Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • je kur. 26-27
  • Kuchunga Kundi la Mungu kwa Umoja

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuchunga Kundi la Mungu kwa Umoja
  • Mashahidi wa Yehova—Wanafanya Mapenzi ya Mungu kwa Umoja Ulimwenguni Pote
  • Habari Zinazolingana
  • Kushirikiana na Baraza Linaloongoza Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Ni Nani Anayewaongoza Watu wa Mungu Leo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Baraza Linaloongoza Hufanyaje Kazi Leo?
    Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Usitawi wa Muundo wa Tengenezo
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Mashahidi wa Yehova—Wanafanya Mapenzi ya Mungu kwa Umoja Ulimwenguni Pote
je kur. 26-27

Kuchunga Kundi la Mungu kwa Umoja

Wengine wanauliza: ‘Kundi la ulimwenguni pote la Mashahidi wa Yehova linaongozwaje?’ Tunajibu hivi: Mpango wenye kuongoza unafuata kiolezo cha kundi la Kikristo la karne ya kwanza.

Katika miaka ya kuanzia 1870 Charles T. Russell na washiriki wake walichukua hatua ya kwanza katika kueneza matokeo ya funzo lao la Biblia kwa njia ya hotuba na vichapo. Kila upande wa nchi, wale waliochagua kushirikiana na kazi hiyo walitegemea Russell na washiriki wake wa karibu kuwa baraza la wanaume walio na ujuzi mwingi zaidi wa kufanya kazi ya Bwana na ambao kutoka kwao wangeweza kupata shauri kuhusu utendaji wao.

Mwaka wa 1884 Shirika Zion’s Watch Tower Tract Society lilianzishwa chini ya sheria za Jumuiya ya Madola ya Pennsylvania. Russell na washiriki wake wenye madaraka walihusika sana na kuelekeza Sosaiti hii na pia utendaji wa Wanafunzi wa Biblia. Mwaka wa 1909 walihamisha makao yao kuyapeleka Brooklyn, New York. Muda wa miaka iliyofuata hapo, wakurugenzi wa Watch Tower Society na wanaume wengine wenye kustahili walioshirikiana kwa ukaribu, wamekuwa wakitumikia wakiwa baraza linaloongoza la Mashahidi wa Yehova.

Katika Baraza Linaloongoza mna kikundi cha wanaume Wakristo wapakwa mafuta (13 katika mwaka wa 1986) kutia na 7 wanaotumikia katika baraza la wakurugenzi wa Watch Tower Society. Hao wanasimamia utendaji wa ulimwenguni pote wa Mashahidi wa Yehova. Wao hawakupuliziwa roho ya Mungu na hivyo si wasioweza kufanya makosa, lakini wanategemea Neno la Mungu lisiloweza kuwa na makosa Mamlaka iliyo kuu zaidi duniani, na pia muda wa maisha wenye ujuzi katika kutii mapenzi ya Mungu. Kila mmoja ana rekodi ya miaka zaidi ya 40 katika huduma ya wakati wote pamoja na Mashahidi wa Yehova.

Baraza Linaloongoza linasimamia yale ambayo Sosaiti inatangaza. Yanayoandikwa yanategemea kutazama mahitaji ya kiroho ya kundi na ni matokeo ya funzo na uchunguzi wa Neno la Mungu unaofanywa kwa sala na kwa uangalifu mwingi. Wanaume hao wanapoendelea kujifunza Biblia na kutazama kutimizwa hatua kwa hatua kwa makusudi ya Mungu, utimizo wa unabii katika matukio ya ulimwengu, na hali ya watu wa Mungu ulimwenguni, nyakati nyingine ni lazima wafanye marekebisho yaliyotiwa nuru katika ufahamu wa mafundisho fulani. Kwa njia hiyo, maarifa ya ukweli yanaendelea kuongezeka. —Zaburi 97:11; Mithali 4:18; Danieli 12:4.

Baraza Linaloongoza limeweka rasmi halmashauri ya tawi ya wanaume watatu au zaidi wenye kustahili kiroho katika kila moja la matawi 90 duniani pote wasimamie utendaji katika nchi na visiwa vya bahari zaidi ya 200. Matawi yanawasiliana na makundi yaliyo chini ya usimamizi wayo. Kuna mawasiliano ya kawaida kati ya Baraza Linaloongoza na Halmashauri za Matawi, na washiriki wa Baraza Linaloongoza wanazuru kibinafsi matawi mengi kila mwaka ili waendelee kujua hali zilizoko.

Wanaume hao si mabwana juu ya imani ya wengine bali ni wahudumu wanaofanya kazi kwa bidii ili wengine wengi waweze kujifunza Neno la Mungu. Hawatumikii kwa kupata faida ya kifedha, bali mahitaji yao ya kimwili yanatolewa kwa njia ile ile kama mahitaji ya washiriki wengine wote wa jamaa za Betheli. Uthibitisho unaoonyesha kwamba wanatumikia kwa uaminifu unaonwa katika bidii, umoja, viwango vya juu vya adili, na ushikamanifu kwa mafundisho ya Biblia unaoonyeshwa na Mashahidi wa Yehova ulimwenguni. —1 Wakorintho 3:5-9; 4:1, 2; 2 Wakorintho 1:24; 3:1-3; 1 Petro 5:2, 3.

• Ni mpango gani wa uongozi uliositawishwa?

• Ni nani wanaotumikia leo katika Baraza Linaloongoza, na madaraka yao ni nini?

• Kazi inasimamiwaje katika nchi nyingine?

[Ramani katika ukurasa wa 26]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

Maeneo ambamo Mashahidi wa Yehova wanafanya mapenzi ya Mungu

[Picha katika ukurasa wa 26]

Wasimamizi wa Watch Tower Society

C. T. Russell, 1884-1916

J. F. Rutherford, 1916-1942

N. H. Knorr, 1942-1977

F. W. Franz, 1977-

[Picha katika ukurasa wa 27]

Chache za afisi za matawi zaidi ya 90 ambazo kupitia hizo utendaji wa ulimwenguni pote wa Mashahidi wa Yehova unasimamiwa

Kanada

Zambia

Ujeremani

Japani

Australia

Brazili

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki