Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • su sura 13 kur. 98-104
  • Wakati wa Uumbaji Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wakati wa Uumbaji Mpya
  • Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • FAIDA ZINAZOPATIKANA SASA KUTOKANA NA DHABIHU YA KRISTO
  • “KATIKA UUMBAJI MPYA”
  • Kufanya Vitu Vyote Kuwa Vipya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Fidia
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Maisha Katika Paradiso Iliyorudishwa
    Amkeni!—2008
  • Sababu Twauhitaji Ufalme wa Yesu Kristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
Pata Habari Zaidi
Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya
su sura 13 kur. 98-104

Sura 13

Wakati wa Uumbaji Mpya

1. (a) Ni nafasi gani nzuri ajabu ambayo waokokaji wa kuingia katika “dunia mpya” wanatazamia? (b) Lakini hiyo itataka nini?

KUUOKOKA mwisho wa ulimwengu mbovu wa sasa ni tazamio zuri ajabu. Sisi tunataka sana mambo yasiyo ya haki, pupa na jeuri ya ulimwengu yaondolewe mbali nasi. Lakini jambo jinginelo linafanya itamanike hata zaidi tuje tuokolewe. Ni jambo gani? Ni uhakika wa kwamba wote wanaokuwa sehemu ya “dunia mpya” watakuwa na nafasi pia ya kukombolewa katika kutokamilika kwao wenyewe, katika magonjwa na maisha yenye maumivu, ndiyo, hata katika kifo. (Ufunuo 21:1-5) Hata hivyo, ili jambo hilo litukie ni lazima dhambi yenyewe ing’olewe kabisa. Hilo lawezekanaje? Linahusiana na kile ambacho Yesu Kristo alikieleza kuwa “uumbaji mpya.”

2. “Uumbaji mpya” unaotajwa katika Mathayo 19:28 ni nini?

2 Yesu aliwaambia mitume wake hivi: “Katika uumbaji mpya, wakati Mwana wa mtu atakapoketi katika kiti cha ufalme chake chenye utukufu, ninyi ambao mmenifuata mimi, ninyi wenyewe pia mtaketi katika viti vya ufalme kumi na viwili, muwe mkihukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.” (Mathayo 19:28, New World Translation) Uumbaji mpya utakuwa wakati wa “kufanya kizazi kipya,” “wakati vyote vitakapofanywa vipya,” kama zinavyosema tafsiri nyingine za Biblia. (The Emphasised Bible, ya Rotherham; The Jerusalem Bible) Kupitia uumbaji mpya huo, itawezekana kwa wanadamu kufurahia tena ule ukamilifu ambao wanadamu walikuwa nao pale mwanzoni.

3. (a) Matokeo ya dhambi ya Adamu yamekuwa nini? (b) Kwa nini hakuna wo wote wa watoto wa Adamu ambao wameweza kujikomboa wenyewe katika matokeo ya dhambi iliyorithiwa?

3 Kwa sababu ya dhambi iliyorithiwa kutoka kwa Adamu, watoto wake wote walilazimika kufa, na wengi wamesumbuliwa na ugonjwa wenye kusikitisha, ukaongoza kwenye kifo. (Warumi 5:12) Hakuna uhuru wa kufanya watu wasife ambao ungeweza kununuliwa na fedha. Hakuna kazi alizoweza mwanadamu asiyekamilika kuzifanya ambazo zingeweza kumpatia kujifungua mwenyewe wala kufunguliwa kwa mtu mwingine. Haki ya kimungu ilitaka kwamba ikiwa wanadamu wangepata tena nafasi ya kufurahia uzima wa milele, ni lazima dhabihu itolewe ikiwa inalingana thamani na kile ambacho Adamu alipoteza, yaani, uhai mkamilifu wa kibinadamu. Hakuna wo wote kati ya watoto wa Adamu waliokuwa na uhai huo wa kutoa uwe dhabihu.—Zaburi 49:7-9; Mhubiri 7:20.

4. (a) Ukombozi uliohitajiwa ulitolewaje? (b) Tunaweza kufaidikaje nao?

4 Kwa rehema, Yehova mwenyewe alifanya mpango uliohitajiwa kwa kumtuma Mwanaye-mzaliwa-pekee, Yesu, aje duniani akiwa binadamu mkamilifu ili atoe uhai wake kuwa “dhabihu inayolingana.” (1 Timotheo 2:5, 6, New World Translation) Huo ulikuwa wonyesho mkuu kama nini wa fadhili zisizostahilika na wa upendo wa Mungu kwa wanadamu! Uhai ambao umewezekana yakiwa ni matokeo ya wonyesho huo hatuwezi kuupata kama mshahara kwa sababu ya kazi zetu, bali ni zawadi kutoka kwa Mungu. Ingawa hivyo, zawadi hiyo wanapewa wale tu wanaokubali kikweli uhitaji wao wa mpango huo wa kimungu, wanaouamini na kuonyesha imani hiyo kwa kumtii Mwana wa Mungu. (Warumi 6:23; Yohana 3:16, 36) Lakini ni wakati gani ambapo wanadamu wangepata faida za dhabihu hiyo?

FAIDA ZINAZOPATIKANA SASA KUTOKANA NA DHABIHU YA KRISTO

5. (a) Ni nani waliokuwa wa kwanza kufaidika na dhabihu ya Kristo? (b) Ni kikundi gani kingine ambacho kimefaidika, na hasa tangu wakati gani?

5 Faida zilianza kugeuza maisha za wanadamu mara Yesu Kristo (akiwa katika cheo cha kuwa Kuhani Mkuu wa Mungu) alipokwisha kutoa mbele za Mungu ubora wa dhabihu yake mbinguni. Kwanza, tangu Pentekoste ya mwaka wa 33 W.K., faida hizo zilianza kuonwa na wale ambao, wakiwa wameitwa wawe warithi pamoja na Kristo, wangetumika wakiwa wafalme na makuhani pamoja naye mbinguni. (Matendo 2:32, 33; Wakolosai 1:13, 14) Halafu, kwa kutokeza katika mwaka wa 1935, watu waliolipokea kwa moyo tumaini la uzima wa milele duniani walianza kujitokeza wenyewe. Tumaini lao, pia, lilifanywa liwezekane kupitia dhabihu ya Kristo. (1 Yohana 2:1, 2) Matumizi ya hatua kwa hatua ya ubora wa dhabihu hiyo yalionyeshwa na matukio yaliyotokea Siku ya Upatanisho ya Israeli wa kale.

6. Simulia kifupi yaliyotukia Siku ya Upatanisho.

6 Aliyekuwa akifanya kazi katika hema takatifu la Israeli, na baadaye katika hekalu, alikuwa kuhani mkuu aliyekuwa mshiriki wa nyumba ya Kilawi ya Haruni. Wanaume wengine wa nyumba ya Haruni walikuwa makuhani wadogo, na wengine kati ya wanaume hao wa kabila la Lawi walitumika wakiwa wasaidizi. Ili kutoa kifuniko cha dhambi, kuhani mkuu alitoa dhabihu ya wanyama wawili, damu ya kila mnyama ilitolewa mbali na ya mnyama mwingine katika Patakatifu Zaidi Sana, kama Yehova alivyoagiza. Kwanza ng’ombe dume alitolewa na kuhani mkuu wa nyumba ya Haruni kwa ajili ya “nafsi yake mwenyewe, na kwa ajili ya nyumba yake,” ambayo ni pamoja na kabila zima la Lawi. (Mambo ya Walawi 16:11, 14) Mnyama aliyefuata kutolewa kuwa toleo la dhambi “kwa ajili ya watu,” yaani, makabila mengine kumi na mawili, ni mbuzi. (Mambo ya Walawi 16:15) Tena, zile dhambi za Israeli wote ziliungamwa juu ya kichwa cha mbuzi aliye hai, kisha akaongozwa mbali mpaka kuingia jangwani. (Mambo ya Walawi 16:21, 22) Yote hayo yalikuwa na maana gani?

7. (a) Ni dhabihu gani moja iliyofananishwa wakati huo? (b) Kwa nini wanyama wa dhabihu zaidi ya mmoja walitumiwa?

7 Mtume Paulo anaeleza kwamba utimizo wa hayo unategemea dhabihu ile moja ya Yesu Kristo. “Kristo hakuingia katika patakatifu palipofanyika kwa mikono, ndio mfano wa patakatifu halisi; bali aliingia mbinguni hasa, aonekane sasa usoni pa Mungu kwa ajili yetu . . . azitangue dhambi kwa dhabihu ya nafsi yake.” (Waebrania 9:24-26) Basi kwa nini damu ya wanyama zaidi ya mmoja iliingizwa katika Patakatifu Zaidi Sana Siku ya Upatanisho wa Israeli? Ilifanywa hivyo ili kuvuta fikira kwenye sehemu mbalimbali za mambo yanayotimizwa na dhabihu kamilifu ya kibinadamu ya Yesu. Na sehemu moja zaidi ilikaziwa kwa ungamo la dhambi za taifa hilo juu ya kichwa cha mbuzi aliye hai kisha akaongozwa mpaka kuingia mbali jangwani.

8. (a) Taratibu za Siku ya Upatanisho zilionyeshaje ni nani wangekuwa wa kwanza kufaidika na dhabihu ya Kristo? (b) Ni matumizi gani ya dhabihu ya Yesu yaliyoonyeshwa kwa lile toleo la dhambi “kwa ajili ya watu”? (c) Ni uhakika gani zaidi uliofananishwa kwa kumwongoza mbuzi mbali mpaka jangwani?

8 Kama vile damu ya ng’ombe dume iliyotolewa kwa ajili ya nyumba ya Haruni ilivyoingizwa kwanza katika Patakatifu Zaidi Sana, ndivyo zile faida za dhabihu ya Yesu zilivyotumiwa kwanza kwa ajili ya wale ambao wangeshirikiana na Kristo katika ukuhani wa kimbingu. Hilo lilifanywa tangu mwaka wa 33 W.K. na kuendelea. Yesu Kristo hakuwa na dhambi za kufanya iwe lazima zifunikwe, kama alivyofanya Haruni, bali wale ambao wangekuwa makuhani wadogo pamoja na Kristo walikuwa nazo. Hao walifananishwa na kabila la Lawi. (1 Petro 2:4, 5) Kutolewa kwa damu kutoka dhabihu ya pili, yule mbuzi wa toleo la dhambi “kwa ajili ya watu,” kulionyesha kwamba wengine kati ya wanadamu wangefaidika na dhabihu ya Yesu baada ya jamii ya kimbingu kufaidika. Hao wangekuwa watu ambao wangepata uzima duniani katika Paradiso itakayorudishwa. Walifananishwa na “kabila kumi na mbili [zisizo za kikuhani] za Israeli” Siku ya Upatanisho. (Mathayo 19:28; Zaburi 37:29) Yesu hakufa kwa ajili ya hao wote tu, bali yeye hasa anazichukua dhambi za wale aliofia kifo cha dhabihu, awaletee faraja. Jambo hilo lilionyeshwa na uhakika wa kwamba, hatimaye, dhambi za Israeli zilipokwisha kuungamwa juu ya mbuzi aliye hai, mbuzi huyo aliongozwa mbali mpaka kuingia jangwani, asionwe tena kamwe.—Zaburi 103:12; Isaya 53:4-6.

9. (a) Ni baraka gani ambazo wale wanaozoea imani katika dhabihu ya Kristo wanafurahia sasa? (b) Ni faida gani zaidi zitakazokuja baadaye?

9 Bila kujali namna yao ya maisha ya zamani, wale wote wanaozoea imani katika mpango wa upendo wa Yehova kupitia Kristo wanaweza kupata sasa msamaha wa kweli wa dhambi, msimamo ulio safi mbele za Mungu. Wanaweza kufurahia baraka yenye thamani sana ya kumtolea Mungu utumishi mtakatifu kwa dhamiri safi. (1 Wakorintho 6:9-11; Waebrania 9:13, 14) Lakini hiyo haimaanishi kwamba kwa sasa wamepewa uzima usio na matokeo yote ya dhambi. (1 Yohana 1:8-10; Warumi 7:21-25) Uzima kama huo utapatikana kwa wale watakaotawala mbinguni pamoja na Kristo, watakapomaliza tu mwendo wao wa kidunia na kufufuliwa kwenye hali ya kutoweza kufa katika mbingu. Kwa wengine kati ya wanadamu, ondoleo kamili la dhambi litafanywa lipatikane kupitia uumbaji mpya.

“KATIKA UUMBAJI MPYA”

10. (a) Uumbaji mpya ulianza lini? (b) Je! wo wote wamepewa viti vya ufalme kwa kutimiza ahadi ya Yesu?

10 Kama Yesu alivyosema, uumbaji mpya ni “wakati Mwana wa mtu [Yesu Kristo] atakapoketi katika kiti cha ufalme chake chenye utukufu.” (Mathayo 19:28, New World Translation) Bila shaka, si kila kitu kilichotukia mara alipotawazwa. Baada ya kutawazwa kwa Yesu mwaka wa 1914 W.K., kwanza alizisafisha mbingu, akamfukuza Shetani na mashetani wake. Ndipo akaanza kufufua wafuasi wake wapakwa-mafuta waende kwenye utukufu wa kimbingu. (Ufunuo 12:5, 7-12; 1 Wathesalonike 4:15-17) Si mitume waaminifu tu wa Kristo waliopewa “viti vya ufalme kumi na viwili” walivyoahidiwa, bali hatua kwa hatua wengine wote wa wale 144,000 wanatawazwa mbinguni wanapofufuliwa kutoka kwa wafu.—Ufunuo 3:21.

11. Ni kwa njia gani “kondoo wengine” tayari wanahisi matokeo ya uumbaji mpya?

11 Kuchaguliwa kwa watu wa kuwa sehemu ya jamii ya kimbingu kulipokaribia kumalizika, kukusanywa kwa umati mkubwa wa “kondoo wengine” kulianza, hasa tangu mwaka wa 1935 na kuendelea. Hao, pia, walianza kufurahia faida za dhabihu ya Kristo, ‘wakifua mavazi yao na kuyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo.’ Sasa wanasaidiwa ‘wauvae utu mpya ulioumbwa kulingana na mapenzi ya Mungu katika uadilifu wa kweli na ushikamanifu.’ (Ufunuo 7:9, 10, 14, Union Version; Waefeso 4:20-24, New World Translation) Wanafaidika kwa hesabu inayoongezeka wakati wote kutokana na maandalizi ya Mungu kupitia Kristo yanayoweza kuwaongoza wakaishi milele katika Paradiso itakayorudishwa.—Ufunuo 7:17; 22:17.

12. (a) Ni nani waliofananishwa na “kabila kumi na mbili za Israeli” ambazo Yesu alitaja hapa? (b) Zaidi ya waokokaji, ni nani wengine watakaofaidika na uumbaji mpya?

12 Karibuni, sasa, ulimwengu mbovu utaharibiwa. Shetani na mashetani wake watafungwa katika shimo refu. Siku ya Hukumu ya miaka elfu moja kwa wanadamu itaanza. Yesu Kristo ndiye atakayekuwa Hakimu Msimamizi, naye atahakikisha kwamba wote wamepewa nafasi kamili na msaada wa kutosha ili waweze kujifunza njia za Yehova za uadilifu na kuzifuata. Wafuasi wale wapakwa-mafuta wa Kristo waliojithibitisha kuwa washika-ukamilifu mpaka kufa watashiriki pamoja naye katika kazi hiyo, ‘wakihukumu kabila kumi na mbili za Israeli.’ (Luka 22:28-30; Ufunuo 20:4, 6) Hiyo haina maana kwamba watahukumu wazao-asili tu wa Israeli. Bali, watahukumu wote waliofananishwa Siku ya Upatanisho na “kabila kumi na mbili [zisizo za kikuhani] za Israeli.” Hao ni pamoja na ulimwengu mzima wa wanadamu waliokombolewa. (1 Wakorintho 6:2) Waokokaji wa dhiki kubwa ndio watakaokuwa wa kwanza kufaidika na programu hiyo ya kuinua hali ya wanadamu. Lakini mabilioni zaidi pia watashiriki, kwa sababu wale watakaohukumiwa ni pamoja na “walio hai na waliokufa.” (2 Timotheo 4:1; Matendo 24:15) Itasisimua kama nini wakati wafu wanaotiwa katika dhabihu ya ukombozi wa Kristo watakaporudi! Wee, machozi ya furaha yatatiririka kama nini wakati wapendwa watakapoungana tena!

13. Matokeo ya Siku ya Hukumu ya miaka elfu moja yatakuwaje uumbaji mpya kweli kweli?

13 Huo utakuwa ndio wakati ambao, hatimaye, wanadamu wataondolewa udhaifu wa mwili na wa akili uliofanyizwa na dhambi. Alipokuwa duniani, Yesu aliponesha mara moja watu waliokuwa wamepooza, wale waliokuwa vipofu au viziwi au wale ambao hawangeweza kusema, na watu ambao mwili wao ulikuwa umeumbuka au ambao nguvu zao zilikuwa zimemalizwa na ugonjwa. Kazi hizo zenye nguvu zilikuwa mwonjo tu wa atakayofanyia wanadamu wote wakati wa Utawala wa Miaka Elfu wake. Kwa sababu nzuri, watu wo wote watakaoshuhudia au kuona ushahidi huo wa ajabu wa fadhili za Yehova kisha waidharau enzi kuu yake wataangamizwa milele. Lakini kwa kuelimishwa katika njia za uadilifu za Yehova, fikira na makusudi ya wale ambao kwa unyofu wa moyo wataonyesha imani na utii, watafanya maendeleo pole kwa pole mpaka wakamilike kabisa. Watu hao wenye kumpenda Yehova watakuwa wamejionea kweli kweli kizazi kipya, uumbaji mpya. Itakuwa kama kwamba wamepewa mwanzo mpya maishani pamoja na baba mpya, yule Baba wa Milele, Yesu Kristo.—Isaya 26:9; 9:6.

14. Ni uhusiano gani wenye thamani sana ambao wote watakaopita jaribu la mwisho watapendelewa kufurahia?

14 Ndipo, baada ya kupita jaribu la mwisho wakati wa kumalizika kwa miaka elfu moja, watafanywa na Yehova Mungu kupitia Kristo wawe wana wa Mungu mwenyewe, sehemu ya jamaa Yake kamilifu ya ulimwengu mzima wote. Lo! hilo ni tazamio lenye kutia moyo wee—si kwa waokokaji tu wa dhiki kubwa bali pia kwa waliokufa wote watakaorudishwa waje waishiriki furaha ya uzima katika dunia-Paradiso!—Warumi 8:20, 21.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki