Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 10/1 uku. 3
  • Ile Ishara Si Historia ya Wakati Uliopita Tu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ile Ishara Si Historia ya Wakati Uliopita Tu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Habari Zinazolingana
  • Matetemeko ya Ardhi Ni Ishara ya Ule Mwisho?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Yesu Anatoa Ishara
    Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
  • Je! “Mwisho wa Ulimwengu” Ni Karibu?
    Furaha​—Namna ya Kuipata
  • Matetemeko Makubwa ya Ardhi—Biblia Ilitabiri Nini?
    Habari Zaidi
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 10/1 uku. 3

Ile Ishara Si Historia ya Wakati Uliopita Tu

KATIKA Yerusalemu, katika Mashariki ya Kati, kuna uwanja wa kihistoria ulio wa kusisimua ambao unadai fikira za watu wenye kufikiri leo. Huo ni lile eneo lililoinuka ambako palikuwa na “hekalu la utajiri mkubwa sana,” kulingana na maneno ya Tasito mwanahistoria Mroma wa karne ya kwanza. Mahali hapo hapana masalio ya hekalu hilo, lakini jukwaa lalo limesalia. Hilo linatoa ushuhuda juu ya ukweli wa ishara fulani ya kiunabii ambayo inakuathiri wewe.

Wachimbuzi wa vitu vya kale wamefanya magunduzi mengi upande wa kusini wa jukwaa hilo la hekalu. “Moja la mapato yaliyo ya kupendeza zaidi,” anataarifu J. A. Thompson katika The Bible and Archaeology, “lilikuwa mawe kadhaa yaliyo makubwa sana ya ujenzi wa Herode ambayo ni wazi yalitupwa chini kutoka juu ya ukuta wa Hekalu wakati wa uharibifu wa Yerusalemu katika A.D. 70.”

Uharibifu wa Yerusalemu na hekalu lao ulitabiriwa miaka 37 kabla haujatukia. Wanahistoria wasiopungua watatu walitia katika kumbukumbu ya maandishi maneno ya Yesu Kristo kwamba “halitasalia jiwe juu ya jiwe ambalo halitabomoshwa.” (Luka 21:6; Mathayo 24:1, 2; Marko 13:1, 2) Maongezi fulani yalifuata ambayo yanaathiri kila mmoja leo, kutia ndani wewe.

“Mwalimu,” wanafunzi wake wakamwuliza, “ni nini ishara ya kuwa mambo hayo ya karibu kutukia?” Kulingana na Yesu, kile kipindi chenye kuongoza kwenye uharibifu wa hekalu hilo kingetiwa alama na vita, matetemeko ya dunia, upungufu wa vyakula, na tauni (magonjwa ya kipuku, NW). “Kizazi hiki,” yeye akaongezea, “hakitapita hata hayo yote yatimie.”​—Luka 21:7, 10, 11, 32.

Je! kizazi hicho kilipatwa na utimizo wa ile “ishara”? Ndiyo. Biblia inarejezea “njaa kubwa” na pia matetemeko ya dunia matatu, mawili kati ya hayo yakiwa ni ‘matetemeko makubwa.’(Matendo 11:28; 16:26; Mathayo 27:51; 28:1, 2) Kulingana na historia ya kilimwengu, matetemeko mengine ya dunia na upungufu wa vyakula yalitukia wakati wa kipindi hicho. Ulikuwa pia wakati wa vita, na viwili kati yavyo vilipigwa na majeshi ya Kiroma dhidi ya wakaaji wa Yerusalemu. Yale mazingiwa ya pili ya Yerusalemu yalitokeza njaa mbaya sana na ugonjwa wa kipuku, hiyo ikiongoza kwenye uharibifu wa jiji hilo na hekalu lalo katika mwaka 70 W.K. Uwanja ulio katika Yerusalemu ambapo hekalu hilo lilikuwa likikaa ni ushuhuda bubu wa kuonyesha hayo matukio mabaya sana ya karne ya kwanza yalitukia.

‘Hilo ni jambo la kupendeza,’ huenda mtu fulani akasema, ‘lakini linaathiri maisha yangu jinsi gani?’ Katika maana ya kwamba ile ishara si historia ya wakati uliopita tu. Hiyo ilitimizwa kwa sehemu tu katika karne ya kwanza. Mathalani, Yesu alitabiri pia wakati ambapo aina ya wanadamu ingekuwa katika hofu kuu kwa sababu ya “ishara katika jua, na mwezi, na nyota” na “uvumi [mngurumo, ZVW] wa bahari.” Sehemu hii ya ishara ingekuwa alama ya ukaribio wa “ufalme wa Mungu”​—serikali ambayo italeta ukombozi wa daima wa kutolewa katika taabu kubwa ya ulimwengu.​—Luka 21:25-31.

Mambo hayo hayakutukia katika karne ya kwanza. Leo, miaka 1,900 baadaye, aina ya wanadamu ingali inangojea ukombozi wa kutolewa katika vita, matetemeko ya dunia, upungufu wa vyakula, na magonjwa ya kipuku. Kwa hiyo, lazima ile ishara iwe ina utimizo wa pili ulio kamili. Kikionyesha wazi jambo hilo, kitabu cha Ufunuo kina picha za kiunabii zinazolingana na ile ishara, na hata hivyo kiliandikwa baada ya uharibifu wa Yerusalemu. (Ufunuo 6:1-8) Hivyo, swali lililo la maana linatokea: Je! ile ishara imeonwa katika siku yetu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki