Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • my hadithi 54
  • Mwanamume Mwenye Nguvu Kuliko Wote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mwanamume Mwenye Nguvu Kuliko Wote
  • Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Yehova Alimfanya Samsoni Awe na Nguvu
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Mtegemee Yehova Kama Samsoni Alivyofanya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
  • Samsoni Ashinda kwa Nguvu za Yehova!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
Pata Habari Zaidi
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
my hadithi 54
Samsoni anaua simba kwa mikono yake tu

HADITHI YA 54

Mwanamume Mwenye Nguvu Kuliko Wote

UNAJUA jina la mwanamume mwenye nguvu kuliko wote? Ni mwamuzi Samsoni. Yehova anampa Samsoni nguvu hizo. Hata kabla ya Samsoni kuzaliwa, Yehova anamwambia mama yake hivi: ‘Upesi utazaa mwana. Ataongoza kuokoa Israeli kutokana na Wafilisti.’

Wafilisti ni watu wabaya wanaoishi Kanaani. Wana wanajeshi wengi, na wanawaumiza Waisraeli sana. Wakati mmoja, Samsoni anapokwenda kwa Wafilisti, simba mkubwa anatokea akinguruma kukutana naye. Lakini Samsoni anamwua simba huyo kwa mikono yake tu. Pia anaua mamia ya Wafilisti wabaya.

Baadaye Samsoni anapendana na mwanamke, Delila. Viongozi Wafilisti wanaahidi kwamba kila mmoja wao atampa Delila vipande 1,100 vya fedha akiwaambia kinachompa Samsoni nguvu nyingi hivyo. Delila anataka fedha zote hizo. Yeye si rafiki wa kweli wa Samsoni, wala wa watu wa Mungu. Anazidi kumwuliza Samsoni kinachompa nguvu nyingi hivyo.

Samsoni na Delila

Mwishowe, Delila amshawishi Samsoni. Naye Samsoni anamwambia siri ya nguvu zake, akisema: ‘Mimi sijanyolewa nywele. Tangu kuzaliwa kwangu, Mungu alinichagua niwe mtumishi wake wa pekee, yaani, Mnadhiri. Nikinyolewa nywele, nitapoteza nguvu.’

Delila anapojua hayo, anamlaza Samsoni katika paja lake. Kisha amwita mtu aje amnyoe nywele. Samsoni anapoamka, anakuta amepoteza nguvu. Ndipo Wafilisti wanakuja kumkamata. Wanamwondoa macho yake mawili, na kumfanya mtumwa wao.

Samsoni anashika nguzo hivi kwamba jengo linawaangukia Wafilisti

Siku moja Wafilisti wanafanya karamu kubwa ili waabudu Dagoni mungu wao. Wanamtoa Samsoni gerezani ili wamcheke. Wakati huo, nywele za Samsoni zimekua tena. Samsoni anamwambia kijana anayemwongoza kwa mkono: ‘Acha nishike nguzo za jengo hili.’ Kisha Samsoni anamwomba Yehova ampe nguvu, naye anashika nguzo hizo. Anapaza sauti hivi: ‘Acha nife pamoja na Wafilisti.’ Wafilisti wanaokula karamu ni 3,000. Samsoni anapoegemea nguzo hizo, jengo laanguka na kuua watu wote hao wabaya.

Waamuzi sura ya 13 mpaka 16.

Maswali ya Funzo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki