Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • su sura 18 kur. 138-144
  • Je! Wewe ni Mshikamanifu kwa Mfalme Mpya wa Dunia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe ni Mshikamanifu kwa Mfalme Mpya wa Dunia?
  • Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MATENDO YA MFALME MWENYEWE YA USHIKAMANIFU
  • UPENDO MSHIKAMANIFU KWA WAPAKWA-MAFUTA WA YEHOVA
  • USHIKAMANIFU UNATUTAKA TUFANYE NINI?
  • “Wewe Peke Yako Ni Mwaminifu-Mshikamanifu”
    Mkaribie Yehova
  • Kukabili Mtihani wa Uaminifu-Mshikamanifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Watazame Wale Waaminifu-Washikamanifu!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Ushikamanifu Kwa “Ufalme wa Bwana Wetu na wa Kristo Wake”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
Pata Habari Zaidi
Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya
su sura 18 kur. 138-144

Sura 18

Je! Wewe ni Mshikamanifu kwa Mfalme Mpya wa Dunia?

1. Yesu alipoonyeshwa kuwa Mfalme mwaka wa 33 W.K., umati wa watu uliitikiaje?

NISANI 9 ya mwaka wa 33 W.K., Yesu Kristo alijionyesha mwenyewe kwa Wayahudi kuwa Mfalme wao, Masihi aliyetabiriwa. Alipokuwa akishuka Mlima wa Mizeituni kuelekea Yerusalemu, umati wa wanafunzi wake ulishangilia ukamsifu Mungu kwa sababu ya kazi za nguvu ambazo Yesu alikuwa amefanya. (Luka 19:37, 38; Zekaria 9:9) Lakini wangejithibitisha kuwa washikamanifu kwa Yeye ambaye walishangilia kuwa Mfalme? Upesi ushikamanifu wao ulijaribiwa.

2. (a) Watu wengi leo wanaitikiaje lile tangazo la kwamba Kristo ni Mfalme mpya wa dunia? (b) Lakini ni maulizo gani yanayostahili kufikiriwa kwa uzito?

2 Tangu mwaka wa 1914 Yesu Kristo aliyetukuzwa akiwa anatawala kwa kutenda kutoka mbinguni ametolewa kwa wanadamu wote kuwa Mfalme mpya wa dunia. Tazamio la kuishi chini ya serikali iliyo mikononi mwa Kristo, ikiwa na njia za kweli kweli za kuondolea matatizo ya wanadamu, limefanya watu wa mataifa yote washangilie. Lakini watajithibitisha kuwa washikamanifu? Vipi sisi mmoja mmoja?

MATENDO YA MFALME MWENYEWE YA USHIKAMANIFU

3. (a) Kwa nini Yesu mwenyewe anatajwa kuwa “mshikamanifu” wa Yehova? (b) Ushikamanifu ni nini?

3 Yesu Kristo ametoa ushahidi mwingi kuonyesha kwamba ushikamanifu wake mwenyewe kwa Yehova, Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu Mzima, si wa kuyumbayumba. Yeye anatajwa kwa kufaa katika Maandiko kuwa “mshikamanifu” wa Yehova. (Zaburi 16:10; Matendo 2:24-27, New World Translation) Neno la Kiebrania linalotumiwa hapa kuwa Ushikamanifu” lina wazo la kuwa mwenye fadhili kwa upendo. Si jambo fulani ambalo ni baridi, lenye kutegemea tu sheria au haki, bali linaongozwa pia na upendo na kuthamini.—Linganisha Zaburi 40:8; Yohana 14:31.

4, 5. (a) Ushikamanifu wa Yesu ulionyeshwaje mbinguni, baada ya kuasi kwa Shetani? (b) Ushikamanifu huo ulionyeshwaje pia duniani?

4 Huko mbinguni, Shetani alipoanza kujitafutia heshima iliyokuwa ya Mungu peke yake na wakati wengine kati ya malaika walipoacha mahali pao penye kufaa katika tengenezo la Yehova la kimbingu, Mwana-mzaliwa wa kwanza wa Mungu hakufuata mfano wa roho yao. Kufanya hivyo kulikuwa jambo lisilofikirika kwa upande wake! Ndivyo alivyojitoa kwa kujinyima hata, katika kutimiza mapenzi ya Baba yake, Mwana huyo mshikamanifu akaacha utukufu wake wa kimbingu, akawa binadamu na hata akajitiisha kwenye kifo juu ya mti wa mateso. Kwa upendo, alihakikisha kwamba, maadamu ilimtegemea yeye, hakuna lo lote alilopangiwa na Maandiko lingekosa kutimizwa—Wafilipi 2:5-8; Luka 24:44-48.

5 Yesu alipokuwa duniani, Shetani alimletea mkazo mkubwa ili kumwondoa katika kazi ambayo Mungu alikuwa amempa aifanye—ikiwa ingewezekana, amshawishe kufanya jambo ambalo lingemfanya Mungu mwenyewe amkatae Mwanaye. Alimwomba sana Yesu atende mambo ambayo yangeweza kutokeza umashuhuri na uwezo—lakini awe sehemu ya ulimwengu ambao Shetani alikuwa mtawala. Yesu alikataa, akatumia Maandiko Matakatifu kuwa mwongozo wake. (Mathayo 4:1-10) Yesu alikuwa na uwezo mbalimbali wenye kutokeza na aliutumia vizuri, lakini sikuzote kupatana na mapenzi ya Baba yake. Alijishughulisha sana na kazi ambayo Mungu alikuwa amemtuma aifanye. (Yohana 7:16-18; 8:28, 29; 14:10) Mfano mzuri kama nini wa ushikamanifu!

6. Ni kwa njia gani ile thawabu aliyopewa Yesu inataka ushikamanifu wetu?

6 Kwa sababu ya ushikamanifu wa Yesu uliojaribiwa, Yehova alimfufua kutoka kwa wafu, “Mungu vilevile alimutukuza sana, na kumupa jina lililo juu ya kila jina; hata kwa jina la Yesu kila goti lipigwe . . . na kila ulimi ukiri ya kuwa Yesu Kristo ni Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.” (Wafilipi 2:9-11, Zaïre Swahili Bible) Hilo “Jina lililo juu ya kila jina” linamaanisha uwezo wa mamlaka aliyopewa Yesu ili aweze kutimiza mapenzi ya Yehova. ‘Kumpigia magoti’ kunamaanisha kukikubali cheo chake na kuitii mamlaka yake. Kunatia ndani kumtii kishikamanifu kuwa Mfalme.

UPENDO MSHIKAMANIFU KWA WAPAKWA-MAFUTA WA YEHOVA

7. Wafuasi wa Yesu wanajaribiwa kama ni washikamanifu juu ya mambo gani?

7 Uhakika wa kwamba, baada ya kupaa kwake mbinguni, Yesu hangeweza kuonwa tena kwa macho ya kibinadamu ungetokeza kwa wafuasi wake majaribu ya ushikamanifu yenye kuchunguza moyo. Je! wangezifuata kanuni ambazo alikuwa amewafundisha? Je! wangeendelea kujitenga na ulimwengu? Je! wangeheshimu wale ambao roho takatifu iliwapa madaraka ya uangalizi? Je! wangeifanya kazi aliyokuwa amewagawia kwa nafsi yote?

8. Ni nini kilichofananishwa na upendo mshikamanifu uliokuwa kati ya Yonathani na Daudi?

8 Kwa wakati wake “kondoo wengine” wangekusanywa waletwe katika ushirika na “kundi dogo” la warithi wa Ufalme wa kimbingu. Je! wangethamini kweli kweli vyeo walivyogawiwa kuhusiana na Kristo akiwa Mfalme na kuhusiana wao kwa wao? Mambo ya hakika yanaonyesha kwamba upendano wa kweli umesitawi kati ya wote walio sehemu ya “kundi moja” chini ya Yesu Kristo. Hilo lilifananishwa na upendo usiovunjika, usiokufa, aliokuwa nao Yonathani mwana wa Mfalme Sauli kwa Daudi. Alipojionea jinsi Daudi alivyojitoa kabisa kwa Yehova na alivyomtegemea Mungu kwa kuliua jitu Goliathi, moyo wa Yonathani ulivutwa sana na “nafsi yake mwenyewe ikaja kufungamana pamoja na nafsi ya Daudi, na Yonathani akaanza kumpenda kama nafsi yake mwenyewe.” Upendo wake haukupungua ilipoonekana wazi kwamba Yehova angempa Daudi umaliki, wala si Yonathani. Yonathani hata alihatirisha uhai wake mara nyingi kwa ajili ya Daudi.—1 Samweli 17:45-47; 18:1, New World Translation; 23:16, 17.

9. Ushikamanifu kama huo ulionyeshwaje na watu wasiokuwa Waisraeli waliotumikia katika jeshi la Daudi?

9 Zaidi ya Yonathani, kulikuwako watu wasio Waisraeli waliojishikamanisha na Daudi. Hao hawakuwa askari wa kukodishwa bali walikuwa wanaume hodari waliotenda hivyo kwa kujitoa kwa Daudi mpakwa wa Yehova. Wakerethi, Wapelethi na wazaliwa wa zamani wa mji wa Kifilisti wa Gathi walikuwa kati ya hao. Waliambatana kwa ushikamanifu na Daudi wakati Absalomu mwanaye alipotafuta kwa udanganyifu kuiba mioyo ya wanaume wa Israeli. Ijapokuwa umashuhuri na ujanja wa Absalomu, hawakuongozwa na mazungumzo yake laini waingie katika mwendo wa uhaini.—2 Samweli 15:6, 10, 18-22.

10. (a) Uhusiano wa karibu sana kati ya Kristo, mabaki wapakwa-mafuta na “kondoo wengine” unafananishwaje katika Zaburi 45? (b) Ni katika maana gani ‘wanawali wenzake wanaingia katika nyumba ya mfalme’?

10 Simulizi jingine lenye kuchangamsha moyo la uhusiano ulio kati ya Kristo, mabaki wapakwa-mafuta na “kondoo wengine” linapatikana katika Zaburi 45. Hilo si shairi zuri tu bali linahusu unabii wa Ufalme wa Kimasihi—Mungu mwenyewe akiwa ndiye ‘kiti cha enzi,’ yaani, ndiye msingi na tegemezo la umaliki wa Yesu. (Zaburi 45:1-7; Waebrania 1:8, 9) Mtunga zaburi anasimulia bibi-arusi wa Kristo, “binti mfalme,” akipelekwa kwa Mfalme siku yake ya arusi. Walio pamoja naye ni “wanawali wenzake wanaomfuata.” Hao ni akina nani? Ndio wanaotazamia sana kuja kuwa raia za kidunia za Ufalme wa Mungu. “Kwa furaha na shangwe” wanafuata jamii ya “bibi-arusi” mpaka yule wa mwisho wa hao atakapoungana na Kristo mbinguni. Pamoja nao, ‘wanaingia katika nyumba ya mfalme,’ si kwa kupanda mbinguni, bali kwa kujitoa wenyewe wafanye utumishi wa Mfalme. Je! wewe umekuwa sehemu ya mwandamano huo wenye furaha?—Zaburi 45:13-15.

USHIKAMANIFU UNATUTAKA TUFANYE NINI?

11. Ni hali gani inayotuweka kwenye jaribu la kama sisi “si sehemu ya ulimwengu”?

11 Hali maishani zisizohesabiwa zinaonyesha sisi ni watu wa aina gani. Je! tunauamini ufalme wa Kimasihi wa Yehova kweli kweli? Je! ni halisi kwetu? Yesu alisema kwamba wafuasi wake wa kweli wangekuwa “si sehemu ya ulimwengu.” Je! ndivyo wewe ulivyo?—Yohana 17:15, 16, New World Translation.

12. Tujapokuwa wasiokamilika, ni kwa njia zipi zaidi tunaweza kutoa ushahidi wa ushikamanifu?

12 Kwetu sisi wanadamu tusiokamilika, ushikamanifu hautudai ukamilifu. Lakini unatutaka tuepuke kuvunja kimakusudi amri za Biblia, hata kama wanadamu wenzetu wanatuona au hawatuoni. Utatuongoza tujitahidi kufuata sana kanuni za Biblia, badala ya kutaka kuona kadiri tunavyoweza kuwa karibu sana na njia za ulimwengu. Utatufanya tusitawishe uchukivu ulio kweli kweli kwa yaliyo mabaya.—Zaburi 97:10.

13. Ushikamanifu utatulindaje na mazungumzo laini ya waasi-imani?

13 Ikiwa tunachukia kweli kweli mabaya, hatutaruhusu utafiti utushawishe tuwe karibu nayo. Kuwa mwenye utafiti juu ya maisha ya watu ambao ni waasherati kwaweza kumwongoza mtu kwenye maangamizi. (Mithali 7:6-23) Vilevile, uangamivu wa kiroho unaweza kuwapata wale ambao kwa utafiti wananunua na kusoma vitabu vinavyochapishwa na waasi-imani ambao wamemwacha Yehova na kuliacha tengenezo lake na ambao halafu wanaanza “kuwapiga” kwa maneno wale waliokuwa washiriki wao zamani. (Mathayo 24:48-51) Mithali 11:9, New World Translation, inaonya hivi: “Kwa kinywa chake yeye aliye mwasi-imani anamleta mwenziye kwenye uangamivu.” Lakini ushikamanifu utatulinda tusipotezwe na mazungumzo yao laini.—2 Yohana 8-11.

14. (a) Ni ipi mojapo njia za maana zaidi sana tunazoweza kuonyesha ushikamanifu wetu kwa Kristo akiwa Mfalme? (b) Kwa nini kazi hiyo ni ya maana sana?

14 Mojapo njia za maana zaidi sana tunazoweza kuonyesha ushikamanifu ni kwa kuifanya kwa nafsi yote kazi ambayo Yesu alifundisha wanafunzi wake wafanye. Yeye binafsi aliweka mfano kwa kwenda mji kwa mji na kijiji kwa kijiji, akizihubiri habari njema za Ufalme wa Mungu. (Luka 8:1) Yesu alitabiri kazi ambayo Wakristo wa kweli wangekuwa wakifanya leo aliposema: “Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.“ (Mathayo 24:14, New World Translation) Lile suala la Ufalme linatolewa kwa watu kila mahali kupitia kuhubiriwa huko kwa habari njema ili waweze kuamua kibinafsi. Uamuzi huo utaongoza umati mkubwa ukahifadhiwe katika dhiki kubwa. (Ufunuo 7:9, 10) Je! wewe unashiriki kwa ushikamanifu kazi hiyo ya haraka?

15. (a) Zaburi 145:10-13 inasema washikamanifu wa Yehova wangekuwa wakizungumza juu ya nini? (b) Hilo linatuhusuje sisi?

15 Hapo kale, Daudi, mtunga zaburi aliandika hivi: “kazi zako zote zitakusifu, Ee Yehova, na washikamanifu wako watakubariki. Watazungumza juu ya utukufu wa umaliki wako, na juu ya uweza wako watasema, ili kuwajulisha wana wa watu matendo yake makuu mno na utukufu wa adhama ya umaliki wake. Umaliki wake ni umaliki wa nyakati zote zisizojulikana, na utawala wako ni wa vizazi vyote vyenye kufuatana.” (Zaburi 145:10-13, New World Translation) Sasa umaliki huo unatumiwa kupitia Ufalme wa Kimasihi ulio katika mikono mishikamanifu ya Yesu Kristo. Na kwa kusema juu yake bila kusita na kwa shauku, tunaonyesha ushikamanifu wetu kwa Mungu na kwa Kristo.

16. Ushikamanifu umepasa uvuteje kadiri tunayoshiriki kuhubiri Ufalme na kinachotuongoza tufanye hivyo?

16 Wewe umeipa kazi hii ya kutoa ushuhuda juu ya Ufalme nafasi kubwa namna gani maishani mwako mwenyewe? Je! kweli unaiweka mbele ya shughuli nyingine? Huenda unayofanya wewe binafsi yakawa mengi au machache zaidi ya wengine. Hali za mtu mmoja mmoja zinatofautiana. Lakini sote tunaweza kupata faida kwa kujiuliza wenyewe maulizo kama haya: ‘Je! kushiriki kwangu kunaonyesha kutimiza wajibu tu, au kunaonyesha tu ninatoa angalau kitu fulani? Je! ninakuona kuwa takwa tu la kutimizwa ili mtu aje aokoke? Au kumpenda Yehova, kujitoa kwa Mfalme wa Kimasihi Wake na kuhangaikia kikweli mwanadamu mwenzangu kunaniongoza nikupe nafasi ya kwanza ili mapendezi mengine maishani mwangu yakutegemee?’ Ushikamanifu utatuongoza tutafute njia za kuonyesha kwamba kazi hiyo ni ya maana kwetu kama ilivyo kwa Mfalme wetu.

17. Yesu “atasema amani” kwa nani atakapowaangamiza waovu?

17 Hivi karibuni Yeye aliyeshangiliwa kwa furaha na wanafunzi wake kuwa Mfalme alipoingia Yerusalemu mwaka wa 33 W.K. atawaangamiza wote wanaokataa enzi kuu ya Yehova inayoonyeshwa kupitia Mfalme wa Kimasihi ambaye Yehova ameweka. Lakini yeye “atasema amani” kwa “mkutano mkubwa” huo wa watu kutoka mataifa yote ambao wamefuata mfano wake mwenyewe wa ushikamanifu. Je! wewe utakuwa mmoja wao?—Zekaria 9:10, New World Translation; Waefeso 4:20-24.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki