Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 93 uku. 216-uku. 217 fu. 5
  • Yesu Arudi Mbinguni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu Arudi Mbinguni
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Mamia Wamwona Kabla ya Pentekoste
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Kutokea Mara ya Mwisho, na Pentekoste ya 33 W.K.
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Kutokea Mara za Mwisho, Na Pentekoste ya 33 W.K.
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Juu ya Mlima wa Mizeituni
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 93 uku. 216-uku. 217 fu. 5
Yesu apaa angani huku mitume wake wakitazama

SOMO LA 93

Yesu Arudi Mbinguni

Alipokuwa Galilaya, Yesu alikutana na wafuasi wake. Aliwapa amri hii muhimu sana: ‘Nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote. Wafundisheni mambo niliyowafundisha, na kuwabatiza.’ Kisha akawaahidi hivi: ‘Kumbukeni, nitakuwa pamoja nanyi sikuzote.’

Kwa siku 40 hivi baada ya kufufuliwa, Yesu aliwatokea mamia ya wanafunzi wake huko Galilaya na Yerusalemu. Aliwafundisha mambo muhimu na kufanya miujiza mingi. Kisha Yesu akakutana na mitume wake kwa mara ya mwisho kwenye Mlima wa Mizeituni. Akasema hivi: ‘Msiondoke Yerusalemu. Endeleeni kusubiri kile ambacho Baba aliwaahidi.’

Mitume wake hawakuelewa alichokuwa akimaanisha. Wakamwuliza hivi: ‘Sasa utakuwa Mfalme wa Israeli?’ Yesu akasema, ‘Wakati wa Yehova wa kuniweka niwe Mfalme haujafika. Hivi karibuni mtapokea nguvu kupitia roho takatifu, nanyi mtakuwa mashahidi wangu. Nendeni mkahubiri katika Yerusalemu, Yudea, Samaria, na mpaka sehemu za mbali zaidi za dunia.’

Kisha Yesu akainuliwa juu angani na wingu likamfunika. Wanafunzi wake wakaendelea kutazama angani, lakini hakuwapo tena.

Wanafunzi wakaondoka kwenye Mlima wa Mizeituni na kwenda Yerusalemu. Wakawa wakikutana pamoja kwa ukawaida katika chumba cha juu na kusali. Walikuwa wakimsubiri Yesu awape maagizo zaidi.

“Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na ndipo ule mwisho utakapokuja.”​—Mathayo 24:14

Maswali: Yesu aliwapa wanafunzi wake amri gani? Ni nini kilichotokea katika Mlima wa Mizeituni?

Mathayo 28:16-20; Luka 24:49-53; Yohana 20:30, 31; Matendo 1:2-14; 1 Wakorintho 15:3-6

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki