Wimbo 149
“Haiwezekani Mungu Kusema Uwongo”
1. Aliposhinda jaribu Abra’mu,
Mungu alimwahidia baraka.
Aliona baraka kwa imani;
Kajua Mungu hasemi uwongo.
2. Mungu akionyesha hageuki,
Mungu alibariki Abrahamu,
Twamutukuza, tuna tumaini,
Kwa kuwa Mungu hasemi uwongo.
3. Kutia nanga tumaini letu,
Ahadi Mungu aliiapia.
Twapinga ’shambulizi; ya imani;
Twajua Mungu hasemi uwongo.
4. Yehova ni mwaminifu wa kweli.
Haachi wamupao haki yake.
Neno, kiapo chake, tuamini.
La, hasha, Mungu hasemi uwongo.