Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • rq somo la 1 uku. 3
  • Jinsi Unavyoweza Kujua Yale Ambayo Mungu Anataka

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi Unavyoweza Kujua Yale Ambayo Mungu Anataka
  • Mungu Anataka Tufanye Nini?
  • Habari Zinazolingana
  • Biblia Ni Ujumbe Kutoka kwa Mungu
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Je, Kweli Habari Njema Imetoka kwa Mungu?
    Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
  • Kwa Nini Ujifunze Kutoka kwa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Barua Kutoka Kwa Mungu Mwenye Upendo
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
Pata Habari Zaidi
Mungu Anataka Tufanye Nini?
rq somo la 1 uku. 3

Somo la 1

Jinsi Unavyoweza Kujua Yale Ambayo Mungu Anataka

Ni habari gani ya maana iliyomo katika Biblia? (1)

Mtungaji wa Biblia ni nani? (2)

Kwa nini ujifunze Biblia? (3)

1. Biblia ni zawadi yenye thamani sana kutoka kwa Mungu. Ni kama barua kutoka kwa baba mwenye upendo kwa watoto wake. Hiyo hutuambia kweli kumhusu Mungu—yeye ni nani na viwango vyake ni nini. Hueleza jinsi ya kukabiliana na matatizo na jinsi ya kupata furaha ya kweli. Biblia pekee hutuambia kile ambacho ni lazima tufanye ili kumpendeza Mungu.—Zaburi 1:1-3; Isaya 48:17, 18.

2. Biblia iliandikwa na watu tofauti-tofauti wapatao 40 kwa kipindi cha miaka 1,600, kuanzia 1513 K.W.K. Imefanyizwa kwa vitabu vidogo 66. Wale walioandika Biblia walipuliziwa na Mungu. Waliandika mawazo yake, si yao wenyewe. Kwa hiyo Mungu aliye mbinguni ndiye Mtungaji wa Biblia, si binadamu yeyote duniani.—2 Timotheo 3:16, 17; 2 Petro 1:20, 21.

3. Mungu alihakikisha kwamba Biblia ilinakiliwa kwa usahihi na kuhifadhiwa. Biblia zaidi zimechapwa kuliko kitabu kingine chochote. Si kila mtu atakayefurahi kukuona ukijifunza Biblia, lakini usiruhusu hilo likuzuie. Wakati ujao wako wa milele wategemea kupata kwako kumjua Mungu na kufanya mapenzi yake ujapokuwa upinzani wowote.—Mathayo 5:10-12; Yohana 17:3.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki