Wimbo 201
Kufurahi Pamoja na Taifa la Mungu
1. Kwa kazi ya kuhubiri
Tunasihi watu wote:
“Sikilizeni Biblia.
Nanyi utafuteni ukweli.”
Mungu anaita,
Watu kutoka musiba,
Wapate taraja zuri,
Mufumo Mupya anaofanya.
(Korasi)
2. Ona! ‘taifa tukufu’
Limeundwa na Yehova
Zizini mwake kwa wakfu,
Litangaze wokovu wa Mungu.
Kibali ’tapewa
Tukitenda kwa adabu,
Kuiga Kristo Mwokozi;
Na tusiache utawa huo.
(Korasi)
3. Katika nchi kubwa bora,
Bila mizozo yoyote,
Ona! umati wa shangwe,
Utumishini mwema wa Mungu.
Hawapigi kite.
Kweli ya Mungu watwaa,
Wafuata Neno lake,
Na jina lake wanatukuza.
(KORASI)
Furahini, E watu!
Semeni ujumbe
Huo na “taifa” la Mungu.
Sujudieni Mungu.
Mwabuduni yeye.
’Jipange na Ufalme wa Mungu.