Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • te sura 43 kur. 175-178
  • Yesu Anatoa Ishara

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu Anatoa Ishara
  • Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi Tunavyoweza Kujua Har-magedoni Imekaribia
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
  • Ile Ishara Si Historia ya Wakati Uliopita Tu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Yesu Atabiri Matukio ya Wakati Ujao Yatakayoikumba Dunia Nzima
    Biblia—Ina Ujumbe Gani?
  • Je, Unatambua Ile Ishara ya Kuwapo kwa Yesu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
Pata Habari Zaidi
Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
te sura 43 kur. 175-178

Sura 43

Yesu Anatoa Ishara

LEO tutazungumza juu ya ishara. Ni vizuri kujua kusoma ishara. Zinaweza kutusaidia. Ishara nyingine zina maneno. Zinatuambia mahali kwa kununua chakula. Zaweza kutuonya tusivuke barabara wakati magari yanapokuja. Wewe umeona ishara gani?—

Ziko ishara za namna nyingine vile vile. Huenda zisiwe na maneno. Nyingine kati ya hizo zinaonyesha kugeuka kwa hali ya hewa. Huenda mawingu yakafunika jua. Labda upepo uanze kuvuma. Umeme unameta-meta. Kuna ngurumo. Wakati unaposikia na kuona mambo haya, yana maana gani? Ndiyo, labda kutakuwako mvua. Si vigumu kusoma ishara hizi, sivyo?

Siku moja mitume wa Yesu walimwomba ishara. Walikuwa wamemsikia akisema kwamba watu wasingemwona tena mpaka wakati fulani ujao. Walitaka kujua huo ungekuwa wakati gani. Ingekuwako ishara gani kwamba wakati huo ulifika?

Mwalimu Mkuu alijua kwamba wafuasi wake wangetaka ishara. Alikuwa akitazamia kurudi mbinguni akawe pamoja na Mungu. Wakati angerudi asingekuwa binadamu. Angekuwa roho. Na je! unaweza kuiona roho?—

Basi, ye yote angejua namna gani kwamba alikuwa amerudi? Basi, Yesu aliwaambia jambo la kutazamia. Aliwaambia juu ya mambo ambayo yangetukia apa hapa duniani.

Wakati Yesu alipokuwa akisema nao, walikuwa karibu na Yerusalemu. Waliweza kuuona ng’ambo ya bonde. Na waliweza kuona hekalu lake zuri. Basi Yesu akawaambia juu ya mambo ambayo yangetukia kwa Yerusalemu na hekalu lake. Na mambo hayo yalitukial

Lakini tena Yesu alisema kwamba mambo yale yale yangetukia tena wakati ujao. Wakati huu yangeupata ulimwengu mzima. Na hii ingekuwa na maana gani? Ingekuwa na maana kwamba Kristo alikuwa amerudi. Ingekuwa na maana kwamba alikuwa ameanza kutawala kutoka mbinguni katika ufalme wa Mungu. Karibuni angeharibu waovu. Karibuni maisha yangekuwa bora sana duniani.

Je! tumeiona ishara ambayo Yesu alitoa?— Mimi nimeiona. Ungependa kusikia juu yake?—

Kama sehemu ya ishara, Yesu alisema hivi: ‘Ninyi mtasikia juu ya vita na ripoti za vita. Taifa litainuka juu ya taifa na ufalme juu ya ufalme.’

Mimi nimeona hilo katika maisha yangu. Mataifa mazima yamefanya vita juu ya mataifa mengine kuyaangamiza. Kwa kweli taabu ilianza katika mwaka wa 1914. Sasa karibu kila siku tunasikia ripoti za habari ya vita. Je! wewe umesikia ripoti hizo kwa radio au kwa televisheni?—

Kuna sehemu nyingine ya ishara ambayo Yesu alitoa. Alisema: ‘Kutakuwako upungufu wa chakula mahali hapa na mahali hapa.’

Si kila mtu aliye na chakula cha kutosha. Ulijua hilo?— Mimi nimesikia kwamba kila siku elfu kumi ya watu wanakufa kwa sababu hawana chakula cha kutosha. Ukosefu wa chakula vile vile unatokeza magonjwa ya kipuku. Yesu alisema kwamba kungekuwako upungufu wa chakula na ugonjwa wa kipuku.

Hii ni sehemu nyingine ya ishara ambayo alitoa: ‘Kutakuwako matetemeko ya dunia mahali hapa na mahali hapa.’

Unajua tetemeko la dunia lilivyo?— Linatetemesha ardhi chini ya miguu yako. Nyumba zinaanguka na mara nyingi watu wanauawa. Tangu mwaka wa 1914 yamekuwako matetemeko ya dunia mengi zaidi kila mwaka kuliko yalivyokuwa zamani. Haya ndiyo mambo ambayo yametukia katika maisha yangu.

Yesu alisema kwamba sehemu nyingine ya ishara ingekuwa ‘uasi zaidi na zaidi.’ Hilo linatukia vile vile. Ndiyo sababu karibu kila mahali watu wanafunga mlango kwa kufuli katika nyumba zao. Wanaogopa asije mtu fulani akajaribu kuvunja nyumba akaingia. Na mahali pengi si salama kutembea katika barabara usiku ukiwa peke yako. Hali haikuwa mbaya sana zamani hata kidogo kama ilivyo sasa.—Mathayo 23:39-24:22.

Huenda watu wengine wakasema kwamba mambo haya yametukia zamani. Lakini zamani hayakutukia katika sehemu nyingi sana za ulimwengu kwa wakati uo huo. Yote haya yana maana ya pekee.

Kumbuka, Yesu alisema kwamba mambo haya yangekuwa ishara. Unaweza kusoma ishara hiyo? Ina maana gani?—

Karibu watu wote wanaona taabu tu. Inawafanya wasifurahi. Lakini ikiwa wangejua maana ya ishara, wangefurahi. Kwa sababu gani?—

Yesu alisema hivi: ‘Wakati mambo haya yanaanza kutukia, viinueni vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu unakaribia.’ Hiyo ina maana kwamba imetupasa tufurahi. Kwa sababu kwa muda mfupi Mungu atamaliza taabu zote katika dunia hii. Maisha yatakuwa yenye kupendeza sana wakati huo.

Wewe hukubali kwamba hii ni habari njema?— Ikiwa kweli tunaiamini, hatutawanyima wengine. Watu wengine wanataka kujua juu yake vile vile.

(Kuna mengi katika Biblia yanayoonyesha kwamba umefika wakati kwa ufalme wa Mungu. Someni pamoja maandiko haya: Luka 21:28-35; 2 Timotheo 3:1-5; 2 Petro 3:3, 4, 13.)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki