Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • jl somo la 20
  • Baraza Linaloongoza Hufanyaje Kazi Leo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Baraza Linaloongoza Hufanyaje Kazi Leo?
  • Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Nani Anayewaongoza Watu wa Mungu Leo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Kushirikiana na Baraza Linaloongoza Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Jukumu la “Mtumwa Mwaminifu na Mwenye Busara”
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
jl somo la 20

SOMO LA 20

Baraza Linaloongoza Hufanyaje Kazi Leo?

Baraza linaloongoza la karne ya kwanza

Baraza linaloongoza la karne ya kwanza

Wakristo wa karne la kwanza wakisoma barua kutoka kwa baraza linaloongoza

Kusomwa kwa barua ya baraza linaloongoza

Katika karne ya kwanza, kikundi kidogo, yaani, “mitume na wazee huko Yerusalemu,” kilitumikia kikiwa baraza linaloongoza lililofanya maamuzi muhimu kwa niaba ya kutaniko zima la Wakristo watiwa mafuta. (Matendo 15:2) Kuzungumzia Maandiko na kukubali mwongozo wa roho ya Mungu kuliwawezesha kufanya uamuzi kwa kauli moja. (Matendo 15:25) Ndivyo ilivyo leo pia.

Linatumiwa na Mungu kufanya mapenzi yake. Ndugu waliotiwa mafuta walio katika Baraza Linaloongoza wanapendezwa sana na Neno la Mungu nao wana uzoefu mwingi wa kutoa mwongozo kuhusu jinsi kazi inavyopaswa kufanywa, na pia kujibu maswali yanayohusiana na mambo ya kiroho. Wao hufanya mkutano kila juma ili kufikiria mahitaji ya ushirika wa akina ndugu ulimwenguni pote. Kama ilivyokuwa katika karne ya kwanza, maagizo yanayotegemea Biblia huandaliwa kupitia barua, waangalizi wanaosafiri, au vinginevyo. Jambo hili huwasaidia watu wa Mungu wawe na umoja. (Matendo 16:4, 5) Baraza Linaloongoza husimamia kuandaliwa kwa chakula cha kiroho, huwatia moyo wote washiriki katika kazi ya kuhubiri Ufalme, nalo husimamia kuwekwa kwa akina ndugu katika majukumu ya usimamizi.

Linafuata mwelekezo wa roho ya Mungu. Baraza Linaloongoza humtegemea Mwenye Enzi Kuu, Yehova, na pia Kichwa cha kutaniko, Yesu, ili kupata mwongozo. (1 Wakorintho 11:3; Waefeso 5:23) Ndugu walio katika baraza hilo hawajioni kuwa viongozi wa watu wa Mungu. Wao, pamoja na Wakristo wote watiwa-mafuta, wanaendelea “kumfuata Mwanakondoo [Yesu] popote anapoenda.” (Ufunuo 14:4) Baraza Linaloongoza huthamini sala zetu kwa niaba yao.

  • Ni nani waliokuwa katika baraza linaloongoza katika karne ya kwanza?

  • Baraza Linaloongoza hutafuta mwongozo wa Mungu jinsi gani leo?

PATA KUJUA MENGI ZAIDI

Soma Matendo 15:1-35, uone jinsi baraza linaloongoza la karne ya kwanza lilivyozungumzia na kutatua bishano fulani kwa kutegemea Maandiko na roho takatifu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki