Sura ya 8
‘Ule Ufalme Umekaribia’
1. Sababu gani maneno ya Yohana katika Mathayo 3:1-10 yalisemwa kwa wakati unaofaa?
NA TUCHUNGUZE habari zaidi za utendaji wa “Masihi Kiongozi” wakati wa kuja kwake mara ya kwanza. Tangazo lenye kushtusha lilisikiwa kwanza kutoka midomo ya Yohana Mbatizaji: “Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia.” (Mathayo 3:2) Yule Mfalme ajaye alikuwa karibu kutokea! Wakati lile ‘juma la sabini,’ “juma” la kibali ya pekee, lilipokaribia, ulikuwa ndio wakati wa Wayahudi kutubu, dhambi zao walizofanya juu ya lile fungu la sheria za uadilifu walizopewa na Mungu wao, Yehova. Maana sasa Israeli walikuwa karibu kuingia siku ya hukumu. Kwa sababu hiyo, Yohana aliendelea kuwaambia wale viongozi wa kidini wanafiki wa taifa hilo: “Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja? Basi zaeni matunda yapasayo toba. Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.”—Mathayo 3:7, 8, 10.
2. (a) Sababu gani ubatizo wa Yesu ulikuwa tofauti? (b) “Alipoanza kazi yake,” alilazimika kupambana na nini?
2 Ndipo Yesu akatoka Galilaya kwenda Yordani na kumwomba Yohana ambatize. Yohana alijua kwamba Yesu hakuwa na dhambi, na kwanza alikataa. Walakini, ubatizo wa Yesu ulipasa uwe tofauti. Ungefananisha kujitoa kwake kwa Yehova afanye kazi ya pekee ambayo Baba yake alikuwa amempa afanye duniani. Kwa kufaa, basi, Yesu akabatizwa katika maji.
“Na, alipokuwa akisali, mbingu ilifunguka na roho takatifu katika umbo la mwili kama njiwa ikashuka juu yake, na sauti ilitoka mbinguni: ‘Wewe ni Mwana wangu, mpendwa; nimekukubali.’ Zaidi ya hayo, Yesu mwenyewe, alipoanza kazi yake, alikuwa mwenye umri wa karibu miaka thelathini.”
Mara hiyo, akiwa Masihi na Mfalme-mwekwa, akawa ndicho kitu cha masharnbulio ya yule Nyoka wa zamani, Ibilisi, na wale viongozi wa kidini Wayahudi, ambao kwa unafiki walijidai kumtumikia Mungu.—Luka 3:21-23, NW.
3. Mwendo wa Yesu alipokuwa akishawisha ulitofautianaje na ule wa Adamu na Hawa?
3 “Basi Yesu, akiwa amejaa roho takatifu, akaondoka Yordani, naye akaongozwa na ile roho katika jangwa muda wa siku arobaini, huku akiwa anashawishwa na yule Ibilisi.” (Luka 4:1, 2, NW) Shetani alitambua Yesu kuwa ndiye ule “Uzao” wa ahadi ya Mungu ambao kwa wakati wake ungemponda-ponda Ibilisi na “uzao” wake mbovu. Je! Shetani angeweza kuzuia kusudi la Yehova lisitimizwe kwa kumfanya Yesu akose kumtii Yeye? Yesu alikuwa amekuwa akifunga kula muda wa siku 40. Basi yule Ibilisi akamkaribisha Yesu mwenye njaa ageuze mawe fulani ya jangwa hilo lisilozaa kitu yawe mikate. Kwa sasa Yesu alikuwa ana uwezo wa kufanya miujiza, lakini, kwa kufaa, akatumia sheria ya uadilifu ya Yehova, akisema:
“Imeandikwa, ‘Ni lazima mtu aishi, si kwa mkate tu, bali kwa kila usemi unaotoka katika kinywa cha Yehova.’ ” (Mathayo 4:1-4; Kumbukumbu la Torati 8:3, “NW”)
4. Ni somo gani tunaweza kujifunza kutokana na namna Yesu alivyoshughulika na kishawishi cha pili?
4 Unyenyekevu wa Yesu na kutegemea kabisa Baba yake ulionyeshwa na namna alivyoshughulika na kishawishi kilichofuata. Shetani alijaribu kumfanya Yesu adhani kwamba yeye, akiwa Mwana wa Mungu, alikuwa mtu wa maana sana—mtu mashuhuri. Ndiyo, acha ajitupe chini bure kutoka kilele cha hekalu, na bila shaka malaika wa Mungu wangemdaka asiumie. Lakini Yesu alikataa wazo hilo la kipumbavu, akitumia tena maneno ya sheria ya Yehova, na kusema:
“Tena imeandikwa, haikupasi kamwe kumweka Yehova Mungu wako kwenye jaribu.’ ” (Mathayo 4:5-7; Kumbukumbu la Torati 6:16, “NW”)
Katika maneno hayo mna somo kwa wote wanaodai kuwa watumishi wa Mungu mpaka leo hii: Mtu asidhani wakati wo wote kwamba kuwa na uhusiano pamoja na Yehova ndilo jambo pekee linalotakwa. Kubarikiwa kwetu na Mungu hakutegemei utumishi wetu wala cheo cha zamani, bali kwategemea kuendelea kumtii yeye kwa unyenyekevu wote, tukionyesha heshima nyingi kwa mipango na matakwa yake.—Wafilipi 2:5-7.
5. (a) Kile kishawishi cha tatu kilikazwa juu ya suala gani kuu? (b) Katika kujibu Yesu alitumiaje tena sheria ya Mungu? (c) Ni kwa njia gani huo ni mfano bora kwetu leo?
5 Sasa, pindi hii ni kishawishi kile cha mwisho kinachopita vyote! 0, kama tu Shetani angeweza kumwangusha Yesu kwa kutumia lile suala kuu la Ufalme! Basi “Ibilisi akamchukua zake kwenye mlima mrefu isivyo kawaida, akamwonyesha falme zote za ulimwengu na utukufu wazo, naye akamwambia: ‘Vitu vyote hivi nitakupa wewe ikiwa unaanguka chini na kufanya kitendo cha ibada kwangu.’ ” Kwa tendo hilo rahisi la kulegeza uimara wake, Shetani akatoa hoja kwamba Yesu angeweza kuutawala ulimwengu mzima wa wanadamu mara hiyo hiyo, asiwe na lazima ya kungojea karne nyingi mpaka wakati wa Yehova ufike. Lakini tena Yesu akaelekeza kwenye sheria ya Yehova, alipojibu:
“Nenda zako, Shetani! Maana imeandikwa, ‘Ni Yehova Mungu wako ambaye ni lazima uabudu, na ni kwake peke yake lazima utoe utumishi mtakatifu.’ ” (Mathayo 4:8-10; Kumbukumbu la Torati 6:13, “NW”)
Tena, ni mfano bora sana kwa wale wanaomtumikia Yehova leo! Hata barabara ionekane kuwa ndefu namna gani, wale wanaotoa utumishi mtakatifu kwa Yehova wasiache kamwe kamwe kuweka ufalme wa Mungu kwanza katika maisha zao. Kamwe wasigeuke upande ili wajiundie “falme” zao ndogo-ndogo katika jamii ya ulimwengu wa Shetani yenye kupenda mali.
“SI SEHEMU YA ULIMWENGU HUU”
6. (a) Ni kwa njia gani sasa ule Ufalme ulikaribia? (b) Kwa kutumia 1 Petro 2:21, ni lazima Wakristo wafuate mfano gani wa Yesu?
6 Ni nini kilichofuata baada ya Yesu kukanusha vile vishawishi vya Ibilisi? Habari ya Biblia inatuambia: “Yesu alianza kuhubiri, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia.”
Ufalme huo ulikuwa umekaribia kwa njia gani? Kwa njia ya kwamba yule aliyepakwa mafuta awe Mfalme, yaani, Yesu Kristo mwenyewe, sasa alikuwapo, “akifundisha . . . na kuihubiri Habari Njema ya ufalme.” Makundi makubwa ya watu yalimfuata kila mahali. (Mathayo 4:17, 23-25) Yesu alisema wazi sana kwamba wale waliokubali mafundisho yake walipaswa kuwa ‘si sehemu ya ule ulimwengu, kama vile yeye hakuwa sehemu ya ule ulimwengu.’ Ni lazima wajitenge na ulimwengu na njia za ujeuri, zisizo za adili. Wale wote wanaotaka kufuata Yesu leo lazima wafanye vivyo hivyo.—Yohana 17:14, 16, NW; 1 Petro 2:21; ona pia Mathayo 5:27, 28; 26:52.
7. Kulingana na maneno ya Yesu katika Yohana 8.44, sababu gani ni jambo la maana sisi leo tuchunguze mafundisho ya viongozi wa kidini kuhusiana na Biblia?
7 Kwa habari ya ibada ya uongo, Yesu aliwaambia viongozi wa kidini wa wakati wake hivi: “Ninyi ni watoto wa baba yenu Shetani, na mnataka tu kutekeleza tamaa za baba yenu. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; hana msimarno katika ukweli kwani ukweli haumo ndani yake. Kila asemapo uwongo huusema kutokana na hali yake ya maumbile, maana yeye ni mwongo na baba wa uwongo.” (Yohane 8:44, HNWW) Huko nyuma lilikuwa jambo la maana sana watu wa kawaida wajiondoe katika mapokeo ya uongo (ambayo baadaye yalitiwa katika kitabu cha sheria za Wayahudi) yaliyokuwa yamesitawi katika dini ya Wayahudi. Na leo, ni lazima wale walio kama Wayahudi hao, ambao wameishi maisha yao yote wakiwa katika dini ya babu zao, wachunguze waone kama viongozi wao wa kidini wamelipuza ama hawakulipuza lile neno la Mungu ili wafundishe mapokeo ya vivi hivi tu ya kibinadamu.—Marko 7:9-13.
8, 9. (a) Sababu gani Yesu alisema ufalme wake “si sehemu ya ulimwengu huu”? (b) Basi, sababu gani Wakristo wa kweli wanapatwa na mateso? (c) Sababu gani imewapasa wawe wajasiri?
8 Alipokuwa akihukumiwa uhai wake, Yesu alitangaza kuhusu zile serikali za kisiasa za wakati wake hivi:
“Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu. Kama ufalme wangu ungalikuwa wa ulimwengu huu, wahudumu wangu wangalipigana nisipate kukabidhiwa kwa Wayahudi. Lakini, kama ilivyo, ufalme wangu si wa kutoka chanzo hiki.”
Kile chanzo cha ufalme wa Yesu kilikuwa cha kimbingu. Ulipata mamlaka kutoka kwa Yehova Mungu, Mwenye Enzi Mkuu, si kutoka kwa Shetani. Kwa hiyo, Shetani alitumia “uzao” wake wa kidunia atese Yesu na wafuasi wake.—Yohana 18:36, NW.
9 Kwa hiyo Yesu aliwaambia wafuasi wake wa kweli hivi: “Mambo haya nawaamuru ninyi, mpate kupendana mmoja na mwenzake. Ulimwengu ukiwachukia ninyi, mwajua kwamba umenichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi. Kama ninyi mngekuwa sehemu ya ulimwengu, ulimwengu ungependa sana kile kilicho chake wenyewe. Sasa kwa sababu ninyi si sehemu ya ulimwengu, bali mimi nimewachagua ninyi kutoka ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu unawachukia ninyi.” (Yohana 15:17-19, NW) Waabudu wa Yehova wanapata chuki na mateso makali mpaka leo hii kwa sababu wanajitenga na siasa zenye upotovu na jeuri ambazo zimeenea sana leo. Lakini thawabu bora wamewekewa akiba wote ambao mwishowe wataushinda ulimwengu. Kama Yesu alivyowahakikishia wanafunzi wake: “Katika ulimwengu ninyi mnapata dhiki, lakini iweni na ushujaa! Mimi nimeushinda ulimwengu.”—Yohana 16:33, NW.
SIFA ZA KIFALME
10, 11. (a) Ni nini kinachoonyesha kwamba watawala wa ulimwengu hawatawali wakiwa na haki ya kimungu? (b) Kwa kutofautisha, Yesu amejionyeshaje kuwa anastahili uufalme?
10 Ni sifa gani ambazo ungetafuta kuona mtawala wa ulimwengu akiwa nazo? Watawala wengi wa historia wamekuwa “wanaume wenye nguvu,” wenye kutakabari, wenye kujitutumua kwa kiburi. Kwa kawaida wametanguliza maendeleo ya kibinafsi kuliko mahitaji ya watu wa kawaida. Wengine wamejivunia kuunda milki kubwa, lakini mwishowe milki zao zote zenye nguvu zimeanguka, ikionyesha maneno haya ya Mfalme Sulemani ni ya kweli: “Yehova mwenyewe asipoijenga nyumba, wajenzi wayo wamejibidiisha juu yayo bure-bure.” (Zaburi 127:1, NW) “Wafalme” hao wameonyesha kikweli kwamba wao hawatawali wakiwa na haki ya kimungu. Enzi yao haikutoka kwa Yehova Mungu.
11 Walakini, Yesu Kristo, Mfalme wa Mungu aliyepakwa mafuta, anasimuliwa kiunabii kuwa akipanda kwenda kupambana na adui zake “katika kusudi la kweli na unyenyekevu na uadilifu.” Imesemwa juu yake hivi: “Wewe umependa uadilifu na unachukia uovu. Ndiyo sababu Mungu, Mungu wako, amekupaka mafuta ya shangwe zaidi ya wenzi wako”—wale wafalme wa ukoo wa Daudi waliomtangulia. (Zaburi 45:4, 7, NW) Kwa kuchukia kila kitu kinachovunja heshima ya jina takatifu la Yehova na kuvunja kanuni za uadilifu za Mungu, kwa wakati wake yule Mfalme wa kimbingu atasafisha uovu wote katika dunia hii, akitayarisha ngiza utawala wa uadilifu. Je! Yesu arnejionyesha kustahili kuwa mtawala huyo? Hakika kabisa!
12. Ni mfano gani wa kufuatwa wa utumishi rntakatifu ambao Yesu alituwekea?
12 Alipokuwa mwanadamu mkamilifu, Yesu alikuwa mfano bora wa kuonyesha upendo kwa Mungu na jirani. Akiwa mshiriki wa taifa Israeli lililojiweka wakf kwa Yehova, Yesu aliuweka mfano kwa kuzitii zile amri mbili zilizo kubwa kuliko zote. Alisema: “Ile [amri] ya kwanza ni, Sikia Ee Israeli, Yehova Mungu wetu ni Yehova mmoja, na wewe lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili zako zote na kwa nguvu zako zote.’ Ile ya pili ni hii: ‘Lazima umpende jirani yako kama wewe mwenyewe.’ ” (Marko 12:29-31; Kumbukumbu la Torati 6:4, 5, NW) Yesu alijitoa kabisa katika utumishi wake kwa Yehova na katika kufundisha jirani zake Wayahudi. Hao walipojaribu kumkawiza ili wasikie mengi zaidi, aliwaambia:
“Pia kwenye miji mingine ni lazima nikazitangaze habari njema za ufalme wa Mungu, kwa sababu kwa ajili hiyo nilitumwa.” (Luka 4:43, “NW”)
Yesu alikuwa mfanya kazi katika kutoa utumishi mtakatifu, akaweka mfano wa kufuatwa na Wakristo wote wa kweli.—Linganisha Yohana 5:17.
13, 14. (a) Yesu alikuwa na maoni gani juu ya watu? (b) Sababu gani alitoka akaenda kuhubiri, na sababu gani alituma wengine? (c) Ni uangalizi wa aina gani ambao wanadamu wanaweza kutazamia chini ya ule Ufalme?
13 Yesu alijionyesha kuwa mwenye upendo na huruma. Katika moyo wake alitamani sana kuona watu wake wakiondolewa mizigo mizito waliyotwikwa na wagandamizi wao wa kidini. Hivyo aliwaambia juu ya ule Ufalme, akatuma wanafunzi wake, akisema:
“Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia.”—Mathayo 9:35-10:7.
