Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yy sura 10 kur. 72-78
  • Unawaonaje Wazazi Wako?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Unawaonaje Wazazi Wako?
  • Kupata Faida Zote za Ujana Wako
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UTII WANAOSTAIHLI WAZAZI
  • MIFANO YA KUJIFUNZA KWA KUTII
  • Kufurahisha Mioyo ya Wazazi Wako
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • Wazazi—Wazoezeni Watoto Wenu Kwa Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Nifanye Nini Wazazi Wangu Wanapogombana?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
  • Kukadiria Mahitaji ya Wazazi Wako
    Amkeni!—1994
Pata Habari Zaidi
Kupata Faida Zote za Ujana Wako
yy sura 10 kur. 72-78

Sura ya 10

Unawaonaje Wazazi Wako?

1-3. (a) Maoni ya mtu juu ya wazazi wake yanaonyesha nini juu yake? (b) Vijana ambao unajua wana maoni gani juu ya wazazi wao? Je! unakubaliana nao? (c) Ni malezi gani yanayoweza kusaidia kijana aheshimu wazazi wake, na kwa sababu gani?

WENGINE wanapokuambia namna wanavyowaona wazazi wao, wanakuambia vilevile namna walivyo. Ndiyo, unalosema na kutendea wazazi wako linafunua yaliyo katika akili na moyo wako mwenyewe. Yanaonyesha ulivyo sasa. Vilevile yanaonyesha waziwazi utakavyokuwa wakati ujao. Hii ni kwa sababu mwendo ambao unasitawisha nyumbani unageuka polepole kuwa kawaida yako.

2 Vijana wengine wanasitawisha maoni mabaya juu ya wazazi wao karibu katika kila jambo. Wengi wanadhani wazazi wao hawawafahamu wala hawajaribu kuwafahamu, kwamba ni watu wanaoshikilia tu mambo ya kale wasiweze kutoa uongozi wo wote unaofaa katika ulimwengu huu wenye maendeleo ya haraka. Maoni haya yanageuka upesi kuwa nia ya uasi inayoonyeshwa na wengi. Yasipozuiwa, yanageuka upesi kuwa mazoea. Yataonekana kwa namna unavyotendea watu wasio wa jamaa yako. Na yanaweza vilevile kukutia katika matata makubwa kabla hujajua, kwa sababu ya kutotaka kutii sheria zinazokusudiwa kuleta faida na kulinda jamii ya kibinadamu.

3 Hata hivyo kuna wengine ambao maoni na matendo yao hayako hivyo. Wanakua wakiheshimu wazazi wao. Vijana hawa wanajua sababu gani ulimwengu una matata mengi mno na wanajua wanayotumainia kupata wakati ujao. Kwa hiyo hawalazimiki kufuata maoni mabaya ya wengine. Wanafahamu kwamba wazazi wao wamewafundisha kuheshimu kanuni bora zaidi za mwendo wa kibinadamu, kanuni zinazopatikana katika Neno la Mungu lililoandikwa. Kama Biblia inavyoshauri: “Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana.” Vijana hawa wameitikia malezi hayo na wanayatii kwa kupenda. Kwa sababu hiyo, wanathamini cheo walicho nacho katika jamaa. Kunakuwa na uhu-siano mzuri nyumbani.—Waefeso 6:4.

UTII WANAOSTAIHLI WAZAZI

4-6. (a) Mpaka sasa wazazi wako wamekutendea nini maishani? (b) Unawezaje kuonyesha kwamba unathamini waliyokutendea? (Waefeso 6:1, 2)

4 Lakini namna gani wale ambao wazazi wao hawajaribu kuwafundisha kanuni za Biblia? Je! inamaanisha si lazima wawaheshimu na kuwatii wazazi wao? Ijapokuwa uongozi mzuri unakosekana pasipo kanuni za Mungu, jambo hili halipunguzi lazima ya vijana hawa kusitawisha maoni mazuri juu ya wazazi wao. Kwa sababu gani? Kuna sababu nyingi.

5 Kwa vile hujapata kujitegemea wakati wo wote, labda huthamini sana mambo yote ambayo wazazi wako wamekufanyia. Lakini simama ufikiri: Baba na mama yako wamekutunza kila siku tangu ulipozaliwa. Wamekupatia chakula na mavazi, na nyumba mwa kuishi, nao wamekusomesha.

