Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • te sura 4 kur. 19-22
  • Mungu Ana Jina

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mungu Ana Jina
  • Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
  • Habari Zinazolingana
  • Mungu Ana Jina
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
  • Mungu Anataka Jina Lake Lijulikane
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Liheshimu Jina Kuu La Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Kwa Nini Ni Lazima Tujue Jina la Mungu
    Jina la Mungu Litakaloendelea Milele
Pata Habari Zaidi
Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
te sura 4 kur. 19-22

Sura ya 4

Mungu Ana Jina

JINA lako nani?— Wewe una jina. Mimi vile vile. Mwanamume wa kwanza duniani alikuwa na jina. Mungu alimwita Adamu. Mwanamke wa kwanza aliitwa Hawa. Kila mwanamume, mwanamke na mtoto ana jina.

Zitazame nyota nyingi mno usiku. Unafikiri zina majina?— Ndiyo, Mungu aliipa kila nyota katika anga jina. Biblia inatuambia: “Huihesabu idadi ya nyota, huzipa zote majina.”—Zaburi 147:4.

Watu na nyota wote wana majina. Basi wafikiri Mungu ana jina?— Mwalimu Mkuu alisema analo. Siku moja alisema kwa Mungu katika sala: ‘Nimewajulisha wafuasi wangu jina lako.’—Yohana 17:26.

Unajua jina la Mungu?— Mungu mwenyewe anatuambia ni jina gani. Anasema: “Mimi ni Yehova. Ndilo jina langu.” Basi jina la Mungu ni YEHOVA.—Isaya 42:8, NW.

Unapenda wakati wengine wanapokumbuka lino lako?— Watu wanapenda waitwe kwa jina lao. Naye Yehova anataka watu wajue jina lake vile vile. Basi imetupasa tutumie jina Yehova wakati tunapozungumza juu ya Mungu.

Mwalimu Mkuu alitumia jina la Mungu Yehova wakati aliposema na watu. Wakati mmoja alisema: “Yakupasa umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote.”—Marko 12:30,NW.

Yesu alijua “Yehova” ni jina la maana sana. Basi akawafundisha wafuasi wake kutumia jina la Mungu. Hata akawafundisha kusema juu ya jina la Mungu katika maombi yao.

Hapo zamani Mungu alionyesha maana ya jina lake kwa mwanadamu Musa. Musa alikuwa mmoja wa wana wa Israeli. Wana wa Israeli waliishi katika nchi inayoitwa Misri. Wamisri waliwafanya wana wa Israeli watumwa na walikuwa wakali sana kwao. Wakati Musa alipokua, alijaribu kumsaidia mmoja wa watu wake. Hii ilimkasirisha mfalme wa Misri. Akataka kumwua Musa! Basi Musa alitoroka kutoka Misri.

Musa alikwenda nchi nyingine. Ilikuwa nchi ya Midiani. Akafanya kazi kama mchungaji huko, akichunga kondoo. Siku moja aliona ajabu. Lo! mti mdogo ulikuwa unawaka moto, lakini haukuteketea! Musa akakaribia zaidi atazame vizuri zaidi.

Unajua kulitukia nini?— Musa akasikia sauti kutoka katikati ya huo mti mdogo unaowaka moto. Ile sauti ikaita, “Musa! Musa!”

Nani alikuwa akisema hivyo— Ni Mungu alikuwa akisema! Mungu alikuwa na kazi kubwa kwa Musa kufanya. Mungu akasema: ‘Njoo nikutume kwa Farao, mfalme wa Misri, ukawatoe watu wangu wana wa Israeli katika Misri.’ Mungu akaahidi kumsaidia Musa.

Lakini Musa akamwambia Mungu: ‘Je! nikifika kwa wana wa Israeli katika Misri na kuwaambia Mungu amenituma, wakiniuliza, Jina lake nani? Nitasemaje?’ Mungu akamwambia Musa awaambie wana wa Israeli hivi: ‘Yehova amenituma kwenu. Yehova ndilo jina langu milele.’—Kutoka 3:1-15, NW.

Hii inaonyesha Mungu alitaka kushika jina Yehova. Mungu alitaka ajulikane milele kwa jina Yehova.

Musa akarudi Misri. Wamisri huko kweli hawakumjua Yehova. Wao walifikiri alikuwa mungu mdogo tu wa wana wa Israeli. Wamisri hawakufikiri Yehova alikuwa Mungu wa dunia nzima. Basi Yehova akamwambia mfalme wa Misri: ‘Mimi nitajulisha jina langu katika dunia yote.’—Kutoka 9:16.

Yehova alijulisha jina lake katika dunia yote. Alimtumia Musa awatoe wana wa Israeli katika Misri. Na watu katika dunia yote wakasikia upesi juu ya Yehova.

Leo watu wengi ni kama Wamisri hao. Hawaamini kwamba Yehova ndiye Mungu wa dunia nzima. Basi Yehova anataka watu wake wawaambie wengine juu yake. Hivi ndivyo Yesu alifanya.

Je! wataka uwe kama Yesu?— Basi waambie wengine kwamba jina la Mungu ni Yehova. Utaona watu wengi hawajui hilo. Basi labda unaweza kuwaonyesha andiko katika Biblia katika Zaburi 83:18. Sasa tuchukue Biblia tuone andiko hilo pamoja. Linasema: “Wajue ya kuwa Wewe, uitwaye jina Iako YEHOVA, ndiwe peke yako Uliye juu, juu ya nchi yote.”

“Yehova” ni jina Ia maana kuliko yote. Ni jina Ia Yeye aliyefanya vitu vyote. Na kumbuka, Yesu alisema imetupasa tumpende Yehova kwa moyo wetu wote. Je! wewe unampenda Yehova?—

Twawezaje kuonyesha twampenda?— Njia moja ni kuwaambia wengine jina lake Yehova. Tena twaweza kuwaambia juu ya mambo ya ajabu ambayo amefanya. Hii itampendeza Yehova, kwa sababu anajua ni lazima watu wajue juu yake. Twaweza kushiriki katika kufanya hivyo, sivyo?—

Si kila mtu atataka kusikiliza tunaposema juu ya Yehova. Watu wengi hawakusikiliza hata wakati Yesu aliposema juu ya Yeye. Lakini hiyo haikumzuia Yesu asiseme juu ya Yehova.

Basi na tuwe kama Yesu. Na tuendelee kusema juu ya Yehova. Tukifanya hivyo, Yehova Mungu atapendezwa nasi kwa sababu twaonyesha upendo kwa jina lake.

(Sasa someni pamoja katika Biblia maandiko zaidi machache yaonyeshayo maana sana ya jina la Mungu: Yohana 17:26; Isaya 12:4, 5; Warumi 10:13.)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki