Sura ya 6
Kujitahidi Kuufikia Ufalme
1. (a) Kwa habari ya serikali, Yehova anatolea watu nini tofauti na kile ambacho wanadamu wametoa? (b) Sababu gani tunaweza kuweka kwa usalama maisha zetu juu ya Neno la Mungu?
UNAPOTOLEWA kitu chenye kutamanika, unaitikiaje? Je! hufikii ukipate? Yehova Mungu anakutolea nafasi ya uzima wa milele chini ya serikali bora. Ni kweli kwamba, katika serikali leo, wanasiasa wengi ni wapotovu na ahadi zao mara nyingi ni za bure. Hata wakiwa na makusudi mazuri, wanadamu wameonekana hawawezi kutoa serikali nzuri isiyotegemea enzi kuu ya Mungu. (Mi-thali 20:24) Lakini wakati wote huo, Mungu amekuwa akichukua hatua za kuendelea mbele kwenye kusimamishwa kwa serikali yake bora ya Ufalme, na anakaribisha wanaopenda uadilifu wafaidike nayo. Kusudi lake linastahili kutumainiwa na ni la kweli. Hawezi kusema uongo. Tunaweza kujenga maisha zetu kwa usalama juu ya Neno lake.—Ufunuo 21:1-5; Tito 1:2.
2. (a) Ni wakati gani na Jinsi gani Mungu alieleza kusudi lake la kusimamisha ufalme wenye uadilifu? (b) Waebrania 11:4-7 hufunua nini juu ya wale waliojitahidi kulifikia tumaini la Ufalme?
2 Kusudi la Mungu la kusimamisha ufalme wenye uadilifu si jipya. Katika Edeni, enzi kuu ya Mungu ilipotiliwa shaka kwa mara ya kwanza, Mungu alieleza kusudi lake la kutokeza “uzao” (mbegu) ambao ‘ungemseta’ Shetani na watoto wake. (Mwanzo 3:15; Warumi 16:20) Katikati ya jeuri ya ulimwengu ule wa kale, Abeli, Enoki na Noa waliiamini ahadi hiyo ya Yehova. Wakiwa na hakika kwamba Mungu angewapa thawabu “wale wamtafutao” kwa bidii, walivumilia masuto, wakachagua ‘kutembea pamoja na Mungu’ na kuhubiri uadilifu. (Waebrania 11:4-7) Ni mifano mizuri kama nini kwa wote wanaokuamini kule ‘kuja’ kwa ufalme wa Mungu!
UKOO WENYE KUTOKEZA
3. Kulingana na Mwanzo 12:1-7, Abrahamu alikuwaje mfano bora kweli kweli wa kufuatwa na sisi?
3 Miaka zaidi ya 400 baada ya ile Gharika, Mungu alieleza wazi kwamba ule “uzao” wa kifalme ulioahidiwa ungetokea katika ukoo wa Abrahamu. Lakini kwa nini Abrahamu? Kwa sababu Mungu alimwona kuwa mwenye imani kubwa. Alimwita Abrahamu atoke katika mji wa kuzaliwa kwake, Uru wa Wakaldayo, akamtuma kwenye nchi ya kigeni, Kanaani, akisema:
“Jamaa zote za ardhi zitajibariki zenyewe hakika kupitia wewe, . . . mbegu yako nitaipa nchi hii.” (Mwanzo 12:3, 7; Matendo 7:4, “NW”)
Badala ya kung’ang’ania lile taifa alimozaliwa, Abrahamu akaliacha, asirudi kamwe. Alikuwa na nia ya kubadili kabisa mtindo wa maisha yake, ili amtolee Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu utii usio na masharti. Mfano bora kweli kweli wa kufuatwa na wote ambao wangependa kufuatia maisha ya kujiweka wakf kwa Yehova leo!
4. Sara alibarikiwaje kwa sababu ya imani yake? (Waebrania 11:11, 12)
4 Ijapokuwa Sara, mkeye, aliendelea kuwa tasa katika uzee wake, baadaye Yehova alimtumainisha Abrahamu, akimwambia: “Nitambariki, naye atakuwa mama wa mataifa, na wafalme wa kabila za watu watatoka kwake.” (Mwanzo 17:16) Akiwa mwenye umri wa miaka 90, Sara mwaminifu akabarikiwa kwa kumzalia Abrahamu mwana kimwujiza, yaani, Isaka, babu ya wafalme wengi.—Mathayo 1:2, 6-11, 16; Ufunuo 17:14.
5. Utii wa Abrahamu na Isaka ulithawabishwaje?
5 Halafu, Yehova akaweka Abrahamu na Isaka katika jaribu la kuwachunguza mioyo. Alimwagiza Abrahamu achukue huyo mwanaye mmoja tu aliyezaa kwa Sara kisha afunge safari ya siku tatu kwenda Mlima Moria, amtoe huko dhabihu ya kuteketezwa. Wakati huu inaelekea sana Isaka alikuwa mwenye umri wa miaka kama 25 na mwenye nguvu za kutosha kubeba mzigo mzito wa kuni kupeleka juu mlimani; mwenye nguvu za kutosha pia kumpinga baba yake mwenye umri wa miaka 125, kama angalitaka kufanya hivyo. Lakini kwa utii baba na mwana waliigiza sehemu zao katika mchezo huo wa kuigiza wenye kusisimua, kufikia wakati malaika wa Yehova alipozuia mkono wa Abrahamu alipokiinua kisu cha machinjo. Kondoo mume alitolewa dhabihu badala ya Isaka.—Mwanzo 22:1-14.
6. (a) Ni kiolezo gani cha unabii kilichoigizwa huko? (b) Sababu gani ile ahadi ya Mwanzo 22:18 inafaa kukupendeza kwa njia ya pekee?
6 Hapa Mungu alikuwa akifanyiza kiolezo cha unabii cha jinsi angetoa Mwanaye mwenyewe kuwa dhabihu, ili aondoe dhambi ya ulimwengu wa wanadamu. (Yohana 1:29; Wagalatia 3:16) Maana ndipo Mungu alipomwambia Abrahamu hivi:
“Kupitia mbegu yako mataifa yote ya dunia yatajibarikia yenyewe hakika kwa sababu ya kwamba umesikiliza sauti yangu.”—Mwanzo 22:15-18, “NW.”
7. Ni mwendo gani wetu ambao Yehova atathawabisha?
7 Abrahamu na Isaka walikuwa mifano ya utii yenye kutokeza sana! Huenda tusiombwe kamwe tutoe dhabihu ya aina yao, lakini ni jambo la maana tumtii Yehova kama walivyomtii, kwa sababu ya kumpenda kweli kweli. (Yakobo 4:7; 2 Wakorintho 9:13) Nia ya kujitoa dhabihu na kuacha mapendezi ya kichoyo, ili kujitahidi kuufikia ‘ule Ufalme unaokuja,’ ni mwendo ambao Yehova anakubali na kuthawabisha daima.—Mathayo 6:33.
8. (a) Ule mwendo wa Yakobo ulitofautianaje na ule wa Esau? (b) Ni baraka gani ambayo Isaka alimpa Yakobo?
8 Yakobo, mwana wa Isaka, ni mtu mwingine aliyejitahidi kuufikia Ufalme. Lakini Esau nduguye-pacha alidharau mambo matakatifu, akapendezwa na wanawake Wakanaani na mali za kichoyo. Naye alimwuzia Yakobo haki yake ya uzaliwa yenye thamani ili apate mlo wa mchuzi tu! (Waebrania 12:16) Yule Yakobo mwenye kufikiria mambo ya kiroho aliithamini sana ile haki ya uzaliwa, na Yehova akaelekeza mambo ili aweze kutunza tuzo hiyo, hata akapokea baraka ya mzee Isaka. Esau alikuwa ameoa wanawake wenye kuabudu mashetani, lakini tofauti na yeye, Yakobo alifunga safari ndefu ya kwenda Mesopotamia akatafute mke miongoni mwa waabudu wa Yehova. Wakati huo Isaka akamtumainisha tena Yakobo kwa maneno haya:
“Mungu Mwenyezi, akubariki, akuzidishe, na kukuongeza, ili uwe mkutano wa makabila.”—Mwanzo 25:27-34; 26:34, 35; 27:1-23; 28:1-4.
9. (a) Sababu gani jina la Yakobo lilibadilishwa likawa Israeli? (b) Tunaweza kufaidikaje na mfano wake?
9 Baadaye, alipokaribia umri wa miaka 100, Yakobo alionyesha tena alivyothamini sana mambo matakatifu. Alishindana mweleka na malaika mmoja usiku kucha ili apate baraka. Kama ishara ya kibali Yake, Ye-hova alibadili huko jina la Yakobo likawa Israeli, maana yake “Mwenye kuendelea na Mungu bila kushindwa.” (Mwanzo 32:24-30) Sisi pia tutapewa thawabu tukiendelea kujitahidi kuzifikia mali za kiroho, huku tukiiepuka ile roho ya ulimwengu mwovu unaotuzunguka.—Mathayo 6:19-21.
10. (a) Ule unabii katika Mwanzo 28:3 ulitimizwaje? (b) Kwa habari ya uaminifu wa mtu mmoja mmoja. ni baadhi ya mifano gani yenye kuchangamsha moyo iliyo katika Waebrania 11:1-12:1?
10 Yehova aliwapanga kweli kweli wazao wa Yakobo kuwa “mkutano wa makabila,” na kupitia Musa, mpatanishi wake, ambaye alimtumia kuanza kuandika Biblia pia, Mungu alilitolea wito taifa hilo la Israeli, akisema:
“Ikiwa mtaitii sauti yangu kweli kweli . . . mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani, na taifa takatifu.” (Kutoka 19:5, 6)
Kwa kusikitisha, kwa sababu ya utovu wa kutii sauti ya Mungu, Israeli wa mwili walishindwa kuwa huo ufalme wa kiroho. Lakini kuhusiana na taifa hilo, watu wengi mmoja mmoja kama vile mahakimu katika Israeli, manabii na hata Rahabu aliyekuwa kahaba zamani, walimwonyesha Mungu ukamilifu wao. Tunaweza kusoma habari za “mashahidi” hao waaminifu katika Waebrania 11:1-12:1, nao ni kitia-moyo kweli kweli kwa watu wa sasa wanaotazamia ‘ufalme wa Mungu uje’!
11. Unaweza kuwa namna gani kama mashahidi hao waaminifu?
11 Je! wewe wataka kuwa mwenye nguvu katika imani? Je! wataka sasa uwe kama wale wanaume na wanawake wenye imani katika ‘kujitahidi kufikia mahali bora, yaani, pale ambapo ni pa mbinguni,’ ndiyo, kujitahidi kuufikia “mji wenye misingi ya kweli kweli, mjenzi na mfanyi wa mji huo akiwa ni Mungu”? (Waebrania 11:10, 16, NW) ‘Lakini,’ labda utauliza, ‘huo ni “mji” gani?’
ULE MJI ULIOJENGWA NA MUNGU
12. Ni “mji” gani ambao watumishi hao wa kale wa Mungu walikuwa wakijitahidi kufikia? (Tazama pia Waebrania 11:22-32: Ruthu 1:8, 16, 17.)
12 “Mji” huo ndio ule ufalme wa Mungu ulioahidiwa. Sababu gani tunasema hivyo? Katika nyakati za kale mara nyingi mji ulikuwa ni ufalme, uliotawalwa na mfalme. Mfalme wa kwanza kutajwa kwa kibali katika Biblia alikuwa “Melkizedeki . . . mfalme wa [mji wa] Salemu, kuhani wa Mungu aliye juu.” Karne zilizofuata, mji huo wa Yerusalemu ulijengwa juu ya mahali pale pale, na, kama vile Salemu, ukafananisha ule ufalme wa kimbingu mikononi mwa yule Mfalme mkuu na Kuhani Mkuu, Yesu Kristo. (Mwanzo 14:1-20; Waebrania 7:1, 2, 15-17; 12:22, 28) Ijapokuwa wakati huo hawakujua habari kwa kirefu, Abrahamu na Sara, pia Isaka na Yakobo, walikuwa wakiutafuta kwa bidii “mji” ambao Masihi angetawala akiwa mfalme. Abrahamu “alilifurahia sana lile taraja.” Wewe, pia, unaweza kuona furaha unapojitahidi kwa imani kufikia mahali katika mpa-ngo huo wa Ufalme.—Waebrania 11:14-16, UV; Yoha-na 8:56, NW.
13, 14. Unabii wa Yakobo aliotoa wakati wa kufa ulianzaje kupata utimizo?
13 Yakobo akawa baba ya wana 12, ambao baadaye wakawa vichwa vya yale makabila 12 ya Israeli. Akiwa katika kitanda chake cha kufia, Yakobo alitabiri ni jipi kati ya makabila 12 ambalo lingetokeza mtawala wa Mungu mwenye mamlaka ya Ufalme, akisema:
“Mwana-simba ni Yuda. . . . Fimbo ya kifalme haitageuka kando ya Yuda . . . mpaka Shilo [maana yake, Yeye Ambaye Ni Chake] aje; na kwake utii wa vikundi vya mataifa utakuwa.” (Mwanzo 49:9, 10, NW)
Je! Shilo alikuja kutoka Yuda? Ndiyo!
14 Utimizo wa unabii wa Yakobo ulianza kufunuka miaka zaidi ya 600 baadaye. Ndipo Yehova alipochagua, kutoka kabila la Yuda, “mtu aupendezaye moyo wake.” Jina lake ni Daudi. Mungu alimfanya huyo ‘simba wa Yuda’ mwenye ushujaa awe kiongozi na mfalme juu ya watu Wake Israeli. (1 Samueli 13:14; 16:7, 12, 13; 1 Mambo ya Nyakati 14:17) Yehova alimwahidi Mfalme Daudi ufalme wa milele.—Zaburi 89:20, 27-29.
15. Sababu gani Yehova aliupindua ufalme wa Kiyudea, na kwa muda gani?
15 Daudi, aliyeanza utawala wake mwaka wa 1077 K.W.K., alikuwa ndiye wa kwanza wa jamaa ya wafalme wa Kiyudea waliotawala katika mji wa Yerusalemu. Taifa lilifanikiwa wakati wo wote mfalme alipomtii Yehova kwa nia. Lakini mfalme alipogeuka kuwa mwovu na kuasi sheria za uadilifu za Yehova, watu waliteseka. (Mithali 29:2) Sedekia, mfalme wa mwisho wa Yuda, alikuwa mwovu sana. Nabii wa Mungu alimtabiria hivi: “ ‘Livue lile taji. . . . Uharibifu, uharibifu, uharibifu nitaufanya . . . mpaka aje yeye aliye na ile haki halali, nami lazima nimpe yeye hiyo.’ ” Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu aliupindua ufalme huo, mpaka wakati mfalme mwenye “haki halali” angetokea.—Ezekieli 21:26, 27, NW.
YULE MFALME MWENYE “HAKI HALALI”
16. Maandiko yanatambulishaje yule mrithi wa dalma wa Ufalme huo?
16 Ni nani ambaye angerithi ile “haki halali” ya ufalme wa Kidaudi? Ile mistari ya kwanza 17 ya kitabu cha Biblia cha Mathayo inatoa jibu. Kwa kuanza na Abrahamu mpaka Daudi, kisha mpaka Yusufu, ambaye kwa wakati wake akawa mume wa Mariamu, mistari hiyo inafuatia ukoo wa ile “mbegu” iliyoahidiwa. Hivyo mwana-mzaliwa wa kwanza wa Mariamu angekuwa na “haki halali” ya kupata ule Ufalme. Basi mapema katika mwaka wa 2 K.W.K., yule malaika Gabrieli alitangaza habari za huyo mwana ambaye angechukuliwa mimba kimwujiza katika tumbo la uzazi la Mariamu:
“Inakupasa kumwita jina lake Yesu. Huyo atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa yule Aliye Jun Zaidi Sana; na Yehova Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake, naye atatawala akiwa mfalme juu ya nyumba ya Yakobo milele, na hakutakuwa na mwisho wa ufalme wake.” (Luka 1:26-33, “NW”)
Kwa njia bora sana katika karne nyingi Yehova alikuwa amekuwa akitimiza kusudi lake ili atokeze mrithi huyo wa daima wa ufalme wa Daudi. Tunapochunguza mambo hayo, je! hayaitii nguvu imani yetu katika ahadi ya Mungu ya ‘ufalme wake unaokuja’?
17, 18. (a) Nani pekee watarithi ufalme wa kimbingu? (b) Ni baadhi ya waaminifu gani watakaofufuliwa duniani? (c) Utimizo huo umepasa ututie moyo tufanye nini?
17 Si kwamba sote tunaweza kutarajia kuwa katika ufalme huo wa kimbingu pamoja na Yesu, maana nafasi hiyo limewekewa “kundi dogo” tu la wanafunzi wake. (Luka 12:32) Hata Mfalme Daudi hakuwa na tumaini hilo. Tunaambiwa hivi: “Daudi hakupanda mbinguni.” (Matendo 2:34) Wala Yohana Mbatizaji na wanaume na wanawake wengine waaminifu wa nya-kati za kale hawauingii “ufalme wa mbinguni.”—Mathayo 11:11; Waebrania 11:39, 40.
18 Walakini, washika-ukamilifu hao waaminifu watafufuliwa apa hapa penye dunia hii, wengi wao wakiwa “wana-wafalme” katika mpango wa Ufalme wa Mungu. (Zaburi 45:16, NW) Wewe hungependa kuwakaribisha wakirudi kutoka kaburini na kufurahia ushirika bora pamoja nao? Bila shaka ungependa! Basi weave pia azimia, ujitahidi kufikia ule “mji” kwa kuwa ‘mtendaji wa kazi kwa ajili ya ufalme wa Mungu pamoja na’ wengine wote leo wanaothamini nafasi hiyo iliyo bora sana.—Wakolosai 4:11.
[Picha katika ukurasa wa 52, 53]
WALIJITAHIDI KUFIKIA UFALME WA MUNGU
ABELI KARIBU NA MWAKA WA 3900 K.W.K.
NOA MWAKA WA 2970-2020 K.W.K
ABRAHAMU, SARA, ISAKA, YAKOBO MWAKA WA 2018-1711 K.W.K
YOSEFU MWAKA WA 1767-1657 K.W.K
MUSA MWAKA WA 1593-1473 K.W.K
RAHABU MWAKA WA 1473 K.W.K.
MAHAKIMU MWAKA 1473-1117 K.W.K
RUTHU, NAOMI KARIBU MWAKA WA 1300 K.W.K
DAUDI MWAKA WA 1107-1037 K.W.K.
MANABII MWAKA WA 1117-442 K.W.K.
YOHANA MBATIZAJI MWAKA WA 2 K.W.K.-31 W.K.