Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • sjj wimbo na. 159
  • Mpe Yehova Utukufu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mpe Yehova Utukufu
  • ‘Mwimbieni Yehova kwa Shangwe’
  • Habari Zinazolingana
  • Shiriki Kuimba Wimbo wa Ufalme!
    ‘Mwimbieni Yehova kwa Shangwe’
  • Shiriki Kuimba Wimbo wa Ufalme!
    Mwimbieni Yehova
  • Wimbo Mpya
    ‘Mwimbieni Yehova kwa Shangwe’
  • Wimbo Mpya
    Mwimbieni Yehova
Pata Habari Zaidi
‘Mwimbieni Yehova kwa Shangwe’
sjj wimbo na. 159

WIMBO NA. 159

Mpe Yehova Utukufu

Makala Iliyochapishwa

(Zaburi 96:8)

  1. 1. Mwenye enzi, Ee Yehova,

    Ukiwa ju’ mbinguni.

    Naweza kukupa nini

    Kwa upendo wako mwingi?

    Nitazamapo angani,

    Naona nguvu zako.

    Mimi ni nani Yehova,

    Unipe kibali chako?

    (KORASI)

    Ee Yehova, ninakuimbia.

    Wimbo wa kukusifu.

    Mungu wangu, mfalme milele,

    Unastahili sifa;

    Utukufu ni wako.

  2. 2. Maisha yangu nakupa.

    Nitakusifu wewe.

    Kutangaza njia zako

    Na kusema wema wako.

    Najivunia Yehova,

    Kukuabudu wewe.

    Wanipa nguvu na shangwe,

    Uniongoze milele.

    (KORASI)

    Ee Yehova, ninakuimbia.

    Wimbo wa kukusifu.

    Mungu wangu, mfalme milele,

    Unastahili sifa;

    Utukufu ni wako.

  3. 3. Mabonde mito bahari,

    Jua mwezi na nyota

    Hunista’jabisha mimi

    Upendo bila kifani.

    Hekima na utukufu:

    Naona mambo hayo.

    Kwa nini nisikusifu

    Kwa vyote ulivyoumba?

    (KORASI)

    Ee Yehova, ninakuimbia.

    Wimbo wa kukusifu.

    Mungu wangu, mfalme milele,

    Unastahili sifa;

    Utukufu ni wako.

(Ona pia Zb. 96:1-10; 148:3, 7.)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki