Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • my hadithi 98
  • Juu ya Mlima wa Mizeituni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Juu ya Mlima wa Mizeituni
  • Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Yesu Arudi Mbinguni
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Kuzikumbuka Siku za Mwisho za Yesu Duniani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • “Saa Imekuja!”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Yesu Anarudi Mbinguni
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
Pata Habari Zaidi
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
my hadithi 98
Yesu anazungumza na baadhi ya mitume wake, juu ya Mlima wa Mizeituni

HADITHI YA 98

Juu ya Mlima wa Mizeituni

HUYU ni Yesu juu ya Mlima wa Mizeituni. Wanaume wanne walio pamoja naye ni mitume wake. Ni ndugu Andrea na Petro, pia ndugu Yakobo na Yohana. Unaloona mbali kule ni hekalu la Mungu katika Yerusalemu.

Hekalu huko Yerusalemu

Zimepita siku mbili tangu Yesu alipopanda mwana-punda kuingia Yerusalemu. Ni Jumanne. Mwanzoni mwa siku hiyo Yesu alikuwa hekaluni. Makuhani walitaka kumkamata Yesu wamwue huko. Lakini waliogopa kufanya hivyo kwa sababu watu wanampenda Yesu.

‘Ninyi nyoka na wana wa nyoka!’ Yesu akawaita hivyo viongozi hao wa dini. Ndipo Yesu anasema kwamba Mungu angewaadhibu kwa mabaya yote waliyofanya. Baada ya hayo Yesu anapanda Mlima wa Mizeituni, ndipo mitume hao wanne wanaanza kumwuliza maulizo. Unajua wanavyomwuliza Yesu?

Mitume hawa wanauliza mambo ya wakati ujao. Wanajua Yesu atamaliza ubaya wote duniani. Lakini wanataka wajue wakati hilo litakapotokea. Yesu atakuja tena atawale wakati gani?

Yesu anajua wafuasi wake duniani hawataweza kumwona anapokuja tena. Ni kwa vile atakuwa mbinguni, hawawezi kumwona huko. Basi Yesu anawaambia mitume wake mambo fulani yatakayokuwa yakitokea duniani anapotawala mbinguni. Ni mambo gani hayo?

Yesu anasema kutakuwako vita vikuu, watu wengi watakuwa wagonjwa na kuona njaa, uvunjaji wa sheria utakuwa mbaya sana, tena kutakuwako matetemeko makubwa ya ardhi. Pia Yesu anasema kwamba habari njema za ufalme wa Mungu zitahubiriwa kila mahali duniani. Je! tumeona hayo yakitokea leo? Ndiyo! Basi twaweza kuwa na hakika kwamba sasa Yesu anatawala mbinguni. Karibuni atamaliza ubaya wote duniani.

Mathayo 21:46; 23:1-39; 24:1-14; Marko 13:3-10.

Maswali ya Funzo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki