Wimbo 26
Kutimiza Matakwa ya Mungu
1. Na tuwe waaminifu,
Tushike ukamilifu.
Tangaza nyumba kwa nyumba
Tukufu za jina la Yah.
Sisi tunawafariji
Wale waombolezao;
Alama na tuwatie,
Mungu awaachilie.
2. Jicho likiwa rahisi,
Ukweli utakazika.
Tukilinda moyo wetu,
Uzima milele wetu.
Tukilihubiri neno,
Wengi, ’tasikia kweli.
Tukinyosha njia zetu,
Shangwe ya ’Falme ’tajaa.
3. Ndugu tuwasaidie,
Jirani tusaidie,
Tukae kwa umoja na,
Waaminifu wa Mungu.
Twathamini hali yetu,
Ya furaha, wahudumu.
Na tusiilaumishe,
Tukweze jina Yehova.