14 Mfalme-mkusudiwa huyo aliwakaribisha watu, akisema: “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.” (Mathayo 11:28-30) Yesu, akiwa Mfalme wa kimbingu wa Mungu juu ya wanadamu wote, ataonyesha huruma ile ile, naye atahakikisha, kama alivyofanya alipokuwa duniani, kwamba washirika wake wa Ufalme wamepangwa ili watoe faraja na uangalizi wenye fadhili ambao wanadamu wanauhitaji kweli kweli. Wote watakaoishi duniani chini ya utawala wa Ufalme wa Yesu watapata kweli burudisho la nafsi zao.
BILA KASORO KATIKA UKAMILIFU
15. Yesu alitoaje jibu kamili kwa shtaka la Shetani?
15 Zaidi ya yote, Mfalme ajaye wa wanadamu alionyesha ukamilifu usio na kasoro na utii kwa Baba yake wa kimbingu, mpaka alipokufa kifo cha ukatili juu ya mti wa mateso. Saa hiyo ya kuuawa ilipokaribia, Yesu alisali kwa Yehova, akisema, “Baba, ulitukuze jina lako.” Sauti ya Yehova ikajibu kutoka mbinguni: “Nimelitukuza, na nitalitukuza tena.” Katika kulitakasa jina la Baba yake, Yesu alitoa jibu kamili kwa shtaka la Shetani. Alionyesha kwamba mwanadamu mkamilifu angeweza kuonyesha uaminifu kwa Mungu chini ya kila aina ya jaribu ambalo huenda yule adui akamletea. Hivyo Yesu angeweza kusema: “Sasa ndio wakati wa ulimwengu huu kuhukumiwa; sasa mtawala wa ulimwengu huu [Shetanil atapinduliwa”—aaibishwe kabisa, aonyeshwe kuwa mwongo. Wale viongozi wa kidini Wayahudi, wakiwa ule ‘uzao wa yule nyoka,’ wangesababisha ule “uzao” wa tengenezo la Mungu lililo kama mwanamke utiwe jeraha lenye uchungu katika “kisigino.” Lakini Mungu angefufua Mwanaye mwenye kustahili aende kwenye uzima wa roho.—Mwanzo 3:15, UV; Yohana 12:27-31, HNWW.
16, 17. (a) Sababu gani tunaweza kuwa na uhakika wenye nguvu na Mfalme wa dunia wa wakati ujao? (b) Maandiko yanaonyeshaje kwamba lile tumaini la dunia-paradiso ni la kweli? (c) Je! namna ya maisha yako ya zamani ikuzuie kujitahidi kulifikia tumaini hilo?
16 Kupenda kwa Yesu uadilifu, kuchukia kwake uvunjaji wa sheria, kupendelea sana wanadamu na, zaidi ya yote, utii wake ulio imara katika kufanya mapenzi ya Baba yake kwa utukufu wa jina la Yehova—yote hayo yanamthibitisha Mwana huyu mshikamanifu kwamba anastahili sana kuwa Mfalme wa dunia wa wakati ujao. Je! wewe hungependa kuingia katika uzima wa milele ukiwa raia mwenye furaha wa mfalme huyo?
17 Hata kama mpaka sasa namna ya maisha yako imekuwa nzuri au mbaya, huenda ukaona utimizo wa tumaini hilo la uzima wa milele katika dunia itakayofanywa kuwa tukufu. Lo! hata yule mwivi mwenye kutubu aliyeuawa pamoja na Yesu alipewa tumaini hilo la ufufuo! Maana alipomwambia Yesu, “Unikumbuke mimi utakapoingia katika ufalme wako,” Yesu alijibu: “Kweli kweli mimi nakuambia leo, Utakuwa pamoja na mimi katika Paradiso.” (Luka 23:42, 43, NW) Upesi, Paradiso itakuwapo. Je! wewe, pia, unajitahidi kwa sala ufikie kule ‘kuja’ kwa Ufalme na baraka ambazo utaleta?
[Picha katika ukurasa wa 77]
MWANAMUME MASHUHURI KUSHINDA WOTE WALIOISH1 DUNIANI
Akiwa Mfalme-mkusudiwa, alionyesha ukamilifu mpaka kufa, na kwa damu yake iliyomwagwa akakomboa wanadamu katika dhambi na kifo