Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • my hadithi 44
  • Rahabu Anaficha Wapelelezi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Rahabu Anaficha Wapelelezi
  • Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Rahabu alimwamini Yehova
    Wafundishe Watoto Wako
  • Rahabu Alisikiliza Habari
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Rahabu Awaficha Wapelelezi
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • ‘Alitangazwa Kuwa Mwadilifu kwa Matendo’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Pata Habari Zaidi
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
my hadithi 44
Rahabu na mmoja wa wapelelezi kwenye dirisha lake lililo na kamba nyekundu

HADITHI YA 44

Rahabu Anaficha Wapelelezi

WANAUME hao wana taabu. Lazima waondoke, ama watauawa. Ni wapelelezi Waisraeli, na anayewasaidia ni Rahabu. Rahabu anakaa katika nyumba hiyo juu ya ukuta wa mji wa Yeriko. Ebu tuone sababu gani wanaume hao wana taabu.

Waisraeli wako tayari kuvuka Mto Yordani waingie Kanaani. Lakini kwanza, Yoshua anatuma wapelelezi wawili. Anawaambia hivi: ‘Nendeni mkaitazame nchi na mji wa Yeriko.’

Mpelelezi mmoja anashuka chini kwa kutumia kamba nyekundu ya Rahabu

Wapelelezi hao wanapoingia Yeriko, wanakwenda nyumbani kwa Rahabu. Lakini mtu fulani anamwambia mfalme hivi: ‘Waisraeli wawili waliingia mjini usiku huu ili wapeleleze nchi.’ Anaposikia hivyo, mfalme anatuma watu kwa Rahabu, wakimwambia hivi: ‘Watoe wale wanaume walioingia nyumbani mwako!’ Lakini Rahabu ameficha wapelelezi hao juu ya dari lake. Anasema: ‘Wanaume fulani walikuja kwangu, lakini sijui walikotoka. Waliondoka kulipoanza kuwa usiku, kabla ya kufungwa lango. Mkifanya haraka, mtawakuta!’ Watu hao wanaanza kuwafuata.

Wakiisha kuondoka, Rahabu anapanda haraka juu ya dari. ‘Najua Yehova atawapa ninyi nchi hii,’ anawaambia wapelelezi hao. ‘Tulisikia alivyoikausha Bahari Nyekundu mlipoondoka Misri, na alivyowaua wafalme Sihoni na Ogu. Nimewahurumia ninyi, basi tafadhali mnipe ahadi, ya kwamba mtanihurumia mimi. Mwokoe baba na mama yangu, ndugu na dada zangu.’

Wapelelezi hao wanaahidi kufanya hivyo, lakini inampasa Rahabu atende jambo fulani. ‘Chukua kamba hii nyekundu uifunge katika dirisha,’ wapelelezi wanamwambia, ‘kisha ukusanye watu wako wote wa ukoo ndani ya nyumba yako pamoja nawe. Tutakaporudi sote kuutwaa Yeriko, tutaiona kamba hii katika dirisha lako tusimwue yeyote nyumbani mwako.’ Wapelelezi hao wanaporudi kwa Yoshua, wanamwambia kila jambo lililotokea.

Yoshua 2:1-24; Waebrania 11:31.

Maswali ya Funzo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki