Wimbo 49
Mungu Mkuu, Yehova!
1. Mungu, Mukuu, Yah wa milele,
Twaimba sifa zako, Twapita njia zako.
U Baba yetu, pia Hakimu.
Daima tutakutolea jibu.
E Mungu, mwema, ndiyo uwe mwema.
Tusaidie tukuabudu.
Tuheshimu jina kulijulisha,
Na tukutumikie kwa uradhi.
Ndiwe Mu’mba, Mulinda Uzima.
Waleta mema yote.
2. Mungu, Mukuu, Mutakatifu,
Tunapata furaha, Kufanya kazi yako.
U Ngome yetu, watupa nguvu.
Twakutumai kwa moyo, akili.
E Mungu, una nguvu ndiyo nguvu.
Ukitulinda hatutakosa.
Na tulijulishe kusudi lako.
Na kukuabudu wewe, pekee.
U ngome yetu, na Ngao yetu,
Tutumaini wewe.
3. Mungu, Mukuu, na Muchungaji,
unatujali sana, Wajali mambo yetu.
U Muokozi, na Mukombozi.
Twakufikia kwa sala daima.
E Mungu u mwema ndiyo u mwema.
Tunakujia kufarijiwa.
Jina lako ni bora, na tuone
Ukiwa ukusudiacho kuwa.
Ewe Yehova, Mungu wa juu,
Ndiwe Mungu pekee.