Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 12/1 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Nani Anayewaongoza Watu wa Mungu Leo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Baraza Linaloongoza Hufanyaje Kazi Leo?
    Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Kushirikiana na Baraza Linaloongoza Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Kristo kwa Kutenda Aongoza Kundi Lake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 12/1 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

◼ Je! mtume Paulo alikuwa sehemu ya baraza linaloongoza la Kikristo?

Ni jambo linalolingana na kuwaza kuzuri kukata shauri kwamba Paulo alikuwa sehemu ya baraza linaloongoza katika karne ya kwanza.

Biblia inatoa maelezo machache tu juu ya waliokuwa katika baraza linaloongoza la kwanza, na nyingi za habari zenyewe zimo katika Matendo sura ya 15. Masimulizi hayo yanaonyesha kwamba kati ya kikundi cha wanaume waliofanywa kuwa sehemu ya baraza linaloongoza mwaka 49 W.K. walikuwamo “mitume na wanaume wazee.” Hao walikuwa akina nani?​—Matendo 15:2, 4, 6.

Yakobo, ndugu-mzazi-mmoja wa Yesu, ndiye aliyesimamia mkutano huo kulizungumza ulizo la kama ilikuwa lazima watu wa Mataifa walioongolewa wafuate Ukristo waishike Torati ya Musa, kutia na tohara. Mtume Petro aliyashiriki mazungumzo hayo. Masimulizi yanamtaja Yuda (anayeitwa Barsaba) na Sila kuwa walikuwa “wanaume mashuhuri miongoni mwa akina ndugu,” lakini hayasemi waziwazi kwamba walikuwa sehemu ya baraza linaloongoza.(Matendo 15:7,13,22, NW) Jambo ni kwamba Biblia haitoi orodha kamili ya majina ya wale waliokuwa katika baraza hilo. Wengine wamekuwa na maoni ya kwamba huenda ikawa Paulo hakutiwa ndani kwa kuwa alikuwa mmisionari mwenye kusafiri na kwa kuwa yeye ndiye aliyelileta ulizo hilo kutoka kundi lililokuwa katika Antiokia ya Siria.

Ni kweli kwamba Paulo hakuwa mmoja wa “wale kumi na wawili” waliokuwa wametembea pamoja na Yesu, kwa maana Mathiya alikuwa amekwisha kuchaguliwa aichukue nafasi ya Yuda Iskariote.a Lakini wala mwanafunzi Yakobo hakuwa mmoja wa hao ijapokuwa ni wazi alikuwa sehemu ya baraza linaloongoza. (Matendo 6:2; 1:15-26) Kuongezea hilo, Yesu alimtokea Paulo akamtaja kuwa ‘chombo kiteule cha kuchukua Jina lake mbele ya Mataifa.’ Hivyo, Paulo akawa “mtume, si mtume wa wanadamu, wala kutumwa na mwanadamu, bali na Yesu Kristo, na Mungu.” Yeye alijiita “mtume wa watu wa Mataifa.”​—Matendo 9:3-6, 15; Wagalatia 1:1; Warumi 11:13; 1 Wakorintho 9:1; 15:7, 8.

Ili kupata kionyesho kingine cha kwamba Paulo alikuja kuwa sehemu ya baraza la “mitume na wanaume wazee” walioyaelekeza makundi, fikiria aliyotenda chini ya uwezo wa Mungu. Paulo aliandika vitabu 14 vya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Petro anayaweka maandishi ya “ndugu yetu mpenzi Paulo” katika usawa mmoja na “maandiko mengine.” (2 Petro 3:15, 16) Paulo aliongoza kwa njia kubwa uenezaji wa Ukristo, naye alitolea makundi mwelekezo mwingi. Maandishi yake yaliyoongozwa na Mungu yanaonyesha kwamba nyakati nyingine Paulo aliamua masuala akiwa peke yake. Hilo ndilo jambo lingeweza kutazamiwa lifanywe wakati huo na mmoja wa baraza linaloongoza aliyekuwa mbali na hilo baraza kuu, akiwa pia bila njia ya haraka ya mawasiliano. (1 Wakorintho 5:11-13; 7:10, 17) Lakini nyakati nyingine alililetea mashauri baraza zima, kama vile masimulizi katika Matendo 15 yanavyoonyesha.

Akimwandikia Tito, “Paulo, mtumwa wa Mungu, na mtume wa Yesu Kristo” alisema: “Nalikuacha Krete, ili uyatengeneze yaliyopunguka, na kuweka wazee katika kila mji kama vile nilivyokuamuru.” (Tito 1:1, 5) Kwa hiyo alipokuwa akisafiri, ni hakika Paulo alinena kwa ajili ya baraza linaloongoza lililo kuu,​—Matendo 16:4,5.

Kwa hiyo, ingawa mgawo aliopewa na Bwana ulihusu kufunga safari za mbali na kuikosa-kosa mikutano fulani ya baraza linaloongoza lililo kuu, ushuhuda wa jinsi yeye alivyotumiwa na Mungu na Kristo unaonyesha kwamba Paulo alikuwa sehemu ya baraza hilo.

[Maelezo ya Chini]

a Kufikia wakati huo mtume Yakobo pia alikuwa ameuawa.​—Matendo 12:2.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki