Sura ya 27
Kachukiwa kwa Kufanya Mema
UNAPENDA mema?— Sote wawili tungesema ndiyo, sivyo? Lakini je! kweli tunapenda sana sana hata tungefanya mema ingawa wengine wangetuchukia kwa kufanya? Kunatakiwa uhodari kufanya hivyo, sivyo?—
Unafikiri Mwalimu Mkuu alikuwa na uhodari wa namna hiyo? Je! alifanya mema hata wengine walipomchukia?—
Mara nyingi watu walimpenda Yesu kwa mema aliyofanya. Siku moja watu wote wa mji walikusanyika mpaka mlangoni pa nyumba alimokuwa akikaa. Walikuja kwa sababu Yesu alikuwa amekuwa akiwaponya wagonjwa.—Marko 1:33.
Lakini mara nyingine mambo ambayo alifundisha Yesu yalionyesha kwamba watu hawakuamini kweli. Je! kila mtu alipenda kumsikia wakati huo?— Je! walitaka kugeuza imani zao?— Si kila mtu. Zaidi, wengine wao walimchukia Yesu sana kwa sababu alisema kweli.
Hii ilitukia siku moja katika mji wa Yesu mwenyewe wa Nazareti. Yesu aliingia katika sinagogi. Sinagogi ni mahali ambapo Wayahudi walikutania.
Yesu akasimama akatoa hotuba nzuri kutoka kwa Maandiko. Kwanza watu wakapenda. Walishangazwa na maneno mazuri yaliyotoka kinywani mwake. Hawakuweza kusadiki kama hu-yu alikuwa kijana mwanamume aliyekulia mjini mwao wenyewe.
Lakini ndipo Yesu aliposema jambo jingine. Alisimulia juu ya nyakati Mungu alipoonyesha kibali cha pekee kwa watu wasiokuwa Wayahudi kama wao. Yesu aliposema hivi, waliokuwamo katika sinagogi walikasirika. Unajua kwa sababu gani?—
Walifikiri wao peke yao ndio waliokuwa na kibali cha pekee cha Mungu. Walifikiri walikuwa bora kuliko watu wengine. Basi wakamchukia Yesu kwa yale aliyosema. Na wajua walilojaribu kumfanyia?—
Biblia inasema: ‘Wakamshika Yesu wakamtoa nje ya mji. Wakampeleka kwenye ukingo wa kilima wapate kumtupa chini na kumwua! Lakini Yesu akawaponyoka.’—Luka 4:16-30.
Ikiwa hilo lingekupata wewe, je ungalirudia kwa watu hao kusema juu ya Mungu tena?— Hilo lingetaka uhodari, sivyo?— Basi, kama mwaka mmoja kutoka hapo Yesu akarudia Nazareti. Na Biblia inasema: “Akawafundisha katika sinagogi lao.” Yesu hakuacha kusema kweli kwa sababu ya kuogopa wanadamu wasiompenda Mungu.—Mathayo 13:54.
Siku nyingine Yesu alikuwa mahali palipokuwa na mtu ambaye mkono wake ulipooza. Yesu alikuwa na nguvu kutoka kwa Mungu ya kumponya mtu yule. Lakini watu wengine waliokuwako walikuwa wakijaribu kumfanyia Yesu matata. Mwalimu Mkuu alifanya nini?—
Kwanza alionyesha lililokuwa jambo zuri kufanya. Akauliza: ‘Ikiwa ungekuwa na kondoo aliyeangukia katika shimo kubwa siku ya sa-bato, ungemtoa nje?’
Ndiyo, wangefanya hivyo kwa kondoo, hata siku ya sabato, siku ambayo wangepumzika. Basi Yesu akasema: ‘Ni bora hata zaidi kumsaidia mtu siku ya sabato, kwa sababu mtu ni bora kuliko kondoo!’ Namna ilivyokuwa wazi Yesu amsaidie mtu huyu kwa kumponya!
Basi Yesu akamwambia yule mtu anyoshe mkono wake. Mara hiyo ukawa mzima kama ule mwingine! Lo! mtu yule alifurahi!
Lakini namna gani wale watu wengine? Je! walifurahi? Hapana. Walimchukia Yesu hata zaidi. Wakatoka wakafanya mipango ya kumwua!—Mathayo 12:9-14.
Watu wako hivyo leo. Wengine wanapenda mema. Wengine hawapendi. Si kitu tufanye nini, hatuwezi kabisa kuwapendeza wote. Hivyo yatupasa tuamue nani ambaye kweli twataka tumpendeze.
Wewe wataka nani wawe rafiki zako? Unataka watu wazuri wawe rafiki? Je! unataka Yehova Mungu awe rafiki yako?— Basi inakupasa sikuzote ufanye mema.
Lakini ukifanya mema, je! lbilisi atakupenda? Na, kwa kweli, je! wataka Ibilisi akupende?—
Kuna watu ambao Ibilisi awapenda. Biblia inawaita “ulimwengu.” “Ulimwengu” ndani ya-ke mna watu wote wasio wafuasi wa Mwalimu Mkuu. Mwalimu Mkuu alisema: “Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake; lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia.—Yohana 15:18, 19.
Watu wengine wa ulimwengu wanasema wanamwamini Yesu, lakini hawafundishi wengine kweli juu ya Mungu, kama alivyofanya Yesu. Ukiwaonyesha katika Biblia kwamba hawafundishi kweli, je! watapenda hilo?— Hapana, karibu wote hawatapenda. Lakini labda utamwona mmoja kama mtu yule mwenye mkono uliopooza. Alikuwa mwenye kushukuru kwa vile Yesu hakuficha kweli.
Kuna watu wengi wanaoficha kweli. Wanaogopa watakachofikiria watu wengine. Wanahangaika sana juu ya jambo ambalo huenda watu watasema hata wanazuia maisha zao zote wasifanye wanalojua ni jema. Lo! sikitiko gani! Wanakosa furaha nyingi katika maisha. Tena wanakosa kibali cha Mungu. Sisi hatutaki tuwe hivyo, sivyo?—
(Someni pamoja maandiko haya kuonyesha kwamba tusiruhusu kabisa kuogopa ambacho watu wengine watafikiri kituzuie kufanya mema: Mithali 29:25; 1 Samweli 25:24; Mathayo 26:69-75; Yohana 12:42, 43.)