6 Kama ungemwandika mtu afanye kazi ambayo wazazi wako wamekufanyia tangu ulipozaliwa, ungelipa fedha nyingi sana. Kwa sababu ya yote hayo, wazazi wako wanastahili heshima. Wakati ujao, utakapooa au kuolewa na kuwa mzazi, utathamini zaidi sana mambo mengi waliyokufanyia wazazi wako. Lakini mbona usionyeshe thamani hiyo sasa? Kama unawapenda wazazi wako kama wanavyokupenda kwa kuwaheshimu na kuwatii, hapo unaonyesha kwamba unaendelea kuwa mtu aliyekomaa, aliye na akili nzuri anayewathamini wale wanaomtendea mema.

7-12. (a) Kijana aoneje makosa ya wazazi wake? (Mathayo 6:14, 15) (b) Mungu amewapa wazazi cheo gani kama inavyoonyeshwa katika Biblia? (Mithali 6:20) Sababu gani huu ni mpango wa lazima? (c) Kukataa kutii wazazi ni jambo zito namna gani?

7 Hivi haina maana kwamba wazazi wako hawana makosa. Bila shaka wanafanya makosa. Wewe wafanya makosa vilevile. Kwa kuwa huna ujuzi wa maisha kama wao, inaelekea unafanya makosa mengi hata zaidi. Je! unalaumu wazazi wako kwa sababu ya makosa yao na kuwatazamia wasiseme lo lote juu ya makosa yako? Ili usawazike, imekupasa ujifunze kuwasamehe makosa yao, kama vile wao wamekusamehe makosa yako. Na kwa vile wanalo daraka zito zaidi, ni wazi kwamba mara nyingi watafanya makosa. Kanuni ya Biblia inasema kweli hivi: “Mtu asiyezoea rehema atapata hukumu yake bila rehema. Rehema inafurahia hukumu kwa ushindi.”—Yakobo 2:13, NW.

8 Walakini, huenda mara nyingine ukadhani wazazi wako wamekosa, kumbe ni kwa vile maoni yao na maoni yako hayapatani tu. Inapokuwa hivyo, nao wazazi wako wamefanya uamuzi juu ya jambo hilo, ufanye nini?

9 Ni lazima ukumbuke kwamba cheo cha wazazi wako si sawa na cheo chako. Mzazi anawakilisha mtu mkubwa zaidi katika mpango wa Mungu. Mungu amewapa wazazi wako mamlaka na daraka usilokuwa nalo bado. Kwa sababu hiyo, wazazi wako ndio wenye mamlaka ya kuamua kabisa mambo yanayokupasa. Ndiyo sababu Neno la Mungu linashauri hivi: “Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote; maana jambo hili lapendeza katika Bwana.” Bila shaka, hii inamaanisha kutii kila jambo wanalotaka wazazi wako lakini lisilovunja sheria za Mungu.—Wakolosai 3:20.

10 Ni lazima uweko utaratibu katika jamii ya wanadamu. Bila utaratibu, kungekuwako fujo, hata ukosefu wa utawala. Kwa mfano, baharia (msafiri wa maji) hamwambii nahodha namna ya kuendesha merikebu, wala mcheza mpira hamwambii msimamizi namna ya kuongoza chama cha mpira. Ni kweli kwamba nahodha mzuri na msimamizi mzuri anakaribisha na kuomba mawazo kutoka kwa wale walio chini yake. Walakini, mamlaka yao ingedharauliwa upesi, tena kungetokea fujo na mvurugo kama wangeruhusu wengine kuwaamuru na kuwaambia jambo la kufanya. Je! sivyo?

11 Vilevile, ni lazima uweko utaratibu katika jamaa. Na humo ndimo Mungu amemweka baba awe kichwa, naye mama akishirikiana sana na baba. Wazazi wote wawili wamewekwa wasimamie watoto wao. Kwa hiyo wazazi wako wanapokuwekea matakwa fulani ya kufuata, kama vile kukuambia wakati ambao inakupasa urudi nyumbani usiku, na mtu unayeweza kushirikiana naye, unavyojipamba, na mambo mengine, nawe unayatii, hapo unaheshimu mpango wa Mungu. Unapokataa kutii wazazi wako, unadharau mpango wa Mungu. Kufanya hivyo ni kupingana na Mungu, Muumba wako wewe na wazazi wako! Nawe wajua mtu atakayepata hasara. Basi, unavyofuata uongozi wa wazazi wako, ndivyo unavyoonyesha maoni yako juu ya Yehova Mungu aliye mkuu kuliko wao, maana inawapasa wamtii.

12 Ndiyo sababu Neno la Mungu linasema hivi: “Jicho la mtu amdhihakiye babaye, na kudharau kumtii mamaye; kunguru wa bondeni wataling’oa, na vifaranga vya tai watalila.” Ndiyo, maoni mabaya juu ya wazazi yanaweza kuangamiza vijana. —Mithali 30:17.

MIFANO YA KUJIFUNZA KWA KUTII

13-17. (a) Kujifunza kuheshimu na kutii wazazi wako kunaweza kukusaidia namna gani utakapokuwa mzazi? (b) Kunaweza kukusaidia namna gani shuleni na unapomfanyia tajiri kazi? (c) Zaidi sana, kutafanya uhusiano (ujamaa) wako na Mungu uwe namna gani?

13 Wakati fulani utakapokuwa mtu mzima na labda uwe na jamaa yako mwenyewe, je! hungetaka watoto wako wakuheshimu na kukutii? Lakini kama hukujifunza kutii wazazi wako mwenyewe, je! inawezekana kwamba utawalea watoto vizuri sana waonyeshe heshima hiyo? Biblia yasema kwamba unachopanda ndicho unachovuna. (Wagalatia 6:7) Jifunze kutii katika cheo kidogo ulicho nacho sasa, na kwa kufanya hivyo utasaidiwa utimize daraka kubwa zaidi la mtu mzima, labda wakati ujao, daraka la kuwa mzazi.

14 Tena, ukisitawisha maoni mabaya juu ya wazazi wako, yanaweza kuonekana katika mambo mengine utakayofanya wakati ujao. Kwa mfano, ukimfanyia tajiri kazi, je! utakuwa ukichukia mamlaka yake anayotumia juu yako? Anapokupa kazi ya kufanya, je! utaona vigumu kutii? Je! utanung’unika sikuzote juu ya kazi yako? Na namna gani maoni yako juu ya wale unaofanya kazi pamoja nao? Labda utajikuta ukiwanung’unikia sikuzote, bila kuwashukuru hata kidogo kwa mambo mema ambayo wanakutendea. Au ukienda shuleni kujifunza kazi, au kama unafundishwa kazi, pengine baada ya juma chache utaanza kujiona kama unajua zaidi kuliko mwalimu wako. Maoni hayo yote yanaweza kukusikitisha na kukutaabisha sana kwa vyepesi. Yanaweza kuwa matokeo ya kusitawisha maoni mabaya juu ya wazazi wako.

15 Kwa hiyo, yakubali maisha ya jamaa na kukikubali cheo ulicho nacho ndani yake. Fahamu kwamba ni njia ya Mungu, na ya kwamba njia yake ndiyo inayofaa zaidi sana.

16 Lakini ukikataa kukubali cheo chako kinachofaa katika jamaa wakati wa ujana wako, basi unajiletea matata. Kufanya hivyo hakutaharibu uhusiano wako na wazazi wako na wengine na maisha yako ya wakati ujao tu; bali zaidi sana, kutaharibu uhusiano wako na Mungu. Naye ndiye mwenye kuamua kama utaishi milele katika taratibu yake mpya au utaharibiwa wakati taratibu hii mbovu ya mambo itakapoharibiwa upesi. Itikia kusihi huku: “Mwanangu, usiisahau sheria yangu, bali moyo wako uzishike amri zangu. Maana zitakuongezea wingi wa siku, na miaka ya uzima, na amani.”—Mithali 3:1, 2.

17 Ebu ifikirie zawadi ambayo watapokea wale watu wanaotii amri za Baba yetu wa kimbinguni na wasiosahau sheria Yake. Zawadi ni “wingi wa siku, na miaka ya uzima, na amani.” Je! ndilo unalotaka? Je! wataka kuishi muda mrefu, ufurahie kweli kweli maisha yenye amani na yenye furaha? Basi hakikisha hivyo kwa kusikiliza maneno ya Mungu ya kukutia moyo uwatii wazazi wako.

[Picha katika ukurasa wa 76]

Je! unaheshimu wazazi wako kama wanavyopaswa kuheshimiwa?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki