Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • te sura 32 kur. 131-134
  • “Wenye Furaha ni Wenye Amani”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Wenye Furaha ni Wenye Amani”
  • Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Ni Vizuri Kupigana?
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
  • Je, Watoto Wako Salama Wakiwa na Mbwa Wako?
    Amkeni!—1997
  • Jinsi ya Kumzoeza Mbwa Wako
    Amkeni!—2004
  • Vile Vita vya Kufanya Yaliyo Mema
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
Pata Habari Zaidi
Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
te sura 32 kur. 131-134

Sura ya 32

“Wenye Furaha ni Wenye Amani”

UNAWAJUA watoto wa kiume wo wote ambao sikuzote wanajaribu kufanya matata? Unapenda kuwa nao? Au ungependelea kuwa na mtu fulani ambaye ni mwenye amani?—

Mwalimu Mkuu anajua ni watu wa namna gani ambao Mungu apenda. Alisema: “Wenye furaha ni wenye amani, kwa kuwa wataitwa ‘wana wa Mungu.’” Ndiyo mtu tunayetaka tuwe naye, sivyo?— Tunataka tuwe wenye amani.—Mathayo 5:9, NW.

Lakini mara nyingine watu wengine wanafanya mambo yanayotukasirisha. Na huenda tukajiona kutaka kujilipiza kisasi. Siku moja jambo hili lilitukia kwa wanafunzi wa Yesu.

Walikuwa wakisafiri na Yesu kuelekea Yerusalemu. Walipokuwa wamekwenda mwendo fulani, Yesu akawatuma wengine watangulie kijijini wawatafutie mahali pa kupumzika. Lakini watu wa huko hawakutaka wakae. Watu hao walikuwa na dini nyingine. Nao hawakumpenda ye yote aliyekwenda kwenye mji wa Yerusalemu kuabudu.

Ikiwa wewe ungalitukiwa na jambo hilo, ungalifanyaje? Je! ungalikasirika? Ungalitaka kujilipiza kisasi?—

Ndivyo wanafunzi Yakobo na Yohana wali-vyotaka kufanya. Wakamwambia Yesu hivi: ‘Wataka tuagize moto ushuke kutoka mbinguni, uwaangamize?’ Lakini Yesu aliwaambia haikuwa vizuri kuwatendea watu wengine hivyo.—Luka 9:51-56.

Ni kweli kwamba mara nyingine huenda watu wakawa wabaya kwetu. Huenda watoto wengine wasitake ucheze michezo yao. Hata huenda wakasema, “Sisi hatukutaki hapa.” Jambo fulani kama hili litukiapo, laweza kutukasirisha, sivyo?— Huenda likatufanya kutaka kufanya jambo fulani ili kujilipiza kisasi. Lakini je! tufanye hivyo?—

Sababu gani usichukue nakala yako ya Biblia? Na tufungue Mithali sura ya 24, mstari wa 29. Hapo panasomwa hivi: “Usiseme, Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; nitamlipa mtu huyo sawasawa na tendo lake.’”

Hilo lina maana gani kwako?— Linasema haitupasi kujaribu kujilipiza kisasi. Haitupasi kuwa wabaya kwa mtu mwingine kwa sababu yeye akawa mbaya kwetu. Mungu hataki tufanye hivyo.

Lakini namna gani ikiwa mtu fulani anataka kupigana na wewe? Pengine atajaribu kukuka-sirisha kwa kukutukana. Huenda akucheke na kusema mwoga wewe. Pengine atakuita goigoi wewe. Imekupasa ufanye nini? Je! uanze kupigana?—

Tena, na tuone Biblia inasema nini. Fungua Mathayo sura ya 5 na mstari wa 39. Hapo Yesu anasema: “Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili.”

Kwa hilo Yesu alimaanisha nini? Je! alimaanisha mtu akikupiga kwa ngumi yake upande mmoja wa uso wako, imekupasa umwache akupige upande mwingine?— Sivyo, hakumaanisha hivyo.

Kupiga si kama pigo la ngumi. Kunafanana zaidi na msukumo. Mtu anafanya hivi aanze vita. Anataka tukasirike. Na tukikasirika na kurudisha msukumo, inakuwa namna gani?— Labda tutaingia katika vita.

Yesu hakutaka wafuasi wake watende hivyo. Hivyo alisema kwamba ikiwa mtu fulani anatupiga, tusirudishe kupiga. Tusikasirike na kuingia katika vita. Tukifanya, tunaonyesha hatuko tofauti na aliyeanzisha vita.

Matata yakianza, afadhali kuondoka. Huenda jamaa mwingine akakusukuma zaidi kidogo. Lakini yaelekea utakuwa ndio mwisho. Unapoondoka, haionyeshi wewe hauna nguvu. Inaonyesha una nguvu kwa kilicho chema.

Sasa, imetupasa tufanye nini tukiona watu wengine wakipigana? Je! imetupasa tujiingize katika kupigana upande huu au huu?—

Biblia inatuambia jambo zuri. Fungua Mithali sura ya 26 na mstari wa 17. Inasema hivi: “Mtu apitaye na kujisumbua kwa ugomvi usio wake; ni kama mtu ashikaye mbwa kwa masikio yake.”

Ingekuwaje ikiwa ungemshika mbwa kwa masikio yake? Ingemwumiza mbwa, angekung’akia, sivyo?— Kadiri mbwa angejaribu kujiondoa, ndivyo ungefinya masikio zaidi. Ndivyo mbwa angekasirika zaidi. Ikiwa ungemwachia, bila shaka angekuuma sana. Lakini je! waweza kusimama hapo na kumshika masikio yake milele?—

Basi, ndiyo matata ambayo katika hayo tungekuwamo ikiwa tungejiingiza katika mapigano kati ya watu wengine. Huenda tusijue nani alianzisha ugomvi au sababu gani walikuwa wakipigana. Huenda mtu mmoja anapigwa, lakini labda alimwibia mwingine kitu fulani. Ikiwa tungemsaidia, tungekuwa tukisaidia mwivi. Hilo lisingekuwa zuri, sivyo?—

Basi, ukiona kuna mapigano imekupasa ufanyeje?— Ikiwa ni shuleni (masomoni), unaweza kukimbia ukamwambie mwalimu. Na ikiwa ni mbali na shule, unaweza kumwita polisi.

Hata wakati watu wengine wanapotaka kupigana, twaweza kuwa wenye amani. Huenda wakataka kupigana. Lakini twaweza kuonyesha tuna nguvu kwa kilicho chema.

(Shauri jema zaidi ambalo laweza kumsaidia mtu aepuke mapigano linapatikana katika Warumi 12:17-21, Zaburi 34:14 na 2 Timotheo 2:24.)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki