Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • my hadithi 36
  • Ndama ya Dhahabu 36

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ndama ya Dhahabu 36
  • Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Walivunja Ahadi Yao
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Yesu Alisema Tunapaswa Kuwatendeaje Wengine?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Kuzijua Njia za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
Pata Habari Zaidi
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
my hadithi 36
Waisraeli wakiimba, wakicheza dansi, na kuabudu ndama ya dhahabu

HADITHI YA 36

Ndama ya Dhahabu 36

MAMA WEE! Sasa watu wanafanya nini? Wanaabudu ndama! Kwa nini wanafanya hivyo?

Musa anapokawia mlimani, watu wasema hivi: ‘Hatujui yaliyompata Musa. Basi na tufanye mungu atutoe katika nchi hii.’

‘Vema,’ Haruni ndugu yake Musa asema. ‘Vueni pete zenu za dhahabu masikioni mniletee.’ Haruni anaziyeyusha na kufanya ndama ya dhahabu. Kisha watu wasema hivi: ‘Huyu ni Mungu wetu, aliyetutoa katika Misri!’ Halafu Waisraeli wanafanya karamu kubwa, na kuiabudu ndama hiyo ya dhahabu.

Yehova anapoona hayo, anakasirika sana. Anamwambia Musa hivi: ‘Fanya haraka ushuke. Watu wanafanya vibaya sana. Wamesahau sheria zangu nao wanaabudu ndama ya dhahabu.’

Musa anavunja mabamba mawili ya mawe yaliyokuwa yameandikwa Amri Kumi

Musa anashuka haraka mlimani. Anapokaribia, anaona hivi. Watu wanaimba na kucheza wakizunguka ndama ya dhahabu! Musa anakasirika sana hata anayatupa chini mabamba mawili ya mawe yenye kuandikwa sheria, nayo yanavunjika-vunjika. Kisha anachukua ndama ya dhahabu na kuiyeyusha kabisa. Halafu anaisaga kuwa unga.

Watu wamefanya jambo baya sana. Musa anawaambia wanaume kati yao wachukue panga zao. ‘Wale watu wabaya walioiabudu ndama ya dhahabu lazima wafe,’ Musa anasema. Basi wanaume hao wanawaua watu 3,000! Inatupasa tumwabudu Yehova pekee kuliko miungu ya uongo, sivyo?

Kutoka 32:1-35.

Maswali ya Funzo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki