Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • my hadithi 58
  • Daudi na Goliathi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Daudi na Goliathi
  • Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • “Vita Ni vya Yehova”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
  • “Vita Ni vya Yehova”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Daudi na Goliathi
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Daudi hakuogopa
    Wafundishe Watoto Wako
Pata Habari Zaidi
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
my hadithi 58
Daudi anatumia kombeo lake huku jeshi la Israeli likimtazama

HADITHI YA 58

Daudi Na Goliathi

TENA Wafilisti wanakuja kupigana na Israeli. Wakati huu ndugu zake Daudi wakubwa watatu wamo katika jeshi la Sauli. Basi siku moja Yese amwambia Daudi hivi: ‘Wapelekee ndugu zako nafaka na mikate. Kaone kama ni wazima.’

Daudi anapofika kwenye kambi ya jeshi, anapiga mbio kwenda kwenye mapigano akawatafute ndugu zake. Goliathi (Goliata), jitu la Wafilisti anajitokeza ili awacheke Waisraeli. Kwa muda wa siku 40 amekuwa akifanya hivyo asubuhi na jioni. Anapaza sauti: ‘Haya, chagueni mmoja apigane nami.’

Goliathi na jeshi la Wafilisti

Daudi anauliza askari fulani hivi: ‘Atapata nini mtu anayemwua Mfilisti huyu na kuwaondolea Waisraeli aibu hii?’

‘Sauli atampa mtu huyo mali nyingi,’ askari anasema. ‘Naye atampa binti yake awe mke wake.’

Lakini Waisraeli wote wanamwogopa Goliathi kwa sababu ni mkubwa mno. Urefu wake ni zaidi ya mita tatu, na ana askari mwingine wa kumchukulia ngao.

Askari fulani wanakwenda kumwambia Mfalme Sauli kwamba Daudi anataka kupigana na Goliathi. Lakini Sauli anamwambia Daudi hivi: ‘Wewe huwezi kupigana na Mfilisti huyu. Wewe ni mtoto tu, yeye amekuwa askari maisha yake yote.’ Daudi anajibu hivi: ‘Mimi niliua dubu na simba aliyechukua kondoo wa baba. Na Mfilisti huyu atakuwa kama huyo. Yehova atanisaidia.’ Basi Sauli anasema: ‘Nenda, Yehova awe nawe.’

Daudi anatelemkia njia ya kijito na kuchagua mawe matano laini, na kuyaweka mfukoni mwake. Kisha anachukua kombeo lake na kwenda kukutana na jitu lile. Goliathi anapomwona anamdharau. Anadhani itakuwa rahisi sana kumwua Daudi.

‘Wewe njoo tu kwangu,’ Goliathi asema, ‘nami nitawapa ndege na wanyama wapate kula mwili wako.’ Lakini Daudi anasema: ‘Wewe unakuja kwangu kwa upanga na mkuki, lakini mimi ninakuja kwako kwa jina la Yehova. Leo hii Yehova atakutia wewe mikononi mwangu nami nitakuangusha chini.’

Papo hapo Daudi anamkimbilia Goliathi. Anachukua jiwe katika mfuko wake, analiweka katika kombeo lake, na kulitupa kwa nguvu zake zote. Jiwe hilo linaingia moja kwa moja kichwani mwa Goliathi, anaanguka na kufa! Wafilisti wanapoona bingwa wao ameanguka, wote wanageuka na kukimbia. Waisraeli wanawafuatia mbio na kushinda vita.

1 Samweli 17:1-54.

Maswali ya Funzo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki