Wimbo 110
Uwe Mwenye Kusamehe
1. Kwa pendo Yehova wetu
Kaufanya mupango,
Wa dhambi, katuma Mwana,
Ili tukombolewe.
Tukitubu kweli kweli,
Tuombe musamaha
Kwa ukombozi wa Kristo,
Katika jina lake.
2. Mungu anasamehe tu
Walio kama yeye,
Wanasamehe wengine,
Wana pendo, huruma.
Sisi si wakamilifu,
Twakosa mara nyingi
Kwa neno, tendo pumbavu.
Twataka musamaha.
3. Siku za huzuni chungu
Samaha lazuia;
Tunaonyesha fadhili
Za kutoka mbinguni.
Tukisamehe kwa moyo
Ni kukomaa kwetu,
Kuonyesha ufahamu
Na huleta amani.
4. Samaha la kweli, wema
Sote tusitawishe.
Tutaepuka kinyongo,
Na uchungu wa chuki.
Tusamehepo kikweli,
Twafanana na Mungu,
Apendaye kusamehe,
Neema twatukuza.