Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yy sura 6 kur. 43-49
  • Kutunza Mwili Wako

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutunza Mwili Wako
  • Kupata Faida Zote za Ujana Wako
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UBORA WA CHAKULA KILICHOSAWAZIKA
  • USAFI UNALETA AFYA
  • LAZIMA YA KUPUMZIKA VIZURI
  • Mwili
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
  • Mungu Anawapenda Watu Walio Safi
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
  • Usafi Unamaanisha Nini Hasa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Nifanye Nini Ili Nipate Chakula Chenye Lishe?
    Vijana Huuliza
Pata Habari Zaidi
Kupata Faida Zote za Ujana Wako
yy sura 6 kur. 43-49

Sura ya 6

Kutunza Mwili Wako

1, 2. Mwili wa mwanadamu ni kazi bora sana katika njia gani?

SULEMANI, mtu mwenye hekima, aliufananisha mwili wa mwanadamu na nyumba yenye madirisha na milango. Karne zilizofuata, Paulo, mtume Mkristo aliuita “nyumba ya maskani.” (Mhubiri 12:3-7; 2 Wakorintho 5:1, 2) Ili ufaidike sana, mwili wako wahitaji kutunzwa kama nyumba.

2 Wewe wautunza mwili wako namna gani? Je! unaona mwili wako kuwa bora sana? Imekupasa uuone hivyo, kwa sababu mwili wa mwanadamu ni kazi iliyo bora sana kati ya kazi zote za uumbaji duniani. Mwili wako umeumbwa katika njia ambayo ni ngumu kufahamu kuliko mashine yo yote kubwa ya kuhesabia au mashine yo yote iliyopata kufanywa. Hata hivyo mwili unafanya kazi vizuri sana, unaweza kutimiza mambo ya ajabu sana na unafaa sana hali zote. Ni jambo lenye kustaajabisha kufikiria namna mifupa yote, mishipa ya damu na mishipa yote ya fahamu pamoja na viungo vingine vyote vya mwili wa mwanadamu vinavyofanya kazi pamoja kama kitu kimoja. Ni kama mtume Paulo alivyoandika kwamba, ujapokuwa na viungo vingi, “mwili ni mmoja.” Inafaa tukumbuke jambo hilo na kufahamu vilevile ukweli wa maneno yake kwamba, “kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia nacho.” Ndiyo, mwili ni kitu kimoja ijapokuwa una mamilioni na mamilioni ya chembe. Ikiwa unataka upate faida zote za ujana wako na maisha yako yote, usiache kutunza sehemu yo yote ya mwili wako.—1 Wakorintho 12:12, 14-26.

3-5. (a) Nani wanaochukizwa ikiwa huutunzi mwili wako vizuri? (Warumi 14:7, 8) (b) ‘Tunavuna tunachopanda’ namna gani kwa namna tunavyoutunza mwili?

3 Lakini kuna sababu ambayo ni bora zaidi ya kutaka kuutunza mwili wako kwa kadiri unavyoweza. Sababu hiyo ni ili uweze kuutumia umheshimu Muumba wako na vilevile wazazi wako, na jirani yako apate faida. Nyumba isiyotunzwa vizuri haimletei sifa aliyepanga namna itakavyojengwa au mwenye kuijenga. Nyumba isiyotengenezwa vizuri, ambayo ni chafu-chafu au inayonuka vibaya sana inaharibu mtaa wote. Ndivyo na sisi tusipoitunza miili yetu.

4 Ile kanuni ya Biblia inayosema kwamba ‘tunavuna tunachopanda’ inafaa utunzaji wetu wa mwili. (Wagalatia 6:7) Ikitegemea sisi, “mavuno” yanaweza kuwa mema au mabaya. Na si lazima mtu azeeke ndipo aanze kuvuna. Kuvuna kunaanza mara nyingine mapema sana sana maishani.

5 Wewe hutaki uepuke tu “kuwa mgonjwa.” Bila shaka unataka ufurahie afya inayotokana na furaha, kazi njema, akili nzuri, na inayokusaidia uwe mtu wa kufurahiwa na wengine. Basi, ni mambo gani yanayofaa kuangaliwa sikuzote?

UBORA WA CHAKULA KILICHOSAWAZIKA

6-8. Eleza faida ya chakula kilichosawazika juu ya (a) carbo-hydrates, (b) proteins, (c) madini, na (d) vitamins.

6 Kile chakula unachokula hakikupi nguvu tu. Kinatoa vifaa vya kujenga vinavyohitajiwa na mwili wako ili ujiendeleze. Vitu vya asili vinavyoitwa carbohydrates kama vinavyopatikana katika sukari, mkate na viazi, vinakupa nguvu. Lakini namna gani kama karibu chakula chako chote unachokula ni kile kinachotoa vitu hivyo tu? Namna gani kama ungetaka kuishi kwa kunywa soda na tamutamu peke yake? Mwili wako ungeanza kuwa dhaifu kwa kukosa vifaa vinavyohitajiwa ili mwili ujitengeneze kila siku.

7 Unahitaji sikuzote protein zinazopatikana katika maziwa, jibini (cheese), maharagwe, nyama na samaki. Zikikosekana, upesi mishipa yako inalainika na kuwa teketeke (dhaifu sana), na mtu hawezi kukua upesi. Unahitaji madini fulani, kwa sababu bila hizo upesi meno yako yataharibika na mifupa yako itakuwa dhaifu. Mboga za majani zina madini tele. Unahitaji vitamin kwa sababu zinasawazisha mageuzi ya mwili na kuulinda mwili usipate magonjwa fulani. Vitamin zinatoka katika matunda na nafaka. Tena unahitaji kunywa maji mengi, kwa sababu damu na mwili wako vinayategemea.

8 Unaweza kupata matokeo ya chakula kizuri au chakula kibaya wakati wewe bado kijana, si wakati una umri wa miaka 60 au 70 tu. Kwa mfano, uchunguzi umeonyesha kwamba wanafunzi walipopewa chakula bora uwezo wao wa kujifunza ukawa bora vilevile. Kwa kawaida chakula kisichofaa hakiwapi watu faida nzuri, nao wanaelekea zaidi kupatwa na mabaya. Kinaharibu upesi afya ya mwili na uzuri wa asili.

USAFI UNALETA AFYA

9-14. (a) Kuoga sikuzote kunawezaje kulinda afya yako? (b) Wengine wanaokutazama wataonaje mazoea yako ya kujisafisha, na kwa sababu gani? (c) Ni kwa sababu gani ni jambo la maana sana kusafisha meno sikuzote na kwa uangalifu? (d) Biblia yenyewe inasema nini juu ya usafi? (Kutoka 30: 17-21; Mathayo 6:17, 18)

9 Kama vile tunavyofurahia sana kuishi katika nyumba safi, ndivyo tunavyofurahia maisha vile-vile tukitunza miili yetu kuwa safi. Kuoga sikuzote kunaburudisha na kuleta afya. Sikuzote mwili wako unakutana na vijidudu vidogo sana katika hewa na katika vitu unavyoshika. Vingine kati ya hivi vyaweza kuleta ugonjwa. Sabuni inaua vijidudu hivi nayo maji yanaviondoa. Zaidi ni la-zima uangalie sana mikono yako, kwa sababu inashika chakula chako na unaweza kushika watu wengine au vitu wanavyotumia kwa mikono yako.

10 Unapojisafisha unajisikia vizuri zaidi na vile-vile kufanya maisha ya wale wanaokuona au kukukaribia yawe yenye kupendeza zaidi. Ukiona nyumba chafu isiyo na utaratibu, watu wanaoishi ndani unawadhania kuwa wa namna gani? Vivyo hivyo watu wanaelekea kukulaumu kwa sura yako. Uchafu katika uso wako, katika masikio yako, katika shingo yako, katika nywele zako, katika mikono yako au katika kucha zako unaweza kuzuia wengine wasiwe rafiki zako, tena wasikuheshimu. Kama unajisafisha, utajiheshimu mwenyewe zaidi vilevile.

11 Mwili unatoa jasho hata mtu asipofanya sana mazoezi au kazi. Ikiwa jasho linakuwa jingi sana, laweza kufanya mwili wako kunuka vibaya. Kuoga sikuzote, kuosha makwapani na sehemu kama hizo, kunafanya watu wakufurahie zaidi. Vilevile, usafi pamoja na chakula kizuri unafanya sura kuwa bora na nzuri zaidi.

12 Meno nayo ni sehemu inayohitaji kuangaliwa. Vipande vidogo vya chakula vinaweza kukaa katikati au juu ya meno. Siki kali sana inayotolewa na vipande vidogo hivi vya chakula inakula tabaka ya nje ya meno yako. Ikiisha kula mara nyingi, kwa muda wa miezi fulani, ile tabaka ngumu ya nje inapenywa na papo meno yanaanza kuoza. Au kama sivyo, unaweza kuona kuwashwa kwa fizi za meno kisha kulegeza meno. Huenda ukapoteza meno fulani. Meno yaliyooza au mwanya wa meno unaharibu sura yako.

13 Vilevile kinywa kilicho safi kinaondoa harufu yenye kuchukiza. Kunywa bilauri nyingi za maji kila siku kunasaidia. Kumbuka, kinywa chako kinafanana kidogo na mlango wa nyumba. Ikiwa sura ya nyumba si nzuri na harufu zinazotoka mlangoni ni mbaya, watu wataepuka nyumba hiyo.

14 Biblia, Neno la Mungu inatia moyo na kufundisha usafi ijapokuwa si kupita kiasi (kama watu wengine). Mara nyingi mikono safi na miili inayooshwa sikuzote inatumiwa kufananisha usafi wa kiroho wa mtu. Naye mtume Paulo alisema kwa kutia moyo hivi: “Na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu.” (2 Wakorintho 7:1) Je! tuko safi ndani, katika mioyo na akili zetu? Ikiwa ni hivyo, inafaa tujaribu kuwa safi na nje vilevile, sivyo?

LAZIMA YA KUPUMZIKA VIZURI

15-18. (a) Ni kwa sababu gani mwili wa mwanadamu unahitaji kupumzika na kulala usingizi? (b) Ni jambo gani litakalokupata kama hupumziki vya kutosha hata ikiwa unajiona una nguvu? (c) Kutunza milli yetu kunaonyeshaje kwamba twamheshimu Mungu?

15 Mamilioni ya chembe za mwili yanaharibika kila siku na ni lazima nyingine zirudi mahali pa zile zinazoharibika. Mwili wako unakusanya uchafu fulani unaolundamana ndani ya nyama kwa sababu ya kazi na mazoezi unayofanya. Uchafu huu ndio unaokufanya ujisikie kuchoka. Ili mwili wako ujiondolee uchafu ambao umelundamana na kuweza kufanyiza vilevile chembe mpya ili uwe na sura nzuri na kujitengeneza wenyewe, ni lazima mwili wako upumzike vya kutosha. Vilevile, ni lazima mishipa yako ya fahamu na ubongo wako ipumzike. Haiwezi kupumzika usipolala usingizi.

16 Kwa vile wewe ni kijana, labda utadhani inakutosha kulala usingizi kidogo tu. Lakini nguvu ya ujana inaweza kuwa yenye kudanganya. Inaweza kuficha dalili (alama) za uharibifu mkubwa ambao pengine unaendelea kwa sababu ya kutokupumzika vya kutosha. Kwa kweli, mwili wa kijana unaokua wahitaji usingizi mwingi kuliko mtu mzima. Kutolala usingizi wa kutosha kunaharibu akili na kuongeza usahaulifu. Kunapunguza utayari na wepesi wa kutenda kwa mwili. Kunaweza kukufanya uwe mwenye kufadhaika, mwenye wasiwasi, mwenye kukasirika upesi na mgumu kupatana na wengine. Hii inakuwa hivyo sana sana wakati wa mikazo mingi.

17 Kwa hiyo, shirikiana na mwili wako kwa kuupumzisha kama unavyohitaji. Wazazi wako wanapokuambia ulale wakati fulani, fahamu kwamba uongozi wao unafaa. Kazi yako itakuwa bora sana nawe utaifanya kwa wepesi ukilala usingizi wa kutosha kila usiku. Utaona maisha yanafurahisha zaidi tena hutakuwa na magumu mengi.

18 Ikiwa tunashukuru kwa vile tuna uzima tunaofurahia katika miili yetu kuwa zawadi, basi imetupasa tuitumie miili hiyo imheshimu Muumba wetu na Mwanawe vilevile, aliyetoa uhai wake ili tupate uzima wa milele. Haitupasi kuitumia vibaya wala kukosa kuitunza miili yetu hata kidogo kwa sababu ya uzembe au upumbavu au kwa sababu tu za kichoyo. Kufanya hivi kungeonyesha hatumheshimu Yeye aliyetupa maisha zetu. Badala ya kufanya hivyo, na tufuate shauri hili pole la Biblia: “Mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.” Kwa kushukuru mipango yake ya upendo, yeye atakupa zawadi nyingi na kukubariki.—1 Wakorintho 10:31.

[Picha katika ukurasa wa 45]

Ili uwe na afya njema ni lazima ule chakula kilichosawazika.

[Picha katika ukurasa wa 49]

Ili mwili wako ujiondolee uchafu ni lazima upumzike vya kutosha

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki