu za Biblia. Waliandika mambo ambayo Mungu angefanya wakati ujao. Walijua mambo hayo namna gani hata mbele ya kutukia?— Mungu alikuwa amesema nao.
Wakati Yesu, Mwalimu Mkuu, alipokuwa duniani, sehemu kubwa ya Biblia ilikuwa imeandikwa. Sasa, kumbuka, Mwalimu Mkuu alikuwa amekuwa mbinguni. Alijua jambo ambalo Mungu alikuwa amefanya. Je! yeye aliamini Biblia ilitoka kwa Mungu? — Ndiyo.
Wakati Yesu aliposema na watu juu ya kazi za Mungu, alisoma katika Biblia. Mara nyingine aliwaambia mambo ambayo Biblia ilisema kwa kukumbuka moyoni.
Yesu tena alituletea habari zaidi kutoka kwa Mungu. Alisema: ‘Mambo niliyosikia kutoka kwa Mungu ninayasema katika ulimwengu.’ Yesu alikuwa amesikia mengi kutoka kwa Mungu kwa sababu alikuwa ameishi na Mungu. Na twaweza kuyasoma wapi mambo hayo aliyosema Yesu?— Katika Biblia. Yote yaliandikwa tusome sisi.—Yohana 8:26.
Ndiyo, Mungu alipotumia wanadamu waandike, waliandika katika lugha ambayo walitumia kila siku. Basi sehemu ya Biblia iliandikwa katika Kiebrania, nyingine katika Kiaramu, na sehemu kubwa katika Kigiriki. Watu zaidi leo hawajui kuzisoma lugha hizo. Wewe wajua?—
Ndiyo sababu Biblia imenakiliwa katika lugha nyingine. Leo ziko sehemu za Biblia katika lugha zaidi ya 1,400. Ebu fikiri! Biblia ni barua ya Mungu kwa watu kila mahali. Hivyo yapaswa iwe katika lugha nyingi. Lakini si kitu imenakiliwa mara ngapi, habari ni ya kutoka kwa Mungu.
Mambo ambayo Biblia inasema ni ya maana kwetu. lliandikwa zamani. Lakini inatuambia juu ya mambo ya-nayotukia leo. Tena inatuambia mambo ambayo Mungu atafanya wakati ujao ulio karibu. Mambo ambayo inasema ni yenye kufurahisha! Yanatupa sisi tumaini la ajabu.
Tena Biblia inatuambia namna Mungu anavyotaka tuishi. Inatuambia yaliyo mema na yaliyo mabaya. Ni lazima wewe na mimi tujue haya. Inatuambia juu ya watu waliofanya mabaya, na yaliyowapata. Hivyo twaweza kuepuka taabu iliyowapata. Tena inatuambia juu ya watu waliofanya mema, na matokeo mazuri yaliyowapata. Yote yaliandikwa kwa faida yetu.
Lakini ili kufaidika na Biblia, lazima tujue jibu la ulizo. Ulizo ni hili: “Nani aliyetupa Biblia?” Wewe ungesema namna gani? Ndiyo, yote ni ya kutoka kwa Mungu.
Lakini watu wengine hawasikilizi mambo ambayo Mungu anasema katika Biblia. Wao wanaishi namna wanavyotaka. Unafikiri ni vizuri?— Unafikiri ye yote anajua zaidi kuliko Mungu?— Njia ambayo tunaweza kuonyesha kwamba sisi ni wenye hekima kweli kweli ni kumsikiliza Mungu. Halafu yatupasa tufanye anayosema.
Basi lazima tupate nafasi ya kusoma Biblia pamoja. Wakati tunapopata barua kutoka kwa fulani tunayempenda sana sana, tunarudia kuisoma. Ina faida kwetu. Ndivyo Biblia imepaswa iwe kwetu, kwa sababu ni barua kutoka kwa Yeye atupendaye zaidi sana. Ni barua kutoka kwa Mungu.
(Tumia dakika chache zaidi sasa msome maandiko haya yanayoonyesha Biblia kuwa kweli Nano la Mungu, lililoandikwa kwa faida yetu: 2 Timotheo 3:16, 17; 2 Petro 1:20, 21; Warumi 15:4)