Sura ya 2
Mfalme wa Umilele
1. Sababu gani imetupasa tuwe na hakika ya kwamba Mungu ni Baba halisi?
YESU alianza “Sala ya Bwana” kwa kumtaja Mungu kuwa “Baba yetu.” Hapana, yeye si Baba ya Yesu Kristo tu, bali mwishowe atakuwa Baba pia ya wanadamu wote wanaomwabudu kwa utii huyo “Msikiaji wa sala” mwenye upendo. (Zaburi 65:2, NW) Akiwa “Mfalme wa umilele” anawahangaikia kikweli na daima viumbe wake, kama baba mwema wa kibinadamu anavyohangaikia watoto wake. (1 Timotheo 1:17, NW) Imetupasa tuwe na hakika ya kwamba “Baba yetu” ni Mtu halisi anayetujali. Bila kujali lugha yetu, rangi ya ngozi yetu au cheo maishani, imetupasa tujione huru kumfikia, maana “Mungu hana ubaguzi. Mtu wa taifa lo lote anayemcha Mungu na kutenda yaliyo haki anapokelewa naye.”—Matendo 10:34, 35, HNWW.
2, 3. Baba yetu amejionyeshaje kuwa Mpaji-Uzima na pia Mwandalizi Mkuu? (Mwanzo 1:1, 2, 31)
2 ‘Baba yetu allye mbinguni’ ndiye Muumba, Yeye aliyewapa wanadamu uzima. (Mathayo 6:9; Zaburi 36:9) Lakini si Mpaji-Uzima wetu tu; ni Mwandalizi Mkuu pia. Tungetazamia baba wa kibinadamu aliye na jukumu aandalie watoto wake makao na chakula, hata kwa kupoteza wakati na jitihada nyingi. Baba yetu wa kimbingu amefanya hivyo, tena kwa njia ya ukarimu sana.
3 Ebu fikiria jinsi huyu “Mfalme wa umilele” mwenye upendo alitayarisha dunia iwe makao yetu. Aliiweka mahali panapofaa kabisa katika anga la mbingu, na kwa nguvu za uweza wake akatokeza hapa duniani kila kitu kilicho cha lazima ili kufanya makao ya kibinadamu yawe yenye furaha. Kisha akaumba mwanamume na mwanamke, akawaweka katika makao hayo yenye kupendeza—zawadi bora kweli kweli kwa “wanadamu”!—Zaburi 115:16; 19:1, 2.
4. (a) Ni busara gani yenye fadhili ambayo Baba yetu alionyesha katika kutayarisha makao yetu? (b) Ni nini kinachotuhakikishia kwamba anataka tuwe wenye furaha?
4 Ni makao yenye kupendeza kama nini ambayo Baba yetu wa kimbingu aliandalia watoto wake hapa duniani! Aliyapanga ili nyakati tulivu za kupumzika usiku zifuate nyakati za mchana za utendaji. Akaagiza kuweko mfuatano wa misimu kwa faida na raha yetu. (Mwanzo 8:22) Akatoa wingi wa maji ambayo ni kifaa cha muhimu kabisa, akayagawa pote duniani ili tupate kuyatumia po pote yanapohitajiwa. Ametandaza zulia lenye kuburudisha la majani mabichi—mamilioni ya kilometa za mraba—katika makao yetu yote ya kidunia. Amelipamba kwa maua yenye rangi nyingi zenye kupendeza. Ameliweka vizuri likiwa na misitu, maziwa na milima ya kupendeza. Chini ya ardhi ameweka akiba kubwa ya makaa-mawe, mafuta na mali nyingine zenye nishati. Anaendelea kujazia ghala ya dunia nafaka, matunda, mboga na vyakula vingine vitamu mpaka kufurika. Baba yetu wa kimbingu ni mwenye hekima na Mwandalizi mwenye kufikiria kama nini! Biblia inamwita “Mungu mwenye furaha.” Kwa wazi, yeye anataka sisi pia tuwe wenye furaha.—1 Timotheo 1:11, NW; Isaya 25:6-8.
“JINA” LA BABA YETU
5. Tamaa ya moyo wetu imepasa iwe nini tunaposali maneno yale ya kwanza ya sala ya kielelezo ya Yesu?
5 Baba yetu wa kimbingu mwenye upendo ana “jina zuri,” sifa njema ya kuwa Mwandalizi Mkuu. Yeye pia ana jina la kibinafsi, kama baba ye yote wa kibinadamu. Kama tuna baba wa kimwili mwenye kustahili, imetupasa tuchukie kuona jina lake na sifa yake ikisutwa. Imetupasa tutake kuona jina lake likiheshimiwa. Hata zaidi hivyo, imetupasa tutamani kuona jina la Baba yetu wa kimbingu likipewa staha. Kwa hiyo, kutokana na ujazi wa mioyo yetu, imetupasa tuweze kuyatumia katika sala yale maneno ambayo Yesu anaweka kwanza katika Sala ya Kielelezo: “Baba yetu uliye katika mbingu, acha jina lako litakaswe.”—Mathayo 6:9; Mithali 22:1, NW, maelezo ya chini.
6. Kwa habari ya Jina la Mungu, wewe ungependa kuona nini?
6 Ndiyo, daima imepasa iwe sala yetu ya bidii kutaka lile jina la Muumba mkuu wa mbingu na dunia liinuliwe juu, likwezwe juu juu ya majina mengine yote, na kuonyeshwa kuwa ndilo jina katika ulimwengu mzima lenye thamani, lenye kujaa maana, lenye kupendeka zaidi sana. Jambo lililo la maana kuliko wokovu wetu wenyewe ni huko kutakaswa kwa jina takatifu la Mungu. Jina na sifa yake lazima vitakaswe—viondolewe masuto yote ambayo viumbe wenye sifa mbaya wamelilundikia.
7. Biblia inaonyesha Mungu ana jina gani la binafsi?
7 Baba yetu wa kimbingu ana jina gani la binafsi? Limefunuliwa katika kifungu cha maneno kinachoonyesha kwamba Mwenye jina hilo tukufu zaidi ana maadui. Katika kusimulia habari za hao, Zaburi 83, mistari ya 17 na 18, inasomwa hivi: “Waaibike, wafadhaike milele, naam, watahayarike na kupotea. Wajue ya kuwa Wewe, uitwaye jina lako YEHOVA, ndiwe peke yako Uliye juu, juu ya nchi yote.”—Ona pia Za-buri 100:3, NW.
8. Maadui wa Mungu wamejaribu kufanya nini na jina lake, na matokeo yakawa nini?
8 Hivyo, jina la Mungu ni YEHOVA. Lakini watu wengi wanaodai kuabudu Mungu wamelidharau sana jina hilo. Wengine hata wamelifuta jina lake katika tafsiri zao za Biblia, na badala yalo wakayaandika majina haya ya,cheo “BWANA” na “MUNGU” kwa herufi kubwa. Si kwamba to zoea hilo linaficha jina maarufu la Mungu, bali pia linafanya iwe vigumu kutofautisha kati ya Bwana Yehova na Bwana Yesu Kristo na “mabwana” na “miungu” wengine wanaotajwa katika Biblia. (Zaburi 110:1; Kumbukumbu la Torati 10:17; Warumi 1:4; 1 Wakorintho 8:5, 6) Watu wanawezaje kusali kwa unyofu jina la Baba litukuzwe, au litakaswe, na hali wanatafuta kuficha jina hilo?
9. (a) Jina la Mungu linaandikwaje katika Kiebrania, na katika lugha nyingine? (b) Biblia inaonyesha Mungu kuwa nafsi ngapi?
9 Jina lisilo na kifani la Mungu linaonyeshwa katika Kiebrania, ile lugha ya kwanza iliyotumiwa kuandika Biblia, kwa herufi hizi , ambazo watu fulani wanatamka Yah’weh. Namna ya jina hilo inayokubaliwa na watu wengi katika Kiswahili ni “Yehova,” na jina hilo linaonyeshwa kwa njia inayofanana na hiyo katika lugha nyingine. Kwa kulitumia jina “Yehova” tunaweza kuonyesha waziwazi mtu anayemaanishwa. Yeye ni “Yehova mmoja.” Yeye si Yesu Kristo, maana Yesu ni Mwana mshikamanifu wa Mungu, “mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumba vyote.”—Wakolosai 1:15, UV; Marko 12:29; Kumbukumbu la Torati 6:4, NW.
10. Jina la Mungu lina maana gani, na ameonyeshaje hivyo?
10 Jina “Yehova” lina maana yenye nguvu. Lina maanisha: “Yeye Anafanya Iwe (au, Anathibitishe Iwe).” Hiyo ni kwa habari yake Mwenyewe, si kwa habari ya kuumba Kwake vitu. Hivyo, yeye alitangaze “Yehova” kuwa jina lake mwenyewe la “ukumbusho” alipokuwa akikaribia kuwa Mkombozi mwenye kufanyiza miujiza wa watu wake Israeli katika miko no ya Farao wa Misri. (Kutoka 3:13-15, NW) Baadaye nabii Yeremia alipomkiri Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova kuwa Mfanya mbingu na dunia ‘kwa uweza wake mkuu na kwa mkono wake ulionyoshwa,’ na kuwa ‘mkuu wa mashauri na mweza katika kutenda,’ Yehova alimhakikishia nabii wake kwamba, kwa wakati Wake mwenyewe, Yeye angefanya tendo lenye kuonekana kuwa lisilowezekana kwa kuwa Mrudishaji wa watu Wake kutoka utumwa wa Milki ya Kibabuloni. Naye akafanya hivyo!—Yeremia 32:17-19, 27, 44; 2 Mambo ya Nyakati 36:15-23.
11. Jina la Mungu linaweza kuambatanishwaje na ufalme wake?
11 Leo, pia, Yehova ndiye Mungu mkuu ‘anayefanya iwe.’ Yeye anaweza binafsi kuwa vyo vyote inavyotakwa, kutimiza jukumu lo lote linalohitajiwa, ili afanye mambo ya ajabu kwa kutumia ufalme wake, kwa kutakasa jina lake na kwa faida ya watu wake. Lo lote analokusudia kufanya linafanywa, kwa kufanikiwa.—Isaya 48:17; 55:11.
JE! JINA LA MUNGU LIMETAKASWA?
12. Wanadamu wamemfikiriaje Mungu?
12 Je! wanadamu wamemthamini, wakampa heshima na upendo Mungu huyu mtukufu, aliye mnyofu na ambaye ameandalia viumbe vyake duniani mambo mazuri ajabu? Tazama kuzunguka dunia hii, nawe utaona jibu. Lo! Mungu amesingiziwa vibaya sana na zile dini za mataifa yanayoitwa ya Kikristo! Mengi ya mataifa hayo yamemwona kuwa Mungu mwenye kupendelea watu fulani, na yamemwomba ayasaidie kupigana na wanadamu wenzao. Mengine yamemfikiria kuwa Mungu mkatili sana, anayehukumu “nafsi zilizokufa” ziende kwenye miali mikali sana ya mateso ya milele. Hata mengine yamemshushia, heshima kwa kumfananisha na mifano isiyo na uhai ya miti au ya mawe. Wengi wamevunja kwa makusudi sheria zake za uadilifu, wakisema Mungu haoni na hajali tena.—Tofautisha Matendo 10:34, 35; Yeremia 7:31; Isaya 42:8 na 1 Petro 5:7.
13. Matokeo ya mwisho yangekuwa nini ikiwa watu wenye kupotoshwa wangeruhusiwa wafuatie njia zao zisizo za upendo?
13 Walakini, ikiwa watu wenye kupotoshwa hawa mpendi Mungu na kutakasa jina lake, watawapendaje wanadamu wenzao? (1 Yohana 4:20, 21; 5:3) Na upendo usiporudishwa kati ya jamaa ya wanadamu, ni lazima mwishowe ulimwengu uwe pori la mgawanyiko, jeuri na fujo. Mahali fulani, tayari uko hivyo. Kwa sa babu ya kuenezwa kwa silaha za nyukilia kati ya mataifa, wakati fulani watu wenye kuchezea silaha wa ngeweza kuiangamiza jamii nzima ya kibinadamu. Lakini hilo ni jambo ambalo Baba yetu mwenye upendo hataruhusu kamwe litukie.—Zaburi 104:5; 119:90; Isaya 45:18.
JINSI MUNGU ANAVYOTAKASA JINA LAKE
14, 15. Nani anaongoza katika kutakasa jina la Mungu, na jinsi gani?
14 Ni nani anayeongoza katika kutakasa jina la Mungu? Ni Yehova mwenyewe! Anafanya hivyo kwa ku chukua hatua atetee viwango vyake vya uadilifu. Atatekeleza hukumu juu ya wote wanaopinga mapenzi yake matakatifu, kutia na wale wanaoonea wanadamu wenzao na wale wanaofundisha mambo ya uongo juu ya Mungu. (Zaburi 140:12, 13; Yeremia 25:29-31 Yehova hawezi kujikana. Yeye ndiye Mungu wa kweli anayestahili kuabudiwa pekee na viumbe vyake vyote. Yeye ndiye Mwenye Enzi Kuu wa Ulimwengu Mzima, anayestahili kutiiwa na viumbe vyote.—Warumi 3:4; Kutoka 34:14; Zaburi 86:9.
15 Katika kulitakasa jina lake, Bwana Yehova Mwenye Enzi Kuu atawaondoa katika dunia hii wanadamu wote wanaoharibu mambo, wanaotenda kinyume cha mapenzi yake. Hiyo ni kwa sababu anachukia uovu na anapenda uadilifu. (Zaburi 11:5-7) Ni kama yeye mwenyewe anavyosema: “Hakika mimi nitajitukiza mwenyewe na kujitakasa mwenyewe na kujijulisha mbele ya macho ya mataifa mengi; nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.” (Ezekieli 38:23, NW) Kwa wazi, basi, ikiwa tunataka kupata kibali ya Yehova, ni lazima sisi pia tulitakase jina lake, tulitendee kuwa takatifu na linalostahili heshima kamili, kisha tuishi kupatana na mapenzi yake.
16. Mwenendo wetu una sehemu gani katika kutakasa jina la Mungu?
16 Mwenendo wa wote wanaomwabudu Yehova ama unaliheshimu jina la Mungu ama unalikosesha heshima. Sisi sote na tuwe na mwenendo utakaofanya wengine wamsifu Mungu mkuu tunayetumikia na utakaofurahisha moyo wa Yehova mwenyewe. (1 Petro 2:12; Mithali 27:11) Kama watoto watiifu, imetupasa tutake kuonyesha shukrani zetu kwa Baba yetu kwa kutupa zawadi zote, kutia na makao yetu yenye kupendeza—dunia hii—yatakayorudishiwa utukufu mkubwa hata zaidi chini ya utawala wa Ufalme wa Mwanaye.—Isaya 6:3; 29:22, 23.
17. Imetupasa tumkaribie “Mfalme wa umilele” tukiwa na mwelekeo gani katika sala?
17 Jinsi inavyotamanika tuingie katika uhusiano wenye kukubaliwa pamoja na huyu “Mfalme wa umilele”! Walakini, hatuwezi kufanya hivyo kwa ustahili wetu wenyewe, maana sote tulichukuliwa mimba na wazazi wenye dhambi tukazaliwa tukiwa wasiokamilika. Lakini tunaweza kusali kwa Mungu kama Mfalme Daudi: “Usitiri uso wako usitazame dhambi zangu; uzifute hatia zangu zote. Ee Mungu, uniumbie moyo safi, uifanye upya roho iliyotulia ndani yangu.” (Zaburi 51:5-10) Tunapojifunza mambo ambayo ‘Baba yetu aliye katika mbingu’ anataka tufanye, tunaweza kusali ili tuje tushiriki zile baraka za milele ambazo ufalme wake utaleta. Ndiyo, tunaweza kusali tukiwa na hakika ufalme wa Mungu uje. Na ufalme huo utakuwa na maana gani kwa wanadamu hapa duniani? Na tuone.