Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 5/15 kur. 4-5
  • Mungu Anataka Jina Lake Lijulikane

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mungu Anataka Jina Lake Lijulikane
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Habari Zinazolingana
  • Mungu Ana Jina
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
  • Mungu Ana Jina
    Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
  • Kuzijua Njia za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Kichaka Kinachowaka Moto
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 5/15 kur. 4-5

Neno la Mungu Li Hai

Mungu Anataka Jina Lake Lijulikane

JE! WEWE ulijua kwamba Mungu ana jina? Yesu, ambaye anaonekana hapa akisali pamoja na wanafunzi wake, anamwambia Mungu hivi: “Naliwajulisha jina lako, tena nitawajulisha hilo.” (Yohana 17:26) Tusishangae kwamba Mungu ana jina. Kila mtu ana jina, hata Mwana wa Mungu mwenyewe, Yesu.​—Luka 1:30-32.

Watu wanapenda kuitwa kwa jina lao. Na Mungu anataka watu wajue jina lake pia. Hiyo ndiyo sababu alimwongoza mtunga zaburi wa Biblia aandike hivi: “Wajue ya kuwa Wewe, uitwaye jina lako YEHOVA, ndiwe peke yako Uliye juu, juu ya nchi yote.” (Zaburi 83:18) Zamani za kale Mungu alionyesha ubora wa jina lake kwa mtu aliyeitwa Musa.

Siku moja Musa alipokuwa akifanya kazi ya mchungaji katika Midiani, akichunga kondoo, aliona kitu cha kustaajabisha. Aliona kichaka chenye moto lakini hakikuwa kikichomeka! Alipokaribia zaidi aone vizuri zaidi, kama unavyoweza kuona hapa, sauti ilitoka katikati ya kichaka hicho chenye moto, ikaita: “Musa! Musa!”

Mungu ndiye aliyekuwa akisema. Alitaka Musa amwendee Farao, mfalme wa Misri, na kuwaondoa watu Wake Misri. Lakini Musa alimwambia Mungu hivi: “Tuseme sasa nimekuja kwa wana wa Israeli nami nawaambia, ‘Yule Mungu wa baba zenu wa kwanza amenituma mimi kwenu,’ nao waniambia: Jina lake nani?’ Mimi nitawaambia nini?” Mungu alimwambia Musa awaambie: “Yehova yule Mungu wa baba zenu wa kwanza . . . amenituma mimi kwenu.”​—Kutoka 3:1-15, NW.

Walakini, Musa alipoenda Misri akaseme na Farao, Wamisri walifikiri Yehova alikuwa kimungu kidogo tu cha wana wa Israeli. Hawakuamini alikuwa ndiye Mungu wa dunia nzima. (Kutoka 5:2) Kwa hiyo Yehova aliagiza Musa aambie Farao kwamba Yeye angefanya ‘jina Lake litangazwe katika dunia yote.’ (Kutoka 9:16) Je! wewe unajua namna Yehova alivyofanya jambo hilo wakati huo?

Yehova Mungu alimwagiza Musa awaondoe Waisraeli Misri, lakini Wamisri wakaenda mbio wakiwafuata. Walipofika kwenye Bahari Nyekundu (ya Shamu) ilionekana hakukuwa na njia ya kuwakimbia Wamisri wenye kuwafuatia. Lakini ndipo Yehova alipoagiza Musa anyoshe fimbo yake juu ya yale maji, nayo maji yakajitenganisha ili kuwaruhusu Waisraeli wenye kukimbia wapite katika nchi kavu. Baadaye Yehova aliagiza Musa anyoshe tena fimbo yake, kama unavyoweza kuona hapa, nayo maji yakawazamisha chini wale Wamisri, wote wakafa maji. Habari za tukio kubwa hilo zilienea kote kote hata watu wa kila mahali wakalijua jina la Mungu.​—Kutoka 14:21-31; Yoshua 2:9-11.

Namna gani leo? Je! bado Mungu anataka jina lake lijulishwe ulimwengu wote? Ndivyo, anataka. Tena ni jambo la maana sana watu leo wajifunze habari za Yehova na kumtumikia. Wasipofanya hivyo, itakuwa kwao kama ilivyokuwa kwa Wamisri wenye vichwa vigumu waliokataa kumjua Yehova. Watapatwa na uharibifu “wakati wa kufunuliwa kwake Bwana Yesu kutoka mbinguni . . . huku akiwalipiza kisasi wao wasiomjua Mungu.”​—2 Wathesalonike 1:7-9.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki