Sura ya 12
Kufurahisha Mioyo ya Wazazi Wako
1. Kwa nini inafaa kuheshimu wazazi?
KWAMBA sisi tungali tu wachanga sana, kwamba tunaelekea kuwa watu wazima, au kwamba sasa tumekuwa wanaume na wanawake wazima, sisi sote ni watoto wa mtu fulani. Ingekuwa vigumu kukadiri kufaa kwa miaka yote 20 ya kutunzwa, kufanya kazi, fedha na jitihada za kujinyima vitu zilizotumiwa juu ya wengine kati yetu tangu uchanga mpaka kuwa watu wazima. Na kwa kweli, wazazi wetu walimpa kila mmoja wa sisi jambo fulani tusiloweza kuwarudishia. Kwa maana, kati ya mambo mengine yote ambayo tumepata kutoka kwao, tumepata uzima wetu tulio nao sasa. Pasipo wao, tusingekuwapo. Kweli hii peke yake iliyo wazi imepaswa iwe sababu ya kutosha zaidi kutufanya tuitii amri hii ya kimungu: “Waheshimu baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi, upate heri, ukae siku nyingi katika dunia.”—Waefeso 6:2, 3.
2. Kwa nini imetupasa tujione kwamba tuna dent na wazazi wetu?
2 Ijapokuwa kwanza tuna deni na Muumba wetu, akiwa Chanzo cha uzima wote, imetupasa tujione kuwa na deni sana na wazazi wetu. Twaweza kuwapa nini badala ya kile walichotupa? Mwana wa Mungu alisema kwamba mali zote za ulimwengu huu haziwezi kununua, uzima, kwa maana huwezi kukadiri bei ya uzima. (Marko 8:36, 37; Zaburi 49:6-8) Neno la Mungu linatuambia hivi: “Musiwe na deni ya mutu, ila kupendana.” (Waroma 13:8, ZSB) Katika njia ya pekee, imetupasa tujione kuongozwa kuendelea kuwapa wazazi wetu upendo kama jambo tunalodaiwa nao muda wote wa kuishi kwao na wa kuishi kwetu. Ijapokuwa hatuwezi kuwapa uzima kama vile walivyotupa, tunaweza kuwapa jambo fulani linalofanya maisha yawe yenye kufaa. Tunaweza kuwapa kitu cha kuwaongezea furaha na kujiona kuridhika sana. Tunaweza kufanya hivyo katika njia ya pekee ambayo labda hakuna watu wengine wanaoweza kuwapa, maana sisi ni watoto wao.
3. Kulingana na Mithali 23:24, 25, ni sifa gani katika mtoto zinazoweza kuwafanya wazazi wake wafurahi?
3 Kama Mithali 23:24, 25 isemavyo: “Baba yake mwenye haki atashangilia; naye amzaaye mtoto mwenye hekima atamfurahia. Na wafurahi baba yako na mama yako; na afurahi aliyekuzaa.” Ni tamaa ya asili ya wazazi kuweza kujivunia mambo ambayo watoto wao wanafanya, kuwafurahia. Je! wazazi wetu wanaona hivyo?
4. Wakolosai 3:20 linaongoza watoto wafanye nini?
4 Jambo hilo lategemea sana kama tunaheshimu sana cheo chao na kusikiliza shauri lao. Kwa wale ambao bado ni watoto, shauri la Mungu ni: “Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote; maana jambo hili lapendeza katika Bwana.” (Wakolosai 3:20) Kwa wazi “mambo yote” hayamaanishi kwamba wazazi wana mamlaka ya kutaka mambo yasiyopatana na Neno la Mungu, lakini linaonyesha kwamba, wakati tungali watoto, wao wana daraka la kutuongoza katika mambo yote ya maisha.—Mithali 1:8.
5. Kijana angejiuliza nini kwa habari ya mambo ambayo angetazamia watoto wake mwenyewe wamfanyie?
5 Je! sasa wewe ni mtoto? Huenda siku moja ukawa mzazi. Je! ungetaka watoto ambao wangekuheshimu, au watoto ambao wangekuwa wakaidi, labda wale ambao wangejifanya tu kama wanasikiliza, kumbe hawangetii wakati wewe hupo? Badala ya kuleta furaha, Mithali 17:25 inasema: “Mwana mpumbavu ni huzuni kwa babaye, na uchungu kwa mamaye aliyemzaa.” Kama vile ulivyo na uwezo wa pekee kufurahisha wazazi wako, vilevile wewe, kuliko watu wengine wo wote, unaweza kuwahuzunisha sana na kuwakatisha tamaa. Mwenendo wako utaonyesha namna itakavyokuwa.
KUJIPATIA HEKIMA KUNACHUKUA WAKATI
6. Ni mfano gani unaoonyesha kwamba kwa kawaida hekima inatokana na uzee?
6 Inawafaa watoto wafahamu kwamba umri ni jambo la maana sana katika kujipatia hekima. Je! sasa wewe una umri wa miaka 10? Unaweza kuona kwamba unajua mengi kuliko wakati ulipokuwa mwenye umri wa miaka mitano, sivyo? Je! sasa una miaka 15? Unajua mengi kuliko ulipokuwa mwenye miaka 10, sivyo? Je! sasa unakaribia kuwa mwenye umri wa miaka 20? Inakupasa ufahamu kwamba bado unajua mengi kuliko wakati ulipokuwa mwenye miaka 15. Ni vyepesi kukumbuka na kuona kwamba umri unakufanya uwe na hekima zaidi, lakini ni vigumu kutazama mbele na kuikubali kweli hii. Hata mtoto ajione ana hekima gani, imempasa afahamu kwamba wakati ujao waweza kuleta hekima kubwa zaidi.
7. Ni soma gani juu ya hekima tunaloweza kujifunza kutokana na shauri alilopewa Mfalme Rehoboamu?
7 Maana ya hayo ni nini? Kwamba wazazi wako wana ujuzi mwingi kuliko wewe kwa sababu wana umri wa miaka mingi kuliko wewe. Kwa kufaa vilevile, wana hekima nyingi ya kushindana na magumu ya maisha na kuyaondoa kuliko wewe. Hilo ni jambo gumu kwa watoto wengi kukubali. Huenda wakawataja wazee kuwa ‘watu wanaoshikilia sana mambo (mitindo) ya kale.’ Huenda wengine wakawa hivyo, lakini wengi hawako hivyo, kama vile si watoto wote walio wavivu kwa sababu tu wengine ni wavivu. Ni jambo la kawaida kwa vijana kujiona kuwa wana hekima nyingi kuliko wazee. Mfalme wa Israeli alifanya kosa hilo la upumbavu, akapata matokeo mabaya. Wakati Rehoboamu mwenye umri wa miaka 41 alipomrithi Sulemani baba yake kuwa mfalme, watu waliomba mizigo yao ipunguzwe uzito. Rehoboamu aliwaomba wazee shauri, nao wakamshauri atumie upole na fadhili. Ndipo alipowaendea vijana nao wakamshauri atumie ukali. Alipokea shauri lao. Matokeo? Makabila kumi kati ya 12 yaliasi naye Rehoboamu akaachwa akiwa na sehemu ndogo sana ya ufalme wake. Ni wazee ndio waliotoa shauri la hekima, si watoto. “Wazee ndio walio na hekima, na katika kuishi siku nyingi iko fahamu.”—Ayubu 12:12; 1 Wafalme 12: 1-16; 14:21.
8. Biblia inatutia moyo tuwe na maoni gani kwa wazee, pamoja na wazazi wetu?
8 Usilione shauri la wazazi wako kuwa lisilofaa wakati huu kwa sababu tu wao si vijana. Badala yake, kama Neno la Mungu linavyosema: “Msikilize baba yako aliyekuzaa, wala usimdharau mama yako akiwa mzee.” Uzee wastahili heshima. “Simama mbele ya wenye imvi na heshimu uso wa muzee, na utaogopa Mungu wako; mimi ni [Yehova].” Ni kweli kwamba watoto wengi wanadharau amri hizo. Lakini kufanya hivyo hakukuwaletea furaha, wala wazazi wao bila shaka.—Mithali 23:22, UV; Walawi 19:32, ZSB.
TIMIZA SEHEMU YAKO
9. Jamaa inakuwa namna gani wakati mrnoja, wa washiriki wake anaponung’unika bila sababu au anapokuwa mkorofi?
9 Hakuna sababu ya kuzunguka kwa maneno—unayofanya yanapasa (yanahusu) watu wengine. Mshiriki mmoja wa jamaa akiumia, wote wanasumbuka. Vilevile, mmoja akiwa mnung’unikaji au mkorofi, amani ya jamaa nzima inaharibika. Yampasa kila mtu atimize sehemu yake ili jamaa iwe na maisha ya furaha.—Linganisha 1 Wakorintho 12:26.
10. Sababu gani ni faida ya watoto kujifunza kufanya kazi nzuri?
10 Kuna mambo yanayofaa, yenye kujenga ambayo unaweza kufanya. Wazazi wanafanya kazi kwa bidii ili watimize mahitaji ya jamaa. Ukiwa mtoto nawe unaishi nyumbani, unaweza kusaidia. Sehemu kubwa ya maisha inatumiwa kazini. Watu wengine wananung’unikia hilo. Lakini ukijifunza kufanya kazi na kuifanya kwa nia nzuri, itakuletea furaha za kweli. Kwa upande mwingine, mtu asiyetimiza fungu lake lakini anatazamia wengine wamfanyie kila jambo, hajui furaha hiyo hata kidogo, naye anawatia wengine uchungu, kama Biblia inavyosema, anakuwa ‘kama moshi katika macho ya mtu.’ (Mithali 10:26; Mhubiri 3:12, 13) Kwa hiyo, unapogawiwa kufanya kazi nyumbani, zifanye, tena uzifanye vizuri. Na ikiwa wataka kweli kufurahisha wazazi wako, fanya kazi zaidi ya hizo, pasipo kuombwa. Labda utaiona kazi hiyo kuwa yenye kufurahisha kuliko zote—kwa kuwa uliifanya kwa sababu moyo wako unataka kuwafurahisha.
11. Maneno au matendo ya mtoto yanaweza kuwaleteaje wazazi wake sifa?
11 Watu wanapovutwa na mtoto, kwa kawaida wanataka wajue ni mtoto wa nani. Kijana Daudi alipoonyesha uhodari na imani ya ajabu, mara hiyo Mfalme Sauli aliuliza hivi: Kijana huyu ni mwana wa nani? (1 Samweli 17:55-58) Unachukua jina la jamaa yako. Unayofanya na namna ulivyo itaonyesha namna watu wanavyoona jina hilo na wazazi waliokupa jina hilo. Kuna njia nyingi sana ambazo unaweza kuleta heshima kwa wazazi wako—katika mtaa wako na katika shule—kwa kuonyesha fadhili, hali ya kusaidia, hali ya kuheshimu na urafiki kwa wengine. Kwa njia hiyo unamheshimu Muumba wako pia.—Mithali 20: 11; Waebrania 13:16.
12. Sababu gani inawafaa watoto washirikiane na jitihada za wazazi wao za kuwalea?
12 Furaha ya wazazi wake inafungamana na furaha yako. Jitihada zao za kukuzoeza zina kusudi la kukupa mwanzo mzuri wa kuelekea kwenye uzima. Shirikiana nao nawe utawapa furaha kubwa, kwa maana wanapendezwa na hali njema yako. Kama mwandikaji aliyeongozwa na Mungu alivyosema: “Mwanangu, kama moyo wako una hekima, moyo wangu utafurahi.” (Mithali 23:15) Wazazi wako wakikubali daraka lao mbele za Mungu wakuongoze katika njia za hekima ya kweli, wasaidie walitimize daraka kilo kwa uaminifu. “Sikiliza shauri na kukubali kutiwa adabu, upate kuwa mwenye hekima siku zako za usoni.”—Mithali 19: 20, NW.
13. Jambo gani laweza kusaidia mtoto awe na maoni yanayofaa juu ya vizuizi anavyowekewa na wazazi wake?
13 Huenda zikawako nyakati unapoona kwamba wazazi wako wanataka mambo mengi mno kutoka kwako au kwamba wanakuwekea vizuizi vingi mno. Si vyepesi kupata usawa unaofaa katika mambo ya adabu. Siku moja, ukiwa na jamaa, labda utaona kwamba unapata ugumu ule ule. Ikiwa wazazi wako wanakuzuia usishirikiane na vijana fulani, au wanakulinda juu ya matumizi ya dawa za kulevya, au wakikuambia uepuke ushirika usiofaa na wanaume au wanawake, fikiria namna hilo lilivyo jambo bora sana kuwa na wazazi wanaokutia adabu kuliko wale wasiojali! (Mithali 13: 20; 3:31) Tii adabu yao wanayokupa. Utajipatia mwenyewe faida na kufurahisha mioyo yao.—Mithali 6:23; 13:1; 15:5; Waebrania 12:7-11.
14, 15. Magumu yanapotokea kati ya washiriki wa jamaa, ni kuthamini kwa kanuni gani za Biblia kunakoweza kusaidia mtoto ahifadhi (alinde) amani?
14 Bila shaka, hali nyingi zinazotokea nyumbani haziletwi na wewe. Lakini maoni yako yanaongoza hali iliyo nyumbani mwenu. Biblia inashauri hivi: “Kama yamkini, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote.” (Warumi 12:18) Si vyepesi sikuzote kufanya hivyo. Sisi sate tuko tofauti; tuna maoni mbalimbali na tunatenda katika njia mbalimbali. Kutakuwako maoni na tamaa mbalimbali. Tuseme tofauti hiyo ikiwa ya ndugu au dada yako. Huenda ukaona kwamba mtu huyo ana choyo. Utafanya nini?
15 Watoto wengine wanapiga kelele mara hiyo, wakishtaki na kudai mmojawapo wa wazazi wao aingilie (azuie) jambo hilo. Au, huenda wakatumia uwezo wao, wakisukuma na kuwapiga wenzao kusudi wapate wanayotaka. Lakini mithali iliyoongozwa na Mungu Ma-sema: Busara ya mtu huiahirisha hasira yake. (Mithali 19:11) Katika njia gani? Kwa vile inavyomfanya afikirie hali zinazoleta hayo na zinazotaka kusamehe. (Labda tendo hilo halikuwa la kukusudia.) Inamfanya akumbuke mara nyingi ambazo yeye mwenyewe amefanya makosa. (Jinsi anavyomshukuru Mungu sana kwa msamaha wake!) Inaweza vilevile kumfanya afahamu kwamba, hata ikiwa ndugu au dada yake amekosa, bado haingemfaa aache hasira yake iharibu amani ya jamaa nzima. Kwa habari ya mtu aliye na busara hiyo, mithali inaendelea kusema: Nayo ni fahari yake kusamehe makosa.—Tazama vilevile Wa-kolosai 3:13, 14.
16. Ni mwenendo gani wa watoto wao unaofurahisha wazazi wanaomwogopa Mungu?
16 Kwanza, jambo linalofurahisha wazazi wanaomwogopa Mungu ni jambo lile lile linaloufurahisha moyo wa Yehova. Jambo linalowakasirisha ni jambo lile lile linalomkasirisha Yehova. (Zaburi 78:36-41) Wazazi wasioijua nia ya Yehova Mungu wanafurahi ikiwa watoto wao wanapendwa sana na ulimwengu, wanajifanyia jina, wanaehuma fedha nyingi, na vivyo hivyo. Lakini, wazazi ambao Yehova ndiye Mungu wao wanajua kwamba ulimwengu huu unapita pamoja na tamaa take, lakini yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele. (1 Yohana 2:15-17) Hivyo, jambo linalowafurahisha kweli kweli ni kuona watoto wao wakimtii Muumba wao, wakifanya mapenzi yake na kuonyesha sifa zake. Ni kweli kwamba wazazi wanaomwabudu Mungu wanafurahi wanapoona watoto wao wakifanikiwa katika masomo yao shuleni. Lakini wanafurahi zaidi wakati mwenendo wao shuleni na mahali penginepo unapoonyesha namna wanavyoshikamana na kanuni za Mungu na kutaka kumpendeza. Nao wanafurahi sana wakati watoto hao wanapoendelea kuzifurahia njia za Yehova bila kuacha mpaka maisha yao ya mtu mzima.
DARAKA LA KUTUNZA WAZAZI
17-19. Wana na mabinti ambao ni watu wazima wanaweza kuonyeshaje kwamba wanawashukuru wazazi wao?
17 Kupendezwa kwetu na wazazi wetu hakupaswi kumalizike ikiwa tunaondoka nyumbani, tunapokuwa watu wazima. Twataka wawe na furaha maisha yao yote. Wametutimizia mahitaji yetu miaka mengi, mara nyingi wakijinyima mambo mengi sana. Ni jambo gani tunaloweza kufanya sasa ili tuonyeshe kwamba tunashukuru sana?
18 Tunaweza kulikumbuka takwa hili la kimungu: Waheshimu baba yako na mama yako. (Mathayo 19:19) Huenda tukawa na kazi nyingi hata tusiwe na nafasi. Lakini inatupasa tufahamu kwamba inafurahisha sana wazazi wetu wakisikia habari kutaka kwetu na kutaka tuwatembelee.
19 Miaka inapozidi kupita, ‘heshima’ hiyo inaweza kuonyeshwa katika njia nyingine. Ukiwapo uhitaji wa msaada wa kimwili, onyesha thamani kwa yote waliyokufanyia, na vilevile matakwa ya haki ya Yehova. Mtume Paulo aliandika habari za wale ambao ni wazee hivi: “Mjane akiwa ana watoto au wajukuu, na wajifunze kwanza kuyatenda yaliyo wajibu wao kwa jamaa zao wenyewe, na kuwalipa wazazi wao. Kwa kuwa hili lakubalika mbele za Mungu.”—1 Timotheo 5:3, 4.
20, 21. (a) Kulingana na Mathayo 15:1-6, kuheshimu wazazi ni pamoja na nini zaidi? (b) Je! kuna jambo ambalo lingemwondolea mtu wajibu wa kuheshimu wazazi wake katika njia hii?
20 Kwamba ‘kuwaheshimu’ wazazi kunaweza kutia ndani kutoa msaada wa kimwili, Maandiko yanaonyesha waziwazi. Pindi moja Mafarisayo walikuwa wamemsemesha Yesu na kuwashtaki wanafunzi wake kwamba wanavunja mapokeo. Yesu alipinga hivi: “Mbona ninyi nanyi huihalifu amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu? Kwa kuwa Mungu alisema, Mheshimu baba yako na mama yako, na, Amtukanaye baba yake au mama yake kufa na afe. Bali ninyi husema, Atakayemwambia babaye au mamaye, Cho chote kikupasacho kusaidiwa na mimi ni wakfu [kwa Mungu] basi asimheshimu baba yake au mama yake. Mkalitangua neno la Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu.”—Mathayo 15: 1-6.
21 Kwa kutangaza kwamba fedha zao au mali zao zilikuwa wakfu (zimetolewa kwa Mungu), kulingana na mapokeo yao, waliondolewa daraka la kutunza wazazi wao. Lakini Yesu hakukubaliana nao. Na sisi leo imetupasa tulifikirie jambo hilo. Ni kweli kwamba, kwa sababu ya mpango wa serikali ulio katika nchi nyingi wa kusaidia watu walio na shida, mahitaji mengine ya wazazi wenye umri wa uzee yanaweza kutimizwa. Lakini msaada huo unaotolewa unatosha kweli? Ikiwa sivyo, au ikiwa hakuna mpango huo hata kidogo, watoto wanaoheshimu wazazi wao watafanya kadiri wawezavyo ili watimize mahitaji yao. Kweli kweli kutunza wazazi wenye umri wa uzee walio na shida ni “wajibu” kama mtume Paulo alivyosema, ni ushuhuda unaoonyesha kwamba mtu amejitoa kwa Yehova Mungu, Mwanzishi wa mpango wa jamaa.
22. Zaidi ya vitu vya kimwili, imetupasa tuwape wazazi wetu nini?
22 Lakini, tusidhani kwamba wazazi wazee wakiwa na chakula kinachofaa, mavazi na nyumba, hakuna zaidi wanayotaka. Wanataka vilevile mambo ya moyoni na ya kiroho. Wanahitaji upendo na uangalifu unaotumainisha, wanahitaji sana hayo mara nyingi. Katika maisha yetu yote tunahitaji tujue kwamba mtu fulani anatupenda, kwamba sisi tuna shirika na mtu fulani, kwamba hatuko peke yetu. Haiwapasi watoto wakose kuwatimizia wazazi wao wazee mahitaji yao ya kimwili au ya moyoni. “Yeye anayemtendea baba yake mambo mabaya na kumfukuza mama yake ni mwana anayetenda kwa kuaibisha na kwa kufedhehesha.”—Mithali 19:26, NW.
23. Mtoto anaweza kuwafurahishaje wazazi wake?
23 Tangu utoto mpaka kuwa mtu mzima, watoto wana sehemu ya maana katika maisha ya wazazi wao. Watoto wengi wanaleta masikitiko mengi na kukata tamaa. Lakini ukiheshimu cheo cha wazazi wako na kusikiliza shauri lao, ukiwaonyesha upendo na shauku ya kweli, unaweza kufurahisha mioyo yao. Ndiyo, “mpe baba yako na mama yako sababu ya kufurahi, mwache mama aliyekuzaa ashangilie.”—Mithali 23: 25, New English Bible.