Sura ya 13
Wale Ambao Wakawa Wanafunzi wa Yesu
NINAFIKIRIA mtumishi bora wa Mungu aliyepata kuishi duniani. Unajua alikuwa nani?— Ndiyo. Yesu Kristo.
Unafikiri wewe na mimi twaweza kuwa kama yeye?— Basi, Biblia inasema kwamba yeye alituwekea sisi mfano tufuate. Naye anatukaribisha tuwe wanafunzi wake.
Ina maana gani kuwa wanafunzi wa Yesu?— Ina maana ya mambo mengi. Kuwa wanafunzi wa Yesu, yatupasa tujifunze kwake. Lakini si hilo tu. Yatupasa tuamini kweli kweli anayosema. Je! wewe kweli unaamini kila neno ambalo Yesu anasema? Ikiwa kweli tunaamini, tutafanya anayotuambia, sivyo?—
Watu wengi wanasema wanamwamini Yesu. Lakini je! wote kweli ni wanafunzi wake? Unafikiri ndivyo?—
Hapana; karibu wote sivyo. Huenda wanakwenda kanisani mara kwa mara. Lakini wengi kati yao hawajapata nafasi wajifunze ambayo Yesu alifundisha. Ukijaribu kusema nao juu ya Yesu, labda watasema hawapendezwi. Na hawashiriki katika kazi ya kuhubiri ambayo Yesu aliwaambia wanafunzi wake kufanya. Basi kweli wao si wanafunzi wake.
Watu wa namna gani wakawa wanafunzi wa Yesu? Unajua? Lingekuwa jambo la kupen-deza kujua wengine kati ya wale waliokuwa wanafunzi wa Yesu alipokuwa mwanadamu duniani.
Wengine kati yao walikuwa wavuvi wa samaki. Siku moja wakati Yesu alipokuwa akitembea kando ya Bahari ya Galilaya yeye alimwona Petro na nduguye Andrea. Walikuwa wakitelemsha wavu baharini. Yesu akaita kwao: “Nifuateni.”
Akiendelea zaidi kidogo, Yesu aliona wanaume wengine wawili waliokuwa ndugu. Majina yao walikuwa Yakobo na Yohana. Walikuwa katika chombo pamoja na baba yao, wakitengeneza nyavu zao. Yesu akawaita Yakobo na Yohana nao wawe wanafunzi wake.
Ikiwa Yesu angalikuita wewe, ungalifanyaje? Je! ungalikwenda na Yesu mara hiyo?— Watu hawa walijua Yesu alikuwa nani. Walijua kwamba Yesu alikuwa ametumwa na Mungu. Hivyo mara hiyo wakaacha kazi yao ya kuvua samaki wakamfuata Yesu.—Mathayo 4:18-22.
Ni wazi kwamba watu hawa walikuwa na nia. Walitaka wafanye yaliyokuwa mazuri, na hilo ni la maana. Lakini hawakuwa wakamilifu. Fikiria Petro. Zilikuwako nyakati aliposema jambo baya, na ikamtia katika taabu. Lakini alikuwa na moyo mzuri. Yeye hakujaribu kufanya ionekane kana kwamba hakuwa amefanya baya hali alijua amefanya baya. Yeye alisikiliza na alikuwa na nia ya kugeuka. Tukiwa na nia kama Petro, twaweza kuwa wanafunzi wa Yesu vile vile.
Yesu tena alisema kwa mtawala kijana tajiri. Je! mtu kama huyu angeweza kuwa mwanafun-zi wa Yesu?— Alionyesha kupendezwa. Alimwuliza Yesu namna ya kupata uzima wa milele. Yesu akaeleza hivi kwake. Lakini yule mtu alipojua kwamba kuwa mwanafunzi wa Yesu kungekuwa kwa manna zaidi katika maisha yake kuliko fedha zake, hakufurahi. Yesu akamkaribisha: “Njoo unifuate.” Lakini yule mtu hakujiunga na yeye. Alipenda fedha zake zaidi kuliko kumpenda Mungu.—Luka 18:18-25.
Yesu alikaribisha namna zote za watu wawe wanafunzi wake. Hata wale waliokuwa wameishi maisha mabaya waliweza kugeuka. Lakini inawapasa wawe na nia ya kujifunza na kugeuka na kufuata njia nzuri. Inawapasa watake kweli kumpendeza Mungu. Je! ndivyo wewe wataka kufanya?—
Wanafunzi peke yao ambao tumesema juu yao mpaka hapa walikuwa wanaume. Je! ina maana ni wanaume peke yao ndio waliweza kuwa wanafunzi wa Yesu?— Hapana. Wanawake vile vile wakawa wana-funzi. Biblia hata inatuambia juu ya jamaa ambayo katika hiyo binti wanne walikuwa na shughuli ya kuwaambia watu wengine juu ya Mungu.—Matendo 21:8, 9.
Wakati Yesu alipokuwa akifundisha, alipendezwa sana na watoto wachanga. Kwa sababu gani alifanya hivyo? Alijua watoto vile vile wangeweza kuwa wanafunzi wake. Ni kweli kwamba watu wazima wanaweza kufanya mambo fulani ambayo watoto hawawezi kufanya. Lakini watu wazima sio peke yao wanaoweza kujifunza kwa Yesu. Wewe vile vile waweza kufanya mambo hayo.
Je! wataka uwe mwanafunzi wa Yesu?— Mimi nataka. Hilo ndilo jambo bora kweli ambalo ye yote wa sisi aweza kufanya.
Lakini, kumbuka, kusema sisi ni Wakristo tu hakutufanyi wanafunzi wa Mwalimu Mkuu, sivyo?— lkiwa kweli sisi ni wanafunzi wake, itaonekana katika kila kitu tunachofanya.
Hatutasingizia kuwa Wakristo tunapokwenda kwenye mikutano ambapo tunasema juu ya Mungu tu, kisha tuwe wabaya nyakati nyingine. Tutaishi kama Wakristo hapa nyumbani.
Je! kuwa Mkristo kunatia vile vile namna unavyotenda wakati unapocheza na watoto wengine?— Je! lazima kuvute mambo ambayo mtu anafanya anapokuwa kazini?— Ndiyo, ikiwa sisi ni wanafunzi wa Yesu kweli kweli, basi yatupasa tutende hivyo siku kutwa, bila kujali mahali tulipo.
(Sasa someni pamoja ambayo Biblia inasema juu ya wanafunzi wa Yesu katika Mathayo 28:19, 20, Yohana 8:31, 32 na Luka 6: 13-15.)