Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • te sura 10 kur. 43-46
  • Mwenye Ukoma Mmoja Alimtukuza Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mwenye Ukoma Mmoja Alimtukuza Mungu
  • Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Wewe Hukumbuka Kusema Asante?
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
  • Watu Kumi wenye Ukoma Waponywa​—Mmoja Ashukuru
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Wakoma Kumi Waponywa Wakati wa Safari ya Mwisho ya Yesu Kwenda Yerusalemu
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Wenye Ukoma Kumi Waponywa Wakati wa Safari ya Mwisho ya Yesu ya Kwenda Yerusalemu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
Pata Habari Zaidi
Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
te sura 10 kur. 43-46

Sura ya 10

Mwenye Ukoma Mmoja Alimtukuza Mungu

JE! MAMA yako alikupatia chakula kizuri leo?— Alikuwa mwema kufanya hivyo, sivyo?— —Je! ulimshukuru?— Mara nyingine tunasahau kusema “Asante” wakati wengine wanapotufanyia wema, sivyo? Wakati Mwalimu Mkuu alipokuwa duniani, walikuwako wenye ukoma wengine waliosahau kusema “Asante.”

Unajua mwenye ukoma alivyo?⁠— Mwenye ukoma ni mtu mwenye ugonjwa unaoitwa ukoma. Ugonjwa huo waweza hata kufanya mwili wa mtu kuoza. Yesu alipoishi duniani, iliwapasa wenye ukoma wajitenge na watu wengine. Na ikiwa mwenye ukoma angemwona mtu mwingine akija, ilimpasa apige kelele: ‘Mimi mwenye ukoma. Jiangalie!’ Ama sivyo huenda watu wakaambukizwa na ugonjwa wa mwenye ukoma.

Yesu alikuwa mwema sana kwa wenye ukoma. Siku moja, akiwa njiani kwenda Yerusalemu, Yesu akaja karibu na mji mdogo. Wenye ukoma kumi wakatoka kumwona.

Wenye ukoma hawakumkaribia Yesu. Walisimama mbali. Lakini walikuwa wamesikia kwamba Yesu alikuwa na uwezo kutoka kwa Mungu kuponya namna zote za ugonjwa, hata ukoma. Basi wakampazia sauti, ‘Yesu, Mwalimu, tusaidie!’

Je! unawasikitikia wagonjwa?⁠— Yesu aliwasikitikia. Yeye alijua namna ilivyokuwa sikitiko kuwa mwenye ukoma. Basi akawajibu, akasema: ‘Nendeni mkajionyeshe wenyewe kwa makuhani wa Mungu.’

Kwa nini Yesu aliwaambia wafanye hivi?— llikuwa kwa sababu ya sheria ambayo Yehova aliwapa watu wake. Sheria hii ilisema kwamba kuhani wa Mungu alipaswa autazame mwili wa mwenye ukoma. Kuhani angemwambia mwenye ukoma wakati ugonjwa wake wote ulipomtoka. Ndipo angeweza kuishi tena pamoja na watu wazima.—Mambo ya Walawi 13:16, 17.

Lakini wenye ukoma kumi hawa bado walikuwa na ugonjwa wao. Basi je! wangekwenda kumwona kuhani kama Yesu alivyosema?— Ndiyo, walikwenda mara hiyo. Watu hawa bila shaka waliamini kwamba Yesu angeondoa ugonjwa wao.

Na kukatukia nini?⁠— Basi, walipokuwa njiani kwenda kwa kuhani, ugonjwa wao uliwatoka. Mwili wao ukaponywa. Wakapona! Imani yao katika uwezo wa Yesu ilipatiwa zawadi. Lo! walifurahi wee!

Lakini, sasa, ingaliwapasa kufanya nini ili kuonyesha walishukuru? Wewe ungalifanya nini?—

Mmoja wa watu walioponywa akarudi kwa Yesu. Alianza kumtukuza Yehova, akisema mambo mema juu ya Mungu. Hilo lilikuwa jambo zuri kufanya, kwa sababu uwezo wa kuponya ulitoka kwa Mungu. Yule mtu alianguka miguuni pa Mwalimu Mkuu akamshukuru. Ali-shukuru sana kwa jambo ambalo Yesu alikuwa ametenda.

Lakini namna gani watu wengine kenda? Yesu akauliza: ‘Wenye ukoma kumi waliponywa, sivyo? Wako wapi wengine kenda? Mmoja tu ndiye karudi kumpa Mungu utukufu?’

Ndiyo, ni kweli. Mmoja tu kati ya wenye ukoma kumi akamtukuza Mungu, akarudi kuja kumshukuru Yesu. Na mtu huyu alikuwa Msamaria, mtu wa nchi nyingine. Wengine kenda hawakumshukuru Mungu; hata twajua hawakumshukuru Yesu.— Luka 17:11-19.

Wewe unafanana na nani kati ya watu hao?⁠— Sisi sote tunataka tuwe kama Msamaria, sivyo?⁠— Basi, mtu akitufanyia wema, imetupasa tukumbuke kufanya nini?⁠— Yatupasa tumshukuru.

Mara nyingi watu wanasahau kusema “Asante.” Lakini ni vizuri kusema “Asante.” Ni jambo jema kufanya. Na wakati unapofanya hivyo, Yehova Mungu na Mwana wake Yesu wanapendezwa.

Ukifikiri juu yake, utakumbuka kwamba watu wamekufanyia vitu vingi. Unakumbuka wakati ulipokuwa mgonjwa?— Labda wewe bado kuwa mgonjwa hata mara moja kama wale wenye ukoma kumi. Lakini labda umeshikwa na mafua, au maumivu tumboni mwako. Je! mama au baba yako alikuangalia? Unafurahi kwa vile walikusaidia upate afya njema?—

Msamaria alimshukuru Yesu kwa kumponya, na hii ikamfurahisha Yesu. Unafikiri mama au baba yako watafurahi ukisema “Asante” wanapokufanyia vitu?— Ndiyo.

Mara nyingine watu wanatufanyia vitu kila siku au kila juma. Labda ni kazi yao kufanya hivi. Hata labda wanafurahia kuifanya. Lakini labda sisi tunasahau kuwashukuru.

Labda mwalimu wako wa masomo anafanya kazi sana kukusaidia ujifunze mambo mengi. Hii ndiyo kazi yake. Lakini atapendezwa ukimshukuru kwa kukusaidia ujifunze.

Mara nyingine watu wanakufanyia vitu vizuri vidogo. Je! mtu ye yote amepata kukufungulia mlango?— Au ye yote amepata kupitisha chakula kwako penye meza ya chakula? Ni vizuri kusema “Asante’ hata kwa mambo haya madogo.

Tukikumbuka kusema “Asante” kwa watu duniani, basi yaelekea sana tutakumbuka kusema “Asante” kwa Baba yetu mbinguni. Na kuna mambo mengi ya kumshukuru Yehova namna gani! Yeye akatupa uhai wetu, na mambo yote mazuri yenye kufurahisha maisha. Basi tunayo kila sababu kumtukuza Mungu kwa kusema mambo mazuri juu yake kila siku.

(Kwa habari ya kushukuru, soma Zaburi 92:1 na Waefeso 5:20.)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki