Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • my hadithi 49
  • Jua Linasimama Tu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jua Linasimama Tu
  • Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Yoshua na Wagibeoni
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Yoshua na Akusaidie Wewe Umtumikie Yehova kwa Uhodari!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • “Yehova Mungu Wetu Ndiye Sisi Tutatumikia”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Kitabu Cha Biblia Namba 6—Yoshua
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
Pata Habari Zaidi
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
my hadithi 49
Yoshua analiambia jua lisimame tu

HADITHI YA 49

Jua Linasimama Tu

MTAZAME Yoshua. Anasema: ‘Jua, simama!’ Jua linasimama. Linakaa siku nzima katikati ya anga. Yehova anafanya hivyo! Lakini ebu tuone kwa nini Yoshua anataka jua liendelee kung’aa.

Wale wafalme wabaya watano katika nchi ya Kanaani wanapoanza kupigana na Wagibeoni, hao Wagibeoni wanamtuma mtu aende kumwomba Yoshua msaada. ‘Njoo kwetu upesi!’ asema. ‘Utuokoe! Wafalme wote wa vilimani wamekuja kupigana na watumishi wako.’

Mara hiyo Yoshua na wanajeshi wake wote wanakwenda. Wanasafiri usiku kucha. Wanapofika Gideoni, wale askari wa wafalme watano wanaogopa na kuanza kukimbia. Ndipo Yehova anaangusha mawe makubwa ya mvua kutoka angani. Askari wengi wanakufa kwa mvua ya mawe kuliko wanaouawa na wanajeshi wa Yoshua.

Yoshua anaona kwamba karibu jua litatua. Kutakuwa usiku, na askari wengi wa wafalme watano wabaya watakimbia. Ndiyo sababu Yoshua anamwomba Yehova na kusema: ‘Jua, simama!’ Jua linapoendelea kung’aa, Waisraeli wanashinda vita.

Kuna wafalme wabaya wengi zaidi katika Kanaani wanaochukia watu wa Mungu. Inamchukua Yoshua na jeshi lake karibu miaka sita kushinda wafalme 31 katika nchi hiyo. Kisha, Yoshua anahakikisha kwamba nchi ya Kanaani imegawanywa ili makabila yanayohitaji eneo, yapewe.

Kunapita miaka mingi, mwishowe Yoshua anakufa akiwa mwenye miaka 110. Wakati yeye na rafiki zake bado hai, watu wanamtii Yehova. Lakini watu hao wema wanapokufa, watu wanaanza kutenda mabaya na kutaabika. Huu ndio wakati wanapohitaji msaada wa Mungu.

Yoshua 10:6-15; 12:7-24; 14:1-5; Waamuzi 2:8-13.

Maswali ya Funzo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki